Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 12

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Love&Pain Sehemu Ya Nne (04)
    Hadithi

    Love&Pain Sehemu Ya Nne (04)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaNovember 12, 2024Updated:November 21, 202411 Comments7 Mins Read3K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Love & Pain
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Usiku Lucia aliondoka Hospitalini akiwa hoi Bin taabani,Β  alipitia baa akaagiza pombe akanywa maana jambo lile halikuwaΒ  la kawaida hasa kwa Mawanaume ambaye alimpenda ila hakuwahiΒ  kumwambia, aliona moyo wake ulikosea njia kisha alijichekaΒ  akiwa anaendelea kupata pombe taratibu, kisha baadaye alikodiΒ  Pikipiki ikamrejesha nyumbani kwao.Β 

    Mama yake alishangaaa sana kumuona Lucia akiwa amelewa kiasiΒ  kile, alikuwa amelewa kupita maelezo hata dereva wa pikipikiΒ  alimpa tahadhari Mama Lucia kuwa Binti huyo alikuwa amekunywaΒ  sana hivyo awe naye makini wakati anampeleka ndani. EndeleaΒ 

    SEHEMU YA NNE

    “Lucia kwanini umekunywa hivi Mwanangu jamani” alisema MamaΒ  Lucia akiwa anamuingiza Lucia ndani, alimpeleka hadi chumbaniΒ  Kwake, alimuweka kitandaniΒ 

    “Lucia umepatwa na nini leo? Sijapata kukuona ukiwa umekunywaΒ  kiasi hiki” Alisema Mama yake Lucia huku Lucia akianguaΒ  kicheko kisha alisema kwa uleviΒ 

    “Ukiwa mzima kila Mtu atakupenda lakini kosa lako uumwe auΒ  ufe, kila Mtu atakuwa adui wa Maisha yako Mama” Alisema LuciaΒ  kisha alibeuwa kidogo, Mama yake alitamani kufahamu niΒ  kwanini Lucia alisema hivyoΒ 

    “Kwanini unasema hivyo?” Alihoji Mama LuciaΒ 

    “Mama sisi Binadamu ni wabaya sana, tunacheka mbele kishaΒ  nyuma tunanuna ha!ha!ha!” Alisema kisha alicheka lakini MamaΒ  Lucia alihisi Mtoto wake pengine amekutana na jambo zitoΒ  sana, ni kweli Lucia alikutana na janbo zito mnoΒ 

    “Pumzika Lucia tutaongea kesho” Alisema Mama Lucia kishaΒ  alitoka chumbani humo, baada ya Mama kutoka Lucia alichukuaΒ  simu yake akampigia Noela, alihitaji msaada kutoka kwa NoelaΒ 

    Wakati simu hii inapigwa usiku huo, Noela alikuwa amelala naΒ  Desmond, Mara moja Noela alishtuka akaipokea huku akiwaΒ  mwingi wa UsingiziΒ 

    “Hello?” Alisema Noela kwa sauti ya Usingizi, Desmond alikuwaΒ  amelalaΒ 

    “Noela nahitaji msaada wako” Alisema LuciaΒ 

    “Msaada gani huo?” Aliuliza Noela huku akinyanyuka kitandaniΒ  na kwenda dirishani ili tu asimpigie kelele Desmond

    “Nataka msaada wa kisheria kwa mgonjwa wangu…ipo hivi….”Β  Lucia alimuelezea Noela alichotaka kusaidiwaΒ 

    “Hivi una uhakika na unachokisema? Unaonekana umelewa sanaΒ  kwanini tusiongee kesho hili jambo?” Aliuliza Noela, LuciaΒ  alikubali kuzungumza na Noela kesho yake.Β 

    Simu ilikatika, kwa Mshituko Noela alipogeuka alimuonaΒ  DesmondΒ 

    “Eeeeh Joshua umeamka?” Alihoji Noela kwa mshtuko maanaΒ  hakutegemea kama angemkuta akiwa amemsimamia nyumaΒ 

    “Ulikuwa unaongea na nani?” Aliuliza DesmondΒ 

    “Aaah ni mteja wangu alikuwa anahitaji msaada wa kisheria,Β  usijali Mpenzi twende tukalale” Alisema Noela, hakujuwa kamaΒ  msaada alioombwa na Lucia ulimuhusu Mtu aliyekuwa naye UsikuΒ  huo, Ndiyo!! Lucia alihitaji msaada wa kisheria kwa MandyΒ  maana alichokiona pale kilimtisha sana.Β 

    Asubuhi mapema sana Lucia alienda Hospitalini kama kawaidaΒ  yake, safari hii alikuwa makini zaidi na Mandy maana alijuwaΒ  kuna jambo linachezwa nyuma ya ufahamu wake, alitembeaΒ  taratibu akizunguka kitanda cha Mandy huku akijiuliza afanyeΒ  nini kuzuia jambo hilo kutokea au kuwa baya zaidi. AlipataΒ  wazo fulani, alimfuata Daktari Mkuu wa Hospitali akamuombaΒ  Mandy aongezewe Huduma zaidi ili kuharakisha afya yake irejeeΒ  kama mwanzo maana ilionekana kuwa na uwezekano wa MandyΒ  kupona japo haikujulikana atapona lini licha ya wasiwasi kuwaΒ  hata kama kiamka hatoweza kukumbuka chochote au anawezaΒ  kukumbuka lakini akawa hawezi kuzungumza wala kufanyaΒ  chochote kile.Β 

    “Kwanini umekuja kuniomba kuhusu hilo jambo?” AliulizaΒ  daktari Mkuu wa HospitaliΒ 

    “Ni jukumu langu Kuhakikisha Mandy anakaa sawa haraka kulikoΒ  ilivyo dhaniwa, naomba sana” Alizidi kuomba LuciaΒ 

    “Aah Lucia hilo jambo ni lazima tumshirikishe Mume wake, kamaΒ  unavyojuwa yeye ndiye msimamizi wa kwanza wa Mandy” AlisemaΒ  Daktari huyoΒ 

    “Hakuna haja ya kumuleza Desmond kuhusu hili jambo, naombaΒ  asijuwe chochote kile” Alisema Lucia na kumfanya DaktariΒ  ashangae, akamuuliza

    “Kwanini hutaki ajuwe?” Nani atazilipa hizo gharama zaΒ  ziada?” AliulizaΒ 

    “Kumbuka Mandy ni mfanyabiashara mkubwa sana hivyo akiamkaΒ  atalipia hizo gharama” Alisema Lucia katika hali ya kuendeleaΒ  kumuomba daktari akubali.Β 

    “Asipoamka?” Aliuliza DaktariΒ 

    “Jukumu letu namba moja ni kuhakikisha wagonjwa wanapona, niΒ  lazima tufanye juu chini kuhakikisha tunasaidia Maisha yake”Β  Alisema Lucia akiwa anamtazama Daktari huyo ambaye alionekanaΒ  kuanza kumuelewa kidogo LuciaΒ 

    “Nakuamini Lucia usiniangushe katika hili, nitafanya kamaΒ  unavyosema” Alisema Daktari huyo, Lucia aliweka mikonoΒ  mdomoni kwa furaha kisha akasemaΒ 

    “Asante sana Mkuu! Umenipa thamani kubwa sana” Alisema LuciaΒ  kisha alimuaga Daktari akaondoka zake, daktari huyo alikuwaΒ  Mzee na ilionesha ndiye mmiliki wa Hospitali hiyoΒ 

    “Aaah” Alisema Daktari kisha alipiga simu alipopajua yeyeΒ  akatoa maelekezo ya Mandy kupelekwa hatua ya pili yaΒ  matibabu.Β 

    β€’β€’β€’β€’β€’β€’β€’Β 

    Baada ya siku kama tatu kupita ilipatikana taarifa kutoka kwaΒ  Askari polisi aliyekuwa akifuatilia kifo cha Mama Mandy,Β  polisi huyo alimpigia simu Desmond akamwambia kuwa kuna gariΒ  iliyopatikana kwenye Bahari, gari hiyo ilikutwa na maiti yaΒ  Mtu. Desmond alichanganikiwa, alikuwa ofisini kwakeΒ  akamuuliza polisi huyoΒ 

    “Gari! Maiti! Imefahamika gari ni ya nani na maiti ya Nani?”Β  Alihoji Desmond akiwa amesimama huku macho yakiwa yamemtokaΒ  pima, alijuwa tu ni ile gari yake aliyomuulia Sanga, harakaΒ  akiwa anasubiria jibu la Polisi huyo alijiuliza kama gari ileΒ  ikitambulika kuwa ni yake itakuwaje?Β 

    “Bado maiti imechukuliwa lakini kimekutwa kitambulisho chaΒ  yule mfanyakazi wako ambaye alikuwa ni mhisiwa namba moja waΒ  Tukio la Mke wako ila mwili ulikuwa umeharibika hivyo imekuwaΒ  ngumu kumtambuwa kwa macho. Mwili unafanyiwa vipimo kubainiΒ  ni Nani” Alisema Polisi huyoΒ 

    “Vipi kuhusu gari imejulikana kuwa ni ya Nani?” AliulizaΒ  Desmond kama Mtu mwenye haraka ya kutaka kujuwa, polisi hakutia shaka sababu aliamini Desmond alihitaji kufahamuΒ  sababu Mandy ni Mke wake pasipo kujuwa Desmond ndiyeΒ  aliyesababisha kila jambo na alikuwa akiwapiga changa askariΒ  ili wasijuwe chochote kile, hata huyo Sanga aliyekuwaΒ  akitafutwa ni yeye ndiye aliyemuuwa Hapo Baharini kwa kutumiaΒ  gari yake.Β 

    “Kazi hiyo inafanywa na kitengo husika ili kubaini gari hiyoΒ  ilikuwa ni ya nani, ndani ya dakika kumi zijazo tutajuwa gariΒ  ni ya Nani pia tutapata taarifa juu ya mwili ule kama ni WaΒ  Sanga au ni wa Mtu mwingine tu” Alisema Polisi huyo kishaΒ  alikata simu baada ya kuhakikisha kuwa alizifikisha taarifaΒ  muhimu kwa Desmond akiamini ni Mtu mzuri anayepaswa kujuwaΒ  kinachoendelea.Β 

    Ofisini kwa Desmond hapakukalika mchana huo kilaΒ  alichofikiria hakikumpa jibu la moja kwa moja, alijuwa niΒ  lazima gari itajulikana kuwa ni ya kwake na polisi watamuhisiΒ  kwa namna moja au nyingine jambo ambalo litasababisha aanzeΒ  kuchunguzwa kuhusu matukio taliyotokea, alizunguka ofisiniΒ  hapo huku akifikiria afanye nini.Β 

    “Oooshit itakuwaje?” Alijiuliza sana Desmond, aliketi akaamkaΒ  akaketi tena huku akitazama saa ya ukutani, alihesabu hadiΒ  dakika kumi alizoambiwa na yule polisi mpelelezi zilipokatikaΒ  kisha alishika simu yake huku akisubiria simu hiyo iite,Β  punde simu iliita na mpigaji alikuwa ni yule polisi, mudaΒ  aliosema kuwa atampa taarifa juu ya ule mwili pamoja na gariΒ  uliwadia, taratibu aliipokea kisha aliiweka sikioni akiwaΒ  amefumba macho yakeΒ 

    “Desmond! Mwili ni wa Sanga mshukiwa namba moja, kesi inazidiΒ  kuwa ngumu na kuhusu gari kuna fumbo zito sana hapa ambaloΒ  linahitaji umakini hasa ukizingatia gari ile…” alisemaΒ  Polisi kisha Desmond alidakiaΒ 

    “Ni ya Nani?” Alihoji kwa hofu kubwa sana, ukimya ulitawalaΒ  huku Desmond akisubiria neno kutoka kwa Polisi huyo, alisemaΒ 

    “Haijulikani, mfumo hauitambui gari hiyo” Alisema Polisi huyoΒ  kitu ambacho kilimshangaza sana Desmond, itakuwaje gari yakeΒ  isitambulike? Kibaya zaidi alikumbuka kuwa hakutoa chochoteΒ  kwenye ile gari ikiwemo kadi ya Gari kitu ambacho kingekuwaΒ  rahisi sana kufahamika, pia alipokuwa akifanya hivyo alijuwaΒ  wazi kina kile kirefu hivyo gari haiwezi kuonekanaΒ 

    “Gari haitambuliki?” Alihoji Desmond akiwa na preshaΒ 

    Nini Kitaendelea? USIKOSE SEHEMU YA TANO

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya kuendelea kutuma SIMULIZI Mpya Na Kuipost HAPA Kwa kumtumia Chochote kupitia

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAΒ 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love & Pain Love &Pain Love & PainΒ 

    Β Β 

    Love&Pain

    11 Comments

    1. Sir, Yowas on November 12, 2024 3:30 pm

      Admin

      Reply
      • Mpenzi wangu on November 13, 2024 11:57 am

        Ongeza nyingne sahz admin mda umewadia jamani tumepooza sanaaa

        Reply
    2. Massay on November 12, 2024 3:34 pm

      Ebwanaeeeh si mchezoooo

      Reply
    3. Reney MkelleπŸ’ž on November 12, 2024 4:05 pm

      Tuma na ingine Admini ooooh ni πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯

      Reply
    4. G shirima on November 12, 2024 4:44 pm

      Mbona sijasoma sanga alivyouuawa

      Reply
    5. Roddrigo on November 12, 2024 6:18 pm

      Muda umewadia kukikaribisha kiza,jioni ya Leo tutakua na Simulizi zetu mpya Za Sofia Solo pamoja na NEGATIVE PLAN
      Bila kusahau vipande vinne vya muendelezo wa Simulizi ya ZEE LA NYWILA,Simulizi isiyotabirika mpaka sasa…

      Stay tuned kisha share sambaza upendo kwa uwapendao.

      https://whatsapp.com/channel/0029VanxLVYJ93wbHawAAh3H/677

      Reply
    6. Hamis on November 12, 2024 7:45 pm

      Mbona kama leo fupi san adimin

      Reply
    7. Veronica on November 12, 2024 11:23 pm

      Nzuri sanaπŸ”₯

      Reply
    8. Fawziya Hassan on November 13, 2024 2:22 pm

      Hee mbona nimesoma kwa dakika mbili leo
      Sehemu ya 4 ni fupi hivi!!?
      Afu Desmond kumbe alipoenda kijijini kwa kina Sanga kumbe alienda kumaliza uhai wake emmmah😒
      Anyway Asante kwa stori nzuri yenye mafunzo na maumivu ndani yake.
      More Love from Kenya ❀️

      Reply
    9. Sharo love malkx πŸ’– on November 13, 2024 3:39 pm

      Katiri uyu
      Muache awe na presha tuu

      Reply
    10. πŸ—ƒ Account Warning; 1.05 BTC transfer attempt. Deny? => https://graph.org/TAKE-YOUR-BITCOIN-07-23?hs=8e68db4e77d645df0ef6c0c71520028f& πŸ—ƒ on August 12, 2025 5:34 pm

      lywwtt

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi October 1, 2025

    In the name of LOVE – 12

    Ilipoishia sehemu ya Kumi na moja ya In the name of LOVE Moyo Wangu na…

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    In the name of LOVE – 09

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.