Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 05

    In the name of LOVE – 04

    In the name of LOVE – 03

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Mungu Amenisahau Sehemu Ya Kwanza (01)
    Hadithi

    Mungu Amenisahau Sehemu Ya Kwanza (01)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaSeptember 23, 2024Updated:October 1, 202413 Comments6 Mins Read7K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mungu Amenisahau
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Chozi lilikuwa likinimwagika, nilikuwa nikimuaga Mama yanguย  kwa mara ya Mwisho Mkoani Tabora.ย 

    “Mama! Umeniacha Mama yangu, nimebaki mwenyewe” Nilisema kwaย  sauti iliyowaumiza wengi, alikuja Mama mmoja alinishikaย  vizuri akaniambiaย 

    “Jojo usilie sana utakufuru, Muache Mama yako apumzike kwaย  Amani” Alisema kwa sauti iliyojaa maumivu pia sababu alikuwaย  ni jirani yetu. Hadi Mama anafariki hakuwahi kunioneshaย  mahali ambapo ndugu zake walikuwa wakiishi hata hivyo alikuwaย  hapendi kuzungumza kuhusu ukoo wao.ย 

    Mama yangu alizikwa katika Ardhi ya Tabora, ukawa mwishoย  wake, nilikumbuka maneno yake kuwa Kila siku Binadamuย  wanakufa, walio hai wanakuwa kwenye hiyo foleni, kila mmojaย  ataenda huko ambako Wafu huenda na hawarudi, alisemaย 

    “Jojo ipo siku tutatengana hatuta onana tena, nikitanguliaย  ishi vizuri na Watu, niombee Mama yako” Alisema siku mojaย  akiwa anaumwa, japo sikupenda sana kusikiliza kauli za Mamaย  ambazo zilikuwa zikiniumiza. Hatimaye maneno yake yalitimia,ย  aliniacha nikiwa bado namuhitaji sana.ย 

    Huzuni ilinijaa, siku mbili zilipita. Nilimkumbuka Mamaย  yangu, alikuwa ni ndugu yangu pekee katika hii Dunia, baadaย  ya Mama walifuata majirani zangu sababu hata Baba yanguย  nilikuwa simjui.ย 

    “Pole Jojo, Mungu atakurudishia tabasamu lako siku moja”ย  Alisema jirani mmoja ambaye alikuwa akichuma mboga katikaย  Bustani yake ndogo iliyo kando ya nyumba yetu iliyo Bomokaย  upande mmoja. Nilimtazama Mama Rafia, niliangalia nyumba yetuย  kisha nilitabasamuย 

    “Ndio, Mungu hawezi kukusahau Jojo, amekupa kila kitu” Mamenoย  ya Mama Rafia yalizidi kunipa tabasamu kidogo, nilikuwaย  nimejikunyata nilimfuata alipokuwa anachuma mboga za majani

    “Chukua kidogo ikusaidie leo” Alisema tena Mama Rafiaย 

    “Nashukuru Mama Rafia” Nilisema, Basi nilichuma kiasi kidogoย  cha mboga kisha nilirudi ndani, Maisha hayakuwa mazuri paleย  nyumbani, sikuwa na kazi yoyote ile.ย 

    Nilikagua Mkaa haukuwepo, Mafuta wala chumvi vyoteย  havikuwepo, niliingia chumbani nilipekuwa kwenye begiย  nilikuta pesa kama Shilingi elfu tatu na senti zake. Niliendaย  kununua Mkaa wa shilingi Elfu moja na mahitaji mengine madogoย  kisha Unga robo ili nisogeze Mchana huo.ย 

    Wakati narudi nilikutana na Mama Rafia, alikuwa ni Mamaย  Mcheshi sana, alikuwa anapenda utani mno. Kila nilipomuonaย  nilijihisi kupona maumivu yanguย 

    Nilipika chakula changu vizuri, nilikula, nilipata muda waย  kupumzika na kutafakari nini nifanye. Umri wangu wa miaka 28ย  haukunitosha kuhisi naweza nikajikwamua, nilishusha pumziย  zangu maana kila nilichokuwa nakifikiria hakikunipa majibuย  yenye uhakika, nilijiegesha Kitandani nikiwa natazama matunduย  ya paa la bati alafu nilijikuta nikicheka maana ilikuwa kamaย  chujio la tui la nazi vile.ย 

    Mara nilisikia sauti ya Mtu akiniita huko Nje, ilikuwa niย  sauti ya Mkaka aliyeitwa Msonjoย 

    “Abee! Nakuja” Nilisema, nilijikurupusha kisha nilitokaย  ndani, alikuwa Mkaka fulani hivi mcheshi na alikuwa maarufuย  sana mtaani kwetu, alikuwa akiyajuwa fika Maisha yetu.ย 

    “Muarabuuu wa Tabora” Alisema Msonjo kwa utani, nilikuwa naย  asili ya uarabuย 

    “Abee!” Niliitika nikiwa nafunga khanga yangu vizuri “Pole kwa kifo cha Mama yako Jojo” Alisema Msonjoย 

    “Nimeshapoa ndiyo Maisha, wacha apumzike ameumwa sana”ย  Nilisema kisha nilifuta choziย 

    “Sasa Jojo, kwa jinsi ulivyo hupaswi kuishi Tabora, unatakiwaย  kwenda kuishi Dar sababu huko ndio kuna Maisha mazuri yaย  kuishi wewe na rangi yako” Alisema Msonjo, nilijiweka makiniย  kumsikilizaย 

    “Una maanisha nini?” Nilimuuliza

    “Kuna Bosi anatafuta wafanyakazi yupo Dar nikasema siweziย  kukuacha ndugu yangu, ni bora ukatafute Maisha huko Mjini”ย  Maneno yake yalinifanya nikumbuke nilichokuwa nakiwaza nikiwaย  ndani.ย 

    “Kazi gani hiyo?”ย 

    “Mmh! Yeye ni tajiri tu sina hakika sana ila anahitajiย  Wafanyakazi, utalipwa vizuri Jojo hebu angalia maisha yako,ย  Mama hayupo tena unafikiri utaishi Maisha ya dhiki hadi lini”ย  Alisema tena Msonjoย 

    “Nimekuelewa Msonjo ila nahitaji muda kupona kwanza kutokanaย  na maumivu ya kumpoteza Mama kisha nikiwa tayari nitakuambia”ย  Nilisemaย 

    “Mh! Haya…Maamuzi ni yako wewe! Ukiwa tayari utasema, alafuย  upo na nani?”ย 

    “Hahaah! Msonjo hebu niache sitaki kucheka” Nilisema kishaย  niliingia ndaniย 

    “Jojo mimi sina Mke kwahiyo kama ukiona vipi wewe niambie tu”ย  Alisema kwa utani akiwa anaondoka, nilishamzoea kwa utaniย  wake.ย 

    Nilipofika chumbani nilikaa kitandani nikatafakariย  alichokisema Msonjo, ni kweli sikuwa na kazi na sikuwa naย  tumaini lolote Tabora, kuhusu uzuri ni kweli nilikuwa mzuriย  mno ila sasa uzuri ndio uwe kigezo cha Mimi kuishi Maishaย  mazuri na kupata kazi? Nilicheka kidogo.ย 

    Siku zilienda, Maisha yalizidi kunichapa Tabora, nililalaย  njaa, nilikula mlo usio na shibe, Mwezi mzima ulikatika.ย  Nilimtafuta Msonjo kuhusu masuala ya kazi huko Dar.ย  Alinieleza kazi yenyewe hadi mwili ulichoka yaani, ilikuwa niย  kazi ya kuwa Baamediย 

    “Hiyo siwezi Msonjo nina shida lakini hiyo kazi hapana”ย  Nilimwambia Msonjo huku nikiwa ninakaa juu ya Tofaliย 

    “Sasa kipi bora ulale njaa hapa Tabora au ukale Maisha Dar?ย  Wewe kule unaenda kwa mipango na malengo yako, hauendi kuishiย  Maisha ya Kibaamedi” Alisema Msonjoย 

    “Mh lakini Msonjo hakuna kazi nyingine?”ย 

    “Jojo, Mchagua jembe siyo Mkulima” Alisema Msonjo akawaย  anaondoka, nilifikiria nikaona ni bora nikubali

    “Msonjo” nilimuita, alisimama kisha alisogea nilipo “Nakusikiliza” Alisemaย 

    “Nipo tayari” nilisemaย 

    “Hayo ndiyo Maneno niliyotaka kusikia kutoka kwako Jojo, hapoย  umenifurahisha ngoja nimpigie huyo Bosi” Alimpigia huyo Bosi,ย  ilitumwa nauli muda huo huo, nilipaswa kujiandaa ili keshoย  yake nianze safari kutoka Tabora kwenda Darย 

    Nilirudi nyumbani, nilimpa taarifa Mama Rafia, alinitafutiaย  Mtu wa kuishi pale kwa kipindi chote ambacho nitakuwa Dar,ย  Nilijiandaa, Usiku Msonjo alinieletea Tiketi ya Basi kishaย  alinipa kiasi cha pesa kwa ajili ya matumizi nikiwa safarini,ย  moyo ulikuwa ukinienda mbio, sikuwahi kwenda Dar ilikuwaย  ndiyo mara yangu ya kwanza.ย 

    Alinipa namba ya huyo Bosi wa kazi, alikuwa ni Mwanaume, kwaย  jinsi alivyonielekeza Msonjo Bosi alikuwa ni Mmiliki waย  migodi huko kusini mwa Tanzania katika Mkoa wa Lindi.ย 

    Alfajiri safari ya kuelekea Dar ilianza. Ilikuwa ni safariย  iliyojaa mawazo, nitaishi vipi, hiyo kazi sijui kamaย  nitaiweza. Tulipofika Dar, nilikuja kupokelewa na Mdada mmojaย  ambaye alijitambulisha kwangu kama Shonaa, alikuwa na umriย  sawa na Mimi, ulikuwa ni usiku.ย 

    Tulienda moja kwa moja anapoishi Shonaa akaniambia kesho yakeย  atanipeleka kwa huyo Bosi, nilikuwa nimechoka hivyo sikuwa naย  maswali mengi zaidi ya kuhitaji Kupumzika tu, kweliย  nilipumzika hadi asubuhi kulivyo pambazuka. Shonaa aliamkaย  mapema sana, alikuwa amepangisha chumba kimoja na sebule,ย  nilienda hadi sebleni nilimsalimiaย 

    “Mambo Dada?” Aliacha alichokuwa anakifanya kisha alitabasamuย  akanijibuย 

    “Poa tu umeamka salama?” Aliniulizaย 

    “Ndiyo nipo sawa! Umedamka hivyo?” Nilimuulizaย 

    “Si unajuwa tena Maisha ya Mjini ndugu yangu, ukiendekezaย  Usingizi utakufa masikini” Alisema kisha tulicheka, nilionaย  nimepata Mtu wa kuzungumza naye na kumuuliza maswali yanguย 

    “Jana ulisema utanipeleka kwa Bosi asubuhi hii” “Usijali, subiria nimalize kupasi nguo zangu” Alijibu Shonaaย 

    Nini Kitaendelea? Usikose SEHEMU YA PILI ya MUNGU AMENISAHAU bila kuacha comments hapo chini

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx

    Mungu Amenisahau

    13 Comments

    1. Daniel on September 23, 2024 5:50 pm

      Imeanza vzr sana

      Reply
      • isaac moses on September 23, 2024 6:57 pm

        inaonekana ina mambo mazuri huko mbele

        Reply
        • Anitha brighton on September 25, 2024 5:37 pm

          Iko vizuri na inaonekana ni yakuzunisha

          Reply
    2. Halinga1 on September 23, 2024 7:15 pm

      ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ‘†

      Reply
      • Fatma on September 25, 2024 12:30 pm

        Vizur๐Ÿ™‚

        Reply
    3. Cevoo on September 23, 2024 8:07 pm

      Asantee adim

      Reply
    4. Renatus Nyambele on September 24, 2024 11:15 am

      Hii story itakuwa tamu acha niendelee kuifatilia

      Reply
    5. Pretty on September 24, 2024 11:17 am

      Ni moto๐Ÿ”ฅ next please mwandishi๐Ÿ˜

      Reply
    6. Luttine on September 24, 2024 11:58 pm

      Kubal xan ๐Ÿ‘Œ

      Reply
    7. Shaweji on September 25, 2024 8:03 am

      Nangoja muendelezo nahisi unakuwa na na visanga

      Reply
    8. Ahmed on October 9, 2024 11:38 am

      Nmeipenda ila nlikua na wazo (ushauri)

      Reply
    9. Godfrey on October 9, 2024 1:20 pm

      Unajua kuandika mwandishi big up

      Reply
    10. ๐Ÿ” Security; Deposit 0.3 BTC incomplete. Verify now โ€บ https://graph.org/OBTAIN-CRYPTO-07-23?hs=5642b20971e6045ec342709b11a6407c& ๐Ÿ” on August 27, 2025 10:37 am

      zfaszw

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi September 15, 2025

    In the name of LOVE – 05

    Ilipoishia sehemu ya tatu ya In the name of LOVE โ€œBasi hakuna shida Zaylisa, mnaweza…

    In the name of LOVE – 04

    In the name of LOVE – 03

    In the name of LOVE – 02

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.