Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Kwanza) KOTI JEUSI – 01
    Hadithi

    KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Kwanza) KOTI JEUSI – 01

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaApril 29, 2024Updated:May 8, 202443 Comments6 Mins Read12K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Riwaya Ya Koti Jeusi
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    UTANGULIZI

    Ulikua ni Usiku mwingi, mvua kubwa ilikua ikinyesha ikisindikizwa na radi za hapa na pale,ndani ya kasri moja la kitajiri palionekana kua kimya sana huku upepo mkali ulikua ukipeperusha pazia za dirishani. 

    Kwenye kasri hili la kitajiri ndani ya chumba kimoja palikua na Binti mmoja wa Miaka 13 aliyeitwa Adela na alikua akijisomea Usiku huo, alikua amevalia pensi, tisheti na miwani yenye kumsaidia kuona vizuri.

    Upepo ulimfanya aache kusoma ili akafunge mapazia ya chumbani kwake, akanyanyuka kisha 

    akasogea dirishani na kufunga na baada ya hapo akarudi ili aendelee na kujisomea, bahati mbaya akajigonga kwenye meza ndogo ambayo ilikua na glasi yenye Maji, glasi ikadondoka chini na kuvunjika

    “Ooooh Mungu wangu, ni nini tena Jamani?” Alijisemea kisha akaokota vipande vya glasi, 

    akaufungua mlango ili akaviweke jikoni, taa zilikua zinawaka na kuzima kutokana na hali ya hewa ilivyokua mbaya Usiku huo, ilimpa wasiwasi akajitahidi kufanya haraka ili awahi kurejea chumbani.

    Alipofika karibu na ngazi ya kushuka chini akahisi kama kuna Mtu ametoka kwenye moja ya chumba akiwa amevalia koti kubwa jeusi na kiatu kikubwa, hakufanikiwa kujua ni nani lakini kutokana na hali ya kuzima na kuwaka kwa taa alihisi labda ni wenge lake. Akajikuta anashindwa kushuka chini na kuweka vipande vya glasi chini kisha akakimbilia chumbani kwake. 

    Akafunga mlango huku hofu ikiwa inazidi kumshika kila alivyomkumbuka yule Mtu ambaye hakufanikiwa kuiona vizuri sura yake isipokua koti Jeusi na kiatu kikubwa.

    Adela hakuhitaji tena kuendelea kusoma, akapanda kitandani kisha akajifunika shuka Gubi-gubi.

    SEHEMU YA KWANZA (01)

    Jiji la Dar-es-salaam lilikua tulivu Usiku huo, purukushani zilishakauka baada ya kufika saa 7 za usiku. Ndani ya jumba la kifahari la tajiri mmoja anayemiliki makampuni ya utengenezaji wa waini ya zabibu anayeitwa Mzee Yusuf palionekana kua na Mtu aliyekua akitembea kwenye korido, mwendo wake ulikua wa taratibu huku akionekana kua na shida kidogo ya kutembea.

    Wakati anafika korido moja ya nyumba hiyo ya ghorofa alisikia mlango ukibamizwa kwa nguvu.

    “Aaaaaaahh” aligugumia kwa kushtuka sana, akashusha pumzi zake kisha akashikilia gauni lake refu lililoonekana kumpa shida ya kutembea vizuri, Mtu huyo alikua ni Bibi ambaye ni Kijakazi wa muda mrefu wa Mzee Yusuf, alimchukulia Bibi huyo kama Mama yake Mzazi.

    Bado umeme ulikua unasumbua kutokana na mvua iliyokua ikinyesha, Bibi huyo mwenye uzito 

    mkubwa alijiuliza “Adela alienda wapi?” alisimama akijipa maswali yasiyo na majibu, aliamua kusogea mbele. Upande wa kulia kwake palikua na chumba cha Mzee Yusuf ambaye alikua akiishi na Mke wake aliyeitwa Salma, Mwanamke huyo kwa kipindi hicho alikua amesafiri kuelekea Uingereza kusimamia moja ya biashara zao huko.

    Mzee Yusuf baada ya kufiwa na Mke wake wa kwanza ndiyo alimuoa Mwanamke huyo wa miaka 39 tu, cha ajabu chumba cha Mzee Yusuf kilikua wazi Usiku huo, jambo lililompa maswali Mengi Bibi huyo aliyeitwa Bi Choro. Alisimama kwa kitambo kidogo hadi alipoamua kubadilisha maamuzi yake, 

    Sasa alikielekea chumba cha Mzee Yusuf kujua kwanini kipo wazi.

    Taa zilikua zinawaka na kuzima, japo hiyo ilimpa hofu Bibi huyo lakini alihitaji kujua kwanini chumba cha bosi wake kipo wazi usiku wa manane na hapakuonekana dalili ya kuingia wala kutoka Mtu yeyote ndani ya chumba hicho. Akiwa ameshakaribia mlango alianza kuona michirizi ya damu mbichi ikichuruzika sakafuni kutoka ndani ya chumba cha Mzee Yusuf, hakusubiri kuona ni kitu gani kilichosababisha hali hiyo, Bi Choro alipiga kelele za kuomba Msaada.

    Kelele hizo ziliwashtua baadhi ya watu waliokua wakiishi ndani ya Jumba hilo, mmoja wao alikua ni Binti wa Mzee Yusuf aliyemwamini sana aliyeitwa Sofia, mwingine ni Kijana wa kiume wa Mzee Yusuf aliyeitwa Hamza. Wote walikutana mahala hapo, waliishuhudia damu ikichuruzika, waliifuata damu hiyo hadi chumbani kwa Mzee Yusuf, walimkuta Mzee huyo akiwa ameegemea Meza akimwaga damu mdomoni na mgongoni, kisu kilikua juu ya Mgongo wake.

    Haraka zilipigwa simu kuelekea Polisi na Hospitali, mara moja wote walikusanyika hapo, wa kwanza kufika alikuwa ni Daktari Bingwa wa Mzee Yusuf. Daktari Huyo alikua wa kwanza kuthibitisha kuwa Mzee huyo alifariki dakika chache zilizopita kwani bado mwili wake ulikua wa moto, vilio vilitanda.

    Sofia alilia kwa kusaga meno, Bi Choro alilia kama Mtoto Mdogo, Hamza pekee ndiye aliyekua na nguvu ya kuzungumza na daktari sababu alikuwa Mtoto wa kwanza wa kiume wa Mzee huyo, ndiye Kaka wa Sofia kwanye hiyo familia yenye Watoto wawili pekee ambao ni Sofia na Hamza.

    Daktari alimshauri Hamza kutokuugusa mwili huo sababu hilo ni tukio la Mauaji. 

    Tayari wapelelezi walikua hapo wakiongozwa na Agent Daudi Mbaga aliyekua kiongozi wa wapelelezi hao, pia gari ya wagonjwa ilikua tayari imefika hapo ikiwa na Madaktari ambao nao walipewa taarifa kuwa Mtu waliyemfuata hapo alikua tayari ameshakufa. 

    Familia ya kitajiri ilizizima kwa Majonzi Usiku huo, wapelelezi waliwataka Wanafamilia kukusanywa sehemu moja, wakagawana kazi za kufanya hapo, Agent Daudi akabakia ndani ya chumba hicho ili kutafuta shahidi za kimazingira wakati timu iliyobakia ikiwa inawahoji wanafamilia.

    Dakika moja ya kutazama eneo hilo la tukio, Daudi aligundua kua kwenye meza ambayo Mzee Yusuf alikua ameilalia palikua na glasi mbili zenye vinywaji, peni moja pia chupa moja ya Waini ikiwa imevunjika kwa chini, vyote vikampa picha ya haraka kua aliyemuuwa Mzee huyo alianza kuzungumza naye Kwanza kisha pakatokea vurugu ndiyo maana chupa ya waini ilianguka kutokea juu ya Meza.

    Mkononi Mzee huyo alikua ameshikilia Bastola nyeusi ndogo, hapa Daudi akashindwa kufasili kwa haraka haraka ni kwanini alikua na Bastola ambayo haikuonekana kutumika. Pia ilionekana kwenye kabati la kuhifadhia makabrasha palikua pamepekuliwa sana, hii ikamfanya Daudi ahitimishe uchunguzi wa awali kua muuwaji alihitaji kitu fulani kutoka kwa Mzee huyo, lakini swali aliloondoka nalo ndani ya Chumba hicho lilikua

    “Nani amemuua Mzee huyo tajiri?”  Usikose KOTI JEUSI Sehemu Ya Pili Sasa

    KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Pili) KOTI JEUSI – 02

    KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Tatu) KOTI JEUSI – 03 

    KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Nne) KOTI JEUSI – 04 

    KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Tano) KOTI JEUSI -05

    KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Sita) KOTI JEUSI -06 

    KOTI JEUSI (Sehemu Ya Saba) KOTI JEUSI – 07

    KOTI JEUSI (Sehemu Ya Nane) KOTI JEUSI -08 

    KOTI JEUSI (Sehemu Ya Tisa) KOTI JEUSI -09 

    KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Kumi) KOTI JEUSI -10 

    KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Kumi Na Moja) KOTI JEUSI -11

    KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Kumi Na Mbili) KOTI JEUSI -12

     

    SOMA MAMBO MBALIMBALI KUTOKA KIJIWENI KWA KUGUSA HAPA PIA

    hadithi za kusisimua KOTI JEUSI riwaya za kijasusi riwaya za kusoma mtandaoni

    43 Comments

    1. Bintii kimmy on April 29, 2024 6:02 pm

      Sehemuu ya pili iendelee Hadith nzur sanaa🔥🔥💪

      Reply
      • Ammar on May 3, 2024 6:07 pm

        Patamu hapo

        Reply
    2. Novath sombe on April 29, 2024 6:04 pm

      Nzuri sana

      Reply
      • Admires on April 29, 2024 9:54 pm

        Nzuli sana

        Reply
      • Juma on May 2, 2024 11:19 am

        Nzurii

        Reply
    3. Peter Masanja on April 29, 2024 6:06 pm

      Angalau mfanye utaratibu wa kuziuza Ili ziwe downloadable

      Reply
    4. Rumbyambya Jr on April 29, 2024 6:12 pm

      Nice story… but kuna vitu jadhaa vya kiuandishi vinahitaji marekebisho all in all it’s a nice story Admin

      Reply
    5. Esther Emmanuel on April 29, 2024 6:20 pm

      Nzuri sana

      Reply
    6. Phoady on April 29, 2024 6:25 pm

      Nice. Iendelee sehemu inayofuata tafadhali

      Reply
    7. Mustaqim Ismaily on April 29, 2024 7:33 pm

      Nzuri sana

      Reply
      • Waziri on April 29, 2024 9:38 pm

        Nzuri sana

        Reply
    8. Amos Steven rohole on April 29, 2024 7:41 pm

      Nzuri sana

      Reply
    9. Emmanuel Boal on April 29, 2024 7:46 pm

      Story nzuri nimeipenda

      Na Mimi nina story yangu inaitwa kifo ni haki yangu ..tuwasiliane ili nikupatie uiweke hapa pia watu wasome
      0711986518

      Reply
      • ZeroGs on April 29, 2024 8:02 pm

        nimependa

        Reply
    10. Iamjullytz on April 29, 2024 8:10 pm

      It seems to be a nice story, we are in this together 🧡

      Reply
      • Temy Peter on April 29, 2024 8:33 pm

        Mwanzo mzuri… Nmeipenda, nikuombe admin kuwa unatuma Kila Siku kwa maana sehemu Moja Moja Kila Siku ili utamu usipoe

        Reply
        • Mhariri on April 29, 2024 10:06 pm

          Hakuna Noma Familia

          Reply
      • Dicter on April 29, 2024 8:45 pm

        Sehem ya pili ienderee good story

        Reply
    11. Msuya on April 29, 2024 8:39 pm

      Daaaahhhhh……..nzuri sana

      Reply
    12. Dicter on April 29, 2024 8:46 pm

      Good story I love it

      Reply
    13. Kenedy on April 29, 2024 8:53 pm

      Story safi nimeipenda sema mwandishi kuna vitu inabidi arekebishe ili story ikae bomba zaidi

      Reply
    14. Frank on April 29, 2024 9:16 pm

      🔥🔥🔥

      Reply
    15. Edward stima on April 29, 2024 10:25 pm

      Vp sehem ya pili inaendelea lini au mpaka tusahau admin

      Reply
      • Mhariri on April 30, 2024 9:31 am

        Leo Jioni Mkuu

        Reply
    16. Dhulfa Yusuph on April 29, 2024 10:28 pm

      Dah mwanzo tu inasikitisha

      Reply
    17. DEBLAX on April 29, 2024 10:57 pm

      I like it. Always I like to read but what to read about was a problem. Now for this I think gonna be a best story, let’s move it admin………..put on ep 2

      Reply
    18. Richie on April 30, 2024 9:55 am

      nimewahi kwanza comment section then nirud kusoma

      Reply
    19. Kibasa on April 30, 2024 2:44 pm

      Ukiwa kijiweni unapata Moja moto Moja Baridi swafi kabsa

      Reply
    20. Nasra on April 30, 2024 2:56 pm

      Hakika Mzee Yusuf kuna kitu alikifanya Hadi kupata huo utajir siyo bire , sehemu ya pili iendeleee ni nzuri sana

      Reply
    21. Twariq Jumanne on April 30, 2024 3:18 pm

      Stori Nzuri Sana Ngoja Tuone Muuaji Ni Nani?

      Reply
    22. Didactics jr on April 30, 2024 7:58 pm

      Good story I like it

      Reply
    23. Dremor on April 30, 2024 8:39 pm

      Nzuri

      Reply
    24. Alhajmwema on May 1, 2024 3:34 pm

      Iko gud

      Reply
    25. Azizi2468 on May 2, 2024 11:26 am

      Sana

      Reply
    26. Godlove on May 2, 2024 1:45 pm

      Adhithi tamu san hii

      Reply
    27. Ms chunnie on May 2, 2024 6:21 pm

      Sehem ya pili chap🥱🥱

      Reply
    28. JOSEPH NICHOLAUS KASULI on May 3, 2024 8:53 am

      Nice story

      Reply
    29. Chacha_Makuru on May 3, 2024 9:25 am

      Iendelee katika sehemu nyingine

      Reply
    30. Young ramson on May 3, 2024 9:47 am

      Nzuri Sana pia ina mafunzo 👪

      Reply
    31. Pingback: KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Pili) KOTI JEUSI - 02 - Kijiweni

    32. Pingback: KOTI JEUSI (Sehemu Ya Kumi Na Tatu) KOTI JEUSI – 14 - Kijiweni

    33. Pingback: KOTI JEUSI (Sehemu Ya Kumi Na Tano) KOTI JEUSI – 15 - Kijiweni

    34. Ammar Hassanain on May 11, 2024 11:07 am

      Riwaya mpya ningeomba itoke mida km hii, maana wengine kushika cmu usiku ni issue….

      Na hii iliyoisha ni bonge moja la PSYCHOLOGICAL THRILLER story, natumai mpya itaizidi hii iliyokwisha.

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.