Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Bayern kunyakua taji la 11 la Bundesliga, Wapigwa za ‘Uso’ kufuzu fainali Kombe la Ujerumani
    Biriani la Ulaya

    Bayern kunyakua taji la 11 la Bundesliga, Wapigwa za ‘Uso’ kufuzu fainali Kombe la Ujerumani

    Brenda UlomiBy Brenda UlomiApril 5, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Lucas Hoeler aliifungia Freiburg bao la dakika ya 95 kwa mkwaju wa penalti na kuwaondoa Bayern Munich katika robo fainali ya Kombe la Ujerumani.

    Bayern walitangulia kupata bao kupitia kichwa cha Dayot Upamecano lakini Nicolas Hoefler aliisawazishia Freiburg baada ya dakika nane.

    Hoeler alifunga penalti baada ya Jamal Musiala kumchezea rafu ndani ya eneo la hatari, na kuiwezesha Freiburg kufuzu kucheza nusu fainali.

    Hii ilikuwa mechi ya pili ya Thomas Tuchel tangu achukue usukani wa Bayern Munich, baada ya kuifunga Borussia Dortmund 4-2 katika ligi siku ya Jumamosi.

    Klabu ya Munich ilimfuta kazi kocha Julian Nagelsmann baada ya kushindwa na Dortmund kwenye msimamo wa Bundesliga na kumleta Tuchel, ambaye aliwahi kuwa kocha wa Dortmund kati ya mwaka 2015 na 2017.

    Upande wa Tuchel ulidhibiti mechi hiyo kwa sehemu kubwa lakini kombora la Hoefler kutoka nje ya eneo la hatari, baada ya Kingsley Coman kushindwa kutoa pasi safi, lilisawazisha kwa Freiburg kabla ya Hoeler kuipatia timu yake ushindi wa kushangaza kwa mkwaju wa penalti dakika za mwisho.

    Freiburg ilipoteza fainali ya mwaka jana kwa mikwaju ya penalti dhidi ya RB Leipzig wakati Bayern haijafuzu kucheza robo fainali kwa miaka mitatu mfululizo.

    Kwingineko, Randal Kolo Muani aliifungia Eintracht Frankfurt mabao mawili ndani ya dakika mbili na kuwaondoa Union Berlin kwenye Kombe la Ujerumani. Frankfurt ilishinda kwa 2-0.

    bayern
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.