Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Mashabiki Na Wachezaji Wana Nguvu Kubwa Ya Uchumi
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Mashabiki Na Wachezaji Wana Nguvu Kubwa Ya Uchumi

    Cosmasy ChogaBy Cosmasy ChogaAugust 13, 2024Updated:August 13, 20241 Comment4 Mins Read965 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mashabiki
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Mwaka 2018 nikiwa nimetulia zangu napekua mambo Google kama ilivyo desturi yangu kufanya hivyo huku nikiwa nimeweka Earphone zangu masikioni kusikiliza redio ambapo kipindi cha michezo kulikuwa kinaanza kwa muda huo,mara namsikia kiongozi mmoja akilalamikia wachezaji na mashabiki wao.

    Alikuwa ni kiongozi wa timu ya Coastal Union na katika kuongea kwake alizungumzia wachezaji kupambana mechi mbili tu na hata hata mashabiki nao kushindwa kuongozana na timu yao pale inaposafiri. Miongoni mwa nukuu zake ilikuwa ni.

    “Tangu nimeteuliwa Kuwa Kiongozi wa Coastal Union huwa nachunga sana mdomo wangu kuongea katika hadhara kuhusu mechi za Coastal union na mapungufu ninayoyaona. Tayari nimechuja maneno yangu, na naomba kuongea kama mpenzi wa Coastal union sasa.”

    “Tatizo walilonalo wachezaji wa Coastal union ni la kisaikolojia na tatizo hilo pia wanalo mashabiki wa Coastal union.”

    “Wachezaji wa Coast wanafikiri wakizifunga Yanga au Simba wataondoka na points(alama) kumi katika mchezo mmoja,wanasahau wakiifunga African Lyon wanaondoka na alama tatu na wakiifunga Yanga wanaondoka na alama tatu vilevile.”

    “Angalia mashabiki wa Coast nao hawakushughulika kusafiri kutoka Tanga kwenda Dar siku ya mechi ya African Lyon ikicheza na Coast badala yake walishugulikia mechi ya Yanga. Wakidhani tukiifunga Yanga tutakuwa tumebeba kombe.”

    “Tujiulize ndani ya nafsi zetu tumekwenda kuishangilia Coast au kuangalia Yanga?. Majibu tunayo wenyewe.”

    “Sasa naongea kama katibu mkuu. Ofisi yangu itakuwa mstari wa mbele kuhamasisha safari za mashabiki ikiwezekana hata kutafuta  usafiri wa bure kwa zile mechi zote za mikoa ya jirani, Tukumbuke mechi zote za ligi kuu ni muhimu. Hivyo mashabiki na wachezaji wanapaswa kuziona kama fainali na kucheza kwa ari kubwa sio kusubiri mechi za Simba na Yanga tu.”

    Mwisho alihitimisha kwa kusema. “Kutoa draw na African Lyon kumeniuma sana kuliko tulivyofungwa na Yanga. Sasa mashabiki twendeni Mabatini kwa wingi siku ya jumamosi tukachukue alama zetu tatu. Go Coastal Go …”

    Yalikuwa ni maneno ya uchungu wa moyoni kabisa toka kwa kiongozi huyo,aliongea kwa masikitiko sana. Japo ukweli siku zote huwa unauma lakini yalikuwa ni maneno yenye somo kubwa sana ndani yake kwa wachezaji na mashabiki. Hapa niongezee hata viongozi nao wapo hivyo.

    Wachezaji wengi wa Kitanzania wapo hivyo huyo kiongozi aliyefunguka hivyo wala hakukosea wachezaji wanapaswa kutambua kila mechi ni muhimu kwa maendeleo ya timu yao. Wanapaswa kujua endapo wataipa ubingwa timu ni sehemu ya CV kubwa kwao hata kwenda nje ya nchi itawezekana tu bila kupitia Simba Sc au Yanga Sc.

    Kama wadau wa soka tumekuwa tukilaum sana viongozi juu ya vilabu hivi kukosa wadhamini ila kuna wakati tunajiuliza pia ni nani ataweka pesa yake kwenye klabu mbovu?. Hakuna ambae atafanya hivyo labda awe na mapenzi tu na timu hiyo kama alivyo Bin Silum na Coastal yake,au tu GSM alivyoingia Majimaji FC kwa kuwa ni mzaliwa wa huko.

    Kama wadau wa soka tumekuwa tukijiuliza pia Mbao FC na baadhi ya timu kwa nini zilikua zinapigania kutoshuka wakati zikikutana na Simba Sc au Yanga Sc zenyewe ziliweza kuongoza kila kitu?.

    Nafikiri wachezaji wanapaswa kujiongeza ipasavyo katika hili,watambue thamani iliyofanya wawepo kwenye hivi vilabu na kulipwa pesa wakati kuna wachezaji hata nafasi ya Daraja la kwanza hawapati.

    Wao kama wachezaji wanapaswa kujua mashabiki wao watawafata popote waendapo wakifanya kazi ya kupendeza. Lakini hata mashabiki wanapaswa kutambua kuwa hakuna shabiki ambae atatoka Dar es Salaam kuvifata vilabu hivyo zaidi ya wao ndani ya mkoa,ikiwa wanaweza kukaa na kulalamika juu ya timu yao ya mkoa basi wajue hata wao ni chanzo cha timu kuyumba.

    Ni nani haikumbuki Mbeya City ya msimu wa kwanza ilipopanda?,nani hakumbuki matawi yaliyozaliwa msimu ule wa Mbeya City ama nani hakumbuki mashabiki wa Mbeya City walivyojitahidi kusafiri na timu yao?. Kila mmoja anajua uwepo wa mashabiki pia unachangamsha akili za wachezaji na kuweza kuipa thamani timu.

    Vyama vya soka mikoa vina dhamana kubwa sana ya kulinda soka la mkoa husika kwa kusaidia viongozi wa timu hizo,pia wale ambao huhangaikia timu kupanda wasitengwe baada ya mafanikio hawa ndio wana ushawishi mkubwa kwa mashabiki na wadau wengine. Ikiwa wanaweza kuchangisha watu Tsh 100/= wakiwa na mechi basi hawatashindwa kutoa hamasa huku pia.

    Nihitimishe kwa kuwapa ushauri wa bure tu wachezaji wanatakiwa kujua kazi zao ndio malipo yao angalau sasa. Amkeni mliolala katika kiza angali umeme umefika vijijini.

    SOMA ZAIDI: Hakuna Simba Na Yanga Bila Msingi Wa Uwepo Wao

    ligi kuu ligi kuu nbc ligi kuu tanzania bara

    1 Comment

    1. Pingback: Heritier Makambo Kitabu Cha Simulizi Walichokataa Wazawa

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.