Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Afrika Kusini vs DR Congo Wachezaji Hawa Ni Balaa
    Africa | CAF

    Afrika Kusini vs DR Congo Wachezaji Hawa Ni Balaa

    Living ShayoBy Living ShayoFebruary 10, 2024No Comments3 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    South Africa vs DR Congo
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Leo ni ile siku ambayo bila shaka waafrika kusini na wakongo watakua makini kabisa bila kusahau mashabiki wa soka barani Afrika kutazama mtanange wa kutafuta mshindi wa 3 wa michuano ya mataifa barani Afrika ambapo South Africa anakutana na DR Congo.

    Ni mchezo ambao unawakutanisha wachezaji wenye vipaji vikubwa sana barani Afrika ambao wanacheza nje ya bara hili lakini pia wale ambao wanacheza soka ndani ya bara hili na hapa tutazame wachezaji ambao unapaswa kuwaangalia kwa jicho la tatu kabisa katika mchezo huu.

    Taboho Mokoena

    Huyu ni kiungo mshambuliaji wa South Africa ambaye amekuwa na mashindano bora ya AFCON na amekuwa mhimili mkubwa kwa taifa ilo kwenye michuano ya msimu huu.Amekuwa akitekeleza majukumu yake mama ya kushambulia ila amekuwa pia akisaidia kukaba, amecheza michezo yote ya AFCON mpaka sasa akiwa amefunga goli 2 na kutengeneza moja, ni moja ya mchezaji wa kuangaliwa kwenye mchezo wa mshindi wa tatu na anavaa jezi namba 4.

    Aubrey Modiba

    Ni kiungo mkabaji wa timu ya taifa ya Afrika Kusini amekuwa akifanya kazi kubwa sana ya kukaba anavaa jezi namba 6 mgongoni. Ni mhimili wa Afrika Kusini kwenye eneo la kiungo mkabaji anakaba kisawasawa na amecheza michezo yote 6 kuonyesha umuhimu wake kikosini, mpe jicho lako kwenye mchezo wa mshindi wa tatu.

    Khuliso Mudau

    Ana miaka 28 anacheza kama beki wa pembeni na wakati mwingine kama kiungo amekuwa akipanda na kushuka kusaidia mashambulizi pamoja na kukaba wakati wakiwa wanashambuliwa. Anavaa jezi namba 20 mgongoni akiwa na kikosi cha Bafana Bafana, mpe umakini wako kwenye mchezo wa leo dhidi ya DR Congo.

    Meshack Elia

    Mshambuliaji wa DR Congo amekuwa sehemu muhimu ya kikosi cha timu hiyo kuanzia michezo ya awali, hatua ya makundi alikuwa akitumika zaidi kipindi cha pili ila kuanzia 16 bora amekuwa akianza kwenye kikosi cha kwanza. Mpaka sasa amechangia magoli 2 akitengeneza pasi ya goli 1 na amefunga goli 1 amekuwa wa kuchangia zaidi mashambulizi kuliko kuzuia ni hatari sana kuanzia eneo la katikati mwa uwanja kuelekea kwenye nusu ya mpinzani, ni moja ya mchezaji wa kuchungwa dhidi ya South Afrika anavaa jezi namba 13.

    Yoanne Wissa

    Ni kiungo mshambuliaji wa DR Congo anavaa jezi namba 20 mgongoni ana miaka 27 akiwa amehusika kwenye magoli 2 na mchango huo amefunga magoli 2. Ni moja ya winga wa kuchungwa na amekuwa winga ambaye anatokea pembeni kuingia ndani ya eneo la mpinzani.

    Arthur Masuaku

    Ni beki wa pembeni wa DR Congo ila ni wa kuchungwa sana kwani mpaka sasa amefunga goli 1 kwenye AFCON. Ni beki ambaye anapanda na kushuka akisaidia majukumu yote mawili kukaba kama jukumu lake mama la eneo analocheza pamoja na kupandisha mashambulizi, ana vaa jezi namba 26 mpe jicho lako kwenye mchezo wa mshindi wa tatu dhidi ya South Afrika “Bafana Bafana”.

    SOMA ZAIDI: Ukiizungumzia Nusu Fainali AFCON Huwezi Yaacha Majina Haya

    dr congo afcon south africa
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.