Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Hawa Ndio Washindi Wa Tuzo Za AFCON Vipengele Vyote
    Africa | CAF

    Hawa Ndio Washindi Wa Tuzo Za AFCON Vipengele Vyote

    Living ShayoBy Living ShayoFebruary 12, 20242 Comments3 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Baada ya michuano ya mataifa barani Afrika kutamatika rasmi kwa fainali ya kibabe ambayo wenyeji Ivory Coast walikua wanakipiga na Nigeria na tembo wa Ivory Coast kuondoka na ubingwa baada ya kuwafunga Nigera bao 2:1. Kama utakua ni mmoja kati ya wale ambao wanajiuliza kuhusu tuzo lakini hapa tumekuandalia vipengele vyote na washindi wa tuzo hizo.

    Mchezaji Bora wa michuano

    Nahodha wa Nigeria William Troost Ekong nayecheza nafasi ya beki wa kati ana miaka 30 tu akiwa anakitumikia kikosi cha PAOK FC ya Ugiriki.AFCON hii amevaa jezi namba 15 ndiyo mchezaji bora wa Mashindano haya amecheza jjmla ya mechi sita na amefunga magoli 3 kwenye mashindano.

    Kipa Bora

    Nahodha wa Bafana Bafana Ronwen Williams akiwa na miaka 32 ndiyo amechaguliwa kuwa kipa bora wa mashindano haya toleo la 34. Amecheza michezo yote 7 ya AFCON kwa kikosi chake cha South Afrika akifungwa jumla ya goli 4 akiondoka na “Clean sheet” 4 kwenye mashindano haya na kuiwezesha Bafana Bafana kumaliza nafasi ya tatu.

    Huyu ndiyo kipa aliyeweka historia ya kudaka mikwaju 4 ya penalti kati ya mikwaju 5 kwenye mchezo wa Robo fainali dhidi ya Cape Verde.

    Mchezaji Bora Kijana

    Kijana anayekipiga Brighton ya England pamoja na kikosi cha Ivory Coast akiwa na miaka 22 tu Simon Adingra anachaguliwa kuwa Mchezaji bora kijana na AFCON nchini Ivory Coast. Amecheza jumla ya michezo5 akifanikiwa kufunga goli moja dhidi ya Mali huku akitengeneza magoli “Assist” 2 kwenye fainali dhidi ya Nigeria na alikuwa akivaa jezi namba 24.

    Mfungaji Bora

    Akiwa na miaka 34 mshambuliaji na nahodha wa Equatorial Guniea Emilio Nsue anaibuka Mfungaji bora wa AFCON toleo la 34 akiwa amefunga jumla ya magoli 5.

    Hata hivyo magoli hayo amefunga kwenye michezo miwili tu akifunga hat trick dhidi ya Guinea Bissau pamoja na mawili dhidi ya Ivory Coast huku akiweka historia ya kufunga hat trick ya kwanza ya AFCON msimu huu.

    Kocha Bora

    Kocha mzawa Emerse Fae amechaguliwa kuwa Kocha bora wa AFCON, alianza michuano hii kama Kocha msaidizi wa Ivory Coast baada ya hatua ya makundi kutamatika akakabidhiwa mikoba ya Kocha mkuu.

    Ameiongoza Ivory Coast kwenye michezo 4 kama Kocha mkuu na amefanikiwa kuibuka na ushindi kwenye michezo yote 4 huku mchezo mmoja wa hatua ya 16 dhidi ya Senegal akiibuka na ushindi kwa mikwaju ya Penalti.

    Fair Play Team

    Timu ya taifa ya Afrika Kusini maarufu Bafana Bafana imechaguliwa kuwa timu iliyoonyesha mchezo wa Kiungwana zaidi maarufu “Fair Play” kwenye michuano hii ya 34 ya AFCON iliyofanyika Ivory Coast. Hata hivyo Bafana Bafana ndiyo washindi 3 wa michuano wakiishia hatua ya Nusu Fainali baada ya kutolewa na Nigeria kwa mikwaju ya Penalti.

    SOMA ZAIDI: Wachezaji Watano Muhimu wa kuwapa ubingwa Ivory Coast.

    afcon AFCON 2023 Afcon today

    2 Comments

    1. Pingback: Takwimu Na Rekodi Zote AFCON Unazopaswa Kuzifahamu - Kijiweni

    2. Pingback: Hiki Hapa Kikosi Bora Cha AFCON 2023 - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.