Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 05

    In the name of LOVE – 04

    In the name of LOVE – 03

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Love & Pain Sehemu Ya Sita (06)
    Hadithi

    Love & Pain Sehemu Ya Sita (06)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaNovember 15, 2024Updated:November 21, 20248 Comments9 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Love & Pain
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Lucia alimpatia Noela bahasha hiyo yenye taarifa muhimu zaย  kesi, Desmond aliona makabidhiano hayo ya Bahasha kishaย  wawili hao waliagana kila mmoja akashika barabara yake.ย  Desmond aliona ni bora amfuatilie Mpenzi wake Noela iliย  kujuwa Bahasha hiyo ilikuwa na nini. Basi, baada ya kutokaย  hapo Noela alielekea moja kwa moja nyumbani kwao, alipoingiaย  ndani aliiweka Bahasha hiyo kwenye Shefu maalum yaย  kuhifahdhia nyaraka zake, alifunga kwa namba maalum kishaย  alijipumzisha kitandani.ย 

    Akiwa hapo nje Desmond alipokea simu ya Polisi mpeleleziย  akaambiwa anahitajika haraka kituoni, mara moja aliwasha gariย  bila kumwambia Noela kuwa alikuwa nje ya nyumba yao,ย  akaelekea kituoni. Huko alioneshwa gari ambayo maitiย  ilikutwa, gari hiyo ilikuwa ni Landlover ya zamani ambayoย  ilidaiwa kuwa usajili wake haukujulikana. Endeleaย 

    SEHEMU YA SITA

    “Hii ndiyo gari yenyewe ambayo ilikutwa ndani ya Bahari ikiwaย  na mwili wa Sanga, hadi kufikia sasa tumempoteza mshukiwaย  namba moja ambaye angetusaidia kujuwa mambo mengiย  yaliyojificha kuhusu kesi ya Mkeo” Alisema Polisi huyo wakiwaย  wamesimama kando ya gari hilo, Desmond alilitazama sana gariย  hilo alafu akakumbuka siku ya tukio kuwa gari aliyoitumiaย  ilikuwa ni Audi A4 na siyo Landlover hiyo chakavu.ย 

    Bado aliendelea kujiuliza Mtu wa tatu ni nani?ย 

    “Kwa maana hiyo uchunguzi wa kesi utaanza upya ili kumpataย  mshukiwa mwingine wa matukio haya, inaonesha Sanga alifungiwaย  ndani ya gari kisha akatupwa Baharini ili afe, yupo Muuwajiย  nyuma ya hili” Alisema tena Polisi huyo huku Desmondย  akijiambiaย 

    “Muuwaji ni Mimi lakini hamtokuja mnijuwe” alisema ndani yaย  nafsi yake, basi baada ya kumaliza kufanya mazungumzo hapoย  Kituoni aliondoka zake, alimfikiria sana huyo Mtu wa tatuย  kisha akili yake ikawa inamwambia kuwa Mtu wa tatu ni Luciaย 

    Akapata wazo la kutaka kujuwa Noela alipokea bahasha ya nini,ย  alimpigia Noela akamuuliza yuko wapi, Noela alimwambia kuwaย  yupo Mjini anaangalia gauni la kuvaa siku ya kuvishwa pete,ย  basi Desmond aliutumia mwanya huo kwenda nyumbani anakoishiaย  Noela na Mama yake.

    Alisalimiana kwa Bashasha na Mama Noela, Mama huyo alikuwaย  akimpenda sana Desmond amuowe Mwanaye hivyo kumuona hapoย  ilikuwa ni jambo la furaha sana, Mama Noela aliingia jikoniย  kumpikia Mkwe wake mtarajiwa, Desmond aliitumia nafasi hiyoย  kuingia chumbani kwa Noela ili aitafute ile Bahasha maanaย  alijuwa tu inaweza kuwa na taarifa mbaya dhidi yakeย 

    Alipekua kila mahali hadi alichoka lakini hakufanikiwaย  kuiyona ile bahasha, aliamini Bahasha ilikuwa mlemle ndani,ย  alizidi kuitafuta bila mafanikio, alitumia muda mrefuย  kufikiria na kuitafuta Bahasha bila kuipata maana aliiwekaย  kwenye shefu ambayo aliificha mahali, jasho lilimtoka Desmondย  huku akizidi kutafakari itakuwa ipo sehemu gani.ย 

    Baadaye alisikia mlio wa gari ya Noela, alipochunguliaย  dirisha alimuona Noela akishuka kwenye gari, haraka alijuwaย  akikutwa hapo ndani bila taarifa atashtukiwa, aliangalia kamaย  kuna kitu ambacho hakikukaa sawa, haraka alikirudisha kishaย  alitoka chumbani, alifuta jasho akaketi sebleni, uzuri niย  kuwa Mama yake Noela muda wote alikuwa jikoni hivyoย  hakufanikiwa kujuwa kama Desmond aliingia Chumbani kwa Noela.ย 

    Alipoingia Sebleni alishangaa kumuona Desmond ambaye alikuwaย  akimfahamu kama Joshuaย 

    “Eeeh Baby umekuja saa ngapi?” Aliuliza Noela akiwa mwenyeย  furaha na mshangao juu tena akiwa anaweka chini mizigoย  aliyokuja nayo, kisha alimrudia Desmondย 

    “Nimekuja muda mrefu sana, nimekaa hapa kwa muda mrefuย  kukusubiria uje” Alijibu Desmond kama siyo yeye vileย  aliyekuwa akipekuwa chumbani kwa Noela kuitafuta ile Bahasha.ย 

    “Ndiyo amekuja muda mrefu nikawa naandaa Chakula” Ilisikikaย  sauti ya Mama yake Noela ( Mlami ) kisha naye alisogea karibuย 

    “Chakula tayari Baba” Mama Noela alimwambia Desmondย 

    “Ah Mama asante sana” Alisema Desmond kisha alienda kupataย  chakula wakati huo Noela akiwa amepumzika kwenye sofaย  akionekana kuchoka, wakiwa mbali mbali Desmond alimtupiaย  Noela swaliย 

    “Unaoneakana umechoka sana vipi ulifanikiwa?” Aliulizaย  kwasababu Noela alienda kuangalia gauni la kuvaa siku yaย  kuvishwa peteย 

    “Ndiyo nimefanikiwa lipo kwenye mfuko” Alijibu noela, Desmondย  aliendelea kula hadi alipomaliza akaaga akaondoka zake bilaย kufanikiwa kuipata ile baasha ambayo ilikuwa ikimpa wasiwasi,ย  baadaye Noela aliingia chumbani lakini aliona kama kunaย  baadhi ya vitu vyake vimekaa tofauti siyo kama alivyoviacha,ย  alipata shahuku ya kuzidi kukagua aliona ishara ile ileย  akahisi moja kwa moja chumba chake kilipekuliwa, alirudiย  sebleni kwa Mama yake akamuulizaย 

    “Mama Nani amepekua chumbani kwangu?” Alihoji Noela akiwaย  mwenye kushangaaย 

    “Kupekua? Mmh mbona hakuna aliyeingia huko…” alijibu Mamaย  Noela sababu hakunuona Desmond akiwa ameingia hukoย 

    “Ina maana kumejipekua kwenyewe eti Mama? Vitu nilivyoachaย  siyo nilivyokuta ndiyo maana nimekuuliza, Mlami utasemajeย  hujui wakati upo nyumbani muda wote?”ย 

    “Aaah au Joshua aliingia huko? Lakini hapana mbona aliketiย  hapa muda wote”ย 

    “aaah” Aligugumia Noela kisha alirudi chumbani, alichukuaย  simu akampigia Desmond akamuuliza kama aliingia chumbaniย  kwake, Desmond alimkatalia kuwa hakuingia huko, basi simuย  ilikatika huku ikimuacha na maswali mengi Noela kuwa ni Naniย  aliingia huko na alienda kufanya nini.ย 

    Ndani ya Hospitali kubwa, Desmond alienda kumuangalia Mkeย  wake ambaye ni adui mkubwa kwake, kilichomshangaza niย  kuzuiliwa kuingia kwenye chumba ambacho Mke wake Mandyย  alikuwa amewekwa kwa ajili ya matibabu, yalikuwa ni maombi yaย  Nesi Lucia kwa daktari mkuu wa Hospitali.ย 

    Alilalamika Desmondย 

    “Nazuiliwa vipi kumuona Mke wangu wa ndoa? Kwanini anapelekwaย  kwenye wodi nyingine bila kunitaarifu Mimi?” Alihoji akiwaย  mbele ya nesi mmoja, Nesi Lucia alikuwa amejibanza mahaliย  akimfuatilia Desmond, alikuwa na mashaka sana na Desmondย  tokea ile siku ambayo Desmond alienda na Mwanasheria paleย  Hospitalini na kumsainisha Mandy kwa alama ya kidole.ย 

    Desmond alichanganikiwa kwa jambo moja, kama Mke wake ataamkaย  atasema Nani alimuuwa Mama yake Kitu ambacho Desmondย  alipambana kuhakikisha hakuna siri inayotoka.ย 

    “Ni maagizo kutoka kwa Dokta Mkuu wa Hospitali nasiย  tunayafuata” Alisema Nesi huyo wa kiume, Desmond hakutakaย  kusema tena baada ya kusikia kuwa maagizo ya kuzuiliwaย  yaliyoka kwa Dakatri Mkuu wa Hospitali hiyo. Alitembea kishaย  aliketi kwenye Kiti akakumbuka jambo

    Alikumbuka siku moja mvua kubwa ilikuwa ikinyesha, mvua hiyoย  iliambatana na radi za hapa na pale, alikuwa akiendesha gariย  huku akionekana kuwa mwenye kutafakari jambo zito kichwani,ย  nyuma yake kulikuwa na gari nyeusi iliyokuwa ikimfuataย  taratibu, Desmond hakuiyona.ย 

    Gari hiyo nyeusi iliyo nyuma yake ndani kulikuwa na Mama Mtuย  mzima, Mama huyo alikuwa ni Mama yake Mandy, Mama Mandyย  alipata taarifa kuwa Desmond amepanga kukutana na Mwanasheriaย  wa Mandy kisha wabadilishe hati za mali za Mandy.ย 

    Mama Mandy alizidi kumfuatilia Desmond Usiku huo ambaoย  uliambatana na mvua na upepo, safari hiyo ilikita nje ya Mjiย  huo waliokuwa wakiishi tena katika ghofu moja ambaloย  Mwanasheria wa Mandy aliyeitwa Joel alikuwa akimsubiriaย  Desmond.ย 

    Mama Mandy alionekana kuwa makini sana kumfuatilia Desmond,ย  alikuwa peke yake, hakujuwa kuwa Desmond alikuwa ameshashtukaย  kuwa kuna gari iliyokuwa ikimfuatilia kwa nyuma, Mama Mandyย  alipoona gari ya Desmond imesimama naye alisimamisha gari kwaย  mbali kidogo kisha alishuka akawa anatembea kwenye mvuaย  taratibu huku akiwa makini mno, alisogea taratibu sana hadiย  kwenye gari ya Desmond lakini hakumuona Desmond, Usiku huoย  ulijaa giza kiasi.ย 

    Alipoangalia vizuri mbele aliona ghofu, alipata wazo kuwaย  huenda Desmond atakuwa ameingia humo, basi alisogea hadiย  ndani ya Ghofu hilo ambalo lilionekana kuwa kimya sana,ย  hakukuwa na Mtu yeyote yule kitu ambacho kilizidiย  kumshangaza.ย 

    Akachukua simu yake ili ampigie Mandy amueleze mahali alipoย  pia amwambie Binti yake juu ya Mchezo mchafu aliokuwaย  akiufanya Desmond, kabla hata hajapiga simu alisikia hatuaย  nyuma yake alipogeuka alimuona Desmond akiwa amesimama nyumaย  yake, alipoangalia mikono ya Desmond haraka aliona amevaliaย  Gloves.ย 

    “Desmond! Unataka kufanya nini?” Aliuliza Mama yake Mandyย  akiwa anavujwa na maji kwenye mwili kutokana na ile mvuaย  iliyompiga kule njeย 

    “Uchafu unaoufanya umefika mwisho Joshua, kila siku nilikuwaย  nikimwambia Mandy kuwa wewe huna mapenzi naye bali unahitajiย  mali za Mtoto wangu, Mwanasheria Joel yupo wapi?” Aliulizaย  Mama Mandy, Desmond alihema kidogo kisha Joel alijitokeza

    “Hadi wewe Joel? Unajuwa ni kiasi gani familia inakuaminiย  Joel? Unashiriki uchafu mkubwa kama Huu, hili siweziย  kulifumbia macho, nyote mnaingia kwenye mikono ya sheria”ย  Alisema Mama Mandy kisha alionekana kutaka kupiga Simu lakiniย  haraka Desmond alimuwahi, akampora simu akaona alikuwaย  anataka kumpigia Mandyย 

    “Unataka kufanya nini Mama? Unataka nifungwe? Unataka niweย  Masikini au unataka Mtoto wako aniache? Hii ni siri ambayoย  hukupaswa kuifuatilia Mama…..” Alisema Desmond hukuย  akijikaza lakini alikuwa akiumia sana ndani ya Moyo wakeย 

    “Mandy ni lazima atajuwa kuwa wewe si Mtu mzuri na ninaย  ushahidi wa video na picha ambazo nimetumiwa, umekuwaย  ukikutana na Joel kila siku Jioni na kupanga mipango yenuย  michafu..” Alisema Mama yake Mandyย 

    “Pole Mama kwasababu hutoweza kufanya hivyo” alisema Desmondย  haraka alikata waya uliokuwa ukining’inia kisha akamnyongaย  Mama yake Mandy hadi alipofanikiwa kummaliza, Mwanasheriaย  Joel alikunja uso wake kuashiria kuwa jambo hilo halikuwa laย  kawaida.ย 

    “Joel Mimi na wewe tumeuwa hapa sawa? Tunapaswa kuondoka naย  kukaa kimya, nipe hizo nyaraka” Alisema Desmond, harakaย  alipewa nyaraka kisha Joel alisemaย 

    “Bado saini ya Mtu mmoja tu, Mkeo Mandy”ย 

    “Nitajuwa nini cha kufanya” Alisema Desmond kisha harakaย  walianza kutoka lakini Desmond aligeuka kuutazama mwili waย  Mama Mandy, alikuwa amevalia cheni ya Dhahabu yenye thamaniย  kubwa sana, alirudi akamvua kisha akaiweka kwenye koti laย  suti yake, alafu alisemaย 

    “Sisi ni Watoto wa kimasikini sana”ย 

    Kumbukumbu ya Desmond iliishia hapo, alitikisa kichwa chakeย  kisha alielekea ofisini kwa Daktari wa Hospitali, Daktariย  alipomuona Desmond alijuwa nini kimemleta, Desmond alianzaย  kumshambulia Daktari huyo kwa manenoย 

    “Umeagiza Mke wangu apelekwe Wodi nyingine alafu Mimiย  nizuiliwe kumuona si ndiyo? Hivi unajuwa ulichokifanya?”ย  Alisema Desmond kwa hasiraย 

    “Desmond hebu kaa kwanza tuongee, hili jambo siyo laย  kulichukulia jazba, tulichofanya ni kupandisha darajaย  matibabu ya Mkeo ili aweze kuamka haraka ” Alisema Daktariย  huyo kwa upole sana

    Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA SABA

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya kuendelea kutuma SIMULIZI Mpya Na Kuipost HAPA Kwa kumtumia Chochote kupitia

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love &Pain Love & Painย 

    ย ย 

    Love & Pain

    8 Comments

    1. Fawziya Hassan on November 15, 2024 4:42 pm

      Eee!! Umaskini utawapeleka watu pahala pabaya sana๐Ÿ˜ฅ

      Asante mtunzi kwa stori yenye mafunzo na mazingatio makubwa.

      More Love from Kenya โค๏ธ

      Reply
    2. Sir, Yowas on November 15, 2024 8:05 pm

      Sawa

      Reply
    3. Junior Jr on November 15, 2024 9:32 pm

      Hii story noma sana

      Reply
    4. Roddrigo on November 16, 2024 7:50 am

      SIMULIZI|SIRI ZA GIZA.
      SIMULIZI ya kijana machachari anayelijua jiji,mkasa huu unamwonesha yumo katika Giza na vingi vya ajabu vinamstaajabisha,anashangaa ulimwengu usiotarajiwa machono pake.

      Isome hapa
      ______

      https://maishakitaaonlinetz.blogspot.com/2024/11/simulizisiri-za-giza.html

      Reply
    5. Rau B on November 16, 2024 5:22 pm

      Update Za michezo na Hadithi fupi
      Njia hii hapa

      https://whatsapp.com/channel/0029VanxLVYJ93wbHawAAh3H/701

      Reply
    6. Sharo love malkx ๐Ÿ’– on November 17, 2024 2:27 pm

      NANDY APEWE NA ULINZI UKO HOSPITALI
      ๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†

      Reply
    7. ๐Ÿ“Œ Email: Operation 1.593059 BTC. Verify =>> https://yandex.com/poll/T1TnDbUc4R9aLX7Nzhj1Cy?hs=5f358d3782c04ec53bb949a82f7b9763& ๐Ÿ“Œ on June 5, 2025 6:23 pm

      rjsuj1

      Reply
    8. ๐Ÿ”Ž Email- SENDING 1,22191 bitcoin. Get => https://graph.org/Payout-from-Blockchaincom-06-26?hs=5f358d3782c04ec53bb949a82f7b9763& ๐Ÿ”Ž on July 8, 2025 9:33 am

      ssghj3

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi September 15, 2025

    In the name of LOVE – 05

    Ilipoishia sehemu ya tatu ya In the name of LOVE โ€œBasi hakuna shida Zaylisa, mnaweza…

    In the name of LOVE – 04

    In the name of LOVE – 03

    In the name of LOVE – 02

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.