Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Azam vs Yanga Tutegemee Fainali Ya Namna Hii Hapa
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Azam vs Yanga Tutegemee Fainali Ya Namna Hii Hapa

    Baraka JohanessBy Baraka JohanessJune 2, 2024Updated:June 3, 20249 Comments3 Mins Read764 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Azam vs Yanga
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Yanga katika msimu wao bora wa 2023 / 2024 hakuna timu iliyowapa changamoto kama klabu ya Azam hii ni kutokana na uwezo mzuri wa wachezaji wa azam mbinu za mwalimu Dabo ambazo zimekuwa zikimpa changamoto kocha wa Yanga Gamondi

    Kabla ya kuangazia mchezo wa leo tuangalie kwanini azam huwa wanampa changamoto yanga katika michezo waliyokutana chini ya mwalimu Dabo . Baada ya mwalimu wa Azam kujua kuwa wachezaji wengi wa timu yake ni wachezaji wenye uwezo wakiwa na mpira mguuni kuliko wakiwa wanaukimbiza mpira akaamua kuwa muumini wa mpira wa kusogea mbele kwa kutumia pasi kuliko mipira mirefu

    Staili hii inawafanya wacheze kwa kasi na kubadilishana nafasi sana kitu ambacho ni changamoto ukitaka kuwakaba katika mstari wa katikati (midblock) na hiki ndicho yanga wamekuwa wakifanya dhidi yao ambacho kilikuwa faida kwa azam katika nyakati kadhaa

    Katika mchezo wa leo wa fainali ya CRDB Federation cup utakuwa ni mchezo wa kimbinu ambao pia utategemea uwezo wa mchezaji mmona mmoja mara nyingi azam akicheza na yanga amependa kutoka nyuma ya mpira katika umbo la wachezaji watatu (mabeki wakati wawili na beki mmoja wa pembeni ) huku yanga wakiwa na wachezaji wawili wakuweka pressure kwenye mpira na kutengeneza umbo la 4-4-2 hivo ni 3-5-2 azam wakiwa na mpira na 4-4-2 yanga wakiwa hawana mpira

    Hii ndivyo inavotokea mda mwingi wakikutana japo haiweki uwakika kuwa leo itakuwa hivi pia

    Yanga wamekuwa wakipenda kuacha idadi kubwa ya wachezaji kwenye boksi lao endapo wanakutana na mpinzani ambaye wanashaka na uwezo binafsi wa wachezaji wa timu hiyo lakini kwa kawaida yanga wamekuwa wakicheza katika mfumo wa 4-2-3-1 ambao umekuwa ukinyumbulika mda ambao wanajaribu kusogeza mpira mbele aidha kuwa (3-4-3) (4-3-3) pia .

    Azam wana madhaifu yakumkosa mtu mwenye uwezo wa kubeba mpira kwenda mbele (ball progressor) hii inaweza ikawa na faida katika kuwavutia wachezaji wa timu pinzani kwenda kuweka presha na kuacha nafasi nyuma yao ambayo inaweza kutumika na washambuliaji wao kitu kinachowalazimu wausogeze mpira kwa kutumia pasi nyingi na kubadilishana nafasi kwa wachezaji.

    Kwa upande wa yanga silaha yao kubwa imekuwa namna Gamondi anavowatumia (pacome , max , aziz ki ) Faida anayopewa na hawa watu watatu imemfanya awe na idadi kubwa ya nafasi zinazotengenezwa kwasababu ya uwezo wao wa kusogeza mpira mbele na kutengeneza nafasi nyingi pia wakisaidiana na Yao pamoja na kibabage au lomalisa kama mabeki wa pembeni

    Timu zote mbili zina faida ya wachezaji wenye uwezo mkubwa (bangala , akamiko , feisal , akamiko ) hawa wote ni wazoefu na wenye uwezo kwa yanga pia (Aziz ki , Max , Pacome , Guede ) wanauwezo wa kuamua mchezo kwa uwezo wao binafsi endapo mbinu za walimu wao zitaenda mlama

    Gamondi ana nafasi yakujiuliza mchezo wa mwisho alizidiwa wapi na  Dabo anajua alifaulu wapi na aongeze nini ili aweza kumiliki na kudhibiti yanga na viungo wao wasitengeneze nafasi nyingi.

    SOMA ZAIDI: Uso Wa Saido Ntibazonkiza Unazungumza Mengi

    azam vs yanga kikosi chayanga leo

    9 Comments

    1. Mzopola Tobias on June 2, 2024 1:54 pm

      Naitakia kila rakheli Azam fc

      Reply
    2. Kumbi salimu on June 2, 2024 2:24 pm

      Naitaka kila la heri yanga
      Pia hongera azama kwa kufika hii hatua

      Reply
    3. Breezy on June 2, 2024 2:34 pm

      Yanga one love leo Mkubwa atajulikana t

      Reply
    4. faraja on June 2, 2024 3:02 pm

      naitakia yanga ushindi mnijuze mechi saangp

      Reply
    5. Elias on June 2, 2024 3:23 pm

      Fei apewe kombe lake mapema

      Reply
    6. Babuu on June 2, 2024 4:43 pm

      Naacha kubeti uwiiiiiiiiiii

      Reply
    7. Pingback: Wachambuzi Wanamuingiza Feitoto Kwenye Chuki

    8. Musa on June 17, 2024 8:14 pm

      Hatimae hawa washenzi wametulia

      Reply
      • Musa on June 17, 2024 8:15 pm

        Ila harmonize

        Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.