Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 12

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Love & Pain Sehemu Ya Kumi (10)
    Hadithi

    Love & Pain Sehemu Ya Kumi (10)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaNovember 22, 2024Updated:November 25, 202415 Comments10 Mins Read7K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Love & Pain
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Joshua naomba tuonane kwenye mgahawa muda huu” Alisema Noelaย  kisha alikata simu, Desmond alishusha pumzi zake baada yaย  kujiridhisha kuwa Noela hajagundua lolote maana kamaย  angedungua asingemuita jina la Joshua bali angemuita Desmond,ย  kumbe Noela alishajuwa kila kitu, alikuwa katika upeleleziย  wake binafsiย 

    Desmond alipotoka pale Hotelini moja kwa moja alienda kuonanaย  na Mchumba wake Noela kama alivyoambiwa, alimkuta Noela akiwaย  amejawa na tabasamu na bashasha kitu ambacho kilimfanyaย  Desmond azidi kujiamini kuwa Noela hajafahamu lolote lile,ย  waliagiza chakula huku Noela akizidi kumsoma Desmond, akiliย  ya Desmond haikutulia kabisa sababu alihitaji kufahamu kamaย  Joel alikuwa amefanikiwa kupeleka Hundi ile kwa Mtu wa Tatu. Endelea

    SEHEMU YA KUMIย 

    “Nimetoka Hospitali, unamkumbuka yule rafiki yangu uliyewahiย  kuniona naye hapa?” aliuliza Noela makusudi ili kuzidiย  kumsoma Desmondย 

    “Eeeh nakumbuka, anaumwa?” alihoji Desmondย 

    “Hapana amekutwa ameuawa huko porini, inasikitisha mno alafuย  kaacha Mama anayeumwa sana” Alisema Noela huku akiwa makiniย  sana na jicho lake la uchunguzi, Desmond alishtuka mno hukuย  macho yake yakiwa yamemtoka pima kama Mjusi aliyebanwa naย  mlangoย 

    “Ameuawa…..Nani aliyemuuwa?” alihoji Desmond akiwa katikaย  hali ya kuchanganikiwa sana, Noela akagundua kuwa alichokuwaย  ametumiwa na marehemu Lucia kilikuwa na ukweli mtupuย 

    “Haijajulikana, polisi wanafanya uchunguzi. Inasemekana piaย  ameacha mgonjwa ambaye yupo mahututi na huyo mgonjwaย  inawezekana kuwa chanzo cha kifo cha Lucia” Alisema Noelaย  huku jicho lake likiongeza umakini wa kumtambua Desmondย 

    “Mgonjwa!! aaah Noela, naomba tuachane na hizo stori,ย  tumekuja hapa kula Mpenzi” Alisema Desmond kisha alimwambiaย  Noelaย 

    “Naenda chooni mara moja” Desmond alinyanyuka akaelekeaย  Chooni bila kujuwa kuwa Noela alikuwa tayari amegundua kuwaย  yeye ni Muuuwajiย 

    Japo moyo ulimuuma sana Noela ila kilichompata Lucia alijionaย  ana kila sababu ya kuleta haki, Desmond alipofika chooniย  alijiinamia kwenye sinki la kunawia maji akiwa amechoka sana,ย  alianza kuhisi ugumu mkubwa sana kwenye Maisha yake,ย  alimpigia simu Joel akamuuliza kama amekutana na huyo Mtu waย  Tatu.ย 

    Joel akiwa ndani ya gari hilo aliloelekezwa alipokea simu,ย  alionekana kuzungumza kwa kutulia sana huku pembeni yakeย  kukiwa na mwanaume mmojaย 

    “Nimeshampatia” Alisema Joelย 

    “Haya basi tukutane mara moja pale tunapokutanaga….naonaย  mambo magumu, Kifo cha Lucia kimekuja kuharibu kila kitu”ย  Alisema Desmond, baada ya simu ya Desmond kukatwa Joelย  alimgeukia Mwanaume ambaye yupo ndani ya hiyo gani akamwambiaย 

    “Ngoma imeanza kuchezwa, Hii Hundi hakikisha unachukua pesaย  na kuziweka kwenye akaunti nyeusi, ni lazima tumtumie Desmondย kuvuna pesa alafu kila kitu kitamuangukia mwenyewe” Aliagizaย  Mwanasheria Joel, kumbe mwanasheria Joel ambaye niย  mwanasheria wa Mandy ndiye Mtu wa tatu ambaye alikuwaย  akijifanya kuzunguka kwenye suala lililojificha ili apateย  pesa kutoka kwa Desmond kwa kujifanya anajuwa siri zaย  Desmond, Mwanaume aliye pembeni yake ndiye yule ambayeย  Desmond alikuwa akimtilia shaka na ndiye aliyekuwa akifanyaย  michezo mingi michafu na ndiye aliyelitoa lile gari kuleย  Baharini kisha akaliweka gari lingine kisha akawapigia simuย  polisiย 

    Basi, Baada ya kumaliza kuongea na Joel akifikiria ni Mtuย  mzuri anayeshirikiana naye alirudi kwa Noela ambayeย  alijifanya yupo bize akipata chakula, angalau baada ya kutokaย  Chooni alionekana kuwa sawa japo Noela alikuwa ameshamgunduaย  muda mrefu, walipata chakula ndipo Noela alipomchomekeaย  Desmondย 

    “Nasikia Mgonjwa wa Marehemu Lucia ameamka leo, ingekuwaย  faraja sana kwa Lucia kumuona mgonjwa aliyemhudumia kwa mudaย  mrefu akiamka” Alisema kwa mtego Mkubwa sana na Desmondย  akaingia mtegoni, alishtuka akaulizaย 

    “Unamaanisha Mandy?” alihoji akiwa ameamka kutoka kitini,ย  ndipo sasa akawa amemdhihirishia wazi Noela kuwa ana Mke piaย  ni Muuwajiย 

    Noela naye akaamka akijifanya kushangaaย 

    “Heee kumbe unamjuwa?” Alihoji Noelaย 

    “Hapana….Hapana simjui, Noela tutaonana baadaye” Alisemaย  Desmond kisha aliondoka mbio kuelelekea Hospitalini bilaย  kujuwa kuwa alikuwa ametegwa, Haraka Noela alimfuata kwaย  nyuma kisha naye aliingia kwenye gari yake akawa anamfuatiliaย  Desmond kwa nyuma, Safari hii ilifika hadi kwenye Hospitaliย  aliyolazwa Mandyย 

    Akiwa amepaki gari eneo lingine la Hospitali tofauti naย  alipopaki Desmond, Noela alipokea ujumbe kuwa Mgonjwa Mandyย  amerudisha fahamu, huu ulikuwa ni ujumbe kutoka kwa Daktariย  Mkuu wa Hospitali sababu alimuachia maagizo kuwa akiamkaย  Mandy apewe taarifa na pia alipewa agizo moja kubwa sana,ย  Noela akakumbuka alichomwambia Daktariย 

    Alimwambia kuwa anafanya uchunguzi wa kifo cha Lucia naย  huwenda mgonjwa huyo akawa ndiyo chanzo cha kifo cha Luciaย  hivyo atakapoamka pengine kuna siri anaifahamu hivyo kitu chaย  kwanza ahakikishe anamuweka sawa kiakili ili Desmondย  asishtuke mapema hadi pale watakapopata ushahidi wa kutosha

    Akiwa mbio mbio, Desmond alifunga breki miguuni mwa Daktariย  Mkuu aliyekuwa akitoka wodini kwa Mandyย 

    “Dokta nimesikia Mke wangu ameamka” Alisema Desmond akiwaย  katika hali ya haraka na hofu mnoย 

    “Ndiyo Mkeo ameamka ila bado hana nguvu, unaweza ukamuona ilaย  usimkumbushe chochote” Alisema Dokta, Basi Desmond aliufunguaย  mlango wa wodi hiyo, kweli alimuona Mandy akiangaza huku naย  kule kama Mtu aliyekuwa akijiuliza yupo wapiย 

    Hofu ilimjaa sana Desmond kisha alimsogelea Mandy taratibuย  huku akiwa mwenye maswali mazito sana ya kuwa Mandy amemjuwaย  Desmond kuwa ni Muuwaji wa Mama ake, Mandy alipomuona Desmondย  alionekana wazi kuwa na maumivu makali moyoni, alimtazamaย  Desmond huku chozi likimbubujika, yule Daktari Mkuu alisimamaย  mlangoni akichungulia tuย 

    Mandy alikumbuka siku ya tukio la yeye kupigizwa ukutani naย  Desmond, siku hiyo ilikuwa hivi, aliiyona cheni ya Mama yakeย  kwenye koti la suti la Desmond, cheni ambayo Desmond aliivuaย  kwenye shingo ya Mama Mandy baada ya kumuuwa kisha akaiwekaย  kwenye koti lake, Mandy alipoiyona ile cheni ndipoย  alipogundua kuwa Desmond ni Muuwaji, wakati anapiga Simuย  Desmond alitokea ndipo vurugu za kufukuzana zilipoanzaย 

    Tuendelee, Basi Desmond alisogea na kumshika mikono Mandyย  akamwambiaย 

    “Umeamka Mama?” alihoji Desmondย 

    “Wewe ni Nani?” aliuliza Mandy, Desmond alishtuka sana kishaย  akajiuliza ina maana Mandy amepoteza kumbukumbu zake,ย  alijikuta akitabasamu maana kama amepoteza kumbukumbuย  hatoweza kumtaja kama Muuwaji wa Mama yake.ย 

    “Pole kwa maumivu sawa Eeh!! Mimi ni Mume wako Desmond”ย  Desmond alijitambulisha pale, Daktari alielekea moja kwa mojaย  kwenye maegesho ya Magari akamwambia Noela kuwa Mandyย  amefanya kama alivyoagizwa yaani kujifanya amepotezaย  kumbukumbu.ย 

    “Safi sana, Desmond ni mchumba wangu na hii pete amenivishaย  jana tu” Alisema Noela kisha aliivua pete hiyoย 

    “Sistahili kuwa na pete yake sababu ni Mume wa Mtu piaย  Muuwaji, kwakuwa ameshajulikana ndiye Muuwaji basi kaziย  iliyobakia niachie Mimi”ย 

    “Sawa!!” Noela aliondoka Hospitalini hapo.

    Desmond alibakia Hospitali kwa ajili ya kuangalia kama kunaย  chochote Mandy anaweza akakumbuka, hii ilimfanya yule Daktariย  ashindwe kumpa taarifa muhimu Noela.ย 

    Jioni ilipoingia ilimkuta Noela akiwa nyumbani kwao akiwaย  kwenye tafakari nzito kuhusu Desmond ambaye alimdanganya jinaย  kama Joshua, alikumbuka vingi ikiwemo walipotoka, alijikutaย  akiangusha chozi lenye maumivu makali sana, mapenzi aliyompaย  Desmond yalikuwa ya dhati sana kwa kipindi chote, kugunduaย  kuwa Desmond alikuwa Muuwaji na Muongo kulimliza sana Noela.ย 

    Alijikuta kwenye wakati mgumu sana, ndiyo alimpenda sanaย  Desmond hadi kufikia hatua ya kuvishwa pete lakini angefanyaย  nini wakati Mwanaume huyo alikuwa Muongo na Muuwaji.ย 

    Jioni hiyo alitoka akarudi kule Hospitali, Desmond alikuwaย  wodini kwa kipindi chote akiwa na mawazo kuwa huwenda Mkeย  wake atarudisha kumbukumbu muda wowote ule, ili kumtoa paleย  Noela alimtumia meseji Desmond akimwambiaย 

    “Mpenzi naelekea kwenye pori ambalo Lucia aliuawa, kunaย  taarifa kuwa alipotoka nyumbani kwao alitoka na kitabu chenyeย  siri pengine nacho kilikuwa ni sababu ya kifo chake,ย  inasemekana kilipotea porini” Alipotuma meseji hiyo alijuwaย  wazi kuwa Desmond ataenda huko porini ili kuhakikishaย  alichoambiwa, kweli muda huo huo Desmond alikurupuka kutokaย  pale wodini akaingia kwenye gari kisha akatoka.ย 

    Lakini wakati anatoka Desmond, yule Mwanaume anayetumwa kaziย  na Mwanasheria Joel alikuwa pale ndani akamuona Desmondย  akitoka kisha Noela aliingia wodini, yule Mwanaume alimpigiaย  simu Joel haraka sana akamwambia alichokiona, basi harakaย  Joel alimpigia simu Desmond na kumueleza kuwa kulikuwa naย  mchezo uliokuwa ukichezwa hapo na kwamba mpenzi wake Noelaย  alikuwa hapo Hospitalini na baada ya yeye kutoka Mpenzi wakeย  huyo aliingia wodini kwa Mke wake Mandy.ย 

    Desmond alisitisha safari ya kwenda eneo ambalo Lucia aliuawaย  baada ya kuambiwa kuwa kuna mchezo mchafu Hospitalini, harakaย  aligeuza gari akarudi kule Hospitalini, akiwa hoi haiย  aliingia wodini na kumkuta Mandy akiwa amelala huku chumbaย  hicho kikiwa kimya sana, Desmond alishangaa sana wakatiย  aliambiwa na Joel kuwa mpenzi wake alikuwa hapo, akaamuwaย  kumpigia simu ili ajihakikishie alichoambiwa, simuย  ilipopokelewa ilionesha wazi kuwa Noela alikuwa barabaraniย  hivyo alishindwa kuthibitisha alichoambiwa, alimpigia simuย  Joel na kumwambia alichokiona lakini Joel alimtaka Desmondย  kuwa makini sana maana Mpenzi wake alikuwa hapo Hospitaliniย  na huwenda anafahamu kuhusu Mandy.

    Alienda kukutana na Mwanasheria Joel ambaye alikuwaย  akimchezea Mchezo mchafu, Joel alimuonesha video Desmondย  iliyomuonesha Noela akiingia na kutoka pale wodini, ndipoย  alipopata picha kamili kuwa Noela alikuwa amefanikiwaย  kumfahamu, Joel alimuulizaย 

    “Huyo ameshajuwa siri kuwa wewe ni Muuwaji, kibaya zaidi huyoย  ni mpenzi wako alafu mpelelezi utafanya nini?” Desmond alikaaย  kimya baada ya sekunde kadhaa akamwambiaย 

    “Nitajuwa cha kufanya” Desmond alitoka kuonana na Joel,ย  alionekana kuwa mwenye mawazo sana ya nini afanye, alimpigiaย  simu Noela akamuuliza kama alifanikiwa kukipata hicho kitabu,ย  alifanya hivyo makusudi ili kumfanya Noela afahamu kuwa badoย  Desmond hajajuwa chochote.ย 

    Noela alimwambia kuwa hawakufanikiwa kukipata kitabu ilaย  uchunguzi bado unaendelea, Desmond alipata wazo la harakaย  nalo ni kuondoa uhai wa Noela maana Mke wake hakumbukiย  chochote hivyo kwa vyovyote Mtu anayeweza kusema ukweli niย  Noela.ย 

    Alimtunia ujumbe wakutane nyumbani kwake usiku wa siku hiyo,ย  baada ya kuupata ujumbe Noela aliwataarifu polisi aliokuwaย  akifanya nao kazi maana alihisi huwenda Desmond alishafahamuย  kuwa anaijuwa ile siri ya Mauwaji. Usiku ulipofika Noelaย  alienda nyumbani kwa Desmond, alimkuta akiwa ameketi mahaliย  anapata biaย 

    Noela aliketi naye akapata chupa ya Bia bila hata kumsemeshaย  Desmond, waligida kidogo kisha Desmond alimuuliza Noelaย 

    “Umemuaga Mama?”ย 

    “Ndiyo!!” Alijibu Noelaย 

    “Siku moja ya uchumba wetu umeshavua pete ya uchumba” Alisemaย  Desmond ndipo Noela aliposhtuka sasa kuwa Desmond alikuwaย  ameshafahamu.ย 

    “Nafikiri ni kitu cha kawaida, inakuwaje kwa Mtu akawa naย  majina mawili, la uhalisia analificha na kutumia jina feki?”ย  Alisema Noela, hakukuwa na siri tena sababu kila jamboย  lilikuwa waziย 

    “Noela umekuwa kikwazo kwangu, ili niwe salama ni lazimaย  nikutangulize” Alisema Desmond kisha alitoa bastola akawaย  anaifutafuta

    “Kwa mpelelezi ambaye amefanya kazi nyingi hawezi kuogopaย  kufanya kazi hata kama ni hatari kiasi gani au inamgusaย  ampendaye, Desmond….kumbe una Mke tena ni Mke ambayeย  ulitaka kuutoa uhai wake kisa pesa, unakumbuka kuhusu Mamaย  Mandy?” aliuliza Noela, Desmond alijawa na hasiraย  akamnyooshea Noelaย 

    “Kabla hujaniuwa Desmond, nataka nikwambie kitu kimoja. Pesaย  haiwezi kukupa kila kitu katika Maisha yako, ila Maishaย  yanaweza kukupa kila kitu ikiwemo na pesa, waliochagua kuishiย  walifanikiwa lakini wewe ulichagua pesa ili uishi”ย 

    “Ishia hapo hapo Noela” Alisema Desmond kisha alifyatuaย  risasi iliyowashtua polisi aliokuja nao Noelaย 

    Haraka waliingia na kumkuta Noela akiwa chini anauguliaย  maumivu ya bega, bastola ikawa udhibiti kwa Desmond,ย  alikamatwa na wale polisi. Taarifa ya kukamatwa kwa Desmondย  ilimfikia Joel, akapata wazo la kuikimbia Nchi maanaย  alishajuwa kuwa atatajwa na kukamatwa, Naam!! alitajwa naย  Desmond, Joel alienda kukamatwa Uwanja wa ndege….ย 

    Taarifa ya kukamatwa kwa Joel na Desmond ilimfanya Mandy alieย  kwa uchungu mkubwa, baada ya kupona kwa Noela, Desmond naย  Joel walifikishwa Mahakamani kwa makosa ya Mauwaji, Mandyย  alisimama kama Shahidi namba moja, Hatimaye Desmond na Joelย  walifungwa kifungo cha Maisha jela, Mandy alimshukuru sanaย  Noela kwa msaada huo hadi kukamatwa kwa Wauwajiย 

    Noela aliishia maisha ya majuto sana sababu aliamini kamaย  angelifanyia kazi mapema bahasha aliyopewa na Lucia basiย  rafiki yake huyo asingeliuaawaย 

    MWISHO

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya kuendelea kutuma SIMULIZI Mpya Na Kuipost HAPA Kwa kumtumia Chochote kupitia

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love &Pain Love & Painย 

    ย ย 

    Love & Pain

    15 Comments

    1. Fawziya Hassan on November 22, 2024 3:17 pm

      Mapenzi na Maumivu โŒโŽ
      Mapenzi ni Maumivu โœ…
      Na Pesa sio kitu
      Utu ndio kila kitu.
      Simulizi ya Maajabu Nzuri yenye mafunzo na mazingatio katik maisha yetu ya kila siku hususan maisha yetu ya saiv.
      Asanteni.
      Mtunzi na Adminโค๏ธ

      Reply
    2. Hamis on November 22, 2024 3:44 pm

      Asant adimin

      Reply
    3. Sharo love malkx ๐Ÿ’– on November 22, 2024 4:36 pm

      Mapenzi na pesa
      Uki ambatanisha na jua
      Oyaa oyaa oyaa
      ๐Ÿƒ๐Ÿƒ๐Ÿƒ๐Ÿƒ๐Ÿƒ

      Reply
    4. Ander on November 22, 2024 5:25 pm

      ๐Ÿ™๐Ÿ™

      Reply
      • Junior Mtata on November 25, 2024 3:00 pm

        Mhmmmmmmmm admin punguza uvivu

        Reply
    5. Bertila on November 22, 2024 6:38 pm

      Imeisha ghafula ๐Ÿฅบ

      Reply
    6. G shirima on November 22, 2024 8:30 pm

      Upendo na maumivu
      .pesa SI Kila kitu. ??
      .Kila kitu ni pesa??
      ๐Ÿฅบ๐Ÿฅบ๐Ÿฅบ๐Ÿฅบ

      Reply
    7. Tina on November 22, 2024 9:28 pm

      Duh

      Reply
    8. Robbiey on November 22, 2024 11:43 pm

      apo safi bora imeisha imenisubirisha sana hii admin siku nyingine tuwekee ratiba mambo ya mpira yakiwa mengi

      Reply
    9. Hamza Abdallah Mwalyawa on November 23, 2024 7:29 am

      Hakika pesa sio kila kitu bali maisha ndiyo kila kitu. Naam nimeyaona maumivu ya mapenzi kwa Noela……… Lucia โ˜ฎ๏ธ shujaa wetu!!!!!!

      Reply
    10. Verena on November 23, 2024 7:58 am

      Maumivu maumivu ya mapenzi ๐Ÿฅน๐Ÿฅน๐Ÿฅน

      Reply
    11. DAUD DEOGRATIAS on November 23, 2024 6:20 pm

      Aisee pesa inanguvu kwenye mapenzi tu lkn siyo kwenye sheria

      Reply
    12. Mwajuma on November 25, 2024 10:57 am

      Mapenzi yanaumiza jamani

      Reply
    13. ๐Ÿ” Alert: Transfer of 0.85 Bitcoin pending. Verify Today => https://graph.org/Get-your-BTC-09-04?hs=0c8db7fd76368ffab40a66c4476bc02b& ๐Ÿ” on September 23, 2025 6:54 pm

      9ooa0q

      Reply
    14. โœ‰ ๐Ÿ”œ Instant Transfer: 0.35 BTC sent. Finalize now >> https://graph.org/Get-your-BTC-09-04?hs=0c8db7fd76368ffab40a66c4476bc02b& โœ‰ on October 19, 2025 12:54 pm

      u6f037

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi October 1, 2025

    In the name of LOVE – 12

    Ilipoishia sehemu ya Kumi na moja ya In the name of LOVE Moyo Wangu na…

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    In the name of LOVE – 09

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.