Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Azam FC kumtema Bruce Kangwa, Fei Toto kuongoza Jeshi
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Azam FC kumtema Bruce Kangwa, Fei Toto kuongoza Jeshi

    David MohamedBy David MohamedJune 13, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Mabosi wa klabu ya Azam FC hawalali kwa mipango ya kusuka jeshi jipya la msimu ujao na sasa inakaribia kumleta beki wa kushoto wa timu ya Taifa ya Senegal na klabu ya Teungueth, Cheikh Sidibe (24) ili kuziba pengo la Bruce Kangwa aliye mbioni kuachwa.

    Awali iliripotiwa kuwepo kwa mvutano wa maamuzi kwa viongozi wa timu hiyo juu ya mustakali wa Kangwa ambaye umri wa miaka 34 unaonekana kutumpa mkono, upo upande ambao wanataka aendelee kuwa kikosini huku mwingine ukitaka aondoke.

    Kwa mujibu wa taarifa za ndani inaelezwa kati ya majina ambayo yapo mezani na yanatazamwa kama mbadala sahihi wa Mzimbabwe huyo ni Sidine ambaye katika fainali za CHAN  pale Algeria alifanya vizuri na kuwaongoza Senegal kutwaa taji kisha kuingia kikosi Bora cha michuano hiyo.

    Kushindwa kwa wachezaji wa ndani kufua dafu mbele ya Kangwa, kumewafanya Azam kufanya mazungumzo na Msenegal huyo na tayari ameonyesha nia ya kujiunga na matajiri hao ambao siku chache zilizopita walimtambulisha, Feisal Salum kuwa sehemu ya kikosi chao kwa ajili ya msimu ujao.

    Mmoja wa viongozi wa Azam (jina tumehifadhi) alithibitishia uwepo wa dili hilo kutokana na timu hiyo kuwa na mpango wa kuachana na Kangwa,”Ambacho watu hawajui ni kwamba tajiri (Yusuf) kwa sasa anataka kuona timu ikifanya vizuri kuanzia kwenye ligi ya ndani na Afrika ndio maana yupo mbele kwenye kila jambo,”

    “Baada ya fainali tegemeeni kuona wachezaji wengine wakubwa wakitambulishwa, wakubwa (viongozi) wamekuwa na vikao vingi hasa vikijikita kwenye namna ya kukiboresha kikosi kulingana na mapungufu ambayo yameonakana msimu huu,” alisema kiongozi huyo.

    Mbali na eneo la beki ya kushoto pia inaelezwa kuwa Azam inataka kuboresha upande wa kulia ambao ameonekana zaidi msimu huu kwenye michezo mikubwa na migumu, Lusajo Mwaikenda akicheza ambaye hiyo sio nafasi yake kiasili.

    Eneo lingine ambalo Azam FC itashusha kifaa ni ushambuliaji, wanataka kuleta mashine ya mabao ambayo itasaidiana na Price Dube, huku Feisal Salum ‘Fei Toto’ kutoka Yanga akiwa ameshasainiwa.

    Soma zaidi hapa kwa taarifa za usajili duniani.

    Azam azam complex azam fc bruce kangwa fei toto ligi kuu nbc tetesi za usajili usajili wa azam
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.