Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Jasusi Sehemu Ya Tisa (09)
    Hadithi

    Jasusi Sehemu Ya Tisa (09)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaDecember 6, 2024Updated:December 7, 202422 Comments13 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Hizi ni risasi zilezile, chukueni maiti hizi na wengineย  fanyeni msako hapa haraka sana” Ilikuwa ni sauti ya mmoja waย  Askari waliokuja pale kanisani, bado Mtaalam Sande, Mzeeย  Dawson na vijana wake wakiwa ndani ya Andaki bila kuwa naย  taarifa kuwa Jesca alikuwa ameuawa na Six, lilipofunguliwa lango kuu la Kanisa ndipo mshituko na Mshangao mkubwaย  ulipowashika polisi hao, walikuta Miili ya watu ikiwaย  inatokwa na mvuke kama vile nyama inayochomwa, harufu yaย  nyama ilitapakaa kanisa zima wakaagiza zima moto kumwaga Majiย  katika kanisa hilo, muda mchache polisi walifanikiwa kuingiaย  ndani ya kanisa na kukuta Miili mingi ikiwa imeharibikaย  vibaya sana.ย 

    Taarifa ilizagaa kwa haraka sana juu ya shambulio hilo laย  kutisha ambalo lilitumia silaha ya sumu na risasi, Sandeย  akawashauri akina Mzee Dawson kuwa hawapaswi kutoka kwaย  wakati huo hadi polisi watakapo maliza msako wao. Endeleaย 

    SEHEMU YA TISA

    “Nina mashaka juu ya uhai wa Jesca, yeye ni mmoja wa walinziย  wa hapa kanisani, sijasikia majibizano ya risasi, huwendaย  amekufa kifo Baridi” Alisema Mzee Dawson akionekana kushindwaย  kuzuia chozi lakeย 

    “Una maanisha nini kusema Kifo Baridi?” Alihoji Mtaalam Sandeย  Olise huku akimtazama Dawson kwa jicho lililo kazaย 

    “Kufa bila kujibu mapigo, Walengwa tunaotafutwa katika vitaย  hii ni sisi. Sitaki makubwa yawakute wasio na hatia” Alinenaย  Dawsonย 

    “Una maaana gani?”ย 

    “Ni bora nijitokeze kupambana nao ili kunusuru Maisha yaย  wengi yanayowekwa rehani, ikiwa kufa Mimi au kupona waoย  ninachotaka ni usawa” Aliongeza Dawsonย 

    “Kumbuka Polisi watakuangalia kama muarifu kuanzia hivi sasa,ย  hautokuwa huru kufanya chochote kama Mkuu wa Kitengo, vitaย  hii ni ngumu Mkuu! Vipi kama Rais ataamuwa kukupaka tope?ย  Utakuwa salama?” Aliuliza Sande Olise, Mzee Dawson akamezaย  funda zito la mate kisha akasemaย 

    “Tusipopambana sasa hivi tutakuja kupambana nje ya muda,ย  tunapaswa kuwa macho zaidi”ย 

    “Unashauri tufanye Nini Mkuu tupo tayari kukusaidia katikaย  vita hii” Alisema Kisko kwa utii Mkubwa, Dawson alikuwa kamaย  Mzazi kwao, ndiye aliyewachukua kutoka katika kituo chaย  Watoto yatima na kuwaonesha Mwanga wa Maisha, Dawsonย  akawageukia na kuwaambiaย 

    “Natamani hii vita msipigane sababu mna kila sababu ya kuwaย  hai ili mje mpigane hapo baadaye sisi tukiwa tumetundikaย  daruga au tukiwa tumekufa. Niliwaandaa mje kuwa hazina muhimu baadaye” Alisema Dawson kwa sauti ya Baba kwa Watoto wake,ย  nyuso za Kisko na Chande zilisinyaa huku macho yao yakitazamaย  chini.ย 

    “Babaa!! ” Aliita Chande, Dawson akageuza macho yakeย  kumtazamaย 

    “Tupo tayari kwa sasa kufa kwa ajili ya Taifa letu, turuhusuย  tukusaidie hii vita” Dawson alipomaliza kumsikiliza Chandeย  akarudisha macho yake kwa Sande Olise, Wakajikutaย  wanatazamana huku sura zao zikizungumza Kijasusiย 

    “Tuangalie tunatokaje hapa Shimoni, haribuni kila kitu iliย  kupoteza ushahidi wa kazi za hapa ndani, kila mmoja avae suraย  bandia haraka sana” Aliagiza Mzee Dawson kwa sauti iliyojaaย  mamlaka ya Kijeshi, kazi ikaanza rasmi.ย 

    MSAKOย 

    “Shit!” Ilikuwa ni sauti ya John Brain baada ya kupokeaย  taarifa usiku huo, hakutegemea kusikia kuwa Dawson na Sandeย  Olise bado wanaendelea kupumua, aliona ni makosa makubwa niย  sawa na kumjeruhi mnyama Mkali.ย 

    “Inawezekanaje wasiwepo kanisani wakati mtoa taarifaย  amehakikisha kuwa Sande aliingia hapo? Endapo Sande na Dawsonย  wakapata muda wa kupanga mipango yao kazi hii itakuwa ngumuย  kwetu” Alisema tena John Brain huku akizitazama sura za Sixย  na Malaika ambao walikuwa wamenywea.ย 

    “Nimefanya msako kanisa zima lakini sikupata kuhisi hataย  harufu zao, huenda walicheza mchezo wa sarafu baada yaย  kugundua kuwa tunawafuatilia” Alijibu Malaikaย 

    “Watakuwa wapi?” Aliuliza John Brain akionesha kutafakariย  jambo peke yake, kisha akawaambiaย 

    “Nendeni lakini Mjiandae kwa msako maalum” Malaika na Sixย  wakaondoka, John Brain akampigia simu Rais na kumjulishaย  taarifa ile ambayo ilionekana kumchanganya sana Raisย 

    “Hivi mnajua mnafanya masihara kwa Watu gani? Hao jamaa wanaย  medali za ushindi kwenye kila jambo, Dawson ana fahamu siriย  yetu hivyo hapaswi kuendelea kuishi” Alisema Rais kama Mtuย  aliyeingia kwenye mshituko ni wazi kuwa alitarajia kusikiaย  kuwa Dawson na Sande wameuawa

    “Tunalijuwa hilo na vijana wangu wanalifanyia kazi jambo laย  muhimu ni kuhakikisha unatupatia Mtu wetu baada ya sikuย  chache, tutakuwa tumeimaliza kazi hii na kuondoka hapaย  Nchini”ย 

    “Msifanye Makosa mengine John , mtajikuta mnawajibishwa!ย  Ngoja nijisafishe haraka sana” Rais alikata simu, alionekanaย  kuwa mwenye msongo wa mawazo huku akionekana kuwa na hofu juuย  ya mpango wake wa siri juu ya Mauwaji ya Makam wa Raisย  kujulikana na kuwekwa hadharani, akanyanyua simu na kumpigiaย  Mkuu wa Idara ya polisi na kumueleza kuwa Dawson ni mharifuย  anapaswa kusakwa kwa kila njia ili apatikane, Rais aliamuwaย  kucheza karata mbili.ย 

    Moja ni kuwatumia Mafia Gang kumfyeka Dawson na nyingine niย  kutumia Jeshi la polisi kumsaka popote alipo, agizo la Raisย  lilianza kutekelezwa, Polisi wakaagizwa kuelekea nyumbani kwaย  Dawson usiku huo huo.ย 

    Rais alikaa katika kiti chake huku akizidi kujiingizaย  mawazoni, Nchi ilikuwa imeingia katika Msako, Polisiย  walivunja nyumba ya Dawson na kufanya msako mkubwa bilaย  mafanikio, wakati huo Dawson na timu yake wakiwa wanatokaย  katika shimo kule kanisani, Polisi wachache walikuwepo eneoย  la tukio kule kanisani usiku huo, Walifanikiwa kuchomoka paleย  kanisani kimya kimya kisha wakaruka ukuta wa kanisa naย  kutokomea.ย 

    Dawson alishajua kuwa polisi wataenda nyumbani kwake hivyoย  akawaambia wasiende huko badala yake waelekee kwenye makaziย  ya siri ambayo alikuwa akiishi Inspekta Zola, ilikuwa niย  safari ya Kilomita kadhaa kutoka pale kanisani hadi kufikaย  huko, walilazimika kutembea kwa mguu sababu polisi walikuwaย  wakikagua magari yanayoingia na kutoka kila kona ya jijiย  hilo, haikuwa salama kwao kutumia usafiri wa gari licha yaย  kuvaa sura bandia, mwendo wa masaa mawili Walifika kwenyeย  makazi hayo, Dawson alifahamu namba za siri za kufunguliaย  milango hiyo ikawa rahisi wao kuingia ndani.ย 

    Kumbukumbu ya Zola iliendelea kuwatesa baada ya kuingia humo,ย  Sande aliiona picha aliyopiga na Zola wakiwa mafunzoni hadiย  chozi lilimbubujika aligundua kuwa Rafiki yake huyo alikuwaย  akimpenda na kumkumbuka sana, walikuwa na ndoto ya kuonanaย  siku moja lakini ndiyo hivyo Sande alichelewa kurudi hadiย  Zola akauawa, Dawson aliifahamu nyumba hii vizuri sana sababuย  mpango wa nyumba hii aliusuka mwenyewe ili Zola aitumieย  nyumba hii kwa kazi zake maalum, akawaonesha chumba ambachoย  kilikuwa na silaha akawataka kujiandaa kwa ajili ya kazi hiyoย  kubwa iliyo mbele yao.

    “Baada ya kupambazuka tutakuwa katika hekaheka nzito yenyeย  maamuzi ya kuondoa uhai wetu au kuturuhusu kuendelea kupumua,ย  kama tuna muda wa kufurahi basi huu Usiku uliobaki unawezaย  kuwa ndio muda pekee wa kufanya hivyo” Alisema Dawson akiwaย  ana mimina mvinyo kwenye glasi, kila mmoja akanyanyua naย  kuanza kunywaย 

    “Kwa ajili ya Zola, tusherehekee Maisha yake sababuย  ameimaliza kazi aliyokula kiapo kuifanya ili kulinda Taifaย  lake” Yalikuwa ni maneno ya Sande Olise ambaye naye aliunganaย  na Mzee Dawson wakanywa Glasi moja moja, Chande na Kiskoย  wakaungana pale wote wakapata Mvinyo kama Ishara ya kuyaenziย  Maisha ya Inspekta Zola ambaye ameuawa ndani ya Ikulu, hadiย  kufikia muda huo hakukuwa na taarifa iliyotolewa popote kuwaย  Inspekta Zola alikuwa amekufa, si akina Dawson wala upande waย  Rais ambao ndio walitekeleza Mauwaji hayo.ย 

    Asubuhi ya siku iliyofuata iliwakuta Dawson na vijana wakeย  wakiwa ndani ya jumba la siri hilo alilokuwa akiishi Mtaalamย  Zola, taarifa kuwa Dawson amelisaliti Taifa ilianza kuzagaa,ย  akatajwa Dawson kama ndiye Mhusika namba moja wa Mauwaji yaย  Waumini kule kanisani, taarifa ikafika mbali na kusema anaย  viashiria kuwa alitaka kuipindua Nchi hiyo kwa kusababishaย  taharuki ikiwemo Mauwaji ya kutisha yaliyokuwa yakifanyikaย  pia Mauwaji ya Makam wa Rais, gunzo lilikuwa limetanda, niย  kama Bundi mweusi alikuwa ameyazunguka Maisha ya Dawson,ย  ikatolewa taarifa kuwa Dawson anashirikiana na Askari mmojaย  wa Usalama wa Taifa aliyeitwa Sande Olise ambaye alikuwaย  akiishi Botswana.ย 

    “Huyu Mjinga anajaribu kuharibu taswira niliyoijenga Miakaย  mingi katika Taifa hili” Alisema Dawson kwa hasira hukuย  akitafuta rimoti ya TV ili aizime, Sande alimzuiaย 

    “Huna haja ya kupaniki, anachokifanya Rais ni kujaribuย  kujisafisha na kuyatia doa Maisha yetu. Kwakuwa anajua unaย  siri zake basi anaitumia hii nafasi kukudidimiza iliย  usiaminike na yeyote yule” Alisema Sande kisha Dawsonย  akamuulizaย 

    “Mimi ni mzalendo kwa Taifa hili, nimekuwa kwenye nafasi hiiย  kwa Marais zaidi ya tano, iweje huyu aje kuharibu kila jemaย  nililopanda kwenye Taifa hili, baada ya kuniulia Rafiki yanguย  anadiriki kuniita Msaliti wa Taifa hili” Dawson alionekanaย  kuchukizwa sana na kitendo kile, akapapasa kiuno chake akatoaย  bastolaย 

    “Unaenda wapi?” Alihoji Sande

    “Ikulu kuondoa uhai wa hayawani yule, hastahili kuishi pale,ย  anastahili kuwa Kaburini au Jela kwa yote aliyoyafanya”ย 

    “Hebu tulia, kumbuka John Brain ni Mtu mwenye akili sana. Huuย  ni mtego na lengo ni kukufanya uchukie, Rais anakujua vizuriย  hupendi mchezo na uzushi, ukitoka hapa hata hufiki mbaliย  wanakuuwa” Alisema Sande huku akimsistiza Dawson atulie,ย  chozi lilikuwa likimbubujika Mzee Dawson, akajitupa kitiniย  kama Mtu aliyekata tamaa.ย 

    “Huna haja ya kukurupuka, Tumetajwa kuwa Wauwaji na wasaliti,ย  tukikamatwa huko nje hatutokaa kuonekana tena, tutaliachaย  Taifa hili katika giza kama ambavyo Zola ameliacha. Nimekujaย  hapa kwa ajili ya kazi hii, nitazame Mimi kwa sasa kamaย  ambavyo ulikuwa ukimtazama Zola na kumuamini, hamisha kilaย  kitu kutoka kwake kisha kiweke kwangu, Mimi ni Zola niliyeย  katika Umbo la Sande, hakuna kitakacho haribika” Yalikuwa niย  maneno ya Kikomandoo kutoka kwa Sande Olise, alisema akiwaย  amefanikiwa kumpokonya Bastola Dawson.ย 

    Akampatia ile Bastola Kisko akamwmbiaย 

    “Ukiitumia vibaya itakupeleka pabaya, tuliza akili ndipoย  uitume ifanye kazi yake” Alimkabidhi kisha Akasemaย 

    “Baada ya miaka mingi narudi kazini kupambana na John Brain,ย  kivuli chake kitaendelea kuitesa hii Nchi, huyu Rais Mpumbavuย  siku zake za kuwa madarkani zinahesabika” Alisema kishaย  akaelekea kwenye moja ya vyumba vya siri vya jengo hiloย  ambavyo vilikuwa vimeshafunguliwa na Mzee Dawon.ย 

    Akakuta Ramani ya mpango wa Zola ikiwa ukutani, akaangaliaย  namna Zola alivyopanga mambo yake pale akajikuta akitabasamuย  kwani kila jambo alikuwa ameliandika katika Ramani hiyo.ย 

    Nyuma ya Sande alikuja kusimama Mzee Dawson huku akimtazamaย  Sande namna alivyokuwa makini kutazama Ramani ya Zolaย 

    “Ulikuwa na askari shujaa sana ambaye hasahau mbinu zako”ย  Alisema Sande Olise kisha aligeuka na kumtazama Mzee Dawsonย  aliyekuwa akifuta chozi lake, kifo cha Zola kilimuumiza sana.ย 

    “Nina uhakika kama utawatunza vijana hawa wawili wanawezaย  kuwa Sande na Zola wa baadaye, kwasasa Mzee Dawson pumzika.ย  Afya yako haikuruhusu kuendelea na vita hii, nitapambana Mimiย  na hawa vijana, utabakia hapa” Aliongeza Sande, ni kweli afyaย  ya Dawson haikuwa nzuri kutokana na pombe na sigara.

    Wakapanga mipango ya kumuondoa Rais Madarakani kisha kuanikaย  uchafu na madudu yake yote, Dawson alitakiwa kubakia paleย  kwenye jumba la siri wakati ambao Sande na vijana wawili waย  Dawson watakapokuwa wanaondoka, wakapewa sura bandia iliย  watakapotoka nje wasijulikane.ย 

    Muda huo Magari mawili meusi yalikuwa yakiingia Ikulu,ย  alikuwa ni John Brain, Six na Malaika, utatu ambaoย  ulilisumbua Taifa kwa muda mrefu, waliitwa na Rais huyoย  Mshenzi. Waliingia wakiwa kama wageni wakiwa ndani ya suraย  bandia ili wasitambulike sababu Vyombo vingi vya habari hasaย  vya nje vilikuwa vikiripoti taarifa zao za Mauwaji na jinsiย  ambavyo walikuwa wakitafutwa, Waliongoza hadi ofisini kwaย  Rais huyo bila Ulinzi wowote kutokana na maagizo ya Rais.ย 

    Rais alipowaona alinyanyuka na kusogea karibu na John Brainย  kisha akamuulizaย 

    “Mnataka niwape nini ili Dawson na Sande wauawe? Mnapaswaย  kujuwa kuwa Dawson ni nyati aliyejeruhiwa akitoka hukoย  mafichoni hatutokuwa salama” Alisema huku akionekanaย  kuchanganikiwa, jasho lilikuwa likimvujaย 

    “Tatizo umechanganya vitu viwili kwa wakati mmoja, Polisiย  wanahangaika kuwatafuta na sisi tunahangaika kuwapata. Kilaย  tunapopiga hatua polisi wanakuwa eneo la tukio, au unatakaย  tusamabratishe na polisi wako?”ย 

    “Kama hilo ni tatizo nitawaingiza katika mfumo wa usalama waย  Taifa mkiwa katika sura hizo, John utakaa pembeni sababu yaย  rangi yako ila Malaika na Six wataingia na kufanya kazi maraย  moja, watakuwa na amri kwa askari pindi wanapokutana katikaย  jukumu la kuwawinda Sande na Dawson,watapewa vitambulishoย  maalum”ย 

    Rais akawaingiza Six na Malaika katika mfumo wa idara yaย  Usalama wa Taifa, wakapewa na Vitambulishoย ย 

    vilivyowatambulisha kama Watu wa Usalama, ikawa rahisi kwaoย  kuwa huru kufanya kazi ya kuwasaka Dawson na Sande Oliseย  ambao walikuwa kizingiti kikubwa kwa Rais na John Brainย  kumpata kijana wake aliyekuwa akishikiliwa na Rais.ย 

    Polisi wakatawanywa kila kona ya Jiji kuhakikisha Dawson naย  Sande hawapigi hata hatua moja, kazi ya polisi ilikuwaย  kuwakamata lakini kazi ya Six na Malaika ni kuwauwa, wakiwaย  ndani ya Sura bandia walirudi pale Kanisani ambakoย  walisababisha Mauwaji ya kutisha ya Waumini na Askari mmojaย  wa siri wa Mzee Dawson, walirudi kama Watu wa Usalama,ย  wakahitaji kuchunguza eneo hilo huku akili zao zikiwaambia kuwa pengine Dawson na Sande bado wapp eneo hilo, walimjuaย  vizuri Dawson jinsi alivyo na akili nyingi.ย 

    Walitumia vyema macho yao ya Kijasusi na mafunzo waliyoyapataย  kutoka kwa John Brain wakagundua kuwa kuna andaki eneo laย  maegesho ya Magariย 

    Six na Malaika wakapeana ishara, haraka bastola zao zikawaย  zinatazmaa eneo hilo ili kama kuna Mtu atatokea basiย  wamdhibiti haraka sana.ย 

    Wakalisukuma gari na kuona mlango wa kuingia ndani, harakaย  wakiwa makini sana wakafungua na kuanza kuingia humo taratibuย  huku masikio yao yakiwa makini kusikiliza ndani ya andakiย  hilo lenye giza sana.ย 

    Walipofika chini wakawasha tochi ya simu kisha wakaona mahaliย  ambapo wangewasha taa, walipowasha wakaona vitu vikiwaย  vimeharibiwa pale, wakakagua kila kona lakini hakukuwa naย  Watu, tayari Mzee Dawson na vijana wake walishaondoka paleย  muda mrefu sana kisha wakaharibu vitu ndani ya andaki hilo,ย  elimu yao ya kijasusi haikuwafanya wao kukata tamaa ya kutakaย  kujuwa andaki hilo lilihusiana na niniย 

    “Kwa vyovyote haya yalikuwa makazi ya siri ya Dawson! Huendaย  ameishi hapa kwa kitambo sana” Alisema Sixย 

    “Hata awe makini vipi ni lazima ataacha alama humu, tutajuaย  kama ni yeye na ameenda wapi” Alisema Malaika, msakoย  uliendelea ndani ya andaki hilo lililoonekana kuwa makazi yaย  kutulia sana, katika upekuzi wao waliona Makaburi manneย  ambayo yalikuwa ndani ya chumba kimoja.ย 

    Walipoangalia vizuri waliona namba za siri ambazo Mzee Dawsonย  aliwapa vijana wake kama majina na alama zao, namba hiziย  zilikuwa za siri sana, ilikuwa ngumu kugundua chochote lakiniย  alizitambua kisha akampigia simu John Brain na kumuelezaย  kuhusu Makaburi hayo manne yenye namba za siri, John Brainย  alikuwa na mtandao mkubwa sana na alizijua siri nyingi zaย  Mataifa mbalimbaliย 

    “Hayo ni majina ya Watu wa siri wa Mzee Dawson, Sande yupoย  hai, moja ya kaburi hapo linaweza kuwa kaburi la Zola,ย  fukueni haraka sana.” Ilisikika sauti ya John Brain, aliaminiย  Dawson ni Mtu mwenye akili sana kwenye mambo yake.ย 

    Mengine yalionekana kuwa ya zamani sana lakini moja lilikuwaย  bado jipya, wakalifukua hilo kwa kutumia chepe iliyo kwenyeย  kona ya chumba hicho chenye makaburi. Kazi hii ilifanywa na Six aliyekuwa amebana rasta zake kwa nyuma. Jasho lilikuwaย  likimtoka, harufu kidogo ilianza kutapakaa pale, haikuwazuiaย  kufanya kazi yao,

    Comments ziwe nyingi apa wikiendi itoke EPISODE NDEFU YA 10ย 

    Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA SABAย  USISAHAU PIA Kununua Kitabu Cha KOTI JEUSI Kupiga Namba+255760871896 Ufikishiwe Mpaka Ulipo

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapaย 

    ย  Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx ย  Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx ย  Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx ย  Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xxย 

    ย ย 

    jasusi riwaya za kijasusi

    22 Comments

    1. yukovich on December 6, 2024 2:29 pm

      unyama

      Reply
    2. Charz jr๐Ÿ˜Ž on December 6, 2024 3:05 pm

      Kazi kazi

      Reply
      • Elsolo on December 7, 2024 9:47 am

        Toa hata tatu mzee baba

        Reply
    3. Charz jr๐Ÿ˜Ž on December 6, 2024 3:06 pm

      Weeknd usitubanie asee

      Reply
    4. G shirima on December 6, 2024 3:25 pm

      Kila unaesima naomba ucoment please

      Reply
    5. DIzzoh on December 6, 2024 4:11 pm

      Too hot๐Ÿ™Œ

      Reply
    6. Areta on December 6, 2024 4:14 pm

      Ya motoo

      Reply
    7. Aisha on December 6, 2024 5:07 pm

      .wendelzo jmn pia zilishwe hata tano kwa siku ๐Ÿฅฐ๐Ÿฅฐ

      Reply
    8. Fawziya Hassan on December 6, 2024 6:13 pm

      Simulizi ya ๐Ÿ”ฅ
      Mtunzi wa Simulizi hii anitafute kuna Zawadi yakeโ™ฅ๏ธโ™ฅ๏ธโ™ฅ๏ธ

      Reply
    9. Anuar on December 6, 2024 6:13 pm

      Daah imefka penyew mkuu uwe unatoa hata mbili basi mkuu
      Stor iko poa sana

      Reply
    10. Buruani on December 6, 2024 8:11 pm

      Hatar iyooรณoo

      Reply
    11. VERONICA on December 6, 2024 9:07 pm

      Nzuri sana

      Reply
    12. Street kid on December 6, 2024 9:13 pm

      Shusha chuma mkuu ๐Ÿคด

      Reply
    13. David on December 6, 2024 10:36 pm

      Weeee

      Reply
    14. Jack bujo jr on December 6, 2024 11:47 pm

      Kesho tuwahishie Basi pia ilefushe hata kidogo maana siku za mpira hua unabana Sana

      Reply
    15. [email protected] on December 6, 2024 11:50 pm

      Jmn huyu malaika na six. Si sande wawauwe fasta wasijeniulia Mzee wangu Dowson jmn

      Reply
    16. [email protected] on December 6, 2024 11:51 pm

      Admin story Kali sn ni km vile mtu unaangalia movie

      Reply
    17. Hamza Abdallah Mwalyawa on December 7, 2024 12:36 am

      Hili ni bomu la kutegwa ardhini kilo mia moja haponi mtu hapo ni mbele kwa mbele ๐Ÿคธ๐Ÿคธ๐Ÿคธ๐Ÿ˜ก

      Reply
    18. Ahmed Samir on December 7, 2024 12:32 pm

      ๐Ÿ’ฅ

      Reply
    19. Hope on December 7, 2024 2:02 pm

      Natamani ingekuwa movie kbs yani uwii admin upewe maua yako โ˜บ๏ธ

      Reply
      • Ally abiz on December 7, 2024 5:44 pm

        Kazi nzuri admin una jitahidi

        Reply
    20. ๐Ÿ“ Ticket- TRANSFER 1,870203 bitcoin. Continue => https://yandex.com/poll/7HqNsFACc4dya6qN3zJ4f5?hs=47eff14450b187be13d1a5e38c52e7a2& ๐Ÿ“ on June 3, 2025 11:01 am

      3exvik

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 23, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nane โ€œNakufahamu Zahoro, wewe ndiye jibu la Laana hii.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-06

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.