Ilipoishiaย
Kupitia daraja la Kigamboni, Mzee Shayo aliendesha Subaruย kama yupo kwenye mbio za Magari, wakati huo Barabara zilikuwaย nyeupe, Watu wengi waliogopa kupoteza uhai wao, walibakiaย majumbani mwao huku wachache wakiendelea kufanya safari,ย ilimuwezesha Mzee Shayo kufika Ikulu ya Magogoni haraka sana,ย alikuta ulinzi umeimarishwa hapo lakini alipowatazama Walinziย hao alijikuta akikata tamaa, aliona ni ngumu sana kupambanaย na huyo Mwanaume anayeitwa Chogo. Endelea
SEHEMU YA PILI
Aliuliza mahali ambapo Rais wa Nchi alikuwa amehifadhiwa kwaย ajili ya usalama, ilikuwa ni ndani ya chumba kimoja ambachoย kilikuwa na milango ya umeme, chumba hicho kilipatikanaย katikati ya jengo la Ikulu.ย
Rais akiwa na waziri Mkuu ndani ya chumba hicho walimuonaย Mzee Shayo akiingia huku sura yake ikionesha kukosa tumaini,ย Rais alimdaka Mzee Shayoย
“Shayo! Nini kinaendelea?” Aliuliza Rais huyo aliyeitwaย Martin Bingoย
“Ugaidi Mkuu” Alijibu kwa utii Mzee Shayoย
“Inakuwaje hadi ugaidi unaingia katika Nchi hii yenye amaniย kwa zaidi ya Miaka 60 sasa, nyie kama jicho la Taifa mkoย wapi?” Alihoji Rais akionekana kuchanganikiwaย
“Mkuu! Ugaidi huu unaratibiwa na Mtanzania, mkazi wa Jiji laย Arusha. Mara moja nitatuma timu kuhakikisha anafuatiliwaย mahali alipozaliwa na kupata taarifa zake, kuanzia hapoย tutajuwa tunapambana vipi kuhakikisha tunamdhibiti” Alisemaย Mzee Shayo, maneno yake yalikuwa kama dhihaka kwa Rais Martinย Bingo, alimtandika kofi Mzee Shayoย
“Tayali kambi la Lugalo lipo chini ya huyo Mtu na kundi lakeย la ESS, anateka kila sehemu nyeti ya Nchi hii, nimepataย taarifa pia kambi la Jeshi la Majimaji nalo lipo chini yake,ย Shayo uzembe wa aina yoyote utasababisha damu nyingiย kumwagika” Alisema kwa hasira huku akimkaripia Mzee Shayoย ambaye kiumri alikuwa Mkubwa kuliko Rais Martinย
“Mkuu! Naomba niende” alisema Mzee Shayoย
“Ndani ya masaa manne nipate majibu ya hili jambo Shayo,ย vinginevyo utahusishwa pia na Ugaidi huu” Alisema Rais, Mzeeย Shayo aligeuka na kuondoka Ikulu, alipoingia kwenye gari lakeย chozi lilimbubujika, alipiga usukani kisha aliondoa gari eneoย hilo.
Tuachane na habari za Kitengo na hasira za Rais Martin juu yaย uvamizi huu wa kutisha, Ndani ya Jiji la Nairobi, Uwanja waย ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyata kulikuwa na ujio waย Msichana mmoja mzuri sana, Mweupe. Alionekana kuwa makiniย sana pindi alipokanyaga ardhi hiyo, kutokana na Ugaidiย uliokuwa umetanda ndani ya Ardhi ya Tanzania, Ulinzi ulikuwaย imara sana ndani ya Uwanja huo, muda mchache baada ya ndegeย hiyo kutua Taifa la Kenya lilitangaza kusimamisha shughuliย zote za anga yaani hakuna ndege nyingine kuingia wala kutoka.ย
Msichana huyo alikaguliwa kisha aliambiwa avue miwani. “Unaitwa Faudhia?” Aliuliza mmoja wa Askari wa Ukaguziย
“Ndiyo!!” Alijibu Msichana huyo ambaye alifahamika kamaย Faudhia, askari alimtazama sana Faudhia kabla ya kumruhusuย aweze kuondoka Uwanjani hapo, Faudhia aliporuhusiwa baada yaย kuwa amekamirisha taratibu zote aliita Taxiย
“Nipeleke Nairobi Hotel” alisema Faudhiaย
“Nairobi Hotel, ni KSH 500” alisema dereva huyo ambayeย alikuwa ni Mwanamke, Faudhia alikuwa siti ya nyuma akamwambiaย
“Muhimu nifike hapo kwa wakati” alisema Faudhia huku Mwanamkeย huyo akiondoa gari lake katika eneo hilo.ย
“Unaonekana upo makini sana, nini kimekuleta hapa Kenya?”ย Aliuliza Mdada huyo ambaye sura yake haikupata kuonekana kwaย Faudhia, lilikuwa ni swali la mtego ambalo Faudhia alilikwepaย haraka sanaย
“Hiyo Hotel ina huduma zote muhimu ee? Nimepata sifa zake”ย Alisema Faudhiaย
“Kenya hakuna Hotel hoi hai, hiyo uliyoitaja ndiyo Hoteliย bora sana hapa Nairobi” Alijibu Mdada huyo ambaye hakupataย kutambulika alikuwa anaitwa nani, hakumuuliza tena kituย kingine Faudhia hadi pale walipofika katika Hoteli ya Nairobiย ambayo ilikuwa mbali kutokea ulipo Uwanja wa Jomo Kenyata.ย
“Here we goo ( tumeshafika ) ” alisema Mdada huyo huku akiwaย amesimamisha gari mbele ya Hoteli hiyo ambayo kwa muda huoย ilikuwa imefungwa kutokana na tahadhali ambazo Taifa la Kenyaย liliamuwa kuchukua.ย
Yule Mdada aliondoka zake, Faudhia alilitazama Tax hadiย lilipozama kisha alisogea getini akatoa kitambulisho maalumย kuwa alishafanya booking ya Chumba Hoteli hiyo, alikaguliwaย na kuruhusiwa kuingia Hotelini.
Akiwa ndani ya chumba chake alipokea simu ya Mtuย aliyemkusudia ndani ya Hoteli hiyo, jamaa huyo aliitwa Khalidย Bangala, alikuwa dalali maarufu sana ndani ya ukanda waย Afrika Mashariki, alikuwa ni miongoni mwa wachache ambaoย walikuwa wakiwindwa sana na Serikali zote kutokana naย Biashara yake ya kusafirisha mizigo, na biashara haramu yaย usafirishaji wa Binadamu wakiwemo wana mgambo wa kundi laย Kigaidi la ESS ambalo lipo Tanzania.ย
Haraka Faudhia alimfungulia mlango jamaa huyo ambaye alikujaย na Watu watatu ndani ya Chumba hichoย
“Mna uhakika nitaingia Tanzania Kabla ya mipaka kufungwa?”ย Aliuliza Faudhia akiwa makini kumtazama Khalid Bangala, jamaaย huyo alicheka kisha akajibu kwa kujimwambafaiย
“Itakuwa ni Biashara yangu ya kwanza kukwama kwenye maishaย yangu, sijawahi kukwamisha biashara yangu” Alisema kishaย Faudhia alishusha pumzi zake, ilikuwa ni majira ya jioni.ย
“Ulisema ni kiasi gani?” Aliuliza Faudhia baada yaย kuhakikishiwa kuwa angesafiri kutoka Kenya hadi Tanzania bilaย tatizo lolote lileย
“Milioni 10 za Kitanzania, hali si shwari huko mpakani,ย Watanzania walio jirani wanakinzana na askari kuihama Nchi”ย Alisema Khalid Bangalaย
“Sawa, nitalipa hiyo fedha yote nikifika Tanzania” Alisemaย Faudhia, Khalid Bangala alimsogelea na kumuuliza kwaย kumdadisiย
“Nchi ambayo Watu wanaanza kuikimbia wewe unatoa Milioni 10ย kuingia huko, una ajenda gani?” Alihoji Khalid Bangalaย
“Nafikiri tuifanye Biashara yetu kwanza Bosi” Alijibu Faudhiaย
“Haya! Utalazimika kuingia ndani ya Sanduku” alisema Khalidย Bangalaย
“Una maanisha Jeneza? Nasafiri nikiwa mfu?” Alihoji Faudhiaย
“Hapana!! Tunachokifanya kitakusaidia kuingia Tanzania,ย vinginevyo itakuwa ngumu kwako” Ilikuwa ni Mtihani mgumu kwaย Faudhia kukubali sharti hilo, haraka alikumbuka jambo fulaniย
Kilichomtoa Mexico kilikuwa ni simu ya dharura kutoka kwaย Mkuu Wa kitengo cha Usalama wa Taifa Mzee Shayo juu ya Ugaidiย Nchini Tanzania. Alishusha pumzi zake akasema
“Safari itaanza saa ngapi?”ย
“Sasa hivi” Alisema Khalid Bangala, mara moja vijana wakeย waliingiza sanduku ndani ya Hoteli hiyo kupitia Mlango waย nyuma wakiwa na mavazi ya waangalizi wa maiti kuhakikishaย Faudhia anaingia Tanzania, jeneza hilo lilikuwa na matunduย ย
madogo madogo ya kuhakikisha hewa inaingia humo ndani.ย
Faudhia aliingia ndani ya sanduku akiwa na kibegi chakeย kidogo sana, safari ilianza. Walipofika nje ya Hoteli Khalidย aliwatakia vijana wake safari njema, mara moja sandukuย liliingizwa ndani ya gari aina ya Toyota Landcruiser yenyeย nembo ya Hospitali ya Nairobi. Safari ilianza ya kuutafutaย mpaka wa Namanga ambapo Faudhia ataachwa hapoย
Gari hiyo ilianza safari kwa mwendo wa taratibu ili kutokaย Mjini, ilikuwa ni safari ya hatari sana lakini kwa Khalidย Bangala na vijana wake ilikuwa ni kazi waliyoizoea, gari hiloย lilitambuliwa kama gari ya kubeba maiti zinazoenda masafa yaย mbali. Walipofika kwenye kizuizi cha kutoka na kuingiaย Nairobi, polisi walianza kulikagua gari hilo ilaย walipojiridhisha kuwa gari hilo lilikuwa na maiti walilipaย ruhusa ya kuendelea na safari.ย
Safari ilikuwa ndefu sana iliyogubikwa na giza, usikuย uliingia huku wakizidi kukata miji na vijiji kuutafuta Mpakaย wa Namanga ambao ulikuwa ndio mpaka salama hadi kufikia mudaย huo, mara kadhaa Faudhia akiwa ndani ya Sanduku hiloย aliwasiliana na Mzee Shayo kutoka kitengo kwa njia ya ujumbeย mfupi wa simu, alimueleza nini anatakiwa kufanya, alitakiwaย kuelekea Kwenye pori dogo lililopo wilaya ya Longido, hapoย atakutana na gari kisha ataelekea Jijini Arusha kwa ajili yaย kuanza safari ya kuelekea Dar.ย
Miji mingi ilianza kutekwa na Magaidi hao wa kundi la ESSย pasipo kuwekwa wazi sababu ya wao kufanya hivyo hukuย ikifahamika wazi kuwa anayekiongoza kikundi hicho anafahamikaย kama Martin Gimbo maarufu kama Chogo.ย
“Ukifika Arusha utapewa kazi ya kufanya huko kwa muda fulani”ย Ulikuwa ni ujumbe wa mwisho wa Mzee Shayo, kazi hii ilikuwaย ndiyo kazi ya Kwanza kwa Faudhia baada ya kuhitimu mafunzoย huko Mexico, akiwa ndani ya sanduku alitoa picha ya rafikiย yake aliyeitwa Diana ambaye naye alihusishwa katika ugaidiย huo, alikumbuka maisha ya nyuma walipokuwa wakisoma woteย shule ya Majengo huko Mkoani Mbeya, roho ilimuuma sana lakiniย lilikuwa ndiyo jukumu lake. Aliiweka picha hiyo mfukoni kishaย alipaza sauti akawauliza vijana wa Khalidi Bangalaย
“Tupo wapi?” Aliuliza huku akigonga sanduku hilo
“Tupo Kilomita chache kufika” Alisema mmoja wa vijana hao,ย masaa yalizidi kukimbia usiku ulizidi kuwa mwingi sana,ย Faudhia aliamua kujipumzisha kidogo.ย
Tuachane na safari ya Faudhia, ndani ya Jiji la Nairobi,ย baada ya kupata kazi itakayo muingizia fedha nyingi Khalidย Bangala. Alikuwa amejipumzisha kwenye moja ya Hoteli, ghaflaย simu yake iliingia ujumbe mfupi, aliichukua simu na kuanzaย kuusomaย
“Khalid, najuwa una msafirisha Mwanamke kuelekea Tanzania,ย mnapitia mpaka upi? Namuhitaji huyo Mwanamke” Khalid Bangalaย baada ya kuusoma ujumbe huo alijawa na mshangao ni naniย alikuwa amemtumia ujumbe huo na alijuwaje kuwa usiku huoย alikuwa akimsafirisha mwanamke kuelekea Tanzania, alibonyezaย kitufe cha kupiga kisha akapiga simu kwenye namba hiyoย
“Khalid” ilisikika sauti ya kiumeย
“Nani wewe na umejuwaje?” Aliuliza kwa umakini sana Khalidย Bangala kisha alishusha pumzi zakeย
“Kwasasa siyo muhimu sana kunifahamu, itabidi uchague kimoja,ย kunipatia msichana nikulipe mara mbili au kunipa Kichwaย chako” Ilisikika tena sauti ya Mwanaume huyo na kumfanyaย Khalid aone jambo hilo lilikuwa siriazi kiasi gani, alikaaย kimya bila kutoa jibu loloteย
“Kuna kiasi kikubwa cha fedha kwenye gari yako hapo chini,ย chukua kisha niambie Msichana anapitia Mpaka upi” Alisemaย tena Mwanaume huyo kisha simu ilikatika, haraka Khalidiย alishuka chini ya Hoteli mahali ambapo gari lake lilikuwaย limesimama, alifungua mlango wa mbele hakuona kitu, akafunguaย mlango wa nyuma ndipo alipokutana n begi dogo, alipolifunguaย begi hilo lilikuwa limejaa noti nyingi, alijikuta akitabasamuย Khalid Bangala kwasababu atakuwa ameingiza kiasi kikubwa chaย fedha, alitoa simu mfukoni kisha alimpigia huyo Mwanaumeย asiye mfahamuย
“Mpaka wa Namanga, baada ya masaa mawili watakuwa hapo”ย Alisema Khalid kisha simu ilikatwa na Mwanaume huyo bila hataย kujibu chochote, fedha zilimuacha Khalid Bangala akiwa mwenyeย tabasamu zito sana, alijulikana kuwa ni mpenda pesa ndioย maana alikuwa akifanya kazi za kuhatarisha maisha yake ili tuย apate pesa.ย
Akiwa anaendelea kutabasamu na kufurahi ghafla alihisi ujioย wa Mtu nyuma yake, alipogeuka tu alikutana na risasi mojaย kichwani, Habari za Khalid Bangala ziliishia hapo, aliyempiga risasi Khalid alikuwa ni mwanamke mmoja aliyefunga nyweleย zake vizuri, alikuwa ndani ya Koti jeusi na suruali nyeusi,ย Huwezi amini Mwanamke huyo ndiye aliyemuendesha Faudhiaย kutoka Uwanja wa ndege hadi Hotelini, alikuwa ni Diana rafikiย wa zamani wa Faudhia, alikuwa ametumwa kuchukua pesa ambazoย waliziweka ndani ya gari ya Khalid Bangalaย
“Kazi imeisha!” Alisema Diana kwa njia ya simuย
“Waoo Good Girl ( Vizuri Msichana mzuri ) ” ilisikika sautiย nzito ya kizeeย
“Rudi Tanzania” Alimalizia kusema Mwanaume huyo kwa njia yaย simu, simu hiyo ilikatika, tayali polisi walishafika nje yaย Hoteli hiyo, Diana alichofanya ni kuingia kwenye chemba yaย maji machafu akaenda kutokea mbali na eneo hilo.ย ย
Nini Kitaendelea USIKOSE SEHEMU YA TATU
JIUNGE NA KIJIWENI WHATSAPP CHANNEL Kwa Kugusa Hapaย
Soma Riwaya Nyingine Za Kijiweni Kwa KUGUSA HAPA
Wewe kama MFANYABIASHARA.. Kuna wakati unatamani kuwafikia watu wengi zaidi na hujui wapi pa kuanzia , USIJALI kwani hapa ndipo ambapo MTAA UNAONGEA na tuko tayari kukusaidia kuwafikia watu wengi kwa BEI YA OFA
Njoo Utangaze Nasi Sasa Kwa Kutuambia Una TANGAZO Gani na unataka kutangaza kwa muda gani kwa kutuma ujumbe hapa WwhatsApp Kupitia Namba +255760871896ย
16 Comments
Hatar sana
Next plz
Iko poa xnaa
Huyo Diana na faudhia wapo upande wa serikali au magaidi๐คท๐ฝโโ๏ธ๐คท๐ฝโโ๏ธ๐ฅฑ๐ฅฑ๐ฅฑ
Faudhia ndo star wa picha
Nzuri
https://shorturl.fm/N6nl1
https://shorturl.fm/a0B2m
https://shorturl.fm/9fnIC
https://shorturl.fm/6539m
https://shorturl.fm/68Y8V
https://shorturl.fm/j3kEj
https://shorturl.fm/hevfE
https://shorturl.fm/fSv4z
https://shorturl.fm/xlGWd
https://shorturl.fm/LdPUr