Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Pumzi Ya Mwisho Sehemu Ya Tano (05)
    Hadithi

    Pumzi Ya Mwisho Sehemu Ya Tano (05)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaOctober 15, 2024Updated:October 28, 202410 Comments7 Mins Read5K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Usijali Jacklin nipo kwa ajili yako mara zote” alisemaΒ  Mosses na kunifanya nitabasamu kwa uchovu, shughuli ilikuwaΒ  pevu na vile nimetoka kuumwa basi nilichoka sana nikalalaΒ  palepale.Β 

    Osman alipofika ofisini alihitaji kuniona ila aliambiwa kuwaΒ  nimetoka, akiwa kama Bosi wangu alihitaji kujuwa niko wapi,Β  alinipigia sana simu lakini haikupokelewa maana nilikuwaΒ  nimelala chakali, basi alipiga kwa Mama na kumuuliza kamaΒ  nitakuwa nimeenda nyumbani, Mama alimwambia Osman kuwa sipoΒ  nyumbani. Endelea

    SEHEMU YA TANO

    “Haya Mama nitaendelea kumtafuta” Alisema Osman, alipokataΒ  simu alijiuliza nilikuwa nimeenda wapi, alishikwa na wivuΒ  fulani hata kazi hakufanya naye aliondoka. Mida ya Jioni kamaΒ  saa moja kasoro hivi ndiyo niliamka, nilikuta MossesΒ  ameniandalia supu, nilikunywa kisha aliniulizaΒ 

    “Osman ndiyo Nani? Amepiga sana simu, ilipokata yake iliingiaΒ  ya Mama yako, walikuwa wakipiga kwa kupokezana” Aliniuliza naΒ  kuelezea kuhusu simu zilizokuwa zimeingiaΒ 

    “Osman ni Bosi wangu labda amenipigia sababu kuna faili zipoΒ  kwangu, ngoja nimpigie Mama” Nilisema, alinisogezea simu maraΒ  moja kisha nilimpigia Mama, alipokea na kinishushia swali juuΒ 

    “Jacklin uko wapi?” Aliuliza kwa sauti iliyoonesha kuwaΒ  alikuwa na shahuku ya kujuwa nilipoΒ 

    “Mama mimi siyo Mtoto sasa swali gani hilo alafu kama vileΒ  una hasira na Mimi!”Β 

    “Ndiyo wewe siyo Mtoto lakini kwanini uondoke kazini kabla yaΒ  muda wa kazi kuisha? Osman amenipigia simu kujuwa kama upoΒ  sawa na upo wapi”Β 

    “Ulimjibuje Mama”Β 

    “Nilimwambia kuwa sijui ulipo sasa kwanini niwe muongo kwaΒ  kijana wa Watu, mwisho wote tuje kuonekana hatuna maana?”Β 

    “Ok Mama usiongee sana nipo kwa Mosses hata hivyo narudi mudaΒ  siyo mrefu” Nilisema, Mama alikata simu.Β 

    “Huyo Mama yako jinsi anavyonichukia usikute amekasirika hukoΒ  kisa wewe kuja kwangu” Alisema MossesΒ 

    “Ah! Mama yangu nimeshamzoea love, ngoja nirudi tu nyumbaniΒ  ila fanya kama tulivyoongea tafuta nyumba kesho unipe jibu”Β  Nilisema kisha nilizama kwenye waleti yangu nikampa MossesΒ  laki na nusuΒ 

    “Hiyo itakusaidia” Nilisema kisha niliondoka zangu pale.Β 

    Nilipofika nyumbani nilimkuta Mama akiwa amefura kama churaΒ  mwenye njaa, alikuwa amekaa nje akinisubiria. NilipomfikiaΒ  aliniuliza swali gumu sanaΒ 

    “Umesahau kila kitu sababu leo upo hai, huyo Mosses alikataaΒ  kusaidia Maisha yako, alinijibu jeuri lakini wewe unamuona waΒ  maana sana kwako, nimefanya makosa kukupigania Jacklin?”Β 

    Lilikuwa ni swali gumu kuwahi kuulizwa katika Maisha yangu,Β  Mama alidondosha chozi lililochuruzika hadi kwenye mashavuΒ  yake, ilinibidi nikae kwanzaΒ 

    “Mama ndiyo maneno gani hayo? Binadamu tunakosea naΒ  kujirekebisha, usimuhukumu Mosses kwa kosa moja tu yule niΒ  Binadamu hajakamilika Mama, hilo haliwezi kuuondoa uthamaniΒ  wake kwangu” Nilimjibu Mama kwa kujikaza sana, hakuna kituΒ  nilikuwa sipendi kama kumuona Mama akilia kwa ajili yangu,Β  anagalau ningekuwa mgonjwa lakini ni mzima na analia kwaΒ  ajili yanguΒ 

    “Mama yako nilisemewa vibaya, Kijana wa Watu alikusaidiaΒ  hakuangalia nyuma. Bila Osman ingekuwa inasimuliwa hadithiΒ  yako Jacklin, lakini leo Mtu aliyekusaidia akabadilisha naΒ  Maisha yetu kututoa kwenye umasikini hadi kwenye hali hiiΒ  haupokei simu zake, unaacha kazi yake na kwenda kwa Mosses?”Β  Alisema Mama, nilihema kwa uchungu na maumivu, ni kweli OsmanΒ  alisaidia Maisha yangu lakini hakusaidia ili niwe mtumwaΒ  kwakeΒ 

    “Mama msaada ambao unakuwa Mtumwa ni msaada wa kizandiki tuu,Β  kama alinisaidia kwa moyo wake hakupaswa kuhitaji malipo,Β  mbona anajuwa kila kitu sasa kwanini apige simu kwako?Β  Amenikosea sana”Β 

    “Unajisikiliza Jacklin au unaongea kwasababu unayo nafasi yaΒ  kufanya hivyo? Hajakusaidia tu bali ameweka maisha yakeΒ  rehani, anatembea na figo moja kwa ajili yako, hupaswiΒ  kumsumbua hivi kijana wa Watu na kama huitaji kazi basiΒ  mwambie ili amtafute Mtu mwingine” Mama alisema kwa hisiaΒ  kaliΒ 

    “Sawa Mama sipendi ukwazike kwa ajili yangu. NitamuombaΒ  msamaha Osman, kuwa na amani Mama nakupenda sana” NilisemaΒ  kisha nilinyanyuka na kuingia ndani, nilimuacha Mama akiwaΒ  amekaa nje peke yake, najuwa jinsi alivyokuwa anajisikia ilaΒ  ningefanya nini wakati moyo wangu upo kwa mwingine? NilizionaΒ  ishara zote kuwa Osman ananipenda ila tayari hisia zangu zipoΒ  kwa Mosses.Β 

    Nilipofika chumbani kwangu niliyatafakari maneno ya MamaΒ  ambayo ni wazi aliyasema kutoka ndani ya nafsi yake,Β  nilijisikia vibaya, nilitamani kumtumia meseji Osman nimuombeΒ  msamaha ila niliona ni bora nimuombe msamaha kesho yakeΒ  Ofisini, nilizitazama Missed Calls zake nilimuonea hurumaΒ  Kijana wa Watu, nilifunua shati langu nikaangalia eneo laΒ  tumbo, nilitabasamu tu hata sijui kwanini nilifanya hivyo.

    Kesho yake kabla ya kwenda ofisini nilipitia duka la MauaΒ  nikanunua ua zuri kwa ajili ya kumpatia Osman ili anisameheΒ  kwa kilichotokea. Nilichagua ua zuri ambalo niliamini litampaΒ  furaha Osman, mvua zilikuwa zinaendelea kunyesha, hali yaΒ  hewa ilikuwa nzuri sana ikanikumbusha siku ya kwanzaΒ  Nilipoanza kuumwa nikasaidiwa na Osman, nilianza kutabasamuΒ  tu hadi Muuza Maua alinishtukia akasemaΒ 

    “Inaelekea unampenda sana Mtu ambaye unampelekea ua hili,Β  Nawaombea penzi lenu lichipue mithiri ya Mtende jangwani”Β  Alisema kisha alinitazama usoni, ghafla sura yangu ilikosaΒ  uchangamfu. Sijui kwanini kila nilipomfikiria OsmanΒ  nilijikuta nikiishia kwenye huzuni. Mara muda huo huo OsmanΒ  alipiga simu kama vile alikuwa akijuwa nilikuwa nikimuwaza,Β  niliiacha iite kidogo kisha niliipokea huku yule Muuza dukaΒ  akinitazama tuΒ 

    “Hello Osman” Nilimsalimia Osman mara baada ya kuwaΒ  nimeshapokea simu na kusikia sauti yakeΒ 

    “Jacklin, leo sijisikii vizuri naomba usimamie kazi zakoΒ  vizuri” Alisema Osman, ni kweli hata sauti yake haikuwa naΒ  uchangamfuΒ 

    “Una shida gani Osman?” NilimuulizaΒ 

    “Nahisi hali ya Homa tuu Jacklin” Alisema tena OsmanΒ 

    “Haya nitafanya hivyo lakini baadaye….” Nilitaka kumwambiaΒ  kuwa nahitaji kuonana naye ila nilisita nikamwambiaΒ 

    “Ugua pole Osman” Nilisema kisha simu ilikatika, nilirudiΒ  kulipia ua lile kisha niliondoka nalo hadi kazini.Β 

    Mdada wa mapokezi aliponiona alinisimamisha, alinifuataΒ  niliposimama akaniulizaΒ 

    “Umempa nini Bosi Osman? Yaani alivyo mkali yule lakini janaΒ  alinywea kabisa, aliposikia haupo naye aliondoka naΒ  alionekana hana raha” Alisema, dakika moja tu ilitoshaΒ  kumtambua alikuwa ni Mtu wa aina gani, alionekana kuwaΒ  mshakunaku, nilitabasamu kisha nikamwambiaΒ 

    “Kazi njema” nilimuacha akiwa ameduwaa, pengine alitegemeaΒ  ningemwambua Mimi ni Mwanamke wa Osman nahisi ndichoΒ  alichokuwa anataka kukisikia.Β 

    Niliketi kwenye kiti, nilishusha pumzi zangu, niliona jinsiΒ  maisha yangu yalivyobadilika. Mara simu yangu iliita,Β  aliyekuwa akinipigia alikuwa ni Mosses, aliniambia kuwaΒ  amepata nyumba hivyo ilikuwa ikihitaji pesa kiasi cha MilioniΒ  14, nilimwambia jioni nitampatia pesa hiyo.Β 

    Siku hiyo, Osman alienda Hospitalini kuangalia afya yake,Β  alienda kwenye Hospitali ya Dokta Simon, Wawili hawa walikuwaΒ  wakifahamiana sana. Alipofika Dokta Simon alimfanyiaΒ  uchunguzi, kwakuwa alikuwa akimfahamu vizuri Osman alijuwa niΒ  kitu gani kilikuwa kikimsumbua Osman, waliketi baada yaΒ  vipimoΒ 

    “Osman! Nilikuonya kuhusu kutoa figo yako hukutaka kunisikia”Β  Alisema Dokta Simon, Osman alikaa kimya kumsikiliza DoktaΒ  SimonΒ 

    “Nilikataa usifanye vile sababu ya tatizo lako, figo mojaΒ  ilikuwa na matatizo hivyo ulikuwa ukitumia zaidi figo mojaΒ  tuu, sasa ile nzima umeiondoa hii iliyobakia inafanya kaziΒ  kwa kiwango kidogo sana na haitokuwa na muda mrefu nayoΒ  itakufa” Alisema Dokta SimonΒ 

    “Kwanini umeamua kuhatarisha Maisha yako Osman? Wewe niΒ  Bilionea mkubwa hapa Nchini, una pesa ya kutosha,Β  unaheshimika kila kona” Aliendelea kusema Dokta SimonΒ 

    “Nilifanya vile kwasababu ya upendo wangu kwa Jacklin,Β  nilikuwa na Maisha yaliyojaa huzuni sana baada ya ZahraΒ  kunitenda vibaya, ghafla sura yangu ilijawa tabasamu maraΒ  baada ya kumuona Jacklin, niliapa sitopenda tena ila baada yaΒ  Jacklin kuja katika Maisha yangu nimejihisi tofauti kabisa”Β  Alisema Osman kisha alishusha pumzi zakeΒ 

    “Kwa mara ya kwanza namuona Bilionea dhahifu zaidi katikaΒ  Maisha yangu, unahatarisha Maisha yako kwa ajili ya MwanamkeΒ  ambaye unajuwa fika ana Mwanaume wake? Unahatarisha MaishaΒ  kwa ajili ya Mwanamke ambaye hata hujawahi kumtamkiaΒ  chochote? Hiyo ni akili yako Osman?? Laiti kama Mzee DhabiΒ  akilijuwa hili ulilofanya ataipoteza familia ya Jacklin naΒ  haitokuja ionekane tena, wewe ni Mtoto wa pekee wa yule Mzee,Β  siku akiligundua hili anaweza hata akaniuwa Mimi” AlisemaΒ  Dokta SimonΒ 

    “Sikia Dokta Simon, naomba hili jambo liwe siri Baina yetu.Β  Baba yangu asijuwe chochote wakati ambao tunatafuta Figo kwaΒ  ajili ya kunipandikiza” Alisema OsmanΒ 

    “Naweza kulificha lakini hali yako inaweza ikaniumbua mbeleΒ  ya Baba yako, vyote nitafanya lakini vipi kama JacklinΒ  akazikataa hisia zako huoni kama utakuwa umekula hasara wewe?” Alimuuliza swali gumu sana, Osman alikunbuka namnaΒ  tukivyogombana kule Dubai, aliona Swali la Dokta SimonΒ  lilikuwa na mashiko sana.Β 

    Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya SITA Ya PUMZI YA MWISHO

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAΒ 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxΒ  Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xx Pumzi Ya Mwisho xxΒ 

    Β 

    Pumzi ya mwisho

    10 Comments

    1. Sir, Yowas on October 15, 2024 9:00 pm

      Asante mtunzi, endelea kutupa burudani

      Reply
    2. Johdam on October 15, 2024 9:01 pm

      Huyu demu ovyoo sanaπŸ™ŒπŸ™Œ

      Reply
    3. Angel on October 15, 2024 9:43 pm

      Mungu naomb jackline atambue kuw mosses hampend arudi kwa osman

      Reply
      • G shirima on October 16, 2024 9:19 am

        Ivi ni kweli kina mwanamke wa ivi

        Reply
    4. Charz jr😎 on October 15, 2024 9:56 pm

      Noma nomaa…..dis iz goin to be badπŸ₯²πŸ₯² osman his going to lose his lifeπŸ₯ΊπŸ₯Ί

      Reply
    5. Jacqueline Mo on October 15, 2024 11:08 pm

      Asitisha mapenzi Kwa Jacklin bn me nakadirishwa na uyu dada duuh

      Reply
    6. Emmy on October 16, 2024 7:51 pm

      Jacklin hakir hana

      Reply
    7. yahaya on October 19, 2024 9:10 pm

      endelezen bas

      Reply
    8. πŸ“” + 1.515729 BTC.GET - https://yandex.com/poll/HYTE3DqXnHUqpZMyFqetue?hs=1e542870227b8225995b481481a5707b& πŸ“” on June 4, 2025 5:22 am

      tm1nmm

      Reply
    9. πŸ“§ Message; + 1,368618 BTC. Receive >> https://yandex.com/poll/enter/BXidu5Ewa8hnAFoFznqSi9?hs=1e542870227b8225995b481481a5707b& πŸ“§ on June 6, 2025 10:48 am

      08l9lu

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya naneΒ  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.