Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Barcelona Yasikiliza Ofa kwa Raphinha kuanzia €70 Milioni
    Biriani la Ulaya

    Barcelona Yasikiliza Ofa kwa Raphinha kuanzia €70 Milioni

    Brenda UlomiBy Brenda UlomiJune 8, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Barcelona Tayari Kusikiliza Ofa Zenye Kuanzia €70 Milioni kwa Mshambuliaji Mwenye Umri wa Miaka 26

    Barcelona itaanza kuondoa wachezaji wengi sana katika dirisha hili la usajili kwa lengo la kupisha usajili mpya katika timu yao.

    Ingawa kipaumbele chao kilikuwa ni kumrejesha Lionel Messi Camp Nou, inaonekana kuwa operesheni hiyo imefeli kwani Margentina huyo anatarajiwa kujiunga na Inter Miami kama mchezaji huru.

    Baada ya kushindwa kumrejesha Messi, Wa-Katalunya wataelekeza nguvu zao kwa malengo mengine muhimu.

    Kwa kawaida, Barcelona itakuwa inatafuta kuwasajili mabeki wa kati, na uhamisho wa Inigo Martinez umekaribia kukamilika, mchezaji mpya wa upande wa kushoto, mshambuliaji wa akiba, kiungo wa kati, na kiungo wa ulinzi baada ya Sergio Busquets kuondoka.

    Ili kuhakikisha wanaimarisha nafasi zote msimu huu wa kiangazi, Barça huenda ikalazimika kufanya maamuzi magumu katika soko la usajili, kama kuuza baadhi ya wachezaji ambao wangependelea kuwabakisha. Mmoja wao anaweza kuwa Raphinha.

    Kulingana na ripoti ya Tiempo de Juego, Barcelona wapo tayari kusikiliza ofa zinazoanza kutoka €70 milioni kwa Mbrazili huyo. Vilabu kadhaa vya Ligi Kuu ya England vinaonyesha nia ya kumsajili.

    Ripoti za awali zilidai kuwa Newcastle United tayari walikuwa wametuma ofa ya €80 milioni kwa Raphinha, ambayo inafanyiwa utafiti na Barcelona. Ingawa wanaelekea kukubali ofa hiyo kutokana na hali yao mbaya kifedha, mchezaji huyo bado hajako tayari kuondoka katika klabu.

    Xavi naye amedai kuwa mchezaji huyo hapatikani kwa uhamisho kwake. Hata hivyo, uamuzi wa mwisho huenda ukafanywa na klabu.

    “Raphinha HAPATIKANI kwenye soko. Atabaki Barcelona na atatusaidia sana. Yeye ni mchezaji muhimu sana kwangu, mchezaji ambaye ana umuhimu mkubwa. Yeye anafanya tofauti,” Xavi alisema.

    Soma zaidi: Habari zetu kama hizi hapa hapa 

    barca laliga usajili
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.