Ilipoishia “Lucia alimpatia Noela bahasha hiyo yenye taarifa muhimu zaย kesi, Desmond aliona makabidhiano hayo ya Bahasha kishaย wawili hao waliagana kila mmoja akashika barabara yake.ย Desmond aliona ni bora amfuatilie Mpenzi wake Noela iliย kujuwa Bahasha hiyo ilikuwa na nini. Basi, baada ya kutokaย hapo Noela alielekea moja kwa moja nyumbani kwao, alipoingiaย ndani aliiweka Bahasha hiyo kwenye Shefu maalum yaย kuhifahdhia nyaraka zake, alifunga kwa namba maalum kishaย alijipumzisha kitandani.ย
Akiwa hapo nje Desmond alipokea simu ya Polisi mpeleleziย akaambiwa anahitajika haraka kituoni, mara moja aliwasha gariย bila kumwambia Noela kuwa alikuwa nje ya nyumba yao,ย akaelekea kituoni. Huko alioneshwa gari ambayo maitiย ilikutwa, gari hiyo ilikuwa ni Landlover ya zamani ambayoย ilidaiwa kuwa usajili wake haukujulikana. Endeleaย
SEHEMU YA SITA
“Hii ndiyo gari yenyewe ambayo ilikutwa ndani ya Bahari ikiwaย na mwili wa Sanga, hadi kufikia sasa tumempoteza mshukiwaย namba moja ambaye angetusaidia kujuwa mambo mengiย yaliyojificha kuhusu kesi ya Mkeo” Alisema Polisi huyo wakiwaย wamesimama kando ya gari hilo, Desmond alilitazama sana gariย hilo alafu akakumbuka siku ya tukio kuwa gari aliyoitumiaย ilikuwa ni Audi A4 na siyo Landlover hiyo chakavu.ย
Bado aliendelea kujiuliza Mtu wa tatu ni nani?ย
“Kwa maana hiyo uchunguzi wa kesi utaanza upya ili kumpataย mshukiwa mwingine wa matukio haya, inaonesha Sanga alifungiwaย ndani ya gari kisha akatupwa Baharini ili afe, yupo Muuwajiย nyuma ya hili” Alisema tena Polisi huyo huku Desmondย akijiambiaย
“Muuwaji ni Mimi lakini hamtokuja mnijuwe” alisema ndani yaย nafsi yake, basi baada ya kumaliza kufanya mazungumzo hapoย Kituoni aliondoka zake, alimfikiria sana huyo Mtu wa tatuย kisha akili yake ikawa inamwambia kuwa Mtu wa tatu ni Luciaย
Akapata wazo la kutaka kujuwa Noela alipokea bahasha ya nini,ย alimpigia Noela akamuuliza yuko wapi, Noela alimwambia kuwaย yupo Mjini anaangalia gauni la kuvaa siku ya kuvishwa pete,ย basi Desmond aliutumia mwanya huo kwenda nyumbani anakoishiaย Noela na Mama yake.
Alisalimiana kwa Bashasha na Mama Noela, Mama huyo alikuwaย akimpenda sana Desmond amuowe Mwanaye hivyo kumuona hapoย ilikuwa ni jambo la furaha sana, Mama Noela aliingia jikoniย kumpikia Mkwe wake mtarajiwa, Desmond aliitumia nafasi hiyoย kuingia chumbani kwa Noela ili aitafute ile Bahasha maanaย alijuwa tu inaweza kuwa na taarifa mbaya dhidi yakeย
Alipekua kila mahali hadi alichoka lakini hakufanikiwaย kuiyona ile bahasha, aliamini Bahasha ilikuwa mlemle ndani,ย alizidi kuitafuta bila mafanikio, alitumia muda mrefuย kufikiria na kuitafuta Bahasha bila kuipata maana aliiwekaย kwenye shefu ambayo aliificha mahali, jasho lilimtoka Desmondย huku akizidi kutafakari itakuwa ipo sehemu gani.ย
Baadaye alisikia mlio wa gari ya Noela, alipochunguliaย dirisha alimuona Noela akishuka kwenye gari, haraka alijuwaย akikutwa hapo ndani bila taarifa atashtukiwa, aliangalia kamaย kuna kitu ambacho hakikukaa sawa, haraka alikirudisha kishaย alitoka chumbani, alifuta jasho akaketi sebleni, uzuri niย kuwa Mama yake Noela muda wote alikuwa jikoni hivyoย hakufanikiwa kujuwa kama Desmond aliingia Chumbani kwa Noela.ย
Alipoingia Sebleni alishangaa kumuona Desmond ambaye alikuwaย akimfahamu kama Joshuaย
“Eeeh Baby umekuja saa ngapi?” Aliuliza Noela akiwa mwenyeย furaha na mshangao juu tena akiwa anaweka chini mizigoย aliyokuja nayo, kisha alimrudia Desmondย
“Nimekuja muda mrefu sana, nimekaa hapa kwa muda mrefuย kukusubiria uje” Alijibu Desmond kama siyo yeye vileย aliyekuwa akipekuwa chumbani kwa Noela kuitafuta ile Bahasha.ย
“Ndiyo amekuja muda mrefu nikawa naandaa Chakula” Ilisikikaย sauti ya Mama yake Noela ( Mlami ) kisha naye alisogea karibuย
“Chakula tayari Baba” Mama Noela alimwambia Desmondย
“Ah Mama asante sana” Alisema Desmond kisha alienda kupataย chakula wakati huo Noela akiwa amepumzika kwenye sofaย akionekana kuchoka, wakiwa mbali mbali Desmond alimtupiaย Noela swaliย
“Unaoneakana umechoka sana vipi ulifanikiwa?” Aliulizaย kwasababu Noela alienda kuangalia gauni la kuvaa siku yaย kuvishwa peteย
“Ndiyo nimefanikiwa lipo kwenye mfuko” Alijibu noela, Desmondย aliendelea kula hadi alipomaliza akaaga akaondoka zake bilaย kufanikiwa kuipata ile baasha ambayo ilikuwa ikimpa wasiwasi,ย baadaye Noela aliingia chumbani lakini aliona kama kunaย baadhi ya vitu vyake vimekaa tofauti siyo kama alivyoviacha,ย alipata shahuku ya kuzidi kukagua aliona ishara ile ileย akahisi moja kwa moja chumba chake kilipekuliwa, alirudiย sebleni kwa Mama yake akamuulizaย
“Mama Nani amepekua chumbani kwangu?” Alihoji Noela akiwaย mwenye kushangaaย
“Kupekua? Mmh mbona hakuna aliyeingia huko…” alijibu Mamaย Noela sababu hakunuona Desmond akiwa ameingia hukoย
“Ina maana kumejipekua kwenyewe eti Mama? Vitu nilivyoachaย siyo nilivyokuta ndiyo maana nimekuuliza, Mlami utasemajeย hujui wakati upo nyumbani muda wote?”ย
“Aaah au Joshua aliingia huko? Lakini hapana mbona aliketiย hapa muda wote”ย
“aaah” Aligugumia Noela kisha alirudi chumbani, alichukuaย simu akampigia Desmond akamuuliza kama aliingia chumbaniย kwake, Desmond alimkatalia kuwa hakuingia huko, basi simuย ilikatika huku ikimuacha na maswali mengi Noela kuwa ni Naniย aliingia huko na alienda kufanya nini.ย
Ndani ya Hospitali kubwa, Desmond alienda kumuangalia Mkeย wake ambaye ni adui mkubwa kwake, kilichomshangaza niย kuzuiliwa kuingia kwenye chumba ambacho Mke wake Mandyย alikuwa amewekwa kwa ajili ya matibabu, yalikuwa ni maombi yaย Nesi Lucia kwa daktari mkuu wa Hospitali.ย
Alilalamika Desmondย
“Nazuiliwa vipi kumuona Mke wangu wa ndoa? Kwanini anapelekwaย kwenye wodi nyingine bila kunitaarifu Mimi?” Alihoji akiwaย mbele ya nesi mmoja, Nesi Lucia alikuwa amejibanza mahaliย akimfuatilia Desmond, alikuwa na mashaka sana na Desmondย tokea ile siku ambayo Desmond alienda na Mwanasheria paleย Hospitalini na kumsainisha Mandy kwa alama ya kidole.ย
Desmond alichanganikiwa kwa jambo moja, kama Mke wake ataamkaย atasema Nani alimuuwa Mama yake Kitu ambacho Desmondย alipambana kuhakikisha hakuna siri inayotoka.ย
“Ni maagizo kutoka kwa Dokta Mkuu wa Hospitali nasiย tunayafuata” Alisema Nesi huyo wa kiume, Desmond hakutakaย kusema tena baada ya kusikia kuwa maagizo ya kuzuiliwaย yaliyoka kwa Dakatri Mkuu wa Hospitali hiyo. Alitembea kishaย aliketi kwenye Kiti akakumbuka jambo
Alikumbuka siku moja mvua kubwa ilikuwa ikinyesha, mvua hiyoย iliambatana na radi za hapa na pale, alikuwa akiendesha gariย huku akionekana kuwa mwenye kutafakari jambo zito kichwani,ย nyuma yake kulikuwa na gari nyeusi iliyokuwa ikimfuataย taratibu, Desmond hakuiyona.ย
Gari hiyo nyeusi iliyo nyuma yake ndani kulikuwa na Mama Mtuย mzima, Mama huyo alikuwa ni Mama yake Mandy, Mama Mandyย alipata taarifa kuwa Desmond amepanga kukutana na Mwanasheriaย wa Mandy kisha wabadilishe hati za mali za Mandy.ย
Mama Mandy alizidi kumfuatilia Desmond Usiku huo ambaoย uliambatana na mvua na upepo, safari hiyo ilikita nje ya Mjiย huo waliokuwa wakiishi tena katika ghofu moja ambaloย Mwanasheria wa Mandy aliyeitwa Joel alikuwa akimsubiriaย Desmond.ย
Mama Mandy alionekana kuwa makini sana kumfuatilia Desmond,ย alikuwa peke yake, hakujuwa kuwa Desmond alikuwa ameshashtukaย kuwa kuna gari iliyokuwa ikimfuatilia kwa nyuma, Mama Mandyย alipoona gari ya Desmond imesimama naye alisimamisha gari kwaย mbali kidogo kisha alishuka akawa anatembea kwenye mvuaย taratibu huku akiwa makini mno, alisogea taratibu sana hadiย kwenye gari ya Desmond lakini hakumuona Desmond, Usiku huoย ulijaa giza kiasi.ย
Alipoangalia vizuri mbele aliona ghofu, alipata wazo kuwaย huenda Desmond atakuwa ameingia humo, basi alisogea hadiย ndani ya Ghofu hilo ambalo lilionekana kuwa kimya sana,ย hakukuwa na Mtu yeyote yule kitu ambacho kilizidiย kumshangaza.ย
Akachukua simu yake ili ampigie Mandy amueleze mahali alipoย pia amwambie Binti yake juu ya Mchezo mchafu aliokuwaย akiufanya Desmond, kabla hata hajapiga simu alisikia hatuaย nyuma yake alipogeuka alimuona Desmond akiwa amesimama nyumaย yake, alipoangalia mikono ya Desmond haraka aliona amevaliaย Gloves.ย
“Desmond! Unataka kufanya nini?” Aliuliza Mama yake Mandyย akiwa anavujwa na maji kwenye mwili kutokana na ile mvuaย iliyompiga kule njeย
“Uchafu unaoufanya umefika mwisho Joshua, kila siku nilikuwaย nikimwambia Mandy kuwa wewe huna mapenzi naye bali unahitajiย mali za Mtoto wangu, Mwanasheria Joel yupo wapi?” Aliulizaย Mama Mandy, Desmond alihema kidogo kisha Joel alijitokeza
“Hadi wewe Joel? Unajuwa ni kiasi gani familia inakuaminiย Joel? Unashiriki uchafu mkubwa kama Huu, hili siweziย kulifumbia macho, nyote mnaingia kwenye mikono ya sheria”ย Alisema Mama Mandy kisha alionekana kutaka kupiga Simu lakiniย haraka Desmond alimuwahi, akampora simu akaona alikuwaย anataka kumpigia Mandyย
“Unataka kufanya nini Mama? Unataka nifungwe? Unataka niweย Masikini au unataka Mtoto wako aniache? Hii ni siri ambayoย hukupaswa kuifuatilia Mama…..” Alisema Desmond hukuย akijikaza lakini alikuwa akiumia sana ndani ya Moyo wakeย
“Mandy ni lazima atajuwa kuwa wewe si Mtu mzuri na ninaย ushahidi wa video na picha ambazo nimetumiwa, umekuwaย ukikutana na Joel kila siku Jioni na kupanga mipango yenuย michafu..” Alisema Mama yake Mandyย
“Pole Mama kwasababu hutoweza kufanya hivyo” alisema Desmondย haraka alikata waya uliokuwa ukining’inia kisha akamnyongaย Mama yake Mandy hadi alipofanikiwa kummaliza, Mwanasheriaย Joel alikunja uso wake kuashiria kuwa jambo hilo halikuwa laย kawaida.ย
“Joel Mimi na wewe tumeuwa hapa sawa? Tunapaswa kuondoka naย kukaa kimya, nipe hizo nyaraka” Alisema Desmond, harakaย alipewa nyaraka kisha Joel alisemaย
“Bado saini ya Mtu mmoja tu, Mkeo Mandy”ย
“Nitajuwa nini cha kufanya” Alisema Desmond kisha harakaย walianza kutoka lakini Desmond aligeuka kuutazama mwili waย Mama Mandy, alikuwa amevalia cheni ya Dhahabu yenye thamaniย kubwa sana, alirudi akamvua kisha akaiweka kwenye koti laย suti yake, alafu alisemaย
“Sisi ni Watoto wa kimasikini sana”ย
Kumbukumbu ya Desmond iliishia hapo, alitikisa kichwa chakeย kisha alielekea ofisini kwa Daktari wa Hospitali, Daktariย alipomuona Desmond alijuwa nini kimemleta, Desmond alianzaย kumshambulia Daktari huyo kwa manenoย
“Umeagiza Mke wangu apelekwe Wodi nyingine alafu Mimiย nizuiliwe kumuona si ndiyo? Hivi unajuwa ulichokifanya?”ย Alisema Desmond kwa hasiraย
“Desmond hebu kaa kwanza tuongee, hili jambo siyo laย kulichukulia jazba, tulichofanya ni kupandisha darajaย matibabu ya Mkeo ili aweze kuamka haraka ” Alisema Daktariย huyo kwa upole sana
Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA SABA
Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya kuendelea kutuma SIMULIZI Mpya Na Kuipost HAPA Kwa kumtumia Chochote kupitia
Lipa Namba: 57900454
Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
Mtandao: VODACOMย ย
SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย
SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย
SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย
JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa
Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love &Pain Love & Painย
ย ย
8 Comments
Eee!! Umaskini utawapeleka watu pahala pabaya sana๐ฅ
Asante mtunzi kwa stori yenye mafunzo na mazingatio makubwa.
More Love from Kenya โค๏ธ
Sawa
Hii story noma sana
SIMULIZI|SIRI ZA GIZA.
SIMULIZI ya kijana machachari anayelijua jiji,mkasa huu unamwonesha yumo katika Giza na vingi vya ajabu vinamstaajabisha,anashangaa ulimwengu usiotarajiwa machono pake.
Isome hapa
______
https://maishakitaaonlinetz.blogspot.com/2024/11/simulizisiri-za-giza.html
Update Za michezo na Hadithi fupi
Njia hii hapa
https://whatsapp.com/channel/0029VanxLVYJ93wbHawAAh3H/701
NANDY APEWE NA ULINZI UKO HOSPITALI
๐๐๐๐
rjsuj1
ssghj3