Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 12

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Mungu Amenisahau Sehemu Ya Pili (02)
    Hadithi

    Mungu Amenisahau Sehemu Ya Pili (02)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaSeptember 24, 2024Updated:October 1, 20249 Comments7 Mins Read5K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mungu Amenisahau
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Tulienda moja kwa moja anapoishi Shonaa akaniambia kesho yakeย  atanipeleka kwa huyo Bosi, nilikuwa nimechoka hivyo sikuwa naย  maswali mengi zaidi ya kuhitaji Kupumzika tu, kweliย  nilipumzika hadi asubuhi kulivyo pambazuka. Shonaa aliamkaย  mapema sana, alikuwa amepangisha chumba kimoja na sebule,ย  nilienda hadi sebleni nilimsalimiaย 

    “Mambo Dada?” Aliacha alichokuwa anakifanya kisha alitabasamuย  akanijibuย 

    “Poa tu umeamka salama?” Aliniulizaย 

    “Ndiyo nipo sawa! Umedamka hivyo?” Nilimuulizaย 

    “Si unajuwa tena Maisha ya Mjini ndugu yangu, ukiendekezaย  Usingizi utakufa masikini” Alisema kisha tulicheka, nilionaย  nimepata Mtu wa kuzungumza naye na kumuuliza maswali yanguย 

    “Jana ulisema utanipeleka kwa Bosi asubuhi hii” “Usijali, subiria nimalize kupasi nguo zangu” Alijibu Shonaaย ย 

    Endeleaย 

    SEHEMU YA PILI

    “Unaitwa Nani?” Nilimuulizaย 

    “Naitwa Shonaa, wewe ni Jojo Eeh?”ย 

    “Ndiyo Naitwa Jojo” nilijibu huku nikiwa ninatabasamu.ย 

    Punde mlango wake uligongwa waliingia wasichana wengineย  wawili ambao walikuwa wamelewa, walisema maneno ya hovyoย  hovyo kisha walipitiliza hadi chumbani, mmoja alinisukumaย  nikaangukia kwenye kochi, kiukweli nilishtuka sana.ย 

    “Usijali Jojo utazoea, ndiyo Maisha yetu” Alisema Shonaaย  nilimsogeleaย 

    “Ndiyo Maisha yenu? Ina maana mnaishi Watatu hapa?”ย  Nilimuuliza Shonaa, alinisogelea akaniambia, Bado watatuย  hawajarudiย 

    “Eeeh?” Nilishangaa Watu sita wanaweza vipi kuishi hapoย 

    “Wewe ni wa saba Jojo, utazoea tu najuwa inakupa wakati Mgumuย  sana. Atakaye wahi kurudi analala Kwenye kitanda, ukichelewaย  kwenye kochi, ukichelewa zaidi unalala chini” Alisema Shonaaย  kisha aliendelea na kazi yake, kusema ule ukweli nilijilaumuย  kwanini nilikuja Dar, niliona ugumu ulio mbele yangu.ย  Nilitoka ndani nikampigia Msonjo ili ikiwezekana nirudiย  Tabora mara moja, niliona ni bora kulala njaa kuliko Maishaย  yaleย 

    “Jojo tutapata wapi nauli ya wewe kurudi haraka hivyo?ย  Vumilia kidogo mbona mapema hivi unakata tamaa jamani?”ย  Ilikuwa ni sauti ya Msonjoย 

    “Sikia Msonjo, yaani siwezi kuvumilia japo kwa sekunde moja,ย  wewe haupo ila Maisha yanatisha hivi Watu wa Mjini ndioย  wanaishi hivi? Chumba kimoja Watu saba?”ย 

    “Jojo! Ngoja niongee na Bosi tuone inakuwaje!” Alisema Msonjoย 

    “Jitahidi nakuomba Msonjo nipo katika nyakati ngumu sana”ย  Nilisema kisha salio liliisha kwenye simu yangu, nilipogeukaย  nyuma nilimuona Shonaa akitikisa kichwa chake, alikuwaย  akisikitika.ย 

    Shonaa alirudi ndani bila kusema chochote ila alikuwaย  amesikia mazungumzo yangu, nilipofika ndani aliniambiaย 

    “Jiandae tuondoke” basi nilielekea chumbani, yaani nilikutaย  mazingira ya hovyo sana, jinsi walivyolala wamewekeana Miguu,ย 

    mwingine alikuwa ametapika karibu na begi langu, kichefuchefuย  kilinizonga. Nilijikaza tu hivyo hivyo nilibadilisha nguo,ย  kisha nilitoka.ย 

    “Ndio unavaa hivyo?” Aliniuliza Shonaaย 

    “Ndiyo kwni kuna tatizo?” Nilimuulizaย 

    “Mmh! Haya twende” Alisema Shonaa kama vile kuna jamboย  alitaka kusema. Tulipanda daladala hadi Sinza kwa Remi,ย  kulikuwa na kumbi kubwa mpya ya Starehe iliyoitwa Dar Cityย  ndiyo ilikuwa ikimilikiwa na huyo Bosi aliyeitwa Muntaza.ย 

    Tulienda hapo kwenye huo ukumbi, palikuwa pameshachangamkaย  asubuhi asubuhi, Watu walikuwa wakipiga mitungi kama hawanaย  akili nzuri, tena ilionesha walikuwa wamekesha hapo hapo,ย  ilikuwa ni siku ya Jumamosi.ย 

    “Shonaa upo na mrembo” Alisema mmoja wa walevi kishaย  alimshika shonaa titi, alafu Shonaa hakuonesha kuchukia ndioย  kwanza alikuwa akicheka, nguvu ziliniishaย 

    “Kama kawaida si unanijuwa Mimi” Alisema Shonaa kishaย  tuliingia kwenye chemba mojaย 

    “Shonaa haya Maisha sitoyaweza” Nilisemaย 

    “Jojo bado hujayaona Maisha tayari unasema hutoweza, sasaย  unaweza kurudi kwenu Tabora na huna pesa hata ya kula? Achaย  ujinga, fanya kazi hata mwezi mmoja kisha ndioย  uondoke…..unakata tamaa mapema, inabidi upambaneย  kuhakikisha unapata pesa, hapa Mjini kila kitu ni pesa”ย  Alisema Shonaa akiwa amenikazia jicho, kisha aliongoza mbeleย  nami nilimfuata. Nilikuwa sijala ila Maisha niliyoyaonaย  yalinifanya nishibe, hebu fikiria Mtu anashikwa Titi mbele zaย  Watu alafu anacheka wakati Tabora Mtu umshike bega tu bilaย  ridhaa yake anakupiga kofi, nilitikisa kichwa changuย 

    Tuliingia kwenye chumba kimoja ambacho alikuwemo huyoย  Muntaza, kilikuwa ni chumba kinachonuka sigara na pombe,ย  alikuwa na wasichana wawili makamo yangu. Aliwaondoa baada yaย  sisi kuwa tumeshaingia na kuketi kwenye sofa jirani naย  alipoketi yeye, nilijikuta naanza kukohoa kutokana na uleย  moshi. Muntaza alikuwa ni pande la Mtu, alikuwa na cheniย  nyingi na pete, alafu alikuwa na kitambi, umri wake ulioneshaย  alikuwa zaidi ya miaka 50ย 

    Basi Shonaa alimsogelea na kumpiga busu huyo Muntaza,ย  nilitazama pembeni nikiwa ninakohoa.

    “Wow!” Alisema Muntazaย 

    “Bosi huyu ni Jojo uliyeniagiza kumpokea” Alisema Shonaa,ย  nilijichekesha kidogo ila kiukweli moyo ulikuwa ukiniendaย  mbio sana.ย 

    “Hukumuelekeza mavazi ya kuyavaa?” Alihoji Muntaza “Ndio Mwanzo Bosi nitaongea naye vizuri”ย 

    “Ok! Muelekeze majukumu yake” Alisema Muntaza kisha aliondokaย  hata bila ya kunisemesha chochote.ย 

    Alpoondoka Muntaza nilizidi kukohoa, nilikuwa nimevaa gauniย  na mtandio kichwani.ย 

    “Jojo ukitaka kuishi hapa vziri kubali hali halisi ilaย  ukileta misimamo isiyo na maana utajikuta Mji unakushindaย  huu. Hapa ndiyo ofisini kwako, kwangu na kwa wale wadadaย  wengine tuliowaacha kule nyumbani, mavazi ya hapa ni kamaย  yangu” Alivyosema hivyo nilimtazama alivyovaa, yaani alivaaย  kikomdomu tu na vest, chini rabaย 

    “Ukizubaa unapotea, kuwa mjanja”ย 

    “Lakini kusema ule ukweli Shonaa haya Maisha sina uhakika waย  kuyaweza kabisa, najilaumu sana kuja huku Dar ilaย  aliyenitafutia kazi nimemuomba anisaidie kuongea na Bosi iliย  anipe nauli nirudi kwetu” Nilisema.ย 

    “Usijidanganye kuhusu kupewa nauli, hata Mimi nilikuja kamaย  wewe miaka miwili iliyopita, nilikuwa muoga nilikuwa nikiliaย  nirudi nyumbani lakini ilishindikana”ย 

    “Lakini Shonaa mimi nimefiwa na Mama yangu mwezi uliopita,ย  nahisi nitakuwa namkosea sana kufanya kazi ya hivi, alinileaย  katika mazingira bora sana” nilisemaย 

    “Sawa alikulea katika mazingira bora ila hakuacha msingiย  wowote, laiti kama angelikuachia msingi basi usingekuja hukuย  kutafuta Maisha, hata Mimi Mama yangu nimemzika mieziย  michache iliyopita huko Kilimanjaro, nimerudi sababu hii niย  kazi inayoendesha Maisha yangu”ย 

    Maneno ya Shonaa yalinikata sana kauli, niliona napaswaย  kukubaliana na hali halisi japo bado tumaini langu lilikuwaย  kwa Msonjo aliyenileta Dar. Kulikuwa na nguo zikizokuwa mleย  kwenye chumba alinipatia nizivae, nilijitahidi kukataa lakiniย  aliniambia hakukuwa na sababu ya kutoka Tabora kuja Dar niย bora ningebaki Tabora. Basi nilizichukua nikabadilisha,ย  sikujiangalia mara mbili, yaani chupi ilikuwa ikionekana,ย  nguo zilibana na kushika mwili wangu, kila kiungoย  kilijichonga. Kibaya zaidi aliniambia nisivae sidiriaย 

    “Shonaa hivi siwezi kusema ukweli nitaweza vipi kutembeaย  jamani mbona unanipa wakati mgumu hivi” nilisema, Shonaaย  alicheka sana. Kabla hata hajaongea chochote aliingia Muntazaย 

    “Yupo tayari?” Aliulizaย 

    “Ndiyo Bosi”ย 

    “Haya akaanze kazi” Alisema kisha alijitupa kwenye Sofa akiwaย  anakohoa. Ningefanyaje unafikiri? Nilitoka na Shonaa bilaย  ubishi wowote ila nilikuwa navuta vuta nguo zangu iliย  zisinichonge hapa mbele kwa Bibi.ย 

    Siku hiyo ndiyo ilikuwa siku yangu ya kwanza katika Maishaย  yangu kufanya kazi ya Ubaamedi, nilikutana na vikwazo vingiย  ikiwemo kushikwa shikwa lakini nilijitahidi kukwepa kadiliย  nilivyoweza. Saa 12 walikuja wengine, Mimi na Shonaa tulirudiย  nyumbani kupumzika. Nilipewa elfu 10 kama pesa ya siku yaย  kazi, niliiweka pembeni ili ikitimia pesa ya Nauli niondokeย  zangu.ย 

    “Umeionaje siku yako ya kwanza kazini?” Aliniuliza Shonaaย 

    “Nzuri tu” Nilisema kisha nilitoa tabasamu feki, sikutakaย  tena kujionesha kuwa kazi hiyo nilikuwa siitaki, kwakuwaย  niliona naweza pewa kila siku elfu 10 hivyo ningeweza kurudiย  Tabora haraka sana.ย 

    “Najuwa unaumia Jojo ila utazoea tu sababu hata Mimi nilikuwaย  kama wewe siku ya kwanza naanza kazi, nilikuwa mnyonge,ย  sikuzoea kuvaa hivi ila ilinibidi nikubali hali halisi”ย 

    Alisema Shonaa akiwa ananiangalia vizuri kama vile alikuwaย  akinikagua, nilionesha lile tabasamu fekiย 

    “Kuna nini?” Nilimuuliza, alinishika nywele zangu akazibanaย  kwa kutumia mpira aliokuwa ameushika mkononiย 

    “Wewe ni mzuri sana Jojo” Alisema kisha aliachia tabasamuย  lililotoka moyoni mwake kabisa, hata mimi niliachia tabasamuย  lililotoka moyoniย 

    “Asante!” Nilimshukuru, tulikuwa wawili tu sababu wengineย  walienda zamu ya Jioni hiyo kurudi hadi asubuhi.

    Nini Kitaendelea? Usikose SEHEMU YA TATU ya MUNGU AMENISAHAU bila kuacha comments hapo chini

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx

    ย ย 

    Mungu Amenisahau

    9 Comments

    1. Yulia kimario on September 24, 2024 4:54 pm

      Fupi sana admin ila tamu โœŒ

      Reply
    2. Kelvin Mushi on September 24, 2024 7:28 pm

      Asantee admini

      Reply
    3. G shirima on September 24, 2024 7:34 pm

      Duh Jamani jojo

      Reply
    4. Sir, Yowas on September 25, 2024 9:56 am

      Maisha hayo jamani

      Reply
    5. Fatma on September 25, 2024 12:42 pm

      Jamani

      Reply
    6. Dessy on September 25, 2024 4:14 pm

      Nzuri sanaaa

      Reply
    7. Baba Jr on September 25, 2024 7:20 pm

      Daah Jojo jaman

      Reply
    8. Halinga1 on September 25, 2024 7:40 pm

      Mbona sehemu ya Tatu ina chelewa? Au ni mimi sijaona

      Reply
    9. yuzzo sailor official on September 26, 2024 1:22 pm

      sehemu ya tatu admin

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi October 1, 2025

    In the name of LOVE – 12

    Ilipoishia sehemu ya Kumi na moja ya In the name of LOVE Moyo Wangu na…

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    In the name of LOVE – 09

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.