Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Raja Mkae kwa Kutulia, Kazi Mnayo, Hii Ndio Sapraizi ya Simba SC
    Africa | CAF

    Raja Mkae kwa Kutulia, Kazi Mnayo, Hii Ndio Sapraizi ya Simba SC

    David MohamedBy David MohamedMarch 25, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Simba SC imerejea mazoezini kuanza kujifua kwa ajili ya mechi ya mwisho ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika ugenini Morocco dhidi ya Raja Casablanca, itakayopigwa April Mosi jijini Casablanca, huku wana Msimbazi hao wakiwa na mpango wa kuwalipa kisasi waarabu hao nyumbani kwao.

    Raja ndio kinara kwenye Kundi C ikiwa na pointi 13, huku Simba ikiwa nafasi ya pili ikikusanya pointi tisa na zote zikiwa zimeshafuzu robo fainali ya michuano hiyo na mechi hiyo ya mwisho ya kufungia hesabu itakuwa ni ya kutafuta heshima ikizingatiwa mchezo wa awali Simba SC walipoteza kwa goli 3-0.

    Kwa kuitambua umuhimu na mechi yenye heshima na ya kulipa kisasi kutokana na kipigo hicho kikubwa ilichopewa timu yake nyumbani, Kocha Mkuu wa Simba Roberto Oliveira ‘Robertinho’ alieleza kuwa ameandaa mkakati tofauti wa kucheza mechi na Raja Casablanca kutokana na wachezaji wake wengi wa kikosi cha kwanza kuwa kwenye majukumu ya timu zao za taifa kwa sasa.

    Wachezaji hao walio katika majukumu ya Timu ya taifa ni Makipa Aishi Manula na Beno Kakolanya, kiungo Mzamiru Yassin (Tanzania), Clatous Chota Chama (Zambia), Henock Inonga (DR Congo), Peter Banda (Malawi), Pape Sakho (Senegal) na Saido Ntibazonkiza (Burundi).

    Robertinho aliongeza na kusema kuwa mechi ya marudiano itakuwa tofauti kidogo, watacheza kimkakati na kuhakikisha wanapata matokeo mazuri licha ya ugumu uliopo na pia kutakuwa na mabadiliko kwenye kikosi, na kuwa timu ina wachezaji wengi na watapata nafasi ya kufanya vizuri kwenye mchezo huo.

    Robertinho alisema moja ya sapraizi aliyowaandalia Raja ni kuwatumia zaidi wachezaji ambao hawatumiki mara kwa mara, huku akiwataja Kennedy Juma, Erasto Nyoni kuwatumia katika pambano hilo la kukamilisha ratiba ya makundi ya michuano hiyo ya CAF.

    Kurejea kwa Hassan Dilunga ni faraja kwa Kocha Robertinho, na kusema kuwa anaendelea kumuangalia zaidi mchezaji huyo licha ya kutokuwepo kwenye usajili na kuongeza kuwa anahitaji muda zaidi ili kufanya tathmini iliyo bora na mwisho wa siku kukamilisha ripoti yote ya kikosi na mahitaji katika uongozi wa Simba SC kwa ajili ya msimu ujao.

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.