Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Al Ahly Na Maajabu Ya Jezi Namba 72 Kabla Ya Mechi
    Africa | CAF

    Al Ahly Na Maajabu Ya Jezi Namba 72 Kabla Ya Mechi

    Nazareth UpeteBy Nazareth UpeteMay 24, 2024Updated:July 26, 20242 Comments2 Mins Read5K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Wachezaji wa Al Ahly na jezi namba 72
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Bila shaka kila ukitazama mechi za Al Ahly kwenye warmup huwa unaona wachezaji wote wamevaa jezi namba 72. Unajua maana yake!? twende sawa.

    Februari Mosi, 2012 kulitokea tukio baya zaidi kwenye historia ya mpira wa Misri pale mashabiki wa Al Masry walipoingia na mapanga, visu, mawe, vilipuka na chupa waliwashambulia mashabiki wa Al Ahly na kuwadhuru.

    Kiasi cha mashabiki 72 wa Al Ahly waliuawa, Polisi 1 na shabiki mmoja wa Al Masry kwenye machafuko hayo huku mashabiki zaidi ya 500 wakijeruhiwa baada ya mashabiki wa Al Masry pale Port Said kuvamia majukwaa na eneo la kuchezea.

    Vifo vingi vilisababishwa na Polisi kukataa kufungua mageti ya uwanja ili mashabiki wanaojinusuru kutoka uwanjani wapite na hali hiyo ya machafuko ilidumu mpaka February 11 na siku 2 baadae ilikoma.

    Siku 2 kabla ya mechi iliachiwa video kwenye You Tube ya mashabiki maarufu wa Al Masry wanaofahamika kama “Ultras Green Eagles” wakitahadharisha kuwa shabiki yoyote wa Ahly atakayeenda uwanjani atauawa na hakukuwa na utani katika hilo.

    Siku ya tukio mabasi mengi ya mashabiki wa Ahly kutoka Cairo yalikataa kwenda Port Said kwa hofu ya usalama na mashabiki wakasafiri kwa treni kutoka Cairo na kufikia umbali wa dakika 15 kutoka Port Said wakisindikizwa na Polisi.

    Mchezo ulichelewa kuanza kwa dakika 30 kutokana na mashabiki wa Al Masry kuingia uwanjani na baada ya kushinda goli 3 waliingia uwanjani wakirusha chupa na visu kwa wachezaji wa Al Ahly ambao walikimbilia vyumbani kwa usaidizi mkali wa Polisi.

    Balaa likahamia kwa mashabiki wa Ahly ambapo uzembe wa Polisi ukasababisha mauaji hayo ya kutisha. Waliwatoa baadhi ya majeruhi kwenye ambulance na kuwaua kikatili mno.

    Kocha wa Ahly Manuel Jose alishambuliwa na shabiki aliyepenya chumbani na baada ya tukio hilo baya kabisa maStaa Mohammed Aboutrika, Mohammed Barakat na Emad Moteab waliamua kustaafu soka.

    Ligi ilisimamishwa na msimu kufutwa, kocha Manuel aliamua kuondoka haraka Misri na baadhi ya watu kadhaa walihukumiwa adhabu za kifo na jela.

    Kwa Al Ahly shabiki ana thamani kubwa na katika kuenzi hilo mpaka sasa huvaa jezi namba 72 kwenye Warm up.

    SOMA ZAIDI: Simba Na Yanga Mmejifunza Nini Ligi Ya Mabingwa?

     

    Al Ahly jezi namba 72 ahly

    2 Comments

    1. Pingback: Kufuzu AFCON 2025 Makundi Yatapangwa Kwa Vigezo Hivi

    2. Rau B on January 1, 2025 12:01 pm

      Jukwaa na connection Za michezo

      Ingia ⤵

      https://whatsapp.com/channel/0029VanxLVYJ93wbHawAAh3H/819

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.