Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Mungu Amenisahau Sehemu Ya Nane (08)
    Hadithi

    Mungu Amenisahau Sehemu Ya Nane (08)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaOctober 4, 2024Updated:October 5, 20248 Comments10 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mungu Amenisahau
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Basi Maisha ndani ya Gereza yaliendelea, siku moja baada yaΒ  kazi ilikuwa ni majira ya saa 7 Mchana, ulikuwa ni muda waΒ  kupata Chakula. Tulikuwa tukipanga mistari miwili kwa ajiliΒ  ya kupata Chakula, msitari wa kwanza nilikuwepo Mimi, sasaΒ  katika tazama tazama nilistaajabu nilimuona Sarafina, yuleΒ  Mdada ambaye alifukuzwa na Shonaa kisa Mimi, nilitamaniΒ  kumuita ila nilikumbuka kuwa alikuwa na hasira na Mimi,Β  nilimgeukia Isabela nikamuulizaΒ 

    “Yule yupo hapa kwa muda gani?” Nilimuonesha kidole SarafinaΒ 

    “Nimemkuta hapa, anaonekana kahukumiwa muda mrefu ilaΒ  inasemekana aliiba pesa kwa tajiri mmoja”Β 

    “Vipi unamjuwa?”Β 

    “Ndio namjuwa” Basi baada ya kuwa tumeshachukua chakulaΒ  tulienda kula, Isabela aliniulizaΒ 

    “Unamjua vipi yule”Β  EndeleaΒ 

    SEHEMU YA NANE

    “Wakati nakuja hapa Dar ndio nilionana naye ila tuliachanaΒ  kwa shari, aliniona mbaya akidai nimesababisha amefukuzwaΒ  pale alipokuwa anaishi” NilisemaΒ 

    “Mh! Sasa itabidi ujiadhari maana yule ana kundi lake hapaΒ  gerezani ambalo linaendesha ubabe mwingi, akijuwa kama upoΒ  hapa utaishi kwa shida sana” Alisema Isabela.Β 

    “Ni kweli lakini nitamkwepa vipi wakati tunaishi kwa uwaziΒ  hivi, ikiwa mimi nimemuona nina imani na yeye ataniona tu.”Β 

    “Cha msingi ni kumkwepa vinginevyo utateseka sana hapa Jojo”Β 

    “Mh! Tutaona itakavyokuwa” Tulipomaliza kula tulirudiΒ  kuendelea na kazi za Shamba, jioni tulihesabiwa kishaΒ  tulikula na kurudishwa kwenye vyumba kwa ajili ya kulala,Β  kila chumba kilikuwa na wafungwa 8 ambao tulikuwa tukilalaΒ  humo. Bahati nzuri chumba chetu hakikuwa na muhuni hataΒ  mmoja, kumbe taarifa ya Mimi kuwepo Gerezani alikuwa nayoΒ  Sarafina, kama Isabela alivyoniambia kuwa Sarafina alikuwa naΒ  kundi la ubabe pale gerezani.Β 

    Usiku tukiwa tumelala tena fofofo maana kazi za pale GerezaniΒ  zilikuwa ngumu mno hivyo Mtu akilala anakuwa kama amekufa.Β  Nilishtuka geti la chumba chetu lilikuwa likifunguliwa alafuΒ  tochi ilinimulika Usoni, aliingia mdada mmoja ambaye hakuwaΒ  Askari, aliniambia nimfuate.Β 

    Niliamka kisha nilimfuata, niliingizwa kwenye chumba kimojaΒ  kisha kilifungwa, kilikuwa ni chumba chenye giza mno kiasiΒ  kwamba sikuweza kuona chochote kileΒ 

    “Nipo wapi?” Nilijiulza kwa sauti ya chini huku nikipapasiaΒ 

    “Dada yangu kwanini umenileta huku?” Niliuliza, sautiΒ  ilijirudia tu katika kile chumba, sikujibiwa. Mara taaΒ  iliwashwa, nilikutana na macho ya SarafinaΒ 

    “Sarafina” Niliita kwa mshituko maana sikutegemea kamaΒ  ningekutana naye katika Mazingira yale, kwa vyovyote vileΒ  aliyenileta alijuwa nini anafanya.Β 

    “Karibu Jojo, Mungu wangu alinisikia kilio changu, hatimayeΒ  nimekutana na wewe” Alisema Sarafina akipiga hatua ndogoΒ  ndogo kusogea nilipokuwa nimesimama.Β 

    “Sarafina sikufanya chochote kibaya dhidi yako, sikutegemeaΒ  kama ingekuwa vile. Nisamehe tafadhali, tuyamalize”

    “Pengine umesahau Jojo, nilikuokoa yule Mwanaume asikubake,Β  nilimpiga mbele yako kukuonesha kuwa sikupenda alichokifanya.Β  Wema wangu kwako ndiyo uliozaa matunda yale, sikuwa na paΒ  kwenda, nilikuacha pale lakini nilisema ipo sikuΒ  nitakuonesha. Siwezi kuwa na haraka na wewe sababu upo kwenyeΒ  himaya yangu” Alisema Sarafina akiwa anazunguka huku na kuleΒ 

    “Sarafina tafadhali sana, nisamehe hujui ni mambo mangapiΒ  magumu nimekutana nayo, nimeishi Maisha magumu sana, hukumuΒ  niliyopewa ni adhabu tosha kwangu…” Nilisema kwa uchunguΒ  sanaΒ 

    “Lakini sio adhabu yangu, yangu itakuwa zaidi ya hiyo hukumuΒ  uliyopewa, wema wangu ukageuka kuwa udhalilishaji, siri yaΒ  ugonjwa wangu iliwekwa wazi, namjuwa Sana Shonaa kulikoΒ  unavyomjuwa wewe ni lazima alinianika kwenye kila jambo”Β  Alisema Sarafina akiwa amefika karibu zaidi na MimiΒ 

    Nilipiga goti nikamuomba Sarafina asinifanye chochote kibayaΒ  maana kama aliweza kupata funguo ya chumba chetu maana yakeΒ  alikuwa na uwezo hata wa kuniuwa na hakuna ambaye angesemaΒ  chochote kile.Β 

    “Magret” Aliita, yule Mdada aliyekuja kunichukua alikujaΒ  ndaniΒ 

    “Mrudishe, nitamalizana naye” Alisema Sarafina kishaΒ  nilirudishwa kwenye chumba chetu cha gereza.Β 

    Nilikuta Watu wa Chumba chetu wakiwa macho ni dhahiri kuwaΒ  walisikia Wakati Mimi ninaondolewa pale gerezani. Mtu waΒ  kwanza kuniuliza alikuwa ni IsabelaΒ 

    “Ulienda wapi Jojo?” Nilivuta pumzi nikamueleza nilipokuwaΒ 

    “Itabidi uwe makini sana Maana Sarafina ni Mtu mkorofi mnoΒ  hapa gerezani, ipo namna anaweza akafanya maisha yako yakawaΒ  si kitu hapa gerezani” Alisema Isabela akadakia MwanamkeΒ  mwingine akasemaΒ 

    “Wakati anafika aliwahi kupigana na askari Watatu naΒ  akawadhibiti vizuri sana, tokea siku hiyo amekuwa na urafikiΒ  na Mkuu wa Gereza hili, mara kadhaa amekuwa akitoka na kurudiΒ  haijajulikana wana ajenda gani, hivyo unapaswa kuwa makiniΒ  sana Jojo vinginevyo hata sisi tutakuwa hatarini. Ana kundiΒ  lake hapa na linatambulika na Mkuu wa Gereza, wao hawafanyiΒ  kazi yoyote ile zaidi ya kutoka na kurudi” Yalikuwa ndiyoΒ  maelezo yake kuhusu Sarafina, hilo la kupiga AskariΒ  halikunitisha sana maana nilikumbuka aliwahi kumpiga yuleΒ  Mwanaume aliyetaka kunibaka.

    “Ina maana anaishi humu gerezani kwa uhuru bila kubugudhiwaΒ  na chochote?”Β 

    “Ndiyo! Ni Mtu hatari sana, anaendesha biashara ya kuuzaΒ  Bangi na Unga hapa Gerezani, anachumba maalumu cha kulala naΒ  anapewa mahitaji yote ayatakayo” alielezea huyo MwanamkeΒ  mwingine, kiukweli nilijawa na woga sana, nilipitia kote ilaΒ  niliona dhahiri Maisha yangu yataishia ndani ya gereza,Β  nilimuuliza IsabelaΒ 

    “Ndugu zako wanakuja kukuona?”Β 

    “Hapana nahisi hawajaambiwa chochote na Mume wangu”Β  Alinijibu, lengo langu lilikuwa kama wanafika niwape maelezoΒ  waende nyumbani kwetu Tabora wakauze kibanda chetu ili wajeΒ  kunikomboa pale gerezani, nilichoka sana.Β 

    Wao walilala maana ulikuwa ni usiku mwingi, ila Mimi nilikuwaΒ  macho hadi Alfajiri ambapo tuliamshwa kwa ajili ya kazi, sikuΒ  zote nilikuwa napewa kazi nafanya na wenzangu ila siku hiyoΒ  ilikuwa tofauti sana, kwanza nilipelekwa kwenye kuvunja maweΒ  adhabu ambayo hupewa Wafungwa waliofungwa kwa kosa laΒ  Mauwaji. Pili niliambiwa natakiwa kuwa peke yangu, basiΒ  nilipelekwa huko na Askari mmoja, kulikuwa ni eneo lenye MaweΒ  yaliyochimbuliwa, nilipewa nyundo kubwa nilianza kazi yaΒ  kuvunja mawe, Mchana ulipoingia nilisikia kengele kwa ajiliΒ  ya kwenda kupata Chakula lakini yule askari alinizuiaΒ  akaniambia siruhusiwi kula kwa siku hiyo.Β 

    Nilikubaliana na hali halisi, nilifanya kazi kwa bidii sanaΒ  bila hata kutegea sababu nilijuwa yalikuwa ni maelekezo yaΒ  Sarafina, Jioni nilipelekwa kulala kwenye chumba cha pekeΒ  yangu, chumba hakikuwa na taa wala sehemu ya kulalia,Β  palikuwa pamemwagwa maji kwenye sakafu. Basi niliketi, japoΒ  nililoa lakini ilinilazimu kwani nisingeliweza kusimama kwaΒ  muda woteΒ 

    Kweli aliyesema Maisha ni popote, msemo ulikuwa na maanaΒ  kubwa sana, licha ya kutokula chochote lakini nililala kwenyeΒ  sakafu yenye maji, niliuchapa Usingizi kutokana na zile kaziΒ  ngumu. Usingizi ulinipitiliza hadi asubuhi sana, jua lilikuwaΒ  limeshatoka nilipata kuushuhudia mwanga wake kupitiaΒ  kidirisha kidogo ambacho kilikuwa juu pale kwenye kileΒ  chumba, mazingira ya chumba yalikuwa maalum, kilionekana kuwaΒ  ni chumba spesho.Β 

    Tofauti na vyumba vingine, chumba hicho kilikuwa na getiΒ  lisiloonyesha nje, kilikuwa na michoro ukutani na harufu kaliΒ  sana ya uchafu, wadudu walikuwa wakitembea kwenye ukuta,Β nilijiinua na kuketi pembeni nikiwa nimeegemea ukuta,Β  nilijiuliza kwanini sikuamshwa siku hiyo, masaa yalisogeaΒ  njaa ilizidi kuniuma, kiu ilizidi kunishika maana tokeaΒ  nilivyokula na kunywa maji siku iliyopita sikula wala kunywaΒ  maji tena.Β 

    Siku iliisha bila geti langu kufunguliwa, giza liliingia, KiuΒ  ilinibana sana na njaa ilizidi kuniuma, niligonga nifunguliweΒ  lakini hakuna aliyefungua mlango na hakukuwa na daliliΒ  iliyoonesha kuwa kulikuwa na Watu karibu. Siku hiyo iliisha,Β  Usiku uliingia, nilijaribu kuutafuta Usingizi lakiniΒ  sikuupata, nilikaa macho hadi kulipopambazuka, mwili ulikuwaΒ  na alama za kung’atwa na Wadudu na mbu.Β 

    “Mnifungulie nitakufa jamani” Nilisema kwa sauti isiyo naΒ  nguvu kabisa, siku mbili bila kula tena nikitoka kufanya kaziΒ  haikuwa rahisi kwangu kukabiliana na hali ile, haikusikikaΒ  sauti yoyote upande ule, niligumia kwa muda mrefu hadiΒ  nilikata tamaa ya Mtu kunisikia, nilirudi nikakaa chiniΒ  nikaegemea ukuta nikiwa nimechoka sanaΒ 

    Baadaye kidogo nilisikia sauti ya geti langu kufunguliwa,Β  niliamka haraka, ilitupwa bakuli moja kisha palifungwa,Β  nilikimbilia kwanza getini kisha nilisemaΒ 

    “Mnitoe humu nitakufa, kwanini mnakuwa wakatili kiasi hicho,Β  mnanitendea hivi kama nimeuwa?” Nilisema kwa sauti ya juu,Β  sauti ya Mtu kutembea ilikoma kisha ukimya ulisikika,Β  niligeuza macho yangu kwenye ile bakuliΒ 

    Nilisogea kuangalia kulikuwa kuna nini, niliifungua kishaΒ  niliona Mchuzi mwepesi sana na kipande kidogo cha MuhogoΒ  kilicho pikwa. Nililishika lile bakuri huku moyo ukiniumaΒ  sana, yaani kukaa siku mbili bila kula alafu niletewe mchuziΒ  na kipande kidogo cha muhogo? Nilitamani nimwage tu maanaΒ  sikuona kama nilistahili, ila nilipokumbuka kuwa nipo JelaΒ  nilifakamia mchuzi huo kisha nilikula muhogo.Β 

    Angalau kidogo nilikuwa nimekata kiu lakini njaa ilibakiaΒ  pale pale. Sekunde chache nilikuwa nimemaliza kula kishaΒ  nilikaa chini, Muda ulizidi kwenda, siku zilienda nikiwaΒ  ndani ya chumba hicho cha Mateso.Β 

    Macho yangu yakazoea giza, Uchafu ukatawala mwili wangu,Β  nilikojoa humo humo na kujisaidia haja kubwa humo humo, njaaΒ  iliponizidi nilikula kinyesi changu sababu nilikuwaΒ  nikiletewa supu kila baada ya siku mbili, nilianza kukonda naΒ  kudhohofika, sura yangu ilinyauka kutokana na kukosa chakula.

    Usiku mmoja nilikuja kuchukuliwa nikiwa hoi bin taabani, haliΒ  yangu ilikuwa mbaya kupita maelezo, nilikuwa nimelegea sanaΒ  hata kuongea siwezi, nilichokuwa nasubiria ni ujio wa MalaikaΒ  mtoa roho pekee aje anichukue maana sikuwa na tumaini tena laΒ  kuendelea kuishi.Β 

    Nilipelekwa kwenye chumba kimoja ambacho kilikuwa na taa,Β  mbele yangu kulikuwa na meza iliyokuwa na chakula chaΒ  kutosha, niliambiwa nile nishibe. Taratibu nilianza kulaΒ  chakula kile ambacho kilikuwa cha moto hivyo kilinipa nguvuΒ  sana.Β 

    Angalau nilipata unafuu sana, mwili uliingia nguvu hadiΒ  nilipata uwezo wa kumuuliza Mdada aliyekuja kunichukua kuleΒ  kwenye chumna chenye matesoΒ 

    “Kwanini mlitaka kuniuwa?” Nilimuuliza kwa sauti ya uchovuΒ  kiasiΒ 

    “Majibu utayapata muda siyo mrefu” Alisema, niliendelea kulaΒ  huku nikisubiria hayo majibu. Punde aliingia SarafinaΒ 

    “Jojo” Alisema kisha aliketi kwenye kiti, alichukua chakulaΒ  kidogo akala kabla ya kusema chochote kile, nilimtazama sanaΒ  SarafinaΒ 

    “Kwanini ulitaka kuniuwa Sarafina, ni kosa gani ambaloΒ  halisameheki hadi kufikia hatua ya kutaka kuondoa uhaiΒ  wangu?” Nilimuuliza Sarafina huku chozi likianzaΒ  kunibubujika.Β 

    “Kiukweli sikutegemea baada ya muda huo uliokaa kule ungetokaΒ  ukiwa hai Jojo, hakika wewe ni miongoni mwa wachache wenyeΒ  roho ngumu sana, wengi walifia mle ila wewe umetoka, Hongera”Β  Alinipongeza Sarafina, ila niliona kama ananikaidisha tuΒ 

    “Unanipongeza kwa lipi ikiwa ulitaka nife? Wewe ni mnyamaΒ  Sarafina…hadithi ya Maisha yangu imebadilika ghafla sana”Β  Nilisema huku nikiwa ninafuta chozi languΒ 

    “Sarafina, kama kifo changu kitakuwa furaha kwako usisiteΒ  kunimaliza ili nipumzike hii mitihani mizito ambayo imekuwaΒ  ikiniandama baada ya Mama yangu kufa, sitaki kuingia kwenyeΒ  mtihani mwingine, imetosha, nimeteseka sana Mimi Sarafina,Β  ona nimedhohofika sina hata nguvu” Nilisema kwa uchungu sanaΒ  huku nikiwa ninabubujikwa mchozi.Β 

    Sarafina alifuta chozi lake lililokuwa linaanza kumtoka,Β  stori yangu ilimfanya alie kidogo japo baadaye alijifanyaΒ  haijamuumiza

    “Sikia Jojo, ukiishi kwa kuhitaji huruma ya wengine utaishiaΒ  kuishi Maisha ya hovyo sana. Lengo la kukutoa mle ni kutakaΒ  kufanya na wewe baadhi ya Majukumu kisha utaachiliwa huru”Β  Nilishtuka sana kusikia kuna majukumu nataka kupewa, nilifutaΒ  chozi kisha nilimuulizaΒ 

    “Majukumu?”Β 

    “Ndiyo! Kwasasa angalia Afya yako kwa mwezi mzima kishaΒ  utakapokuwa sawa nitakuchukua tena” Hakunipa hata nafasi yaΒ  kumuuliza chochote kile, aliondoka zake. Yule Mdada mwingineΒ  alisogea akaniambiaΒ 

    “Unapaswa kwenda Hospitali” Alininyanyua kisha alinitoa pale,Β  Ulikuwa ni usiku mwingi sana, nilipelekwa Kwenye hospitali yaΒ  pale pale Magereza.Β Β 

    Nini Kitaendeea?Β  Nione COMMENT NYINGI LEO au MSHAICHOKA TUACHE KUIPOST?Β 

    Usikose SEHEMU YA TISA ya MUNGU AMENISAHAU bila kuacha comments hapo chini

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAΒ 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xx Β Mungu Amenisahau xxΒ 

     

    Mungu Amenisahau

    8 Comments

    1. Deo on October 4, 2024 8:05 pm

      Nomaaaa

      Reply
    2. Nelca on October 4, 2024 8:33 pm

      Kazi nzuriπŸ’ͺπŸ”₯πŸ”₯

      Reply
    3. Nelca on October 4, 2024 8:34 pm

      Kaz nzuri πŸ’ͺπŸ”₯πŸ”₯

      Reply
    4. G shirima on October 4, 2024 8:53 pm

      Nyie mnafikiri ni majukumu gani anapewa

      Reply
    5. Kelvin Mushi on October 4, 2024 9:19 pm

      Dah hii ya leo mpaka machoz

      Reply
    6. Stella on October 7, 2024 7:18 am

      Dah pole Sana sarafina

      Reply
    7. Majaliw on October 9, 2024 3:13 pm

      Napenda tahalifa za kijiwen

      Reply
    8. πŸ“ Reminder; Operation 1.765906 bitcoin. Verify >>> https://graph.org/Payout-from-Blockchaincom-06-26?hs=e1b8260f34e0f4652029a1b382f9e336& πŸ“ on July 16, 2025 8:58 am

      f4lc82

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 23, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nane β€œNakufahamu Zahoro, wewe ndiye jibu la Laana hii.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-06

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.