Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Je Simba Na Azam Wana Nafasi Ya Kumzuia Yanga Msimu Ujao?
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Je Simba Na Azam Wana Nafasi Ya Kumzuia Yanga Msimu Ujao?

    Baraka JohanessBy Baraka JohanessMay 14, 2024Updated:May 15, 20243 Comments3 Mins Read999 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Yanga vs Simba sc
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Klabu ya Yanga imefanikisha kutetea kikombe cha ligi kuu ya NBC msimu huu wa 2023/2024 baada ya kuibuka na ubigwa wa kombe hilo kwa mara ya nne mfululizo huku azam na simba wakichuana kwa ajili ya nafasi ya pili.

    Kabla ya kurejea kwenye swali nikutajie vitu viwili ambavyo vimemfanya Yanga kuwa bingwa msimu huu kwanza ni kushinda mechi nyingi dhidi ya vilabu vidogo kwa magoli mengi lakini pia kuwa na idadi ya wachezaji wengi kwenye kikosi wenye uwezo takribani unaoshabihiana kitu kilicho punguza madhara ya majeraha.

    Hizi ndio sababu ninazohitaji kuziongelea ambazo nani yuko tayari kuzifanya msimu ujao wa NBC ambaye atakuwa tayari basi ndio bingwa wa ligi hiyo.

    Hakikisha unakusanya point nyingi dhidi ya vilabu vidogo Simba na Azam wameshindwa kufanya hivyo wamegawana points na vilabu vingi na muda mwingine kuviachia vilabu hivo point zote tatu hili lilikuwa kosa la kwanza.

    Kikosi cha Azam na Simba nikikuuliza leo Chama amekosekana nani atakuwa mbadala sahihi wa Chama ambaye ataweza kutoa walau asilimia 70% ya anachokitoa Chama vipi Feisal kwa Azam wakimkosa wanaweza bado wakashinda michezo.

    Kwa Yanga jibu ni ndio wamemkosa Aziz ki, Pacome, Aucho, Lomalisa, Yao katika nyakati tofauti ila walikuwa na mbadala wa wachezaji hao hivo haikuwapa changamoto Yanga.

    Kwa point hizo mbili Simba na Azam inabidi wahakikishe walau kila namba ina mbadala wa mchezaji husika endapo akiumia sio Tanzania tu hata ulaya mara nyingi Liverpool ameshindwa kubeba kombe mbele ya Man City sababu ya ufinyu wa kikosi.

    Yanga wata drop baadhi ya wachezaji kuelekea msimu ujao , Simba na Azam pia je sajili za kufidia wachezaji hao zitawashirikisha makocha na zitakuwa sahihi kutokana na kocha husika?

    Najua kwa mpira wa tanzania ni ngumu sana kocha kushiriki kwa asilimia 100% katika usajili ila kuna faida hizi kama kocha atakuwa sehemu ya maamuzi kwanza kujua mfumo halisi wakuendana na kikosi chake pia na matumizi mazuri ya mchezaji husika sababu kupitia mkono wake ndio usajili umetokea.

    Kwa Azam sina hoja juu ya swala la kocha ila kwa simba je watabaki na juma au kuna mbadala wa juma kama upo utakuja mda gani ili upate nafasi ya kufahamiana na wachezaji na kutengeneza aina yake ya uchezaji kutokana na timu ni mada ndefu sana kwenye mambo ya kimbinu naimani tutaiongelea siku nyingine kwa sasa tuyashike hayo .

    Kwa ufupi tu Azam na Simba wakifanya haya msimu ujao watawapa Yanga changamoto zaidi kwanza kushinda mechi dhidi ya timu ndogo lakini pia kuwa na upana wa kikosi bila kusahau kushiriki kwa kocha wakati wa usajili angalau 60%.

    SOMA ZAIDI: Je Yusuph Kagoma Ni Mbadala Sahihi Wa Khalid Aucho Yanga?

    mabingwa yanga ubingwa wa 30 yanga usajili wa msimu ujao Yanga yanga bingwa

    3 Comments

    1. Slavius nguvumali on May 14, 2024 3:11 pm

      Mimi naona kama team ya simba watakuwa na mbadala wa kocha wangefanya mapema ili kocha ajipange yeye mwenyewe nime semea simba kwasababu simba ndio tunaongoza kwa kubadili makocha

      Reply
    2. Luhinda Luhinda on May 16, 2024 10:48 am

      Simba bwana hahahahah

      Reply
    3. Pingback: Dodoma Jiji vs Simba Sc Vita Ya Nafasi Ya Pili Makao Makuu - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.