Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Tatu) KOTI JEUSI – 03
    Hadithi

    KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Tatu) KOTI JEUSI – 03

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaMay 1, 2024Updated:June 1, 202418 Comments5 Mins Read7K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Riwaya Ya Koti Jeusi
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia jana ” Pili alifikia maamuzi ya kukubali kua Muuaji aliyapanga vizuri Mauaji hayo kwa maana aliweza 

    kufuta picha kadhaa kwenye Mboni ya Mzee Yusuf na kuacha moja ambayo haitoshi kutoa taswira halisi kua ni nani Muuaji? “

    Tuendelee sasa 

    SEHEMU YA TATU (03)

    Asubuhi ya siku ya Tatu baada ya kifo cha Mfanyabiashara Mzee Yusuf ambaye kifo chake kilianza kumsumbua Mpelelezi Daudi Mbaga, Ndani ya kijumba kidogo chenye hadhi kubwa huko nje kidogo ya Jiji la Dar-es-salaam, alionekana Mama Mmoja Mtu mzima aliyekua amekaa kwenye sofa akiitazama picha moja.

    Mama huyo alikua amevalia miwani ya macho akiwa amejitanda vizuri kwa mtandio ulioendana na Baibui yake nyeusi, mlangoni akatokea Msichana mmoja mzuri, mwembamba, mweusi kidogo aliyebana vizuri nywele zake, hakua mrefu wala mfupi. Alikua amevalia Baibui nyeusi pia kama Mama huyo, alisogea kisha akamwambia Mama huyo

    “Twende Mama” alisema akiwa anajiweka vizuri, kisha alichezea simu yake na kupiga mahali

    “Beka tupo tayari” alipomaliza kuongea na simu alimrudia Mama yake ambaye alikua bize kuitazama 

    picha hiyo, picha hiyo ilikua ikimwonesha Mzee Yusuf

    “Mama, Beka anakuja kutukuchukua. Ni vyena tukawahi” alisema Msichana huyo.

    “Martha, kifo cha huyu Yusuf kimeniuhuzunisha sana. Natamani polisi wamjuwe kwa haraka Mtu  aliyesababisha kifo chake.”

    “Ni mipango ya Mungu Mama, kila jambo lina wakati sahihi, ukifika wakati wa kumpata Muuwaji basi Muuwaji atakamatwa tu” alisema Martha.

    Basi, Martha na Mama yake waliokua wakiishi Bunju walitoka nje ya nyumba hiyo na kukuta Tax ikiwa imefika, wakapanda Tax na kuanza safari yao. 

    Safari yao iliishia nje ya Msikiti wa Maamur Upanga ambako ibada ya Mazishi ya Mzee Yusuf ilikua ikifanyika, Daudi Mbaga aliruhusu Maiti ya Mzee Yusuf iweze kuzikwa baada ya kukamilisha taratibu za kipelelezi, majira ya saa saba Mchana Magari yaliekea Makaburi ya Kinondoni kisha mazishi ya Mzee Yusuf yalifanyika. Martha na Mama yake waliongozana na familia ya wafiwa kurudi nyumbani kwa Mzee Yusuf.

    Ndugu wachache walibakia kuomboleza, Martha alimfuata Sofia na kumpoza machungu hayo ya 

    kufiwa, walikua wakifahamiana sababu familia zao zilikua na urafiki yaani Family Friend.

    “Inauma Martha, Baba alikua muhimu sana na nguzo muhimu ya Familia hii. Kifo chake ni pengo na mzigo mzito kwetu, hatujui hata tunaanzaje bila yeye” alisema Sofia akiwa ameketi kwenye kiti, 

    Martha alimuonea huruma sana Sofia

    “Najua inaumiza kiasi gani lakini kua jasiri kwa ajili ya Binti yako Adela”

    “Asante sana Mdogo wangu Martha, kiukweli napaswa kujikaza sana” Mama yake Martha naye 

    alikua akizungumza na baadhi ya ndugu wa Mzee Yusuf ambao walikua katika Majonzi mazito, muda huo huo Salma aliingia akitokea Uingereza. 

    Aliangusha kilio ambacho kwa upande wa Sofia alikiona ni kilio cha kinafiki sana, hakujali bali aliingia ndani na kuwaacha watu wengine wakimpa pole Salma. Kabla Salma hajaondoka kuelekea Uingereza palikua na mgogoro mdogo kati yake na Mzee Yusuf, alipofika ndani Sofia alinyanyua simuna kumpigia Mpelelezi Daudi Mbaga kua Salma amerejea na wanapaswa kumhoji ili aseme mgogoro wao ulikua unahusu nini na huenda Mgogoro huo ukawa ndiyo chanzo cha Mauwaji hayo yaliyojaa Utata.

    Mara moja polisi walifika hapo wakiwa wametumwa na Daudi Mbaga, walimtia nguvuni Salma hali iliyozua taharuki kwa wengi.

    “Jamani kuna nini?” aliuliza Hamza ambaye ni Kaka wa Sofia, Mtoto wa kwanza wa Mzee Yusuf.

    “Tumepigiwa simu kuwa kabla ya kifo cha Mzee Yusuf palikua na ugomvi baina ya Salma na Mzee Yusuf hivyo tunamchukua ili tukamhoji, atarudi” alisema mmoja wa askari hao waliotumwa kumkamata Salma.

    Macho ya Salma aliyatupa Mlangoni akamwona Sofia akiwa katika pozi ambalo lilimwonesha wazi kuwa aliyepiga simu hiyo alikua ni Yeye, akamsogelea na kumwambia

    “You will pay for this ( Utalipia kwa hili)” alisema kwa hasira kiasi kwamba kila aliyeko hapo 

    alitambua msuguano mzito uliopo baina ya Sofia na Mama yake Mdogo Salma.

    Aliingizwa kwenye ndinga ya Polisi na kupelekwa moja kwa moja Ostabey, alikutana kwa mara ya  kwanza na mpelelezi Daudi Mbaga

    “Unaitwa Salma si ndiyo?” aliuliza Daudi wakiwa chumba cha Mahojiano

    “Ndiyo”

    “Inasemekana kua wewe na Mzee Yusuf Mliingia kwenye ugomvi mdogo siku chache kabla ya kifo chake, ukaondoka kuelekea Uingereza” alisema Daudi akionekana kua Mtu makini sana

    “Ndiyo” alijibu Salma

    “Kwanini mligombana?”

    “Alihisi nina Mwanaume mwingine nje ya Nchi, hakutaka niende Uingereza. Nami sikua tayari kwa hilo”

    “Ni kweli ulikua na Mwanaume huko na ulikua ukichukua mali za Mzee Yusuf taratibu?”

    “Hapana, sijawahi kumsaliti Mume wangu hata mara moja”

    “Kifo chake kimegubikwa na fumbo zito la Nani amemuuwa, nikisema unahusika ninaweza kua nipo 

    sawa?”

    “Kamwe siwezi kutenda unyama kwa Mume wangu, hata kama angelikua Mtu baki nisingeliweza kukatisha Maisha yake. Mzee Yusuf alisaidia Maisha yangu nikiwa nimepoteza dira ya Maisha, akanisaidia na kubadilisha Maisha yangu, siwezi kumlipa kwa unyama hata kidogo” alisema Salma huku akidondosha chozi, hata sauti yake ilijaa kilio. Basi Mbaga akampatia kitambaa Salma afute chozi lake kisha akamwambia

    “Kwasasa nenda kaomboleze lakini nitakuhitaji tena hapa” Salma akanyanyuka na kuondoka.

    Haraka Salma alichukua Taxi akarejea nyumbani kwake, alikuta bado ndugu wapo wakimsubiria  maana alishapiga simu kua ameachiwa huru. 

    Kumuachia huru SALMA ni kosa kubwa ambalo Ajenti Mbaga amelifanya unajua kwanini? USIKOSE SEHEMU YA 4

    KAMA ULIPITWA:

    KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Pili) KOTI JEUSI – 02

    KOTI JEUSI Koti Jeusi Kijiweni riwaya ya koti jeusi

    18 Comments

    1. Godlove4 on May 1, 2024 5:16 pm

      Hahahah nimependa itimisho apo

      Reply
    2. Gray on May 1, 2024 5:21 pm

      Kesho tena

      Reply
    3. Jenipha on May 1, 2024 5:22 pm

      🔥🔥🔥🔥

      Reply
    4. Mabadiliko on May 1, 2024 5:31 pm

      Part 4 mbna fupi iv duuuuh inanoga snaaa👍👍👍

      Reply
      • Serah on May 1, 2024 6:28 pm

        Hata mimi nimeona fupi jaman😔iwe kama part 2 kidogo ndefu

        Reply
      • Sensible on May 2, 2024 7:48 pm

        Ni moto kabisa

        Reply
    5. Serah on May 1, 2024 6:28 pm

      Hata mimi nimeona fupi jaman😔iwe kama part 2 kidogo ndefu

      Reply
    6. Alex on May 1, 2024 7:05 pm

      Fupi tam

      Reply
    7. Junias on May 1, 2024 7:40 pm

      Nzur sana

      Reply
    8. Kibasa on May 1, 2024 9:31 pm

      Good mwandishi una kiu na Kalamu ila wasomaji tuna kiu na Maandishi yako jitahidi uongeze kidogo paragraph ya Leo fupi sana

      Reply
    9. Dorry on May 2, 2024 12:15 am

      🔥🔥🔥can’t wait part 4😂

      Reply
    10. [email protected] on May 2, 2024 12:27 am

      Salma kwenye ubora wake kama namuona 😅😅

      Reply
    11. Brama05 on May 2, 2024 1:00 am

      Dah! Imekuwa na paragraph fupi Sana Leo tofaut nazingne,,kesho mapema sana

      Reply
    12. Greyson on May 2, 2024 8:05 am

      Naomba jmn part 4 iwe ndefuu kama part two

      Reply
    13. Gabriel Marwa on May 4, 2024 10:02 am

      nice story

      Reply
    14. Pingback: KOTI JEUSI (Sehemu Ya Kumi Na Tatu) KOTI JEUSI – 13 - Kijiweni

    15. Pingback: KOTI JEUSI (Sehemu Ya Kumi Na Tatu) KOTI JEUSI – 14 - Kijiweni

    16. Pingback: KOTI JEUSI (Sehemu Ya Kumi Na Tano) KOTI JEUSI – 15 - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.