Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » El Shenawy Aonya Kuhusu Changamoto Dhidi ya Simba
    Africa | CAF

    El Shenawy Aonya Kuhusu Changamoto Dhidi ya Simba

    Brenda UlomiBy Brenda UlomiOctober 20, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    230914F_CSC_ALAPRECONF_WM
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Mohamed El Shenawy, Nahodha wa Al Ahly, anasema timu yake inatarajia mchezo mgumu wanapokutana na Simba SC, mabingwa wa Tanzania, katika mchezo wa ufunguzi wa Ligi ya Soka ya Afrika (AFL) huko Dar es Salaam siku ya Ijumaa.

    Makomandoo Wekundu walifika jijini Dar es Salaam siku ya Jumatano usiku kuelekea kwenye mtanange unaotabiriwa kuwa na msisimko mkubwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa.

    Akizungumza siku moja kabla ya mchezo katika mkutano wa waandishi wa habari kabla ya mchezo, El Shenawy anasema Simba wameonyesha miaka kadhaa iliyopita kuwa ni wapinzani wakali, na mabingwa mara 11 wa Ligi ya Mabingwa ya CAF TotalEnergies wanajua kwamba haitakuwa rahisi wanapokutana na Wekundu wa Msimbazi.

    “Simba ni timu nzuri sana na tumejifunza hilo tunapocheza hapa. Wanacheza nyumbani na haitakuwa mchezo wa kirahisi. Tumefanya jitihada kubwa kujiandaa vizuri na tuko tayari kupambana kwa ajili ya ushindi,” mlinzi huyo alisema.

    Al Ahly wameshapambana na Simba mara mbili huko Dar es Salaam katika Ligi ya Mabingwa ya CAF, na katika mara zote hizo, wamepoteza kwa kufungwa bao 1-0, matokeo yaliyofanana.

    Ziara yao ya mwisho nchini Tanzania ilikuwa mwaka 2021, walipoteza kwa bao lililofungwa na Luis Miquisonne, ambaye baadaye aliichezea Al Ahly kwa muda mfupi.

     

    Licha ya kufungwa katika michezo yao ya awali, Shenawy anasisitiza kwamba wanaweza kuanza sura mpya wanapocheza Ijumaa.

    “Katika mara zote mbili, tulipopoteza hapa, tulifikia fainali na katika moja ya hizo tulishinda kombe.

    “Kwa hiyo, kwa upande wetu, jambo muhimu ni dakika 180, siyo tu dakika 90 hapa Dar es Salaam.

    “Tunajua kuwa hii ni nusu moja tu ya mchezo na tuna nusu nyingine Cairo,” alisema mwenye umri wa miaka 34.

    Ahly, mabingwa mara 11 wa Afrika, wanatafuta kuonyesha umahiri wao katika mashindano mapya, na wana uhakika wa kuanza vizuri.

    “Hii ndiyo tabia yetu Al Ahly, daima tunataka kupigania kushinda.

    “Tangu kila mmoja wetu azaliwe, ndivyo tulivyo. Lazima tuwe daima katika mapambano kwa ajili ya taji linalofuata.

    “Tuzo tulizoshinda awali ni historia na hatuitazami. Tunataka kufanikisha jambo jipya, na tunataka kufanya hivyo kupitia mashindano haya mapya,” El Shenawy alisema.

    Ahly wamefanikiwa kurejea kutoka kwa kushindwa dhidi ya USM Alger katika Kombe la Super Cup la CAF TotalEnergies mwanzoni mwa msimu, na wameendelea kushinda mechi tano katika mashindano yote bila kuruhusu bao isipokuwa mara moja.

    Soma zaidi: Habari zetu kama hizi hapa

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 23, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nane “Nakufahamu Zahoro, wewe ndiye jibu la Laana hii.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-06

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.