Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Ijue Historia ya Mechi ya Algeria vs Angola AFCON
    Africa | CAF

    Ijue Historia ya Mechi ya Algeria vs Angola AFCON

    Brenda UlomiBy Brenda UlomiJanuary 15, 2024No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Hii ni mara ya pili kwa Algeria vs Angola kukutana kwenye CAF Africa Cup of Nations.

    Algeria vs Angola Mechi yao ya kwanza ilimalizika kwa sare ya bila kufungana wakati wa hatua za makundi kwenye toleo la 2010.

    Historia ya Algeria katika CAF Africa Cup of Nations:

    Algeria inashiriki mara ya 20 kwenye CAF Africa Cup of Nations.

    Wamefanikiwa kutwaa taji hilo mara mbili awali, mwaka 1990 na 2019.

    Mataji yote mawili ya Algeria yalipatikana kwenye ardhi ya Kaskazini mwa Afrika nyumbani mwao mwaka 1990 na nchini Misri mwaka 2019.

    Mara ya mwisho Algeria kufika fainali nje ya Kaskazini mwa Afrika ilikuwa mwaka 1980 nchini Nigeria.

    Hii ni mara ya sita mfululizo kwa Algeria kushiriki katika CAF AFCON, rekodi yao ndefu tangu kufuzu kwa mashindano hayo mara saba mfululizo kati ya 1980 na 1992.

    Katika CAF Africa Cup of Nations mwaka 2021, Algeria walifunga bao moja tu kati ya mashuti yao 46, lakini walifanikiwa kufunga 13 kati ya mashuti yao 77 walipotwaa taji mwaka 2019.

    Historia ya Angola katika CAF Africa Cup of Nations:

    Angola inashiriki mara ya tisa kwenye CAF Africa Cup of Nations.

    Wamefanikiwa kusonga mbele kutoka hatua ya makundi mara mbili tu (2008 na 2010, wakati wa uenyeji), lakini hawajawahi kushinda mchezo katika awamu ya mtoano.

    Angola haijashinda katika mechi zao nane za mwisho za CAF Africa Cup of Nations (droo nne, kufungwa nne).

    Matokeo ya mechi zao tatu za mwisho mwaka 2023 yalimalizika kwa sare bila kufungana.

    Angola haijapoteza mchezo wa kwanza kwenye CAF AFCON kwa mechi zao tano zilizopita (ushindi mmoja, droo nne).

    Mara ya mwisho walipopoteza mchezo wao wa kwanza ilikuwa mwaka 2006 dhidi ya Cameroon (1-3).

    Mohamed Amoura alikuwa mchezaji pekee wa Algeria aliyefunga zaidi ya bao moja katika mechi za kufuzu kwa mashindano ya mwaka huu, akiwa na magoli matatu.

    Soma zaidi: Makala zetu hapa

    africa cup of nations algeria angola caf
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.