Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 12

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua (01)
    Hadithi

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua (01)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaJanuary 3, 2025Updated:January 6, 202522 Comments10 Mins Read9K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Sijui kwako ndoa ina maana gani lakini kwangu Mimi ndoa ilinipotezea Muda wangu, iliniacha naย  Maumivu na kilema cha Maisha yangu.ย 

    Sikuwahi kuwaza chochote kuhusu ndoa wala kuitamani, lakini siku moja nilikua natoka sokoniย  Mabibo naelekea nyumbani Magomeni Usalama, niliposhuka kwenye daladala kwa bahatiย  mbaya niliteleza na kuanguka wakati navuka barabara. Mfuko wenye vitu nilivyonunua sokoniย  uliangukia pembeni.ย 

    Nilihisi aibu sana siku ile na kibaya zaidi mvua ilikua imenyesha majira ya asubuhi, lilijaa topeย  lililoniharibia Baibui langu. Eneo nililoangukia palikua na kijiwe cha Bodaboda. Kamaย  uwajuavyo walianza kushangilia anguko langu kitu kilichozidi kunipa hasira lakini sikuwa na laย  kufanya zaidi ya kujiokotanisha pale.ย 

    โ€œPole sana Dadaโ€ niliisikia sauti hii nikiwa nasimama, aliyenipa pole alinipatia na mfuko wanguย  akiwa ameokotanisha vitu vyangu. Alikua kijana mzuri mtanashati sana, nilijikuta nikiwa naย  kigugumizi kumjibuย 

    โ€œUnaelekea wapi?โ€ย ย 

    โ€œNyuma ya sheli, usijaliโ€ nilisema nikiwa najipangusa tope kutoka kwenye Baibui langu jeusi,ย  akanipa mkono wakeย 

    โ€œNaitwa Salehe Mwinyimkuuโ€ Alijitambulisha kwangu, nilimtazama kwa sekunde kadhaa kishaย  nilimjibuย 

    โ€œNaitwa Saidaโ€ย 

    โ€œNimefurahi kukufahamu, wacha nikusogezeโ€ alisema, kwa msaada alionipa isingelikuwa hisaniย  kukataa alichokiomba. Taratibu tuliikanyaga ardhi kuelekea karibu na nyumbani kwetu. Kwaย  muda mchache nilihisi kumjua kidogo, niligundua ni mpole, mwemye hekima na busara teleย  licha ya kuniambia ana Miaka 27 tu.ย 

    โ€œMimi nina Miaka 23โ€ nilijitanbulisha kwake huku nikianza kunogewa na mazungumzo yake.ย  Tuliongea mengi hadi kubadilishana namba za simu kitu ambacho sikuwahi kukifanya kwa Mtuย  nisiyemjua.

    Tulizidi kuwasiliana kwa zaidi ya mwezi mzima huku tukiwa marafiki wa kawaida tu lakiniย  baadaye Salehe alinitongoza.ย ย 

    Nisiwe mwongo wala mnafiki hata kabla ya kunitongoza nilianza kumpenda hivyo kunitongozaย  alikua anatimiza wajibu wake kama Mwanaume kwani nisingeliweza kumwambia Nampendaย  isitoshe Mimi nilikua Bikra kwa wakati ule.ย ย 

    Tulianza mahusiano ya Kimapenzi lakini nilimwambia Salehe kuwa Mimi nimelelewa kwenyeย  familia ya Dini sana, Baba yangu ni msaidizi wa Shekh Mkuu wa Msikiti wa Magomeni hivyoย  kama ananipenda kweli basi awaone wazazi wangu kwanza. Sijui tuseme alikua na kiu sana auย  alikua anahitaji Mke sana maana alilifanya hilo siku tatu tu baada ya kumwambiaย 

    Baba yangu alifurahi sana, Mama pia alifurahi zaidi akaniambiaย 

    โ€œMwanangu ndoa ni Nusu ya Dini, sisi Wazazi wako tunakutakia kila lililo jema, Munguย  akuongozeโ€ Daima Mama yangu alikua Mtu wa karibu sana kwangu, alisimama na Mimiย  kwenye kila jambo hata ambalo Baba yangu alipingana na Mimi.ย 

    Salehe hakutaka kuchelewesha alilipa Mahali siku iliyofuata.ย 

    โ€œWewe Kijana ni Mtu wa wapi?โ€ Baba alimuuliza Salehe wakiwa katika mazungumzo yaย  kawaida, kama Mzazi ni lazima ahakikishe usalama wa Binti yakeย 

    โ€œKwetu Rukwa lakini nipo Hapa Dar Likizoโ€ alisema Saleheย 

    โ€œOoh! Unajishughulisha na nini?โ€ย 

    โ€œNimeajiliwa, Mwalimu wa Shule ya Msingi Rukwa Mjiniโ€ย 

    โ€œUtamtunza Binti yangu?โ€ย 

    Kwanza Salehe alicheka kidogo kisha akamwambia Babaย 

    โ€œNisipomtunza Mke wangu nitamtunza Nani, wanasema Mbuzi unayemlisha ndiye utakaye mkamua maziwaโ€ Basi Baba na Salehe wakaishia kuangua vicheko, ilileta raha sana.ย ย 

    **ย 

    Ndugu wa Salehe walifika tena waliazimia kuwa ndoa ipite kabla likizo ya Salehe haijaisha iliย  tuondoke wote kuelekea Rukwa, sikuwahi kufikiria kuwa siku moja nitaolewa na kwenda mbaliย  kama Rukwa. Kidogo nilipata huzuni, nilimzoea Mama yanguย 

    โ€œUsijali, hata Mimi niliwaacha Wazazi wangu Morogoro nikaja kuishi na Baba yako Saida. Umriย  ukifika hakuna la kukuzuia kuanzisha Familia yakoโ€ Mama yangu hakuacha kunitia Moyo. Babaย  aliachia tabasamu maana tulikuwa wote sebleni

    โ€œNgoja niwaache muongee maongezi yenu ya kikeโ€ alisema Baba akaelekea zake Msikitini,ย  zilipita siku kadhaa hadi siku ya ndoa ilipowadia. Ndoa ilipita salama, Siku ya pili tulianza safariย  ya kuelekea Rukwa Mimi na Mume wangu Salehe.ย ย 

    Bado nilikua Bikra wala hakunigusa usiku wa kwanza wa ndoa yetu hotelini kabla ya Kuanzaย  safari, kwakua nami nikikua mgeni wala sikudai chochote kile. Tulifika Rukwa Usiku sana tenaย  nikiwa ninasinzia, tulichukua Taxi hadi nyumbani kwa Saleheย 

    โ€œKaribu nyumbani Mke wangu, jisikie uko nyumbani kabisa na hapa ndipo tutakapoishiโ€ alisemaย  tukiwa tunashuka kwenye taxi, tulisimama mbele ya nyumba moja iliyo giza sana, sikushangaaย  sababu mwenye nyumba hakuwepo kwa muda mrefu. Nilijiegemeza kwenye bega la Saleheย  nikamwambiaย 

    โ€œMume wangu, ulipo nipo na nitaendelea kuwepo siku zoteโ€ lile Taxi liliondoka, kazi yaย  kuhamishia mabegi ndani ilianza. Salehe alikua ametangulia nami nilibakia nyuma nikikokotaย  begi. Sijui ni mawazo yangu au nilisikia kitu halisi kabisa, nilisikia sauti za Watoto wakiombaย  Msaadaย 

    โ€œSubhannahโ€ผโ€ nilishtuka, sikuisikia tena ile sauti maana mwanzo ilitokea ndani ya ile nyumbaย  ambayo tulikua tukielekea. Mapigo ya moyo yalinienda mbio, niliposikiliza vizuri walaย  sikuzisikia tena nikajua ni fikra zangu tu. Basi niliendeelea kuvuta begi hadi ndani, taaย  zikawashwaย 

    Palikua kimya sana, uzuri sikua na njaa wala hamu ya kula zaidi ya Kulala kutokana na Uchovuย  wa safari. Nilisimama kusuburia Salehe anioneshe chumba chetu, akaufunga mlango kishaย  akaniongoza hadi chumbani, nilipofika nilijitupa Kitandani na kujilaza kama pono bila kujaliย  kuwa kitandani palikua vumbi tupu.ย 

    Nililala Usingizi wa nusu kifo hadi mapambazuko, sauti ya jogoo kuwika niliisikia ikiniamsha naย  kuniambia ni muda muafaka wa kuanza majukumu ya nyumbani. Macho yalijawa na Ukunguย  usio kifani, nilijinyoosha kama Kinda la ndege halafu nikajikuta nikipigwa na Butwaa zito sanaย  ambalo kiukweli nilishangazwa mno na nilichokionaย 

    โ€œNipo wapi hapa?โ€ Nilijiuliza swali hili, niliipapasa akili yangu inikumbushe jambo lakiniย  haikua tayari kufanya hivyo, Salehe hakuwepo Kitandani. Moyo ulinienda hali Jojo,ย  nilinyanyuka taratibu kutoka kitandani.ย 

    Nitakueleza kwanini nilipigwa na Butwaa la ajabu, kwanza harufu ya Udi wenye harufu mbayaย  ilizagaa kote ndani, pili nilisikia sauti ya Mtu akitwanga na kwa hakika alikua akitwangia ndaniย  halafu sauti ya Mtoto Mchanga anayelia nilizidi kuisikia. Taratibu nilitaka kujuwa nipo wapiย  haswa maana tayari nilianza kupata hofu fulaniย 

    Nilipiga hatua za taratibu hadi mlango wa kutokea chumbani, ile sauti ilitoweka na palikuaย  kimya sana. Moyo wangu haukutulia kabisa licha ya ukimya wa ghafla niliousikia, jua lilikuaย  tayari limeshatoka

    Nyumba ilikua safi sana. Ilikua na korido ndefu yenye vyumba kadhaa japo kwa wakati huoย  sikuhesabu kutokana na hali niliyokua nikiihisi. Basi Mimi Saida nilijiulizaย 

    โ€œAh ni mawazo gani haya Jamani, Ewee Allah niepushie Mbaliโ€ nilisema kisha nilirudiย  Chumbani kutafuta simu yangu nimpigie Salehe aniambie alipo si unajua maisha ya Ugeni yanavyoanza. Nilikumbuka mara ya mwisho simu niliiweka kwenye mkoba wanguย 

    Sikuwa na shaka sana kuhusu simu yangu, niliikuta lakini kwa bahati mbaya ilikua imeisha chaji.ย  Niliketi kitandani nikiwaza mambo kadhaa lakini niliona ni bora niweke simu chaji niwasilianeย  na Saleheย 

    Nilipomaliza kuweka chaji na kuhakikisha simu yangu inaingia chaji nilipata nafasi yaย  kukiangalia kwa uzuri chumba, kilipangwa vizuri sana hadi nilijikuta nikitabasamu, nilijuwa niย  Mume wangu Salehe alikua ameamka mapema na kuweka mazingira sawa. Nilijiona ni mwenyeย  Bahati sana kuitwa Mke wa Salehe, nilikua na nguo zangu zilezile nilizokuja nazo hivyo wazo laย  kubadilisha nguo lilinijia lakini kabla ya kufanya hivyo nilisikia Mlango wa nje ukigongwa.ย 

    Sikujua naanzia wapi kuitikia wito huo, nilisogea hadi mlango wa chumba na kusikiliza vizuri.ย  Mgongaji wa mlango alikua ni Mwanamke na sauti yake ilikua karibu sana hivyo kwa harakaย  niliamini anagonga mlango wa Nyumba ya Salehe. Hakuna aliyeitikia ile hodi hadi paleย  nilipoamuwa kumkaribisha nikiwa ndani tena kwa sauti ambayo aliisikia vizuri, nilijiangaliaย  kama nilikua nipo sawa kutoka ndani kisha nilianza safari mara moja kutembea kwenye koridoย  kuuelekea Mlangoni.ย 

    Niliufungua mlango wa kwanza kwa kutekenya kitasa tu kisha nikauelekea mlango wa Uwaniย  ambao ndio mgongaji alikua hapo, nilipoufungua nilikutana na Mama Mmoja aliyebeba tenga laย  mboga mboga kichwani, alikua ameshakata tamaa alikua akiondoka nikamwitaย 

    โ€œMamaaaโ€ผโ€ alipogeuka alirudi hadi Mlangoniย 

    โ€œShikamoo Mamaโ€ nilimsalimia kwa adabu, ndivyo nilivyofundishwa kwetu kwa wazazi wangu,ย  yule Mama alitabasamu kisha akaniulizaย 

    โ€œHauchukui Mboga leo?โ€ Nilitabasamu maana aliuliza kana kwamba alishawahi kuniuzia mbogaย  ila nilielewa Lugha ya Kibiashara huwa hivyo mara zoteย 

    โ€œMimi ni mgeni hapa Mama, labda kesho nikiwa nimeyafahamu vizuri mazingira nawezaย  kuchukua. Usiache kupitishaโ€ nilisema kisha yule Mama aliondoka huku akiitikiaย 

    โ€œNapita kila siku Mtaa huu, Wahiiii mboga mbogaโ€ alienda mbele zaidi kisha alitokomeaย  machoni pangu. Kuzungumza na yule Mama ni kama kulinisahaulisha kuhusu Salehe lakiniย  alipoondoka nilijiulizaย 

    โ€œSalehe ameenda wapi mbona hajaniaga?โ€ Niliufunga mlango kisha nilirudi ndani, Nyumbaย  ilikua kubwa ya Kisasa lakini ilikua kimya sana sikusikia hata sauti ya ndege kuruka. Uwaniย 

    palikua na sehemu ya kukaa nikaona ni bora nikae hapo kwanza nipate upepo, nilijikutaย  nikipitiwa na Usingizi wa ghafla tu.ย 

    Ndoto za hapa na pale zilinifuata usingizini na kunipa hekaheka hadi nikashtuka. Niliposhtukaย  nilikutana na sura mbili, moja ilikua ya Salehe na nyingine ni ya Mzee mmoja mweusi aliyevaliaย  Baraghashia nyeupe na kanzu nyeupe. Macho yao yalikua kwanguย 

    โ€œEeeh imekuaje umelala hapo Mke wangu?โ€ aliniuliza Salehe, nilijitabasamisha kidogo kamaย  Mtu anayezuga ili asinione kuwa mvivuย ย 

    โ€œHewa ya hapa inavutia, kaupepo nikajikuta nasinzia tuโ€ย 

    โ€œSawa, huyu ni Baba yangu anaitwa Mzee MwinyiMkuu. Ni Baba yangu Mzaziโ€ alisema Salehe,ย  nilimsalimia yule Mzee kwa heshima sana hata naye alifurahia na kuona ni namna gani ninaย  heshima.ย 

    โ€œMarhaba Mkwe wangu mzuri, hakika Mwanangu hakukoseaโ€™โ€™ akasema kwa Utani tukajikutaย  tukicheka kidogoย 

    โ€œSamahani, najua umenitafuta ila nilienda kumpokea Baba maana aliniambia nikirudi tu atakujaย  kwa ajili ya kukusalimia wewe Mke wanguโ€ alijielezea Salehe, ni kweli Mzee MwinyiMkuu alikuja na begi dogo la Mgongoni lililochakaa sana.ย ย 

    โ€œAaaah! Nimefurahi sana kumuona Baba yako Salehe, karibu Baba.โ€ Nilisema kisha nilisimamaย  na kulishika begi la Mzee MwinyiMkuu ambalo lilikua sakafuni, kabla sijaliinua yule Mzeeย  alinishika mkono kwa nguvu sana hadi nilishtuka, nikamtazama Usoni alikua amenikazia suraย  yakeย ย 

    โ€œHili begi halishikwi na kila Mtu, Salehe unajua pa kulipelekaโ€ alisema Mzee MwinyiMkuu,ย  nilihemwa maana sikutegemea lakini hata kama ningelichukua ningelipeleka wapi wakati naย  Mimi ni Mgeni pale. Nilishusha pumzi, kilinishuka nikarudi kukaa, Salehe akaniambiaย 

    โ€œMzoee Baba yangu ana utani sana Saida, wacha nikaweke begi lake nakujaโ€ Mara mojaย  alipomaliza kusema alinyanyuka Salehe na kuelekea ndani, yule Mzee hakuacha kunitazama kwaย  jicho kali kama vile kuna kitu nimeharibu hadi nilianza kumwogopa, ikanilazimu kumwombaย  Msamahaย 

    โ€œSamahani Baba sikujuaโ€ย 

    โ€œSiku nyingine uwe unauliza, umeelewa?โ€ย 

    โ€œNdiyo Babaโ€ Nilipomjibu alinikata jicho fulani la husda kisha akatoa mguno fulani wa kichekoย  cha dhihaka halafu akanyanyuka na kuiburuza kanzu yake akaingia zake ndani,nilishusha pumziย  zote kama Mgonjwa wa Pumu. Niliusikia moyo wangu namna ulivyoamka nakuanza kudundaย  tena, hata koo ilianza kupitisha mate kwa kasi. Yaani sijui nikueleze vipi unielewe namnaย  nilivyokua nimeshikwa na woga kupitiliza, sura ya yule Mzee niliyona imekaa kikatili sana

    Wakati naendelea kujiuliza mara Mume wanu Salehe alirudi kutoka ndani, akaketi mahaliย  alipokua ameketi Baba yakeย 

    โ€œBaba yako ni Mkali sana Salehe hadi nimeogopa. Nimefanya kipi kibaya, kumsaidia Begi niย  vibaya eti?โ€ Nilimuuliza Mume wangu, yeye akanishika bega akaniambiaย 

    โ€œUtamzoea, si unajuwa wazee wa zamani. Pengine hakutaka wewe ushike begi kwasababu zilizoย  kaa kitamaduni tu za Kizamani au kabila letu lakini ni mcheshi utamzoea kwa muda atakaokaaย  hapa.ย ย 

    โ€œIna maana atakuwa anaishi hapa na Sisi?โ€ย 

    โ€œNdiyo, ila muda mchache tu atakua ameondoka. Vipi umeshakula?โ€ Basi kuzungumza naย  Salehe kulinifanya nisahau kilichotokea, tuliongea sana hadi Mchana tuliposikia adhana. Saleheย  akawa wa kwanza kunikumbusha kufanya Ibada, nilitabasamu nikashusha pumzi kidogo hukuย  dimpozi zangu zikionekanaย ย 

    Comments ziwe nyingi apa LEO kwa Kaka Mkubwa

    Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA PILI YA NILIOLEWANA MTU NISIYEMJUA… USISAHAU PIA Kununua Kitabu Cha KOTI JEUSI Kwa Kupiga Simu Namba+255760871896 Ufikishiwe Mpaka Ulipo

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapaย 

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua xx

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    22 Comments

    1. Massay on January 3, 2025 2:10 pm

      Heri ya Mwaka Mpya 2025
      Riwaya nzuri sana, Asante sana kwa utunzi mzuri ubarikiwe

      Reply
      • Shabani matimba on January 3, 2025 2:48 pm

        Unyama uendelee

        Reply
      • Hamisa Joseph on January 4, 2025 10:02 am

        Japo jasusi hamkuimalizia

        Reply
    2. Hope on January 3, 2025 2:16 pm

      Hii balaa ๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅmwanzo tu linaonekana big up kaka mkubwa

      Reply
    3. Salkhan on January 3, 2025 2:17 pm

      Uhakika ni hatariii mwendelezo please

      Reply
      • HAJI RAMADHAN KISENDI on January 3, 2025 6:32 pm

        Iko poa xna

        Reply
    4. Fawziya Hassan on January 3, 2025 2:22 pm

      MAUZA UZA
      Saida kaolewa na Msukule๐Ÿ˜
      Baba mkwe Msukule
      Asante Admin โค๏ธ baada ya kimya kirefu saivi tunaburudika tena na
      KAKA MAKUBWA more Love from Zanzibar โค๏ธโค๏ธ

      Reply
      • Fawziya Hassan on January 3, 2025 3:59 pm

        Kaka MKUBWA โค๏ธโค๏ธโค๏ธ

        Reply
      • Amani shonde on January 3, 2025 9:10 pm

        Duuuh kitu usicho kujua ni sawasawa na usiku wa giza

        Reply
    5. Charz jr๐Ÿ˜Ž on January 3, 2025 2:22 pm

      ๐Ÿƒโ€โ™‚๏ธ๐Ÿƒ๐Ÿƒkumeanza kuchangamkaa

      Reply
    6. Ahmed on January 3, 2025 2:58 pm

      Atajua ajui ngoja mda wa kwenda kulima usiku ufike ,kwenye begi bado ajasemaaaa

      Reply
    7. Allen on January 3, 2025 3:27 pm

      Eeh hapoo uhakikaa kaka mkubwa ongeza kitu

      Reply
      • Sharo love malkx ๐Ÿ’– on January 6, 2025 10:37 am

        Familia ya kichawi iyo
        Mhh

        Reply
    8. Abdalaman on January 3, 2025 8:08 pm

      [email protected]

      Reply
    9. Halinga1 on January 3, 2025 9:34 pm

      Umetisha

      Reply
    10. Calvin paul on January 3, 2025 10:37 pm

      Ulituacha mbali kidogo tungesahau

      Reply
    11. mwanah on January 4, 2025 12:57 am

      Ubaya ubwela

      Reply
    12. Sharo love malkx ๐Ÿ’– on January 6, 2025 10:35 am

      Familia ya kichawi iyo
      Mhh

      Reply
    13. Mahdiya on January 6, 2025 1:15 pm

      Ya pili please

      Reply
    14. Michaelkhan on January 7, 2025 10:17 am

      Aisee Mwanzo Ni wamoto ,Pameanza na Mushkeli๐Ÿ˜ƒ

      Reply
    15. Doricas semu on January 11, 2025 4:47 pm

      Riwaya nzuri jaman nmechelewa kuianza

      Reply
    16. Dickson on January 13, 2025 6:53 pm

      Nice

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi October 1, 2025

    In the name of LOVE – 12

    Ilipoishia sehemu ya Kumi na moja ya In the name of LOVE Moyo Wangu na…

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    In the name of LOVE – 09

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.