Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Love & Pain Sehemu Ya Sita (06)
    Hadithi

    Love & Pain Sehemu Ya Sita (06)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaNovember 15, 2024Updated:November 21, 20247 Comments9 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Love & Pain
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Lucia alimpatia Noela bahasha hiyo yenye taarifa muhimu zaΒ  kesi, Desmond aliona makabidhiano hayo ya Bahasha kishaΒ  wawili hao waliagana kila mmoja akashika barabara yake.Β  Desmond aliona ni bora amfuatilie Mpenzi wake Noela iliΒ  kujuwa Bahasha hiyo ilikuwa na nini. Basi, baada ya kutokaΒ  hapo Noela alielekea moja kwa moja nyumbani kwao, alipoingiaΒ  ndani aliiweka Bahasha hiyo kwenye Shefu maalum yaΒ  kuhifahdhia nyaraka zake, alifunga kwa namba maalum kishaΒ  alijipumzisha kitandani.Β 

    Akiwa hapo nje Desmond alipokea simu ya Polisi mpeleleziΒ  akaambiwa anahitajika haraka kituoni, mara moja aliwasha gariΒ  bila kumwambia Noela kuwa alikuwa nje ya nyumba yao,Β  akaelekea kituoni. Huko alioneshwa gari ambayo maitiΒ  ilikutwa, gari hiyo ilikuwa ni Landlover ya zamani ambayoΒ  ilidaiwa kuwa usajili wake haukujulikana. EndeleaΒ 

    SEHEMU YA SITA

    “Hii ndiyo gari yenyewe ambayo ilikutwa ndani ya Bahari ikiwaΒ  na mwili wa Sanga, hadi kufikia sasa tumempoteza mshukiwaΒ  namba moja ambaye angetusaidia kujuwa mambo mengiΒ  yaliyojificha kuhusu kesi ya Mkeo” Alisema Polisi huyo wakiwaΒ  wamesimama kando ya gari hilo, Desmond alilitazama sana gariΒ  hilo alafu akakumbuka siku ya tukio kuwa gari aliyoitumiaΒ  ilikuwa ni Audi A4 na siyo Landlover hiyo chakavu.Β 

    Bado aliendelea kujiuliza Mtu wa tatu ni nani?Β 

    “Kwa maana hiyo uchunguzi wa kesi utaanza upya ili kumpataΒ  mshukiwa mwingine wa matukio haya, inaonesha Sanga alifungiwaΒ  ndani ya gari kisha akatupwa Baharini ili afe, yupo MuuwajiΒ  nyuma ya hili” Alisema tena Polisi huyo huku DesmondΒ  akijiambiaΒ 

    “Muuwaji ni Mimi lakini hamtokuja mnijuwe” alisema ndani yaΒ  nafsi yake, basi baada ya kumaliza kufanya mazungumzo hapoΒ  Kituoni aliondoka zake, alimfikiria sana huyo Mtu wa tatuΒ  kisha akili yake ikawa inamwambia kuwa Mtu wa tatu ni LuciaΒ 

    Akapata wazo la kutaka kujuwa Noela alipokea bahasha ya nini,Β  alimpigia Noela akamuuliza yuko wapi, Noela alimwambia kuwaΒ  yupo Mjini anaangalia gauni la kuvaa siku ya kuvishwa pete,Β  basi Desmond aliutumia mwanya huo kwenda nyumbani anakoishiaΒ  Noela na Mama yake.

    Alisalimiana kwa Bashasha na Mama Noela, Mama huyo alikuwaΒ  akimpenda sana Desmond amuowe Mwanaye hivyo kumuona hapoΒ  ilikuwa ni jambo la furaha sana, Mama Noela aliingia jikoniΒ  kumpikia Mkwe wake mtarajiwa, Desmond aliitumia nafasi hiyoΒ  kuingia chumbani kwa Noela ili aitafute ile Bahasha maanaΒ  alijuwa tu inaweza kuwa na taarifa mbaya dhidi yakeΒ 

    Alipekua kila mahali hadi alichoka lakini hakufanikiwaΒ  kuiyona ile bahasha, aliamini Bahasha ilikuwa mlemle ndani,Β  alizidi kuitafuta bila mafanikio, alitumia muda mrefuΒ  kufikiria na kuitafuta Bahasha bila kuipata maana aliiwekaΒ  kwenye shefu ambayo aliificha mahali, jasho lilimtoka DesmondΒ  huku akizidi kutafakari itakuwa ipo sehemu gani.Β 

    Baadaye alisikia mlio wa gari ya Noela, alipochunguliaΒ  dirisha alimuona Noela akishuka kwenye gari, haraka alijuwaΒ  akikutwa hapo ndani bila taarifa atashtukiwa, aliangalia kamaΒ  kuna kitu ambacho hakikukaa sawa, haraka alikirudisha kishaΒ  alitoka chumbani, alifuta jasho akaketi sebleni, uzuri niΒ  kuwa Mama yake Noela muda wote alikuwa jikoni hivyoΒ  hakufanikiwa kujuwa kama Desmond aliingia Chumbani kwa Noela.Β 

    Alipoingia Sebleni alishangaa kumuona Desmond ambaye alikuwaΒ  akimfahamu kama JoshuaΒ 

    “Eeeh Baby umekuja saa ngapi?” Aliuliza Noela akiwa mwenyeΒ  furaha na mshangao juu tena akiwa anaweka chini mizigoΒ  aliyokuja nayo, kisha alimrudia DesmondΒ 

    “Nimekuja muda mrefu sana, nimekaa hapa kwa muda mrefuΒ  kukusubiria uje” Alijibu Desmond kama siyo yeye vileΒ  aliyekuwa akipekuwa chumbani kwa Noela kuitafuta ile Bahasha.Β 

    “Ndiyo amekuja muda mrefu nikawa naandaa Chakula” IlisikikaΒ  sauti ya Mama yake Noela ( Mlami ) kisha naye alisogea karibuΒ 

    “Chakula tayari Baba” Mama Noela alimwambia DesmondΒ 

    “Ah Mama asante sana” Alisema Desmond kisha alienda kupataΒ  chakula wakati huo Noela akiwa amepumzika kwenye sofaΒ  akionekana kuchoka, wakiwa mbali mbali Desmond alimtupiaΒ  Noela swaliΒ 

    “Unaoneakana umechoka sana vipi ulifanikiwa?” AliulizaΒ  kwasababu Noela alienda kuangalia gauni la kuvaa siku yaΒ  kuvishwa peteΒ 

    “Ndiyo nimefanikiwa lipo kwenye mfuko” Alijibu noela, DesmondΒ  aliendelea kula hadi alipomaliza akaaga akaondoka zake bilaΒ kufanikiwa kuipata ile baasha ambayo ilikuwa ikimpa wasiwasi,Β  baadaye Noela aliingia chumbani lakini aliona kama kunaΒ  baadhi ya vitu vyake vimekaa tofauti siyo kama alivyoviacha,Β  alipata shahuku ya kuzidi kukagua aliona ishara ile ileΒ  akahisi moja kwa moja chumba chake kilipekuliwa, alirudiΒ  sebleni kwa Mama yake akamuulizaΒ 

    “Mama Nani amepekua chumbani kwangu?” Alihoji Noela akiwaΒ  mwenye kushangaaΒ 

    “Kupekua? Mmh mbona hakuna aliyeingia huko…” alijibu MamaΒ  Noela sababu hakunuona Desmond akiwa ameingia hukoΒ 

    “Ina maana kumejipekua kwenyewe eti Mama? Vitu nilivyoachaΒ  siyo nilivyokuta ndiyo maana nimekuuliza, Mlami utasemajeΒ  hujui wakati upo nyumbani muda wote?”Β 

    “Aaah au Joshua aliingia huko? Lakini hapana mbona aliketiΒ  hapa muda wote”Β 

    “aaah” Aligugumia Noela kisha alirudi chumbani, alichukuaΒ  simu akampigia Desmond akamuuliza kama aliingia chumbaniΒ  kwake, Desmond alimkatalia kuwa hakuingia huko, basi simuΒ  ilikatika huku ikimuacha na maswali mengi Noela kuwa ni NaniΒ  aliingia huko na alienda kufanya nini.Β 

    Ndani ya Hospitali kubwa, Desmond alienda kumuangalia MkeΒ  wake ambaye ni adui mkubwa kwake, kilichomshangaza niΒ  kuzuiliwa kuingia kwenye chumba ambacho Mke wake MandyΒ  alikuwa amewekwa kwa ajili ya matibabu, yalikuwa ni maombi yaΒ  Nesi Lucia kwa daktari mkuu wa Hospitali.Β 

    Alilalamika DesmondΒ 

    “Nazuiliwa vipi kumuona Mke wangu wa ndoa? Kwanini anapelekwaΒ  kwenye wodi nyingine bila kunitaarifu Mimi?” Alihoji akiwaΒ  mbele ya nesi mmoja, Nesi Lucia alikuwa amejibanza mahaliΒ  akimfuatilia Desmond, alikuwa na mashaka sana na DesmondΒ  tokea ile siku ambayo Desmond alienda na Mwanasheria paleΒ  Hospitalini na kumsainisha Mandy kwa alama ya kidole.Β 

    Desmond alichanganikiwa kwa jambo moja, kama Mke wake ataamkaΒ  atasema Nani alimuuwa Mama yake Kitu ambacho DesmondΒ  alipambana kuhakikisha hakuna siri inayotoka.Β 

    “Ni maagizo kutoka kwa Dokta Mkuu wa Hospitali nasiΒ  tunayafuata” Alisema Nesi huyo wa kiume, Desmond hakutakaΒ  kusema tena baada ya kusikia kuwa maagizo ya kuzuiliwaΒ  yaliyoka kwa Dakatri Mkuu wa Hospitali hiyo. Alitembea kishaΒ  aliketi kwenye Kiti akakumbuka jambo

    Alikumbuka siku moja mvua kubwa ilikuwa ikinyesha, mvua hiyoΒ  iliambatana na radi za hapa na pale, alikuwa akiendesha gariΒ  huku akionekana kuwa mwenye kutafakari jambo zito kichwani,Β  nyuma yake kulikuwa na gari nyeusi iliyokuwa ikimfuataΒ  taratibu, Desmond hakuiyona.Β 

    Gari hiyo nyeusi iliyo nyuma yake ndani kulikuwa na Mama MtuΒ  mzima, Mama huyo alikuwa ni Mama yake Mandy, Mama MandyΒ  alipata taarifa kuwa Desmond amepanga kukutana na MwanasheriaΒ  wa Mandy kisha wabadilishe hati za mali za Mandy.Β 

    Mama Mandy alizidi kumfuatilia Desmond Usiku huo ambaoΒ  uliambatana na mvua na upepo, safari hiyo ilikita nje ya MjiΒ  huo waliokuwa wakiishi tena katika ghofu moja ambaloΒ  Mwanasheria wa Mandy aliyeitwa Joel alikuwa akimsubiriaΒ  Desmond.Β 

    Mama Mandy alionekana kuwa makini sana kumfuatilia Desmond,Β  alikuwa peke yake, hakujuwa kuwa Desmond alikuwa ameshashtukaΒ  kuwa kuna gari iliyokuwa ikimfuatilia kwa nyuma, Mama MandyΒ  alipoona gari ya Desmond imesimama naye alisimamisha gari kwaΒ  mbali kidogo kisha alishuka akawa anatembea kwenye mvuaΒ  taratibu huku akiwa makini mno, alisogea taratibu sana hadiΒ  kwenye gari ya Desmond lakini hakumuona Desmond, Usiku huoΒ  ulijaa giza kiasi.Β 

    Alipoangalia vizuri mbele aliona ghofu, alipata wazo kuwaΒ  huenda Desmond atakuwa ameingia humo, basi alisogea hadiΒ  ndani ya Ghofu hilo ambalo lilionekana kuwa kimya sana,Β  hakukuwa na Mtu yeyote yule kitu ambacho kilizidiΒ  kumshangaza.Β 

    Akachukua simu yake ili ampigie Mandy amueleze mahali alipoΒ  pia amwambie Binti yake juu ya Mchezo mchafu aliokuwaΒ  akiufanya Desmond, kabla hata hajapiga simu alisikia hatuaΒ  nyuma yake alipogeuka alimuona Desmond akiwa amesimama nyumaΒ  yake, alipoangalia mikono ya Desmond haraka aliona amevaliaΒ  Gloves.Β 

    “Desmond! Unataka kufanya nini?” Aliuliza Mama yake MandyΒ  akiwa anavujwa na maji kwenye mwili kutokana na ile mvuaΒ  iliyompiga kule njeΒ 

    “Uchafu unaoufanya umefika mwisho Joshua, kila siku nilikuwaΒ  nikimwambia Mandy kuwa wewe huna mapenzi naye bali unahitajiΒ  mali za Mtoto wangu, Mwanasheria Joel yupo wapi?” AliulizaΒ  Mama Mandy, Desmond alihema kidogo kisha Joel alijitokeza

    “Hadi wewe Joel? Unajuwa ni kiasi gani familia inakuaminiΒ  Joel? Unashiriki uchafu mkubwa kama Huu, hili siweziΒ  kulifumbia macho, nyote mnaingia kwenye mikono ya sheria”Β  Alisema Mama Mandy kisha alionekana kutaka kupiga Simu lakiniΒ  haraka Desmond alimuwahi, akampora simu akaona alikuwaΒ  anataka kumpigia MandyΒ 

    “Unataka kufanya nini Mama? Unataka nifungwe? Unataka niweΒ  Masikini au unataka Mtoto wako aniache? Hii ni siri ambayoΒ  hukupaswa kuifuatilia Mama…..” Alisema Desmond hukuΒ  akijikaza lakini alikuwa akiumia sana ndani ya Moyo wakeΒ 

    “Mandy ni lazima atajuwa kuwa wewe si Mtu mzuri na ninaΒ  ushahidi wa video na picha ambazo nimetumiwa, umekuwaΒ  ukikutana na Joel kila siku Jioni na kupanga mipango yenuΒ  michafu..” Alisema Mama yake MandyΒ 

    “Pole Mama kwasababu hutoweza kufanya hivyo” alisema DesmondΒ  haraka alikata waya uliokuwa ukining’inia kisha akamnyongaΒ  Mama yake Mandy hadi alipofanikiwa kummaliza, MwanasheriaΒ  Joel alikunja uso wake kuashiria kuwa jambo hilo halikuwa laΒ  kawaida.Β 

    “Joel Mimi na wewe tumeuwa hapa sawa? Tunapaswa kuondoka naΒ  kukaa kimya, nipe hizo nyaraka” Alisema Desmond, harakaΒ  alipewa nyaraka kisha Joel alisemaΒ 

    “Bado saini ya Mtu mmoja tu, Mkeo Mandy”Β 

    “Nitajuwa nini cha kufanya” Alisema Desmond kisha harakaΒ  walianza kutoka lakini Desmond aligeuka kuutazama mwili waΒ  Mama Mandy, alikuwa amevalia cheni ya Dhahabu yenye thamaniΒ  kubwa sana, alirudi akamvua kisha akaiweka kwenye koti laΒ  suti yake, alafu alisemaΒ 

    “Sisi ni Watoto wa kimasikini sana”Β 

    Kumbukumbu ya Desmond iliishia hapo, alitikisa kichwa chakeΒ  kisha alielekea ofisini kwa Daktari wa Hospitali, DaktariΒ  alipomuona Desmond alijuwa nini kimemleta, Desmond alianzaΒ  kumshambulia Daktari huyo kwa manenoΒ 

    “Umeagiza Mke wangu apelekwe Wodi nyingine alafu MimiΒ  nizuiliwe kumuona si ndiyo? Hivi unajuwa ulichokifanya?”Β  Alisema Desmond kwa hasiraΒ 

    “Desmond hebu kaa kwanza tuongee, hili jambo siyo laΒ  kulichukulia jazba, tulichofanya ni kupandisha darajaΒ  matibabu ya Mkeo ili aweze kuamka haraka ” Alisema DaktariΒ  huyo kwa upole sana

    Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA SABA

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya kuendelea kutuma SIMULIZI Mpya Na Kuipost HAPA Kwa kumtumia Chochote kupitia

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAΒ 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love &Pain Love & PainΒ 

    Β Β 

    Love & Pain

    7 Comments

    1. Fawziya Hassan on November 15, 2024 4:42 pm

      Eee!! Umaskini utawapeleka watu pahala pabaya sanaπŸ˜₯

      Asante mtunzi kwa stori yenye mafunzo na mazingatio makubwa.

      More Love from Kenya ❀️

      Reply
    2. Sir, Yowas on November 15, 2024 8:05 pm

      Sawa

      Reply
    3. Junior Jr on November 15, 2024 9:32 pm

      Hii story noma sana

      Reply
    4. Roddrigo on November 16, 2024 7:50 am

      SIMULIZI|SIRI ZA GIZA.
      SIMULIZI ya kijana machachari anayelijua jiji,mkasa huu unamwonesha yumo katika Giza na vingi vya ajabu vinamstaajabisha,anashangaa ulimwengu usiotarajiwa machono pake.

      Isome hapa
      ______

      https://maishakitaaonlinetz.blogspot.com/2024/11/simulizisiri-za-giza.html

      Reply
    5. Rau B on November 16, 2024 5:22 pm

      Update Za michezo na Hadithi fupi
      Njia hii hapa

      https://whatsapp.com/channel/0029VanxLVYJ93wbHawAAh3H/701

      Reply
    6. Sharo love malkx πŸ’– on November 17, 2024 2:27 pm

      NANDY APEWE NA ULINZI UKO HOSPITALI
      πŸ˜†πŸ˜†πŸ˜†πŸ˜†

      Reply
    7. πŸ“Œ Email: Operation 1.593059 BTC. Verify =>> https://yandex.com/poll/T1TnDbUc4R9aLX7Nzhj1Cy?hs=5f358d3782c04ec53bb949a82f7b9763& πŸ“Œ on June 5, 2025 6:23 pm

      rjsuj1

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya naneΒ  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.