Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto
    AFCON

    Ratiba ya kusisimua ya 16 Bora yakamilika AFCON Morocco 2025

    Hapa MSUVA Pale MPENJA Ofa Kibao Kutoka LEONBET

    In the name of LOVE – 12

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Pumzi Ya Mwisho Sehemu Ya Tano (05)
    Hadithi

    Pumzi Ya Mwisho Sehemu Ya Tano (05)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaOctober 15, 2024Updated:October 28, 202417 Comments7 Mins Read5K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Usijali Jacklin nipo kwa ajili yako mara zote” alisema  Mosses na kunifanya nitabasamu kwa uchovu, shughuli ilikuwa  pevu na vile nimetoka kuumwa basi nilichoka sana nikalala  palepale. 

    Osman alipofika ofisini alihitaji kuniona ila aliambiwa kuwa  nimetoka, akiwa kama Bosi wangu alihitaji kujuwa niko wapi,  alinipigia sana simu lakini haikupokelewa maana nilikuwa  nimelala chakali, basi alipiga kwa Mama na kumuuliza kama  nitakuwa nimeenda nyumbani, Mama alimwambia Osman kuwa sipo  nyumbani. Endelea

    SEHEMU YA TANO

    “Haya Mama nitaendelea kumtafuta” Alisema Osman, alipokata  simu alijiuliza nilikuwa nimeenda wapi, alishikwa na wivu  fulani hata kazi hakufanya naye aliondoka. Mida ya Jioni kama  saa moja kasoro hivi ndiyo niliamka, nilikuta Mosses  ameniandalia supu, nilikunywa kisha aliniuliza 

    “Osman ndiyo Nani? Amepiga sana simu, ilipokata yake iliingia  ya Mama yako, walikuwa wakipiga kwa kupokezana” Aliniuliza na  kuelezea kuhusu simu zilizokuwa zimeingia 

    “Osman ni Bosi wangu labda amenipigia sababu kuna faili zipo  kwangu, ngoja nimpigie Mama” Nilisema, alinisogezea simu mara  moja kisha nilimpigia Mama, alipokea na kinishushia swali juu 

    “Jacklin uko wapi?” Aliuliza kwa sauti iliyoonesha kuwa  alikuwa na shahuku ya kujuwa nilipo 

    “Mama mimi siyo Mtoto sasa swali gani hilo alafu kama vile  una hasira na Mimi!” 

    “Ndiyo wewe siyo Mtoto lakini kwanini uondoke kazini kabla ya  muda wa kazi kuisha? Osman amenipigia simu kujuwa kama upo  sawa na upo wapi” 

    “Ulimjibuje Mama” 

    “Nilimwambia kuwa sijui ulipo sasa kwanini niwe muongo kwa  kijana wa Watu, mwisho wote tuje kuonekana hatuna maana?” 

    “Ok Mama usiongee sana nipo kwa Mosses hata hivyo narudi muda  siyo mrefu” Nilisema, Mama alikata simu. 

    “Huyo Mama yako jinsi anavyonichukia usikute amekasirika huko  kisa wewe kuja kwangu” Alisema Mosses 

    “Ah! Mama yangu nimeshamzoea love, ngoja nirudi tu nyumbani  ila fanya kama tulivyoongea tafuta nyumba kesho unipe jibu”  Nilisema kisha nilizama kwenye waleti yangu nikampa Mosses  laki na nusu 

    “Hiyo itakusaidia” Nilisema kisha niliondoka zangu pale. 

    Nilipofika nyumbani nilimkuta Mama akiwa amefura kama chura  mwenye njaa, alikuwa amekaa nje akinisubiria. Nilipomfikia  aliniuliza swali gumu sana 

    “Umesahau kila kitu sababu leo upo hai, huyo Mosses alikataa  kusaidia Maisha yako, alinijibu jeuri lakini wewe unamuona wa  maana sana kwako, nimefanya makosa kukupigania Jacklin?” 

    Lilikuwa ni swali gumu kuwahi kuulizwa katika Maisha yangu,  Mama alidondosha chozi lililochuruzika hadi kwenye mashavu  yake, ilinibidi nikae kwanza 

    “Mama ndiyo maneno gani hayo? Binadamu tunakosea na  kujirekebisha, usimuhukumu Mosses kwa kosa moja tu yule ni  Binadamu hajakamilika Mama, hilo haliwezi kuuondoa uthamani  wake kwangu” Nilimjibu Mama kwa kujikaza sana, hakuna kitu  nilikuwa sipendi kama kumuona Mama akilia kwa ajili yangu,  anagalau ningekuwa mgonjwa lakini ni mzima na analia kwa  ajili yangu 

    “Mama yako nilisemewa vibaya, Kijana wa Watu alikusaidia  hakuangalia nyuma. Bila Osman ingekuwa inasimuliwa hadithi  yako Jacklin, lakini leo Mtu aliyekusaidia akabadilisha na  Maisha yetu kututoa kwenye umasikini hadi kwenye hali hii  haupokei simu zake, unaacha kazi yake na kwenda kwa Mosses?”  Alisema Mama, nilihema kwa uchungu na maumivu, ni kweli Osman  alisaidia Maisha yangu lakini hakusaidia ili niwe mtumwa  kwake 

    “Mama msaada ambao unakuwa Mtumwa ni msaada wa kizandiki tuu,  kama alinisaidia kwa moyo wake hakupaswa kuhitaji malipo,  mbona anajuwa kila kitu sasa kwanini apige simu kwako?  Amenikosea sana” 

    “Unajisikiliza Jacklin au unaongea kwasababu unayo nafasi ya  kufanya hivyo? Hajakusaidia tu bali ameweka maisha yake  rehani, anatembea na figo moja kwa ajili yako, hupaswi  kumsumbua hivi kijana wa Watu na kama huitaji kazi basi  mwambie ili amtafute Mtu mwingine” Mama alisema kwa hisia  kali 

    “Sawa Mama sipendi ukwazike kwa ajili yangu. Nitamuomba  msamaha Osman, kuwa na amani Mama nakupenda sana” Nilisema  kisha nilinyanyuka na kuingia ndani, nilimuacha Mama akiwa  amekaa nje peke yake, najuwa jinsi alivyokuwa anajisikia ila  ningefanya nini wakati moyo wangu upo kwa mwingine? Niliziona  ishara zote kuwa Osman ananipenda ila tayari hisia zangu zipo  kwa Mosses. 

    Nilipofika chumbani kwangu niliyatafakari maneno ya Mama  ambayo ni wazi aliyasema kutoka ndani ya nafsi yake,  nilijisikia vibaya, nilitamani kumtumia meseji Osman nimuombe  msamaha ila niliona ni bora nimuombe msamaha kesho yake  Ofisini, nilizitazama Missed Calls zake nilimuonea huruma  Kijana wa Watu, nilifunua shati langu nikaangalia eneo la  tumbo, nilitabasamu tu hata sijui kwanini nilifanya hivyo.

    Kesho yake kabla ya kwenda ofisini nilipitia duka la Maua  nikanunua ua zuri kwa ajili ya kumpatia Osman ili anisamehe  kwa kilichotokea. Nilichagua ua zuri ambalo niliamini litampa  furaha Osman, mvua zilikuwa zinaendelea kunyesha, hali ya  hewa ilikuwa nzuri sana ikanikumbusha siku ya kwanza  Nilipoanza kuumwa nikasaidiwa na Osman, nilianza kutabasamu  tu hadi Muuza Maua alinishtukia akasema 

    “Inaelekea unampenda sana Mtu ambaye unampelekea ua hili,  Nawaombea penzi lenu lichipue mithiri ya Mtende jangwani”  Alisema kisha alinitazama usoni, ghafla sura yangu ilikosa  uchangamfu. Sijui kwanini kila nilipomfikiria Osman  nilijikuta nikiishia kwenye huzuni. Mara muda huo huo Osman  alipiga simu kama vile alikuwa akijuwa nilikuwa nikimuwaza,  niliiacha iite kidogo kisha niliipokea huku yule Muuza duka  akinitazama tu 

    “Hello Osman” Nilimsalimia Osman mara baada ya kuwa  nimeshapokea simu na kusikia sauti yake 

    “Jacklin, leo sijisikii vizuri naomba usimamie kazi zako  vizuri” Alisema Osman, ni kweli hata sauti yake haikuwa na  uchangamfu 

    “Una shida gani Osman?” Nilimuuliza 

    “Nahisi hali ya Homa tuu Jacklin” Alisema tena Osman 

    “Haya nitafanya hivyo lakini baadaye….” Nilitaka kumwambia  kuwa nahitaji kuonana naye ila nilisita nikamwambia 

    “Ugua pole Osman” Nilisema kisha simu ilikatika, nilirudi  kulipia ua lile kisha niliondoka nalo hadi kazini. 

    Mdada wa mapokezi aliponiona alinisimamisha, alinifuata  niliposimama akaniuliza 

    “Umempa nini Bosi Osman? Yaani alivyo mkali yule lakini jana  alinywea kabisa, aliposikia haupo naye aliondoka na  alionekana hana raha” Alisema, dakika moja tu ilitosha  kumtambua alikuwa ni Mtu wa aina gani, alionekana kuwa  mshakunaku, nilitabasamu kisha nikamwambia 

    “Kazi njema” nilimuacha akiwa ameduwaa, pengine alitegemea  ningemwambua Mimi ni Mwanamke wa Osman nahisi ndicho  alichokuwa anataka kukisikia. 

    Niliketi kwenye kiti, nilishusha pumzi zangu, niliona jinsi  maisha yangu yalivyobadilika. Mara simu yangu iliita,  aliyekuwa akinipigia alikuwa ni Mosses, aliniambia kuwa  amepata nyumba hivyo ilikuwa ikihitaji pesa kiasi cha Milioni  14, nilimwambia jioni nitampatia pesa hiyo. 

    Siku hiyo, Osman alienda Hospitalini kuangalia afya yake,  alienda kwenye Hospitali ya Dokta Simon, Wawili hawa walikuwa  wakifahamiana sana. Alipofika Dokta Simon alimfanyia  uchunguzi, kwakuwa alikuwa akimfahamu vizuri Osman alijuwa ni  kitu gani kilikuwa kikimsumbua Osman, waliketi baada ya  vipimo 

    “Osman! Nilikuonya kuhusu kutoa figo yako hukutaka kunisikia”  Alisema Dokta Simon, Osman alikaa kimya kumsikiliza Dokta  Simon 

    “Nilikataa usifanye vile sababu ya tatizo lako, figo moja  ilikuwa na matatizo hivyo ulikuwa ukitumia zaidi figo moja  tuu, sasa ile nzima umeiondoa hii iliyobakia inafanya kazi  kwa kiwango kidogo sana na haitokuwa na muda mrefu nayo  itakufa” Alisema Dokta Simon 

    “Kwanini umeamua kuhatarisha Maisha yako Osman? Wewe ni  Bilionea mkubwa hapa Nchini, una pesa ya kutosha,  unaheshimika kila kona” Aliendelea kusema Dokta Simon 

    “Nilifanya vile kwasababu ya upendo wangu kwa Jacklin,  nilikuwa na Maisha yaliyojaa huzuni sana baada ya Zahra  kunitenda vibaya, ghafla sura yangu ilijawa tabasamu mara  baada ya kumuona Jacklin, niliapa sitopenda tena ila baada ya  Jacklin kuja katika Maisha yangu nimejihisi tofauti kabisa”  Alisema Osman kisha alishusha pumzi zake 

    “Kwa mara ya kwanza namuona Bilionea dhahifu zaidi katika  Maisha yangu, unahatarisha Maisha yako kwa ajili ya Mwanamke  ambaye unajuwa fika ana Mwanaume wake? Unahatarisha Maisha  kwa ajili ya Mwanamke ambaye hata hujawahi kumtamkia  chochote? Hiyo ni akili yako Osman?? Laiti kama Mzee Dhabi  akilijuwa hili ulilofanya ataipoteza familia ya Jacklin na  haitokuja ionekane tena, wewe ni Mtoto wa pekee wa yule Mzee,  siku akiligundua hili anaweza hata akaniuwa Mimi” Alisema  Dokta Simon 

    “Sikia Dokta Simon, naomba hili jambo liwe siri Baina yetu.  Baba yangu asijuwe chochote wakati ambao tunatafuta Figo kwa  ajili ya kunipandikiza” Alisema Osman 

    “Naweza kulificha lakini hali yako inaweza ikaniumbua mbele  ya Baba yako, vyote nitafanya lakini vipi kama Jacklin  akazikataa hisia zako huoni kama utakuwa umekula hasara wewe?” Alimuuliza swali gumu sana, Osman alikunbuka namna  tukivyogombana kule Dubai, aliona Swali la Dokta Simon  lilikuwa na mashiko sana. 

    Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya SITA Ya PUMZI YA MWISHO

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOM  

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPA 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINI 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPA 

    SOMA KISASI CHANGU HAPA  

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx  Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx 

     

    Pumzi ya mwisho

    17 Comments

    1. Sir, Yowas on October 15, 2024 9:00 pm

      Asante mtunzi, endelea kutupa burudani

      Reply
    2. Johdam on October 15, 2024 9:01 pm

      Huyu demu ovyoo sana🙌🙌

      Reply
    3. Angel on October 15, 2024 9:43 pm

      Mungu naomb jackline atambue kuw mosses hampend arudi kwa osman

      Reply
      • G shirima on October 16, 2024 9:19 am

        Ivi ni kweli kina mwanamke wa ivi

        Reply
    4. Charz jr😎 on October 15, 2024 9:56 pm

      Noma nomaa…..dis iz goin to be bad🥲🥲 osman his going to lose his life🥺🥺

      Reply
    5. Jacqueline Mo on October 15, 2024 11:08 pm

      Asitisha mapenzi Kwa Jacklin bn me nakadirishwa na uyu dada duuh

      Reply
    6. Emmy on October 16, 2024 7:51 pm

      Jacklin hakir hana

      Reply
    7. yahaya on October 19, 2024 9:10 pm

      endelezen bas

      Reply
    8. 📔 + 1.515729 BTC.GET - https://yandex.com/poll/HYTE3DqXnHUqpZMyFqetue?hs=1e542870227b8225995b481481a5707b& 📔 on June 4, 2025 5:22 am

      tm1nmm

      Reply
    9. 📧 Message; + 1,368618 BTC. Receive >> https://yandex.com/poll/enter/BXidu5Ewa8hnAFoFznqSi9?hs=1e542870227b8225995b481481a5707b& 📧 on June 6, 2025 10:48 am

      08l9lu

      Reply
    10. 💻 📩 Incoming Transfer: 1.0 BTC from unknown sender. Accept? >> https://graph.org/REDEEM-BTC-07-23?hs=1e542870227b8225995b481481a5707b& 💻 on August 29, 2025 2:39 am

      d0eb92

      Reply
    11. 🗓 Account Notice; 1.05 Bitcoin withdrawal attempt. Authorize? >> https://graph.org/Get-your-BTC-09-04?hs=1e542870227b8225995b481481a5707b& 🗓 on September 21, 2025 3:09 am

      9nd9cg

      Reply
    12. 創建免費帳戶 on November 23, 2025 5:28 am

      Your point of view caught my eye and was very interesting. Thanks. I have a question for you. https://accounts.binance.info/lv/register-person?ref=SMUBFN5I

      Reply
    13. فريق تشيلي لكرة القدم on December 12, 2025 5:30 am

      As the admin of this web page is working, no uncertainty very soon it will be well-known, due to its quality contents.

      Reply
    14. winpot on January 22, 2026 7:46 pm

      Today, I went to the beachfront with my children. I found
      a sea shell and gave it to my 4 year old daughter and said
      “You can hear the ocean if you put this to your ear.” She put the shell to her ear and screamed.
      There was a hermit crab inside and it pinched her ear.
      She never wants to go back! LoL I know this is entirely off topic but I had to tell someone!

      Reply
    15. mitolyn reviews on January 26, 2026 3:39 am

      **mitolyn reviews**

      Mitolyn is a carefully developed, plant-based formula created to help support metabolic efficiency and encourage healthy, lasting weight management.

      Reply
    16. 日本 av on January 30, 2026 7:02 am

      Thank you a lot for sharing this with all people you actually realize what
      you’re talking approximately! Bookmarked. Please additionally talk
      over with my website =). We may have a link alternate arrangement between us

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    AFCON
    Africa | CAF January 1, 2026

    Ratiba ya kusisimua ya 16 Bora yakamilika AFCON Morocco 2025

    Ratiba ya Hatua ya 16 Bora ya michuano ya TotalEnergies CAF AFCON Morocco 2025 imekamilika…

    Hapa MSUVA Pale MPENJA Ofa Kibao Kutoka LEONBET

    In the name of LOVE – 12

    In the name of LOVE – 11

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.