Ilipoishia “Lucia alimpatia Noela bahasha hiyo yenye taarifa muhimu zaΒ kesi, Desmond aliona makabidhiano hayo ya Bahasha kishaΒ wawili hao waliagana kila mmoja akashika barabara yake.Β Desmond aliona ni bora amfuatilie Mpenzi wake Noela iliΒ kujuwa Bahasha hiyo ilikuwa na nini. Basi, baada ya kutokaΒ hapo Noela alielekea moja kwa moja nyumbani kwao, alipoingiaΒ ndani aliiweka Bahasha hiyo kwenye Shefu maalum yaΒ kuhifahdhia nyaraka zake, alifunga kwa namba maalum kishaΒ alijipumzisha kitandani.Β
Akiwa hapo nje Desmond alipokea simu ya Polisi mpeleleziΒ akaambiwa anahitajika haraka kituoni, mara moja aliwasha gariΒ bila kumwambia Noela kuwa alikuwa nje ya nyumba yao,Β akaelekea kituoni. Huko alioneshwa gari ambayo maitiΒ ilikutwa, gari hiyo ilikuwa ni Landlover ya zamani ambayoΒ ilidaiwa kuwa usajili wake haukujulikana. EndeleaΒ
SEHEMU YA SITA
“Hii ndiyo gari yenyewe ambayo ilikutwa ndani ya Bahari ikiwaΒ na mwili wa Sanga, hadi kufikia sasa tumempoteza mshukiwaΒ namba moja ambaye angetusaidia kujuwa mambo mengiΒ yaliyojificha kuhusu kesi ya Mkeo” Alisema Polisi huyo wakiwaΒ wamesimama kando ya gari hilo, Desmond alilitazama sana gariΒ hilo alafu akakumbuka siku ya tukio kuwa gari aliyoitumiaΒ ilikuwa ni Audi A4 na siyo Landlover hiyo chakavu.Β
Bado aliendelea kujiuliza Mtu wa tatu ni nani?Β
“Kwa maana hiyo uchunguzi wa kesi utaanza upya ili kumpataΒ mshukiwa mwingine wa matukio haya, inaonesha Sanga alifungiwaΒ ndani ya gari kisha akatupwa Baharini ili afe, yupo MuuwajiΒ nyuma ya hili” Alisema tena Polisi huyo huku DesmondΒ akijiambiaΒ
“Muuwaji ni Mimi lakini hamtokuja mnijuwe” alisema ndani yaΒ nafsi yake, basi baada ya kumaliza kufanya mazungumzo hapoΒ Kituoni aliondoka zake, alimfikiria sana huyo Mtu wa tatuΒ kisha akili yake ikawa inamwambia kuwa Mtu wa tatu ni LuciaΒ
Akapata wazo la kutaka kujuwa Noela alipokea bahasha ya nini,Β alimpigia Noela akamuuliza yuko wapi, Noela alimwambia kuwaΒ yupo Mjini anaangalia gauni la kuvaa siku ya kuvishwa pete,Β basi Desmond aliutumia mwanya huo kwenda nyumbani anakoishiaΒ Noela na Mama yake.
Alisalimiana kwa Bashasha na Mama Noela, Mama huyo alikuwaΒ akimpenda sana Desmond amuowe Mwanaye hivyo kumuona hapoΒ ilikuwa ni jambo la furaha sana, Mama Noela aliingia jikoniΒ kumpikia Mkwe wake mtarajiwa, Desmond aliitumia nafasi hiyoΒ kuingia chumbani kwa Noela ili aitafute ile Bahasha maanaΒ alijuwa tu inaweza kuwa na taarifa mbaya dhidi yakeΒ
Alipekua kila mahali hadi alichoka lakini hakufanikiwaΒ kuiyona ile bahasha, aliamini Bahasha ilikuwa mlemle ndani,Β alizidi kuitafuta bila mafanikio, alitumia muda mrefuΒ kufikiria na kuitafuta Bahasha bila kuipata maana aliiwekaΒ kwenye shefu ambayo aliificha mahali, jasho lilimtoka DesmondΒ huku akizidi kutafakari itakuwa ipo sehemu gani.Β
Baadaye alisikia mlio wa gari ya Noela, alipochunguliaΒ dirisha alimuona Noela akishuka kwenye gari, haraka alijuwaΒ akikutwa hapo ndani bila taarifa atashtukiwa, aliangalia kamaΒ kuna kitu ambacho hakikukaa sawa, haraka alikirudisha kishaΒ alitoka chumbani, alifuta jasho akaketi sebleni, uzuri niΒ kuwa Mama yake Noela muda wote alikuwa jikoni hivyoΒ hakufanikiwa kujuwa kama Desmond aliingia Chumbani kwa Noela.Β
Alipoingia Sebleni alishangaa kumuona Desmond ambaye alikuwaΒ akimfahamu kama JoshuaΒ
“Eeeh Baby umekuja saa ngapi?” Aliuliza Noela akiwa mwenyeΒ furaha na mshangao juu tena akiwa anaweka chini mizigoΒ aliyokuja nayo, kisha alimrudia DesmondΒ
“Nimekuja muda mrefu sana, nimekaa hapa kwa muda mrefuΒ kukusubiria uje” Alijibu Desmond kama siyo yeye vileΒ aliyekuwa akipekuwa chumbani kwa Noela kuitafuta ile Bahasha.Β
“Ndiyo amekuja muda mrefu nikawa naandaa Chakula” IlisikikaΒ sauti ya Mama yake Noela ( Mlami ) kisha naye alisogea karibuΒ
“Chakula tayari Baba” Mama Noela alimwambia DesmondΒ
“Ah Mama asante sana” Alisema Desmond kisha alienda kupataΒ chakula wakati huo Noela akiwa amepumzika kwenye sofaΒ akionekana kuchoka, wakiwa mbali mbali Desmond alimtupiaΒ Noela swaliΒ
“Unaoneakana umechoka sana vipi ulifanikiwa?” AliulizaΒ kwasababu Noela alienda kuangalia gauni la kuvaa siku yaΒ kuvishwa peteΒ
“Ndiyo nimefanikiwa lipo kwenye mfuko” Alijibu noela, DesmondΒ aliendelea kula hadi alipomaliza akaaga akaondoka zake bilaΒ kufanikiwa kuipata ile baasha ambayo ilikuwa ikimpa wasiwasi,Β baadaye Noela aliingia chumbani lakini aliona kama kunaΒ baadhi ya vitu vyake vimekaa tofauti siyo kama alivyoviacha,Β alipata shahuku ya kuzidi kukagua aliona ishara ile ileΒ akahisi moja kwa moja chumba chake kilipekuliwa, alirudiΒ sebleni kwa Mama yake akamuulizaΒ
“Mama Nani amepekua chumbani kwangu?” Alihoji Noela akiwaΒ mwenye kushangaaΒ
“Kupekua? Mmh mbona hakuna aliyeingia huko…” alijibu MamaΒ Noela sababu hakunuona Desmond akiwa ameingia hukoΒ
“Ina maana kumejipekua kwenyewe eti Mama? Vitu nilivyoachaΒ siyo nilivyokuta ndiyo maana nimekuuliza, Mlami utasemajeΒ hujui wakati upo nyumbani muda wote?”Β
“Aaah au Joshua aliingia huko? Lakini hapana mbona aliketiΒ hapa muda wote”Β
“aaah” Aligugumia Noela kisha alirudi chumbani, alichukuaΒ simu akampigia Desmond akamuuliza kama aliingia chumbaniΒ kwake, Desmond alimkatalia kuwa hakuingia huko, basi simuΒ ilikatika huku ikimuacha na maswali mengi Noela kuwa ni NaniΒ aliingia huko na alienda kufanya nini.Β
Ndani ya Hospitali kubwa, Desmond alienda kumuangalia MkeΒ wake ambaye ni adui mkubwa kwake, kilichomshangaza niΒ kuzuiliwa kuingia kwenye chumba ambacho Mke wake MandyΒ alikuwa amewekwa kwa ajili ya matibabu, yalikuwa ni maombi yaΒ Nesi Lucia kwa daktari mkuu wa Hospitali.Β
Alilalamika DesmondΒ
“Nazuiliwa vipi kumuona Mke wangu wa ndoa? Kwanini anapelekwaΒ kwenye wodi nyingine bila kunitaarifu Mimi?” Alihoji akiwaΒ mbele ya nesi mmoja, Nesi Lucia alikuwa amejibanza mahaliΒ akimfuatilia Desmond, alikuwa na mashaka sana na DesmondΒ tokea ile siku ambayo Desmond alienda na Mwanasheria paleΒ Hospitalini na kumsainisha Mandy kwa alama ya kidole.Β
Desmond alichanganikiwa kwa jambo moja, kama Mke wake ataamkaΒ atasema Nani alimuuwa Mama yake Kitu ambacho DesmondΒ alipambana kuhakikisha hakuna siri inayotoka.Β
“Ni maagizo kutoka kwa Dokta Mkuu wa Hospitali nasiΒ tunayafuata” Alisema Nesi huyo wa kiume, Desmond hakutakaΒ kusema tena baada ya kusikia kuwa maagizo ya kuzuiliwaΒ yaliyoka kwa Dakatri Mkuu wa Hospitali hiyo. Alitembea kishaΒ aliketi kwenye Kiti akakumbuka jambo
Alikumbuka siku moja mvua kubwa ilikuwa ikinyesha, mvua hiyoΒ iliambatana na radi za hapa na pale, alikuwa akiendesha gariΒ huku akionekana kuwa mwenye kutafakari jambo zito kichwani,Β nyuma yake kulikuwa na gari nyeusi iliyokuwa ikimfuataΒ taratibu, Desmond hakuiyona.Β
Gari hiyo nyeusi iliyo nyuma yake ndani kulikuwa na Mama MtuΒ mzima, Mama huyo alikuwa ni Mama yake Mandy, Mama MandyΒ alipata taarifa kuwa Desmond amepanga kukutana na MwanasheriaΒ wa Mandy kisha wabadilishe hati za mali za Mandy.Β
Mama Mandy alizidi kumfuatilia Desmond Usiku huo ambaoΒ uliambatana na mvua na upepo, safari hiyo ilikita nje ya MjiΒ huo waliokuwa wakiishi tena katika ghofu moja ambaloΒ Mwanasheria wa Mandy aliyeitwa Joel alikuwa akimsubiriaΒ Desmond.Β
Mama Mandy alionekana kuwa makini sana kumfuatilia Desmond,Β alikuwa peke yake, hakujuwa kuwa Desmond alikuwa ameshashtukaΒ kuwa kuna gari iliyokuwa ikimfuatilia kwa nyuma, Mama MandyΒ alipoona gari ya Desmond imesimama naye alisimamisha gari kwaΒ mbali kidogo kisha alishuka akawa anatembea kwenye mvuaΒ taratibu huku akiwa makini mno, alisogea taratibu sana hadiΒ kwenye gari ya Desmond lakini hakumuona Desmond, Usiku huoΒ ulijaa giza kiasi.Β
Alipoangalia vizuri mbele aliona ghofu, alipata wazo kuwaΒ huenda Desmond atakuwa ameingia humo, basi alisogea hadiΒ ndani ya Ghofu hilo ambalo lilionekana kuwa kimya sana,Β hakukuwa na Mtu yeyote yule kitu ambacho kilizidiΒ kumshangaza.Β
Akachukua simu yake ili ampigie Mandy amueleze mahali alipoΒ pia amwambie Binti yake juu ya Mchezo mchafu aliokuwaΒ akiufanya Desmond, kabla hata hajapiga simu alisikia hatuaΒ nyuma yake alipogeuka alimuona Desmond akiwa amesimama nyumaΒ yake, alipoangalia mikono ya Desmond haraka aliona amevaliaΒ Gloves.Β
“Desmond! Unataka kufanya nini?” Aliuliza Mama yake MandyΒ akiwa anavujwa na maji kwenye mwili kutokana na ile mvuaΒ iliyompiga kule njeΒ
“Uchafu unaoufanya umefika mwisho Joshua, kila siku nilikuwaΒ nikimwambia Mandy kuwa wewe huna mapenzi naye bali unahitajiΒ mali za Mtoto wangu, Mwanasheria Joel yupo wapi?” AliulizaΒ Mama Mandy, Desmond alihema kidogo kisha Joel alijitokeza
“Hadi wewe Joel? Unajuwa ni kiasi gani familia inakuaminiΒ Joel? Unashiriki uchafu mkubwa kama Huu, hili siweziΒ kulifumbia macho, nyote mnaingia kwenye mikono ya sheria”Β Alisema Mama Mandy kisha alionekana kutaka kupiga Simu lakiniΒ haraka Desmond alimuwahi, akampora simu akaona alikuwaΒ anataka kumpigia MandyΒ
“Unataka kufanya nini Mama? Unataka nifungwe? Unataka niweΒ Masikini au unataka Mtoto wako aniache? Hii ni siri ambayoΒ hukupaswa kuifuatilia Mama…..” Alisema Desmond hukuΒ akijikaza lakini alikuwa akiumia sana ndani ya Moyo wakeΒ
“Mandy ni lazima atajuwa kuwa wewe si Mtu mzuri na ninaΒ ushahidi wa video na picha ambazo nimetumiwa, umekuwaΒ ukikutana na Joel kila siku Jioni na kupanga mipango yenuΒ michafu..” Alisema Mama yake MandyΒ
“Pole Mama kwasababu hutoweza kufanya hivyo” alisema DesmondΒ haraka alikata waya uliokuwa ukining’inia kisha akamnyongaΒ Mama yake Mandy hadi alipofanikiwa kummaliza, MwanasheriaΒ Joel alikunja uso wake kuashiria kuwa jambo hilo halikuwa laΒ kawaida.Β
“Joel Mimi na wewe tumeuwa hapa sawa? Tunapaswa kuondoka naΒ kukaa kimya, nipe hizo nyaraka” Alisema Desmond, harakaΒ alipewa nyaraka kisha Joel alisemaΒ
“Bado saini ya Mtu mmoja tu, Mkeo Mandy”Β
“Nitajuwa nini cha kufanya” Alisema Desmond kisha harakaΒ walianza kutoka lakini Desmond aligeuka kuutazama mwili waΒ Mama Mandy, alikuwa amevalia cheni ya Dhahabu yenye thamaniΒ kubwa sana, alirudi akamvua kisha akaiweka kwenye koti laΒ suti yake, alafu alisemaΒ
“Sisi ni Watoto wa kimasikini sana”Β
Kumbukumbu ya Desmond iliishia hapo, alitikisa kichwa chakeΒ kisha alielekea ofisini kwa Daktari wa Hospitali, DaktariΒ alipomuona Desmond alijuwa nini kimemleta, Desmond alianzaΒ kumshambulia Daktari huyo kwa manenoΒ
“Umeagiza Mke wangu apelekwe Wodi nyingine alafu MimiΒ nizuiliwe kumuona si ndiyo? Hivi unajuwa ulichokifanya?”Β Alisema Desmond kwa hasiraΒ
“Desmond hebu kaa kwanza tuongee, hili jambo siyo laΒ kulichukulia jazba, tulichofanya ni kupandisha darajaΒ matibabu ya Mkeo ili aweze kuamka haraka ” Alisema DaktariΒ huyo kwa upole sana
Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA SABA
Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya kuendelea kutuma SIMULIZI Mpya Na Kuipost HAPA Kwa kumtumia Chochote kupitia
Lipa Namba: 57900454
Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
Mtandao: VODACOMΒ Β
SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAΒ
SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ
SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ
JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa
Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love &Pain Love & PainΒ
Β Β
7 Comments
Eee!! Umaskini utawapeleka watu pahala pabaya sanaπ₯
Asante mtunzi kwa stori yenye mafunzo na mazingatio makubwa.
More Love from Kenya β€οΈ
Sawa
Hii story noma sana
SIMULIZI|SIRI ZA GIZA.
SIMULIZI ya kijana machachari anayelijua jiji,mkasa huu unamwonesha yumo katika Giza na vingi vya ajabu vinamstaajabisha,anashangaa ulimwengu usiotarajiwa machono pake.
Isome hapa
______
https://maishakitaaonlinetz.blogspot.com/2024/11/simulizisiri-za-giza.html
Update Za michezo na Hadithi fupi
Njia hii hapa
https://whatsapp.com/channel/0029VanxLVYJ93wbHawAAh3H/701
NANDY APEWE NA ULINZI UKO HOSPITALI
ππππ
rjsuj1