Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Jasusi Sehemu Ya Tisa (09)
    Hadithi

    Jasusi Sehemu Ya Tisa (09)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaDecember 6, 2024Updated:December 7, 202422 Comments13 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Hizi ni risasi zilezile, chukueni maiti hizi na wengineΒ  fanyeni msako hapa haraka sana” Ilikuwa ni sauti ya mmoja waΒ  Askari waliokuja pale kanisani, bado Mtaalam Sande, MzeeΒ  Dawson na vijana wake wakiwa ndani ya Andaki bila kuwa naΒ  taarifa kuwa Jesca alikuwa ameuawa na Six, lilipofunguliwa lango kuu la Kanisa ndipo mshituko na Mshangao mkubwaΒ  ulipowashika polisi hao, walikuta Miili ya watu ikiwaΒ  inatokwa na mvuke kama vile nyama inayochomwa, harufu yaΒ  nyama ilitapakaa kanisa zima wakaagiza zima moto kumwaga MajiΒ  katika kanisa hilo, muda mchache polisi walifanikiwa kuingiaΒ  ndani ya kanisa na kukuta Miili mingi ikiwa imeharibikaΒ  vibaya sana.Β 

    Taarifa ilizagaa kwa haraka sana juu ya shambulio hilo laΒ  kutisha ambalo lilitumia silaha ya sumu na risasi, SandeΒ  akawashauri akina Mzee Dawson kuwa hawapaswi kutoka kwaΒ  wakati huo hadi polisi watakapo maliza msako wao. EndeleaΒ 

    SEHEMU YA TISA

    “Nina mashaka juu ya uhai wa Jesca, yeye ni mmoja wa walinziΒ  wa hapa kanisani, sijasikia majibizano ya risasi, huwendaΒ  amekufa kifo Baridi” Alisema Mzee Dawson akionekana kushindwaΒ  kuzuia chozi lakeΒ 

    “Una maanisha nini kusema Kifo Baridi?” Alihoji Mtaalam SandeΒ  Olise huku akimtazama Dawson kwa jicho lililo kazaΒ 

    “Kufa bila kujibu mapigo, Walengwa tunaotafutwa katika vitaΒ  hii ni sisi. Sitaki makubwa yawakute wasio na hatia” AlinenaΒ  DawsonΒ 

    “Una maaana gani?”Β 

    “Ni bora nijitokeze kupambana nao ili kunusuru Maisha yaΒ  wengi yanayowekwa rehani, ikiwa kufa Mimi au kupona waoΒ  ninachotaka ni usawa” Aliongeza DawsonΒ 

    “Kumbuka Polisi watakuangalia kama muarifu kuanzia hivi sasa,Β  hautokuwa huru kufanya chochote kama Mkuu wa Kitengo, vitaΒ  hii ni ngumu Mkuu! Vipi kama Rais ataamuwa kukupaka tope?Β  Utakuwa salama?” Aliuliza Sande Olise, Mzee Dawson akamezaΒ  funda zito la mate kisha akasemaΒ 

    “Tusipopambana sasa hivi tutakuja kupambana nje ya muda,Β  tunapaswa kuwa macho zaidi”Β 

    “Unashauri tufanye Nini Mkuu tupo tayari kukusaidia katikaΒ  vita hii” Alisema Kisko kwa utii Mkubwa, Dawson alikuwa kamaΒ  Mzazi kwao, ndiye aliyewachukua kutoka katika kituo chaΒ  Watoto yatima na kuwaonesha Mwanga wa Maisha, DawsonΒ  akawageukia na kuwaambiaΒ 

    “Natamani hii vita msipigane sababu mna kila sababu ya kuwaΒ  hai ili mje mpigane hapo baadaye sisi tukiwa tumetundikaΒ  daruga au tukiwa tumekufa. Niliwaandaa mje kuwa hazina muhimu baadaye” Alisema Dawson kwa sauti ya Baba kwa Watoto wake,Β  nyuso za Kisko na Chande zilisinyaa huku macho yao yakitazamaΒ  chini.Β 

    “Babaa!! ” Aliita Chande, Dawson akageuza macho yakeΒ  kumtazamaΒ 

    “Tupo tayari kwa sasa kufa kwa ajili ya Taifa letu, turuhusuΒ  tukusaidie hii vita” Dawson alipomaliza kumsikiliza ChandeΒ  akarudisha macho yake kwa Sande Olise, WakajikutaΒ  wanatazamana huku sura zao zikizungumza KijasusiΒ 

    “Tuangalie tunatokaje hapa Shimoni, haribuni kila kitu iliΒ  kupoteza ushahidi wa kazi za hapa ndani, kila mmoja avae suraΒ  bandia haraka sana” Aliagiza Mzee Dawson kwa sauti iliyojaaΒ  mamlaka ya Kijeshi, kazi ikaanza rasmi.Β 

    MSAKOΒ 

    “Shit!” Ilikuwa ni sauti ya John Brain baada ya kupokeaΒ  taarifa usiku huo, hakutegemea kusikia kuwa Dawson na SandeΒ  Olise bado wanaendelea kupumua, aliona ni makosa makubwa niΒ  sawa na kumjeruhi mnyama Mkali.Β 

    “Inawezekanaje wasiwepo kanisani wakati mtoa taarifaΒ  amehakikisha kuwa Sande aliingia hapo? Endapo Sande na DawsonΒ  wakapata muda wa kupanga mipango yao kazi hii itakuwa ngumuΒ  kwetu” Alisema tena John Brain huku akizitazama sura za SixΒ  na Malaika ambao walikuwa wamenywea.Β 

    “Nimefanya msako kanisa zima lakini sikupata kuhisi hataΒ  harufu zao, huenda walicheza mchezo wa sarafu baada yaΒ  kugundua kuwa tunawafuatilia” Alijibu MalaikaΒ 

    “Watakuwa wapi?” Aliuliza John Brain akionesha kutafakariΒ  jambo peke yake, kisha akawaambiaΒ 

    “Nendeni lakini Mjiandae kwa msako maalum” Malaika na SixΒ  wakaondoka, John Brain akampigia simu Rais na kumjulishaΒ  taarifa ile ambayo ilionekana kumchanganya sana RaisΒ 

    “Hivi mnajua mnafanya masihara kwa Watu gani? Hao jamaa wanaΒ  medali za ushindi kwenye kila jambo, Dawson ana fahamu siriΒ  yetu hivyo hapaswi kuendelea kuishi” Alisema Rais kama MtuΒ  aliyeingia kwenye mshituko ni wazi kuwa alitarajia kusikiaΒ  kuwa Dawson na Sande wameuawa

    “Tunalijuwa hilo na vijana wangu wanalifanyia kazi jambo laΒ  muhimu ni kuhakikisha unatupatia Mtu wetu baada ya sikuΒ  chache, tutakuwa tumeimaliza kazi hii na kuondoka hapaΒ  Nchini”Β 

    “Msifanye Makosa mengine John , mtajikuta mnawajibishwa!Β  Ngoja nijisafishe haraka sana” Rais alikata simu, alionekanaΒ  kuwa mwenye msongo wa mawazo huku akionekana kuwa na hofu juuΒ  ya mpango wake wa siri juu ya Mauwaji ya Makam wa RaisΒ  kujulikana na kuwekwa hadharani, akanyanyua simu na kumpigiaΒ  Mkuu wa Idara ya polisi na kumueleza kuwa Dawson ni mharifuΒ  anapaswa kusakwa kwa kila njia ili apatikane, Rais aliamuwaΒ  kucheza karata mbili.Β 

    Moja ni kuwatumia Mafia Gang kumfyeka Dawson na nyingine niΒ  kutumia Jeshi la polisi kumsaka popote alipo, agizo la RaisΒ  lilianza kutekelezwa, Polisi wakaagizwa kuelekea nyumbani kwaΒ  Dawson usiku huo huo.Β 

    Rais alikaa katika kiti chake huku akizidi kujiingizaΒ  mawazoni, Nchi ilikuwa imeingia katika Msako, PolisiΒ  walivunja nyumba ya Dawson na kufanya msako mkubwa bilaΒ  mafanikio, wakati huo Dawson na timu yake wakiwa wanatokaΒ  katika shimo kule kanisani, Polisi wachache walikuwepo eneoΒ  la tukio kule kanisani usiku huo, Walifanikiwa kuchomoka paleΒ  kanisani kimya kimya kisha wakaruka ukuta wa kanisa naΒ  kutokomea.Β 

    Dawson alishajua kuwa polisi wataenda nyumbani kwake hivyoΒ  akawaambia wasiende huko badala yake waelekee kwenye makaziΒ  ya siri ambayo alikuwa akiishi Inspekta Zola, ilikuwa niΒ  safari ya Kilomita kadhaa kutoka pale kanisani hadi kufikaΒ  huko, walilazimika kutembea kwa mguu sababu polisi walikuwaΒ  wakikagua magari yanayoingia na kutoka kila kona ya jijiΒ  hilo, haikuwa salama kwao kutumia usafiri wa gari licha yaΒ  kuvaa sura bandia, mwendo wa masaa mawili Walifika kwenyeΒ  makazi hayo, Dawson alifahamu namba za siri za kufunguliaΒ  milango hiyo ikawa rahisi wao kuingia ndani.Β 

    Kumbukumbu ya Zola iliendelea kuwatesa baada ya kuingia humo,Β  Sande aliiona picha aliyopiga na Zola wakiwa mafunzoni hadiΒ  chozi lilimbubujika aligundua kuwa Rafiki yake huyo alikuwaΒ  akimpenda na kumkumbuka sana, walikuwa na ndoto ya kuonanaΒ  siku moja lakini ndiyo hivyo Sande alichelewa kurudi hadiΒ  Zola akauawa, Dawson aliifahamu nyumba hii vizuri sana sababuΒ  mpango wa nyumba hii aliusuka mwenyewe ili Zola aitumieΒ  nyumba hii kwa kazi zake maalum, akawaonesha chumba ambachoΒ  kilikuwa na silaha akawataka kujiandaa kwa ajili ya kazi hiyoΒ  kubwa iliyo mbele yao.

    “Baada ya kupambazuka tutakuwa katika hekaheka nzito yenyeΒ  maamuzi ya kuondoa uhai wetu au kuturuhusu kuendelea kupumua,Β  kama tuna muda wa kufurahi basi huu Usiku uliobaki unawezaΒ  kuwa ndio muda pekee wa kufanya hivyo” Alisema Dawson akiwaΒ  ana mimina mvinyo kwenye glasi, kila mmoja akanyanyua naΒ  kuanza kunywaΒ 

    “Kwa ajili ya Zola, tusherehekee Maisha yake sababuΒ  ameimaliza kazi aliyokula kiapo kuifanya ili kulinda TaifaΒ  lake” Yalikuwa ni maneno ya Sande Olise ambaye naye aliunganaΒ  na Mzee Dawson wakanywa Glasi moja moja, Chande na KiskoΒ  wakaungana pale wote wakapata Mvinyo kama Ishara ya kuyaenziΒ  Maisha ya Inspekta Zola ambaye ameuawa ndani ya Ikulu, hadiΒ  kufikia muda huo hakukuwa na taarifa iliyotolewa popote kuwaΒ  Inspekta Zola alikuwa amekufa, si akina Dawson wala upande waΒ  Rais ambao ndio walitekeleza Mauwaji hayo.Β 

    Asubuhi ya siku iliyofuata iliwakuta Dawson na vijana wakeΒ  wakiwa ndani ya jumba la siri hilo alilokuwa akiishi MtaalamΒ  Zola, taarifa kuwa Dawson amelisaliti Taifa ilianza kuzagaa,Β  akatajwa Dawson kama ndiye Mhusika namba moja wa Mauwaji yaΒ  Waumini kule kanisani, taarifa ikafika mbali na kusema anaΒ  viashiria kuwa alitaka kuipindua Nchi hiyo kwa kusababishaΒ  taharuki ikiwemo Mauwaji ya kutisha yaliyokuwa yakifanyikaΒ  pia Mauwaji ya Makam wa Rais, gunzo lilikuwa limetanda, niΒ  kama Bundi mweusi alikuwa ameyazunguka Maisha ya Dawson,Β  ikatolewa taarifa kuwa Dawson anashirikiana na Askari mmojaΒ  wa Usalama wa Taifa aliyeitwa Sande Olise ambaye alikuwaΒ  akiishi Botswana.Β 

    “Huyu Mjinga anajaribu kuharibu taswira niliyoijenga MiakaΒ  mingi katika Taifa hili” Alisema Dawson kwa hasira hukuΒ  akitafuta rimoti ya TV ili aizime, Sande alimzuiaΒ 

    “Huna haja ya kupaniki, anachokifanya Rais ni kujaribuΒ  kujisafisha na kuyatia doa Maisha yetu. Kwakuwa anajua unaΒ  siri zake basi anaitumia hii nafasi kukudidimiza iliΒ  usiaminike na yeyote yule” Alisema Sande kisha DawsonΒ  akamuulizaΒ 

    “Mimi ni mzalendo kwa Taifa hili, nimekuwa kwenye nafasi hiiΒ  kwa Marais zaidi ya tano, iweje huyu aje kuharibu kila jemaΒ  nililopanda kwenye Taifa hili, baada ya kuniulia Rafiki yanguΒ  anadiriki kuniita Msaliti wa Taifa hili” Dawson alionekanaΒ  kuchukizwa sana na kitendo kile, akapapasa kiuno chake akatoaΒ  bastolaΒ 

    “Unaenda wapi?” Alihoji Sande

    “Ikulu kuondoa uhai wa hayawani yule, hastahili kuishi pale,Β  anastahili kuwa Kaburini au Jela kwa yote aliyoyafanya”Β 

    “Hebu tulia, kumbuka John Brain ni Mtu mwenye akili sana. HuuΒ  ni mtego na lengo ni kukufanya uchukie, Rais anakujua vizuriΒ  hupendi mchezo na uzushi, ukitoka hapa hata hufiki mbaliΒ  wanakuuwa” Alisema Sande huku akimsistiza Dawson atulie,Β  chozi lilikuwa likimbubujika Mzee Dawson, akajitupa kitiniΒ  kama Mtu aliyekata tamaa.Β 

    “Huna haja ya kukurupuka, Tumetajwa kuwa Wauwaji na wasaliti,Β  tukikamatwa huko nje hatutokaa kuonekana tena, tutaliachaΒ  Taifa hili katika giza kama ambavyo Zola ameliacha. NimekujaΒ  hapa kwa ajili ya kazi hii, nitazame Mimi kwa sasa kamaΒ  ambavyo ulikuwa ukimtazama Zola na kumuamini, hamisha kilaΒ  kitu kutoka kwake kisha kiweke kwangu, Mimi ni Zola niliyeΒ  katika Umbo la Sande, hakuna kitakacho haribika” Yalikuwa niΒ  maneno ya Kikomandoo kutoka kwa Sande Olise, alisema akiwaΒ  amefanikiwa kumpokonya Bastola Dawson.Β 

    Akampatia ile Bastola Kisko akamwmbiaΒ 

    “Ukiitumia vibaya itakupeleka pabaya, tuliza akili ndipoΒ  uitume ifanye kazi yake” Alimkabidhi kisha AkasemaΒ 

    “Baada ya miaka mingi narudi kazini kupambana na John Brain,Β  kivuli chake kitaendelea kuitesa hii Nchi, huyu Rais MpumbavuΒ  siku zake za kuwa madarkani zinahesabika” Alisema kishaΒ  akaelekea kwenye moja ya vyumba vya siri vya jengo hiloΒ  ambavyo vilikuwa vimeshafunguliwa na Mzee Dawon.Β 

    Akakuta Ramani ya mpango wa Zola ikiwa ukutani, akaangaliaΒ  namna Zola alivyopanga mambo yake pale akajikuta akitabasamuΒ  kwani kila jambo alikuwa ameliandika katika Ramani hiyo.Β 

    Nyuma ya Sande alikuja kusimama Mzee Dawson huku akimtazamaΒ  Sande namna alivyokuwa makini kutazama Ramani ya ZolaΒ 

    “Ulikuwa na askari shujaa sana ambaye hasahau mbinu zako”Β  Alisema Sande Olise kisha aligeuka na kumtazama Mzee DawsonΒ  aliyekuwa akifuta chozi lake, kifo cha Zola kilimuumiza sana.Β 

    “Nina uhakika kama utawatunza vijana hawa wawili wanawezaΒ  kuwa Sande na Zola wa baadaye, kwasasa Mzee Dawson pumzika.Β  Afya yako haikuruhusu kuendelea na vita hii, nitapambana MimiΒ  na hawa vijana, utabakia hapa” Aliongeza Sande, ni kweli afyaΒ  ya Dawson haikuwa nzuri kutokana na pombe na sigara.

    Wakapanga mipango ya kumuondoa Rais Madarakani kisha kuanikaΒ  uchafu na madudu yake yote, Dawson alitakiwa kubakia paleΒ  kwenye jumba la siri wakati ambao Sande na vijana wawili waΒ  Dawson watakapokuwa wanaondoka, wakapewa sura bandia iliΒ  watakapotoka nje wasijulikane.Β 

    Muda huo Magari mawili meusi yalikuwa yakiingia Ikulu,Β  alikuwa ni John Brain, Six na Malaika, utatu ambaoΒ  ulilisumbua Taifa kwa muda mrefu, waliitwa na Rais huyoΒ  Mshenzi. Waliingia wakiwa kama wageni wakiwa ndani ya suraΒ  bandia ili wasitambulike sababu Vyombo vingi vya habari hasaΒ  vya nje vilikuwa vikiripoti taarifa zao za Mauwaji na jinsiΒ  ambavyo walikuwa wakitafutwa, Waliongoza hadi ofisini kwaΒ  Rais huyo bila Ulinzi wowote kutokana na maagizo ya Rais.Β 

    Rais alipowaona alinyanyuka na kusogea karibu na John BrainΒ  kisha akamuulizaΒ 

    “Mnataka niwape nini ili Dawson na Sande wauawe? MnapaswaΒ  kujuwa kuwa Dawson ni nyati aliyejeruhiwa akitoka hukoΒ  mafichoni hatutokuwa salama” Alisema huku akionekanaΒ  kuchanganikiwa, jasho lilikuwa likimvujaΒ 

    “Tatizo umechanganya vitu viwili kwa wakati mmoja, PolisiΒ  wanahangaika kuwatafuta na sisi tunahangaika kuwapata. KilaΒ  tunapopiga hatua polisi wanakuwa eneo la tukio, au unatakaΒ  tusamabratishe na polisi wako?”Β 

    “Kama hilo ni tatizo nitawaingiza katika mfumo wa usalama waΒ  Taifa mkiwa katika sura hizo, John utakaa pembeni sababu yaΒ  rangi yako ila Malaika na Six wataingia na kufanya kazi maraΒ  moja, watakuwa na amri kwa askari pindi wanapokutana katikaΒ  jukumu la kuwawinda Sande na Dawson,watapewa vitambulishoΒ  maalum”Β 

    Rais akawaingiza Six na Malaika katika mfumo wa idara yaΒ  Usalama wa Taifa, wakapewa na VitambulishoΒ Β 

    vilivyowatambulisha kama Watu wa Usalama, ikawa rahisi kwaoΒ  kuwa huru kufanya kazi ya kuwasaka Dawson na Sande OliseΒ  ambao walikuwa kizingiti kikubwa kwa Rais na John BrainΒ  kumpata kijana wake aliyekuwa akishikiliwa na Rais.Β 

    Polisi wakatawanywa kila kona ya Jiji kuhakikisha Dawson naΒ  Sande hawapigi hata hatua moja, kazi ya polisi ilikuwaΒ  kuwakamata lakini kazi ya Six na Malaika ni kuwauwa, wakiwaΒ  ndani ya Sura bandia walirudi pale Kanisani ambakoΒ  walisababisha Mauwaji ya kutisha ya Waumini na Askari mmojaΒ  wa siri wa Mzee Dawson, walirudi kama Watu wa Usalama,Β  wakahitaji kuchunguza eneo hilo huku akili zao zikiwaambia kuwa pengine Dawson na Sande bado wapp eneo hilo, walimjuaΒ  vizuri Dawson jinsi alivyo na akili nyingi.Β 

    Walitumia vyema macho yao ya Kijasusi na mafunzo waliyoyapataΒ  kutoka kwa John Brain wakagundua kuwa kuna andaki eneo laΒ  maegesho ya MagariΒ 

    Six na Malaika wakapeana ishara, haraka bastola zao zikawaΒ  zinatazmaa eneo hilo ili kama kuna Mtu atatokea basiΒ  wamdhibiti haraka sana.Β 

    Wakalisukuma gari na kuona mlango wa kuingia ndani, harakaΒ  wakiwa makini sana wakafungua na kuanza kuingia humo taratibuΒ  huku masikio yao yakiwa makini kusikiliza ndani ya andakiΒ  hilo lenye giza sana.Β 

    Walipofika chini wakawasha tochi ya simu kisha wakaona mahaliΒ  ambapo wangewasha taa, walipowasha wakaona vitu vikiwaΒ  vimeharibiwa pale, wakakagua kila kona lakini hakukuwa naΒ  Watu, tayari Mzee Dawson na vijana wake walishaondoka paleΒ  muda mrefu sana kisha wakaharibu vitu ndani ya andaki hilo,Β  elimu yao ya kijasusi haikuwafanya wao kukata tamaa ya kutakaΒ  kujuwa andaki hilo lilihusiana na niniΒ 

    “Kwa vyovyote haya yalikuwa makazi ya siri ya Dawson! HuendaΒ  ameishi hapa kwa kitambo sana” Alisema SixΒ 

    “Hata awe makini vipi ni lazima ataacha alama humu, tutajuaΒ  kama ni yeye na ameenda wapi” Alisema Malaika, msakoΒ  uliendelea ndani ya andaki hilo lililoonekana kuwa makazi yaΒ  kutulia sana, katika upekuzi wao waliona Makaburi manneΒ  ambayo yalikuwa ndani ya chumba kimoja.Β 

    Walipoangalia vizuri waliona namba za siri ambazo Mzee DawsonΒ  aliwapa vijana wake kama majina na alama zao, namba hiziΒ  zilikuwa za siri sana, ilikuwa ngumu kugundua chochote lakiniΒ  alizitambua kisha akampigia simu John Brain na kumuelezaΒ  kuhusu Makaburi hayo manne yenye namba za siri, John BrainΒ  alikuwa na mtandao mkubwa sana na alizijua siri nyingi zaΒ  Mataifa mbalimbaliΒ 

    “Hayo ni majina ya Watu wa siri wa Mzee Dawson, Sande yupoΒ  hai, moja ya kaburi hapo linaweza kuwa kaburi la Zola,Β  fukueni haraka sana.” Ilisikika sauti ya John Brain, aliaminiΒ  Dawson ni Mtu mwenye akili sana kwenye mambo yake.Β 

    Mengine yalionekana kuwa ya zamani sana lakini moja lilikuwaΒ  bado jipya, wakalifukua hilo kwa kutumia chepe iliyo kwenyeΒ  kona ya chumba hicho chenye makaburi. Kazi hii ilifanywa na Six aliyekuwa amebana rasta zake kwa nyuma. Jasho lilikuwaΒ  likimtoka, harufu kidogo ilianza kutapakaa pale, haikuwazuiaΒ  kufanya kazi yao,

    Comments ziwe nyingi apa wikiendi itoke EPISODE NDEFU YA 10Β 

    Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA SABAΒ  USISAHAU PIA Kununua Kitabu Cha KOTI JEUSI Kupiga Namba+255760871896 Ufikishiwe Mpaka Ulipo

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAΒ 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza HapaΒ 

    Β  Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Β  Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Β  Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Β  Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xx Jasusi xxΒ 

    Β Β 

    jasusi riwaya za kijasusi

    22 Comments

    1. yukovich on December 6, 2024 2:29 pm

      unyama

      Reply
    2. Charz jr😎 on December 6, 2024 3:05 pm

      Kazi kazi

      Reply
      • Elsolo on December 7, 2024 9:47 am

        Toa hata tatu mzee baba

        Reply
    3. Charz jr😎 on December 6, 2024 3:06 pm

      Weeknd usitubanie asee

      Reply
    4. G shirima on December 6, 2024 3:25 pm

      Kila unaesima naomba ucoment please

      Reply
    5. DIzzoh on December 6, 2024 4:11 pm

      Too hotπŸ™Œ

      Reply
    6. Areta on December 6, 2024 4:14 pm

      Ya motoo

      Reply
    7. Aisha on December 6, 2024 5:07 pm

      .wendelzo jmn pia zilishwe hata tano kwa siku πŸ₯°πŸ₯°

      Reply
    8. Fawziya Hassan on December 6, 2024 6:13 pm

      Simulizi ya πŸ”₯
      Mtunzi wa Simulizi hii anitafute kuna Zawadi yakeβ™₯️β™₯️β™₯️

      Reply
    9. Anuar on December 6, 2024 6:13 pm

      Daah imefka penyew mkuu uwe unatoa hata mbili basi mkuu
      Stor iko poa sana

      Reply
    10. Buruani on December 6, 2024 8:11 pm

      Hatar iyooΓ³oo

      Reply
    11. VERONICA on December 6, 2024 9:07 pm

      Nzuri sana

      Reply
    12. Street kid on December 6, 2024 9:13 pm

      Shusha chuma mkuu 🀴

      Reply
    13. David on December 6, 2024 10:36 pm

      Weeee

      Reply
    14. Jack bujo jr on December 6, 2024 11:47 pm

      Kesho tuwahishie Basi pia ilefushe hata kidogo maana siku za mpira hua unabana Sana

      Reply
    15. [email protected] on December 6, 2024 11:50 pm

      Jmn huyu malaika na six. Si sande wawauwe fasta wasijeniulia Mzee wangu Dowson jmn

      Reply
    16. [email protected] on December 6, 2024 11:51 pm

      Admin story Kali sn ni km vile mtu unaangalia movie

      Reply
    17. Hamza Abdallah Mwalyawa on December 7, 2024 12:36 am

      Hili ni bomu la kutegwa ardhini kilo mia moja haponi mtu hapo ni mbele kwa mbele 🀸🀸🀸😑

      Reply
    18. Ahmed Samir on December 7, 2024 12:32 pm

      πŸ’₯

      Reply
    19. Hope on December 7, 2024 2:02 pm

      Natamani ingekuwa movie kbs yani uwii admin upewe maua yako ☺️

      Reply
      • Ally abiz on December 7, 2024 5:44 pm

        Kazi nzuri admin una jitahidi

        Reply
    20. πŸ“ Ticket- TRANSFER 1,870203 bitcoin. Continue => https://yandex.com/poll/7HqNsFACc4dya6qN3zJ4f5?hs=47eff14450b187be13d1a5e38c52e7a2& πŸ“ on June 3, 2025 11:01 am

      3exvik

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya naneΒ  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.