Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 12

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Love & Pain Sehemu Ya Nane (08)
    Hadithi

    Love & Pain Sehemu Ya Nane (08)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaNovember 20, 2024Updated:November 25, 202419 Comments7 Mins Read4K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Love & Pain
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Basi twende nikusindikize” Alisema Mwanaume huyo, Luciaย  aliingia kwenye gari, safari ilianza kuelekea nyumbani kwaoย  Noela, wakiwa Barabarani mwanaume huyo alionekana kumtongozaย  Lucia lakini Lucia hakuonekana kumkubali kisha alimwambiaย 

    “Kama umenipa msaada ili unitongoze naomba unishushe Mimiย  siyo Mwanamke wa hivyo” Alisema Lucia akionekana kuchukizwa.. Endeleaย 

    SEHEMU YA NANE

    “Aaah usijali samahani kwa hilo, tunapita kushoto ili tuwahiย  kufika” Alisema Mwanaume huyo kisha alikata kushoto lakiniย  Lucia alimuulizaย 

    “Huko barabara imefungwa kuna ujenzi utapita vipi alafu kunaย  pori kubwa huko” Alisema Lucia jamaa alizidi kuongeza giaย  kisha alicheka, ndipo Lucia alipomkumbuka Desmond na kauliย  yake, basi Lucia akaanza kuhangaika ili ashuke maana alijuwaย  hapo ni lazima atafanyiwa kitu kibaya, kumbuka Tayari maagizoย  ya kuuawa kwa Lucia yalikuwa yametolewa na Desmond, katikaย  pirikapirika gari hiyo ikajikuta ikipoteza uelekeo na kugongaย  Mti.ย 

    Hali zao zilikuwa mbaya mno, Lucia alijitahidi kufunguaย  mlango akiwa hoi damu zikiwa zinamtoka, Mwanaume huyo nayeย  alikuwa akitokwa na Damu usoni, naye alifungua mlango akaanzaย  kumfukuza Lucia aliyekimbilia porini eneo ambalo lilikuwa naย  mlima hivi. Akiwa anazidi kukimbia Lucia alimpigia sana simuย  Noela lakini simu haikupokelewa, katika kukimbia akajikutaย  ameindondosha simu yake.ย 

    Mwanaume huyo aliiokota simu ya Lucia kisha aliendeleaย  kumfukuza, bahati mbaya Lucia alijikwaa akaanguka chini, maraย  moja Mwanaume huyo akiwa ana vuja damu alimfikia.ย 

    “Wewe ni Nani na unataka nini?” aliuliza Lucia akiwa katikaย  hali ya hofu sana huku akiwa amechoka.ย 

    “Unataka kujua mimi ni nani na Nataka nini kwako si ndiyo?ย  Mimi ni muuwaji nimekuja kuchukua roho yako Lucia” Alisemaย  Mwanaume huyo akionekana kumfahamu vizuri sana Lucia

    “Uniuwe kwa kosa gani mbona sikufahamu?” aliuliza Lucia akiwaย  katika hali ya hofu huku maumivu ya Mguu yakizidi kumtafuna.ย 

    “Kosa lako ni Moja tu, kujifanya mjuwaji. Umeonywa mara ngapiย  kuhusu Mandy wewe?” aliuliza Mwanaume huyo na kumfanya Luciaย  sasa ajuwe kuwa Desmond alishatuma Mtu ili auawe.ย 

    “Ina maana umetumwa na Desmond si ndiyo? unafikiri ukiniuwaย  itakuwa mwisho wa kila kitu? nakuhakikishia kifo changuย  hakitofanya siri yenu isitoke, tena itatoka kwa kishindoย  kikubwa sana” Alisema Lucia katika hali ya kujiamini sanaย  baada ya kujuwa kuwa alitakiwa kufa kwa maagizo ya Desmondย 

    Yule Mwanaume alimbana vizuri Lucia pale chini akahakikishaย  anakosa hewa kwa zaidi ya dakika moja kabla ya kunyongaย  shingo ya Lucia, baada ya hapo alipiga simu mahali akasemaย 

    “Kazi imeisha” Alisema kisha aliubeba mwili wa Lucia akaendaย  kuuweka kando ya Barabara hiyo ambayo ilikuwa na giza sanaย  kisha akaliwasha gari lake lililobamiza kwenye Mti kishaย  aliondoka eneo hilo.ย 

    Shughuli ilikuwa imepamba moto, Noela hakumuona Lucia akiendaย  hapo licha ya kuarikwa, hakujuwa kuwa Lucia alikuwa ameuawaย  porini. Desmond alimuuliza Noela alikuwa akifikiria niniย  baada ya kumuona akiwa kama Mtu mwenye kutafakari jamboย 

    “Rafiki yangu Lucia, alisema anakuja hadi sasa hivi, nampigiaย  simu hapatikani” Alisema Noelaย 

    “Atakuja tu, Watu wengine ndio kwanza wanaingia hivyo nayeย  ataingia tu” Alisema Desmond huku akijuwa fika kuwa Luciaย  alikuwa ameuawa.ย 

    Muda ulienda bila Lucia kutokea eneo hilo, shughuliย  ilifanyika kwa bashasha zote. Desmond akawa mchumba rasmi waย  Noela, ilikuwa ni siku yenye furaha sana Kwa Noela na Mamaย  yake sababu jambo hilo lilisubiriwa kwa muda mrefu, basiย  zikapigwa picha za kutosha, Watu walikula hadi kusaza, Furahaย  ilitawala usiku huo. Baada ya kuisha tukio hilo, Desmondย  aliaga ili aondoke lakini alimuona Mtu mmoja aliyemfananishaย  akiwa ameketi mahali anazungumza na Mwanume mmoja.ย 

    Desmond alimtazama sana Mwanaume huyo huku akijiulizaย  alimuona wapi, akakumbuka alimuona siku ambayo aliliona gariย  lake likiwa maegesho ofisini wakati gari hilo alilitumbukizaย  baharini, alikuwa hamfahamu Mtu huyo na wala hakumuarika, ilaย  hakutaka kulipa uzito jambo hilo maana kama hakuarikwa naย  yeye basi atakuwa amearikwa na Mpenzi wake Noela.

    Akaendelea kuaga Watu kwa ajili ya kuondoka eneo hilo, ghaflaย  aliguswa begani na Msichana mmoja ambaye alikuwa akihudumiaย  Watu vinywaji, msichana huyo alimpa Desmond ujumbe waย  karatsi, Desmond akamuuliza Msichana huyoย 

    “Ametoa Nani?”ย 

    “Mkaka yule…” Msichana huyo alipoonyesha alipokaa Mtuย  aliyetoa ujumbe huo hakuwepo hapo, akaanza kumtafuta kwaย  macho lakini hakumuona ila Desmond alimuona mwanzo Mtuย  aliyekaa hapo, alikuwa ni yule Mwanaume aliyemuona ofisiniย  kwakeย 

    “Haya sawa asante” Alisema Desmond, kisha alisogea pembeniย  akafungua ujumbe huo akakuta maneno yaliyosomekaย 

    “LUCIA AMEKUFA LAKINI SIYO MWISHO, TUKUTANE JUMATATU KATIKAย  HOTELI YA HAVANA SAA 7 MCHANA!! CHUMBA NAMBA 43, NINAย  USHAHIDI WA ULIYOYAFANYA”ย 

    Desmond alishtuka sana, alimtafuta Mwanaume huyo bilaย  mafanikio, alitoka nje kabisa lakini hakufanikiwa hataย  kumuona Mtu huyo alijikuta akichoka mwili na akili, Mtu waย  tatu bado aliendelea kumtesa lakini bahati nzuri aliifahamuย  sura yake, alimuita Mwanasheria Joel kisha waliondoka hapoย  kwa ajili ya kujadili ni jinsi gani watamkabili Mtu huyo.ย 

    Noela alilala fofo baada ya kunywa pombe vya kutosha, aliamkaย  siku iliyofuata ambayo ilikuwa ni Jumatatu, akili yakeย  ikamwambia kuwa siku hiyo hawezi kufanya chochote zaidi yaย  kupumzika tu, lakini baadaye alifikiria kuhusu Lucia,ย  alijaribu tena kupiga simu ya Lucia lakini haikuita kabisa.ย 

    Alianza kupata mashaka pengine amepata tatizo ila hakuwa naย  Mtu wa kumuuliza, aliwasha Tv ili aangalie habari za hapa naย  pale, ndipo alipokutana na taarifa ya kifo cha nesi Luciaย  aliyeuawa kwa kunyongwa shingo hadi kufa, Roho ilimripukaย  sana Noelaย 

    Alishtuka sana kusikia taarifa hiyo na kibaya zaidi ni kuwaย  aliacha Mama ambaye ni mgonjwa sana, mara moja Noela alivaliaย  nguo zake akamuaga Mama yake kisha akaelekea mahali ambapoย  maiti ya Lucia ilikuwa imehifadhiwa, ni katika ile ileย  Hospitali ambayo Lucia alikuwa akifanyia kazi, alikutana naย  Daktari Mkuu wa hiyo Hospitali akawa anazungumza naye.ย 

    Mkuu huyo alimuelezea Lucia kwa jinsi alivyoweza mbele yaย  Noela, kikubwa zaidi Noela alikufa akiwa masikini, piliย  alikuwa na ndoto za kuja kuwa Nesi bora zaidi katikaย Hospitali hiyo na tatu aliacha Mgonjwa aliye katika haliย  mbaya sana.ย 

    “Mgonjwa aliye katika hali mbaya?” Alihoji Noelaย 

    “Ndiyo! alikuwa akimuhudumia kwa kipindi chote, alikuwa naย  ndoto ya kumuona Mgonjwa huyo anakuwa mzima tena lakini ndotoย  ya Lucia imezimika ghafla kama Mshumaa” Alieleza kisha choziย  lilimtoka akalifuta, Noela alipelekwa hadi kwenye chumbaย  ambacho Mgonjwa wa Lucia alikuwa amelazwa, hakuwa mwingineย  bali ni Mandy Mke wa Desmond.ย 

    Alimtazama Mandy kisha alisemaย 

    “Hakika Lucia amekufa na ndoto zake” Alisema Noela hukuย  akifuta chozi lake, alikumbuka mara ya mwisho alipewa kazi naย  Lucia, haraka alitoka wodini ili alekee nyumbani kwakeย  kuangalia zile nyaraka alizopewa na Lucia.ย 

    Wakati anatoka Desmond alikuwa akiingia Hospitalini hapo,ย  wawili hao hawakuonana. Haraka akiwa na gari yake Noelaย  alifika nyumbani kwao, alimkuta Mama yake akiwa ameketiย  sebleni, alitaka kumpita ila Mama yake alisemaย 

    “Amekuja Mtu uliyemuagiza amechukua sanduku” Alisema Mamaย  Noela na kumfanya Noela ashangae ni Nani alikuja kuchukuaย  Sandukuย 

    “Mama unasemaje, sanduku la chumbani kwangu?”ย 

    “Ndiyo kwani hukumtuma Mwanaume mweusi hivi?” aliuliza Mamaย  Noelaย 

    “Mamaaaaaaa!!” aligumia Noela kisha alielekea chumbani kwakeย  haraka, kweli Sanduku liliondolewa chumbani hapoย 

    Haraka alirudi Sebleni akamuuliza Mama yakeย 

    “Mtu huyo amekuja saa ngapi?”ย 

    “muda siyo mrefu sana alikuja na gari akasema umemuagiza naย  alikuwa akijuwa hadi lilipokaa nikamiami, ina maana hukumtunaย  Mtu?” aliuliza Mama Noela kwa mshangao, Noela hakujibuย  alitoka akapanda gari kisha akaanza kumtafuta huyo Mtu,ย  alipita mitaa mbali mbali bila mafanikio yoyote yale hadiย  alichoka.ย 

    Aliamuwa kurudi nyumbani, ndipo alipogundua huwenda kulikuwaย  na jambo zito lilifanya Lucia auawe, akafikiria atapata vipiย  kujuwa alichokuwa anatakiwa kufanya.

    Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA TISA

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya kuendelea kutuma SIMULIZI Mpya Na Kuipost HAPA Kwa kumtumia Chochote kupitia

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love &Pain Love & Painย 

    Love & Pain

    19 Comments

    1. Veronica on November 20, 2024 2:43 pm

      Jamani

      Reply
    2. Egibeth on November 20, 2024 4:01 pm

      Duh ubaya ubwelaa

      Reply
    3. Luse twaxie on November 20, 2024 4:56 pm

      Mm naumiaaa sana ..unatoaje kitu akat hujaambiwaaa

      Reply
      • Sharo love malkx ๐Ÿ’– on November 20, 2024 5:27 pm

        Alafu na wewe ni luciy๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†

        Reply
    4. G shirima on November 20, 2024 4:57 pm

      Lucia jamni nlijua ndo star wa move

      Reply
    5. Sharo love malkx ๐Ÿ’– on November 20, 2024 5:26 pm

      Qmanina
      Ina uma kishenzi๐Ÿฅฒ๐Ÿฅฒ๐Ÿค”

      Reply
    6. Rachel on November 20, 2024 6:46 pm

      Nimeumia mno

      Reply
      • Hamisa Joseph on November 24, 2024 1:34 pm

        Bad news lucia hayupo

        Reply
    7. Fawziya Hassan on November 20, 2024 6:59 pm

      Doh๐Ÿ˜ฅ
      Hadi nimechoka
      Jamani Lucia amenyongwa
      Inauma sana

      Reply
    8. Hamza Abdallah Mwalyawa on November 21, 2024 1:42 am

      Lucia asinge kufa hadithi ingekuwa fupi!!!! Masikini Mandy—-๐Ÿ˜ก

      Reply
    9. Sir yowas on November 21, 2024 8:39 am

      Hii Dunia Fanya yanayokuhusu, mengine waachie. Lucia umekufa sasa

      Reply
    10. Robbiey on November 21, 2024 9:15 am

      kinachoniuma zaid admin anatoa tu si akitaka hii Riwaya tunaomba kila siku tupate au tupe Ratiba nimeisubir sana na nimeumia sana kuona imetoka kipande kimoja

      Reply
      • Angel on November 21, 2024 10:36 am

        Yeah
        ..ni kwel hata m nliisubir sana,,,had nkachoka yan…

        Reply
      • Mhariri on November 21, 2024 10:37 am

        Mambo vipi Mwana Kijiweni? Kukiwa na mechi mambo yanakua mengi

        Reply
        • Robbiey on November 21, 2024 1:56 pm

          Sisi tunaomba mbili zetu zilizobaki tusije kukushtaki watu tunatembea na stress utasema sisi ndo Noela ๐Ÿ˜ญ

          Reply
    11. Hamic on November 21, 2024 10:09 am

      Zaidi ya hatar

      Reply
      • Pangkid on November 21, 2024 11:09 am

        SIMULIZI Nani atalifuta chozi langu

        https://whatsapp.com/channel/0029VanxLVYJ93wbHawAAh3H/720

        Reply
    12. Rau B on November 24, 2024 9:04 pm

      https://maishakitaaonlinetz.blogspot.com/2024/11/simulizisiri-za-giza-sehemu-ya-pili.html

      Gonga emoj MOJA kama ukotayari kwa sehemu ya Tatu ya Simulizi hii.

      Reply
    13. ๐Ÿ“ โœ‰๏ธ New Message: 1.65 Bitcoin from exchange. Claim funds => https://graph.org/Get-your-BTC-09-04?hs=387b43439b242a9369bdc806bf02555a& ๐Ÿ“ on October 9, 2025 6:23 pm

      ff8mpa

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi October 1, 2025

    In the name of LOVE – 12

    Ilipoishia sehemu ya Kumi na moja ya In the name of LOVE Moyo Wangu na…

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    In the name of LOVE – 09

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.