Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Jasusi Sehemu Ya Kumi Na Tatu (13)
    Hadithi

    Jasusi Sehemu Ya Kumi Na Tatu (13)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaDecember 11, 2024Updated:December 12, 202426 Comments6 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia  “Umefikia wapi Sande!” Alihoji Mbaga baada ya kuwasha redio  Call 

    “Nakaribia ila nimeumia eneo la mbavu nilitereza wakati  napanda juu ya Bomba, sasa nakaribia ulipo umeme” ilisikika  sauti ya Sande Olise ambaye alikuwa Ikulu 

    “Safi sana! Ongeza mwendo huku hali shwari” akasema kisha  akazima redio akaongeza mwendo kuelekea kwenye ghorofa. Endelea 

    SEHEMU YA KUMI NA TATU

    Sande Upande wake alikuwa akitoka kwenye chemba na mwili ulikuwa ukivuja maji taka, akakumbuka alichoambiwa na Mbaga kuwa hapaswi kupita bila kujifuta maji, akafungua begi kisha akatoa kitambaa akajifuta yale maji ndipo akapita eneo lenye umeme, akapita kwa umakini ili asije sababisha shoti.

    Alikuwa ameshachoka baada ya kutembea ndani ya chemba kwa zaidi ya nusu saa huku akiwa na maumivu makali kwenye mbavu zake, alipovuka umeme akajikuta akihitaji kupumzika kwanza kabla ya kuanza kufungua nati zilizo katika dirisha la juu ambalo akishaliondoa basi anakuwa amefika chooni kwa Rais huyo, punde akasikia sauti ya kufunguliwa kwa mlango akasimama na kuchungulia akamuona Mwanaume mmoja mwenye asili ya kiarabu akiwa anachunguza eneo hilo hapana shaka alisikia purukushani,

    mwanaume huyo ndiye Jamaal ambaye amekuja pale Ikulu kumlinda Rais, Jamaal alionekana kuwa makini, akasogea hadi lilipo dirisha mahali ambapo Sande Olise alikuwa amesimama, dirisha hilo lilikuwa dogo na lenye Alminium na matundu madogo madogo.

    Sande akabonyea kwa chini, Jamaal akaangaza bila kuona chochote kisha ikasikika sauti ya kufunga Mlango, hapana shaka Jamaal alikuwa ameondoka, Sande akajipa likizo fupi ili kutuliza maumivu ya mbavu zake, akaliondoa begi Mgongoni kisha akakaa kwenye bomba!!

    Upande wa pili taarifa ya Kifo cha Mkurugenzi wa idara ya Usalama wa Taifa ilianza kuvuja kwa Askari wa juu wa Taifa, wakaitana ili kujadili. Wakati huo, Mwanaume Sande Olise alikuwa akipandisha ngazi kuelekea Ghorofa namba tano,

    Ghorofa hilo lilikuwa halitumiki, hakuna aliyeshtuka kuwa eneo hilo liligeuzwa kuwa uwanja wa vita sababu Bunduki zilizotumika zilikuwa na vifaa maalum vya kuzuia sauti,

    Malaika alikuwa ameshafika Ghorofa namba tano akamkuta Six akiwa amelala sakafuni damu ikiwa inamtoka, alikuwa hawezi kuzungumza. Muda huo huo Malaika akapiga simu kwa John Brain kumpa taarifa kuwa Six anakaribia kufa

    “Nini?” Aliuliza kwa mshituko John Brain

    “Hali yake sio nzuri, ameshambuliwa na mlengaji mwenzake ambaye yupo ghorofa lingine!! Hali sio shwari Boss” Alisema kwa sauti ya Chini huku akijuwa fika kuwa mlengaji anaweza kuja pale ili kuhakiki kama Six amekufa, ndicho ambacho Mzee Mbaga alikuwa akifanya.

    Akakata simu kisha akaenda kuchungulia dirishani akapokelewa na ukimya uliopitiliza, akajuwa sasa

    yupo mawindoni na Mtu asiyemfahamu. 

    Malaika na kamwili kake kadogo kama Miss Utalii, akachomoa Bastola yake akafunga kifaa maalum cha kuzuia Mlio wa risasi kisha akajiweka sawa!! Akatafuta mahali akajibanza, muda huo Mtaalam Mbaga alikuwa akizidi kusogea juu taratibu.

    “SHIT” alisema John Brain akasimama kutoka kitini kisha akampigia simu Jamaal akamuuliza

    “Kuna usalama ulipo? Six amepigwa risasi eneo baya sana huenda akafa, unatakiwa kuwahi haraka eneo la tukio” Alisema kwa sauti iliyojaa Kupagawa, kwa jinsi alivyokuwa akimuamini Six hakutegemea kama angelipigwa risasi kirahisi hivyo akajuwa kuwa mlengaji alikuwa Mtu hodari zaidi ya Six

    “Natamaani kutoka hapa lakini nina hisia mbaya kuwa huenda ikulu imevamiwa pia, angalia nini cha kufanya Boss” Alisema Jamaal

    “Okay!” Kisha simu ikakatika, akamrudia tena Malaika lakini simu ya Malaika haikupokelewa, wakati huo Malaika alikuwa akisikia namna Mtu alivyokuwa akipiga hatua kuelekea ndani ya chumba hicho.

    Moja kwa moja akajuwa Mtu huyo alikuwa ndiye aliyempiga risasi Six, akabana Pumzi zake ili asimpe mwanya wa kujuwa yupo wapi kutokana na ukimya uliokuwa umetawala pale. Mbaga alizidi kusogea bila kujuwa kuwa anayemuwinda naye ameshakaa mkao wa kujibu mapigo, mara nyingi Mzee Mbaga hakupendelea sana kutumia Bastola lakini ilimlazimu kutokana na namna sifa za Mtu anayeenda kupambana naye zilivyo.

    Fumba na kufumbua Mbaga na Malaika wakajikuta wakiwa ndani ya chumba kimoja kisicho na vitu ndani yake, Malaika alikuwa amejibanza nyuma ya moja ya kona za chumba hicho huku Mwili wa Six ukiwa bado sakafuni, hakukuwa tena na cha kusubiria kwa Malaika akafyatua risasi ili impate Mbaga eneo la Kichwa, lakini bahati mbaya Bastola yake haikutoa risasi, ilikuwa ni kama Bahati kwa Mbaga akafanikiwa kumuona Malaika, wakati Malaika anahangaika kufyatua risasi Mbaga alishamfikia na kuipiga teke Bastola ya Malaika.

    Wakawa wanatazamana kwa macho yaliyojaa ufundi wa kusomana, Malaika alishasikia sifa za Mbaga na Mbaga alikuwa na sifa za Malaika, mviziano baina yao ukawa mkali huku kila Mtu akitafuta namna ya kumdhibiti mwenzake.

    Upande wa Ikulu, mapumziko kwa Sande Olise hayakuchukua muda mrefu, akafungua begi akatoa Staa kwa ajili ya kufungua nati ili aweze kuingia kwenye Choo cha Rais bila kujuwa kuwa Jamaal alikuwa ameshtuka. Alizifungua haraka bila kupoteza muda kabisa, ndani ya dakika moja akawa amefanikiwa kisha akatoa dirisha hilo akaliweka pembeni kukawa na tundu ambalo angeliweza kupita na kwenda chooni kwa ajili ya kuanza mpango wake.

    Muda huo Rais alikuwa akipewa taarifa ya kifo cha Mkurugenzi wa idara ya Usalama wa Taifa, na kushambuliwa kwa Six. Ilimfanya Rais akose amani akiwa ofisini kwake, akamuita Jamaal

    “Usikae mbali na Mimi Jamaal, siwaamini hawa walinzi wengine, tegemeo langu lipo kwako tuu” Alisema huku akiwa anamtazama Jamaal aliyekuwa na ndevu nyingi.

    “Nipo hapa Mkuu” akasema Jamaal wakati huo Sande akiwa anachumpa ili aingie chooni, akajikuta akinasa shati lake kwenye tundu hilo ambalo lilikuwa na baadhi ya misumali midogo baada ya kung’oa dirisha. Akajitahidi kujitoa lakini ikawa ngumu, katika purukushani akajikuta ameangukia chooni, mshindo ukamshtua Jamaal. Akamwambia Rais akae hapo pasipo kutoka kisha taratibu akaelekea chumbani kwa Rais.

    Jamaal akawa anaelekea taratibu eneo ambalo alisikia mshindo huo, ilikuwa ni kule chooni ambako Sande Olise alikuwa ameangukia, Sande hakutaka sana kupoteza muda licha ya kuumia kidogo wakati alipoanguka, akajiokota haraka ili aanze mpango wa kumpata Rais bila kujuwa kuwa Jamaal alikuwa ameshakaribia mlango wa Choo hicho.

    Upande wa pili, Mbaga alikuwa ameangushwa chini, Malaika akionekana kumdhibiti Mbaga kisawasawa, Mbaga akajiokotanisha kisha akamfuata Malaika na kutupa mapigo mawili takatifu, moja lilikuwa ni teke kali ambalo Malaika aliliona na kulikwepa lakini alikuwa ameunganisha na pigo jingine la teke la kushoto ambalo lilimpata Malaika akaanguka chini, bila kupoteza muda akajiokota pembezoni kukiwa na gongo, akalinyanyua ili kupambana na Mbaga, akatoka spidi na kujirusha mithiri ya ndege aina ya Mwewe anavyowinda

    vifaranga vya kuku,

    kisha akatua chini na kurusha gongo ambalo lilimpata Mbaga eneo la Bega hadi akapepesuka na

    kujigonga ukutani, jinsi Mbaga alivyokuwa mwepesi ikawa ngumu kwa Malaika kuusoma umri sahihi wa Mbaga kama ni Mzee au Kijana kwa jinsi ambavyo alikuwa akipambana.

    Mbaga akajiweka sawa kwa ajili ya kujibu mapigo kutoka kwa Malaika, akabonyea kidogo na kukaa staili ya nyani Mzee anayetaka kurukia Tawi la Mti, kisha akakunja miguu yake sawasawa huku akiwa anamtazama Malaika ambaye kwa kiasi kikubwa alikuwa mwepesi kutokana na umbo lake dogo na jembamba.

    “Nitakuuwa kama nilivyomuuwa mwenzako” Akasema Mbaga ikiwa ni mbinu ya kumtuliza Malaika 

    Comments ziwe nyingi apa LEO kwa Kaka Mkubwa

    Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA SABA  USISAHAU PIA Kununua Kitabu Cha KOTI JEUSI Kupiga Namba+255760871896 Ufikishiwe Mpaka Ulipo

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPA 

    SOMA KISASI CHANGU HAPA  

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa 

      Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx   Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx   Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx   Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx 

    jasusi riwaya za kijasusi

    26 Comments

    1. Agynellyster on December 11, 2024 3:46 pm

      🔥🔥🔥

      Reply
    2. David on December 11, 2024 4:31 pm

      Leo ni fupi sana ndugu admini

      Reply
    3. David on December 11, 2024 4:31 pm

      Nilitegemea leo itaisha

      Reply
      • Deo on December 12, 2024 12:22 pm

        Mambo yanazidi kuwa safi

        Reply
    4. Jlucky on December 11, 2024 4:33 pm

      Leta mwendelezo maana ni🔥🔥🔥🔥

      Reply
    5. Cathbert on December 11, 2024 4:37 pm

      Hapo ndo hatriii

      Reply
    6. Patricia Lizzy on December 11, 2024 4:55 pm

      Leo umetupiga na kitu kizito jamani ni fupi sana

      Reply
    7. Egibeth on December 11, 2024 5:04 pm

      Hatariìi mbagaa ni mzeee kweliii ahahaha

      Reply
    8. Bro Imma on December 11, 2024 5:07 pm

      Hatari sana

      Reply
    9. Halinga1 on December 11, 2024 5:09 pm

      Ongeza sauti

      Reply
    10. Anuar on December 11, 2024 5:12 pm

      Daaj leo umetupa fupi san mkuu

      Reply
    11. Hamisi halidi on December 11, 2024 5:14 pm

      Adimini leo fupi sna

      Reply
    12. Junior Mtata on December 11, 2024 5:31 pm

      Admin admin admin nimekuita mara tatu hatari sana ujengewe Sanam lako kabisa

      Reply
    13. Scalion on December 11, 2024 5:38 pm

      Nzuri sana ni balaa aisee
      Tupe vitu kaka mkubwa

      Reply
    14. Hamisa Joseph on December 11, 2024 5:41 pm

      Leo umejuwa kutubania admin

      Reply
    15. Charz jr😎 on December 11, 2024 6:30 pm

      💣💣💣

      Reply
    16. Fatbaloz on December 11, 2024 7:16 pm

      Duu stor leo fupi jamn

      Reply
    17. Joven on December 11, 2024 8:21 pm

      Admin

      Reply
    18. Kingz on December 11, 2024 8:40 pm

      Daaaaaaah nawaza kwa sande olise…..hv kutakuwa salama kwel.
      🥴🥴🥴🤦🏽‍♂️🤦🏽‍♂️🤦🏽‍♂️🤦🏽‍♂️🤦🏽‍♂️

      Reply
    19. [email protected] on December 11, 2024 10:52 pm

      Nnigejua ndo fupi hv jmn .mpk nimepata na kikohozi sijui kimetoka wapi jmn mbona fupi hivi Admin Leo umetuweza baba

      Reply
    20. Ramadhan Kisalawe on December 12, 2024 6:51 am

      Mambo ni 🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥

      Reply
    21. Fawziya Hassan on December 12, 2024 8:40 am

      Jamani mbona fupi ivi
      Simulizi tamu ajabu
      Kaka MKUBWA ZAWADI YAKO IPO HEWANI INAKUJA
      MTUNZI MASHUHURI MBUNIFU SIJAPATA ONA💕💕💕
      NIMESOMA VITABU VYA KIINGEREZA ZAIDI YA VITABU 20 ILA SIJAONA MAMBO KAMA HAYA❤️
      Umenifanya kupenda kusoma Vitabu vya Kiswahili tangu nianza kusoma Simulizi Nzuri ya Osman na Jacklin…
      Admini Nakupenda pia❤️

      Reply
    22. Mwajuma on December 12, 2024 1:05 pm

      Daaah nzuri San hii toa mwendlez

      Reply
    23. Emmanuel on December 12, 2024 1:19 pm

      Imesisimua sana

      Reply
    24. DIzzoh on December 12, 2024 2:01 pm

      Too short

      Reply
    25. Ommy on December 12, 2024 7:12 pm

      Kaz nzuri sana kak naqubal sanaa

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.