Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 05

    In the name of LOVE – 04

    In the name of LOVE – 03

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Mungu Amenisahau Sehemu Ya Nane (08)
    Hadithi

    Mungu Amenisahau Sehemu Ya Nane (08)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaOctober 4, 2024Updated:October 5, 20249 Comments10 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mungu Amenisahau
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Basi Maisha ndani ya Gereza yaliendelea, siku moja baada yaย  kazi ilikuwa ni majira ya saa 7 Mchana, ulikuwa ni muda waย  kupata Chakula. Tulikuwa tukipanga mistari miwili kwa ajiliย  ya kupata Chakula, msitari wa kwanza nilikuwepo Mimi, sasaย  katika tazama tazama nilistaajabu nilimuona Sarafina, yuleย  Mdada ambaye alifukuzwa na Shonaa kisa Mimi, nilitamaniย  kumuita ila nilikumbuka kuwa alikuwa na hasira na Mimi,ย  nilimgeukia Isabela nikamuulizaย 

    “Yule yupo hapa kwa muda gani?” Nilimuonesha kidole Sarafinaย 

    “Nimemkuta hapa, anaonekana kahukumiwa muda mrefu ilaย  inasemekana aliiba pesa kwa tajiri mmoja”ย 

    “Vipi unamjuwa?”ย 

    “Ndio namjuwa” Basi baada ya kuwa tumeshachukua chakulaย  tulienda kula, Isabela aliniulizaย 

    “Unamjua vipi yule”ย  Endeleaย 

    SEHEMU YA NANE

    “Wakati nakuja hapa Dar ndio nilionana naye ila tuliachanaย  kwa shari, aliniona mbaya akidai nimesababisha amefukuzwaย  pale alipokuwa anaishi” Nilisemaย 

    “Mh! Sasa itabidi ujiadhari maana yule ana kundi lake hapaย  gerezani ambalo linaendesha ubabe mwingi, akijuwa kama upoย  hapa utaishi kwa shida sana” Alisema Isabela.ย 

    “Ni kweli lakini nitamkwepa vipi wakati tunaishi kwa uwaziย  hivi, ikiwa mimi nimemuona nina imani na yeye ataniona tu.”ย 

    “Cha msingi ni kumkwepa vinginevyo utateseka sana hapa Jojo”ย 

    “Mh! Tutaona itakavyokuwa” Tulipomaliza kula tulirudiย  kuendelea na kazi za Shamba, jioni tulihesabiwa kishaย  tulikula na kurudishwa kwenye vyumba kwa ajili ya kulala,ย  kila chumba kilikuwa na wafungwa 8 ambao tulikuwa tukilalaย  humo. Bahati nzuri chumba chetu hakikuwa na muhuni hataย  mmoja, kumbe taarifa ya Mimi kuwepo Gerezani alikuwa nayoย  Sarafina, kama Isabela alivyoniambia kuwa Sarafina alikuwa naย  kundi la ubabe pale gerezani.ย 

    Usiku tukiwa tumelala tena fofofo maana kazi za pale Gerezaniย  zilikuwa ngumu mno hivyo Mtu akilala anakuwa kama amekufa.ย  Nilishtuka geti la chumba chetu lilikuwa likifunguliwa alafuย  tochi ilinimulika Usoni, aliingia mdada mmoja ambaye hakuwaย  Askari, aliniambia nimfuate.ย 

    Niliamka kisha nilimfuata, niliingizwa kwenye chumba kimojaย  kisha kilifungwa, kilikuwa ni chumba chenye giza mno kiasiย  kwamba sikuweza kuona chochote kileย 

    “Nipo wapi?” Nilijiulza kwa sauti ya chini huku nikipapasiaย 

    “Dada yangu kwanini umenileta huku?” Niliuliza, sautiย  ilijirudia tu katika kile chumba, sikujibiwa. Mara taaย  iliwashwa, nilikutana na macho ya Sarafinaย 

    “Sarafina” Niliita kwa mshituko maana sikutegemea kamaย  ningekutana naye katika Mazingira yale, kwa vyovyote vileย  aliyenileta alijuwa nini anafanya.ย 

    “Karibu Jojo, Mungu wangu alinisikia kilio changu, hatimayeย  nimekutana na wewe” Alisema Sarafina akipiga hatua ndogoย  ndogo kusogea nilipokuwa nimesimama.ย 

    “Sarafina sikufanya chochote kibaya dhidi yako, sikutegemeaย  kama ingekuwa vile. Nisamehe tafadhali, tuyamalize”

    “Pengine umesahau Jojo, nilikuokoa yule Mwanaume asikubake,ย  nilimpiga mbele yako kukuonesha kuwa sikupenda alichokifanya.ย  Wema wangu kwako ndiyo uliozaa matunda yale, sikuwa na paย  kwenda, nilikuacha pale lakini nilisema ipo sikuย  nitakuonesha. Siwezi kuwa na haraka na wewe sababu upo kwenyeย  himaya yangu” Alisema Sarafina akiwa anazunguka huku na kuleย 

    “Sarafina tafadhali sana, nisamehe hujui ni mambo mangapiย  magumu nimekutana nayo, nimeishi Maisha magumu sana, hukumuย  niliyopewa ni adhabu tosha kwangu…” Nilisema kwa uchunguย  sanaย 

    “Lakini sio adhabu yangu, yangu itakuwa zaidi ya hiyo hukumuย  uliyopewa, wema wangu ukageuka kuwa udhalilishaji, siri yaย  ugonjwa wangu iliwekwa wazi, namjuwa Sana Shonaa kulikoย  unavyomjuwa wewe ni lazima alinianika kwenye kila jambo”ย  Alisema Sarafina akiwa amefika karibu zaidi na Mimiย 

    Nilipiga goti nikamuomba Sarafina asinifanye chochote kibayaย  maana kama aliweza kupata funguo ya chumba chetu maana yakeย  alikuwa na uwezo hata wa kuniuwa na hakuna ambaye angesemaย  chochote kile.ย 

    “Magret” Aliita, yule Mdada aliyekuja kunichukua alikujaย  ndaniย 

    “Mrudishe, nitamalizana naye” Alisema Sarafina kishaย  nilirudishwa kwenye chumba chetu cha gereza.ย 

    Nilikuta Watu wa Chumba chetu wakiwa macho ni dhahiri kuwaย  walisikia Wakati Mimi ninaondolewa pale gerezani. Mtu waย  kwanza kuniuliza alikuwa ni Isabelaย 

    “Ulienda wapi Jojo?” Nilivuta pumzi nikamueleza nilipokuwaย 

    “Itabidi uwe makini sana Maana Sarafina ni Mtu mkorofi mnoย  hapa gerezani, ipo namna anaweza akafanya maisha yako yakawaย  si kitu hapa gerezani” Alisema Isabela akadakia Mwanamkeย  mwingine akasemaย 

    “Wakati anafika aliwahi kupigana na askari Watatu naย  akawadhibiti vizuri sana, tokea siku hiyo amekuwa na urafikiย  na Mkuu wa Gereza hili, mara kadhaa amekuwa akitoka na kurudiย  haijajulikana wana ajenda gani, hivyo unapaswa kuwa makiniย  sana Jojo vinginevyo hata sisi tutakuwa hatarini. Ana kundiย  lake hapa na linatambulika na Mkuu wa Gereza, wao hawafanyiย  kazi yoyote ile zaidi ya kutoka na kurudi” Yalikuwa ndiyoย  maelezo yake kuhusu Sarafina, hilo la kupiga Askariย  halikunitisha sana maana nilikumbuka aliwahi kumpiga yuleย  Mwanaume aliyetaka kunibaka.

    “Ina maana anaishi humu gerezani kwa uhuru bila kubugudhiwaย  na chochote?”ย 

    “Ndiyo! Ni Mtu hatari sana, anaendesha biashara ya kuuzaย  Bangi na Unga hapa Gerezani, anachumba maalumu cha kulala naย  anapewa mahitaji yote ayatakayo” alielezea huyo Mwanamkeย  mwingine, kiukweli nilijawa na woga sana, nilipitia kote ilaย  niliona dhahiri Maisha yangu yataishia ndani ya gereza,ย  nilimuuliza Isabelaย 

    “Ndugu zako wanakuja kukuona?”ย 

    “Hapana nahisi hawajaambiwa chochote na Mume wangu”ย  Alinijibu, lengo langu lilikuwa kama wanafika niwape maelezoย  waende nyumbani kwetu Tabora wakauze kibanda chetu ili wajeย  kunikomboa pale gerezani, nilichoka sana.ย 

    Wao walilala maana ulikuwa ni usiku mwingi, ila Mimi nilikuwaย  macho hadi Alfajiri ambapo tuliamshwa kwa ajili ya kazi, sikuย  zote nilikuwa napewa kazi nafanya na wenzangu ila siku hiyoย  ilikuwa tofauti sana, kwanza nilipelekwa kwenye kuvunja maweย  adhabu ambayo hupewa Wafungwa waliofungwa kwa kosa laย  Mauwaji. Pili niliambiwa natakiwa kuwa peke yangu, basiย  nilipelekwa huko na Askari mmoja, kulikuwa ni eneo lenye Maweย  yaliyochimbuliwa, nilipewa nyundo kubwa nilianza kazi yaย  kuvunja mawe, Mchana ulipoingia nilisikia kengele kwa ajiliย  ya kwenda kupata Chakula lakini yule askari alinizuiaย  akaniambia siruhusiwi kula kwa siku hiyo.ย 

    Nilikubaliana na hali halisi, nilifanya kazi kwa bidii sanaย  bila hata kutegea sababu nilijuwa yalikuwa ni maelekezo yaย  Sarafina, Jioni nilipelekwa kulala kwenye chumba cha pekeย  yangu, chumba hakikuwa na taa wala sehemu ya kulalia,ย  palikuwa pamemwagwa maji kwenye sakafu. Basi niliketi, japoย  nililoa lakini ilinilazimu kwani nisingeliweza kusimama kwaย  muda woteย 

    Kweli aliyesema Maisha ni popote, msemo ulikuwa na maanaย  kubwa sana, licha ya kutokula chochote lakini nililala kwenyeย  sakafu yenye maji, niliuchapa Usingizi kutokana na zile kaziย  ngumu. Usingizi ulinipitiliza hadi asubuhi sana, jua lilikuwaย  limeshatoka nilipata kuushuhudia mwanga wake kupitiaย  kidirisha kidogo ambacho kilikuwa juu pale kwenye kileย  chumba, mazingira ya chumba yalikuwa maalum, kilionekana kuwaย  ni chumba spesho.ย 

    Tofauti na vyumba vingine, chumba hicho kilikuwa na getiย  lisiloonyesha nje, kilikuwa na michoro ukutani na harufu kaliย  sana ya uchafu, wadudu walikuwa wakitembea kwenye ukuta,ย nilijiinua na kuketi pembeni nikiwa nimeegemea ukuta,ย  nilijiuliza kwanini sikuamshwa siku hiyo, masaa yalisogeaย  njaa ilizidi kuniuma, kiu ilizidi kunishika maana tokeaย  nilivyokula na kunywa maji siku iliyopita sikula wala kunywaย  maji tena.ย 

    Siku iliisha bila geti langu kufunguliwa, giza liliingia, Kiuย  ilinibana sana na njaa ilizidi kuniuma, niligonga nifunguliweย  lakini hakuna aliyefungua mlango na hakukuwa na daliliย  iliyoonesha kuwa kulikuwa na Watu karibu. Siku hiyo iliisha,ย  Usiku uliingia, nilijaribu kuutafuta Usingizi lakiniย  sikuupata, nilikaa macho hadi kulipopambazuka, mwili ulikuwaย  na alama za kung’atwa na Wadudu na mbu.ย 

    “Mnifungulie nitakufa jamani” Nilisema kwa sauti isiyo naย  nguvu kabisa, siku mbili bila kula tena nikitoka kufanya kaziย  haikuwa rahisi kwangu kukabiliana na hali ile, haikusikikaย  sauti yoyote upande ule, niligumia kwa muda mrefu hadiย  nilikata tamaa ya Mtu kunisikia, nilirudi nikakaa chiniย  nikaegemea ukuta nikiwa nimechoka sanaย 

    Baadaye kidogo nilisikia sauti ya geti langu kufunguliwa,ย  niliamka haraka, ilitupwa bakuli moja kisha palifungwa,ย  nilikimbilia kwanza getini kisha nilisemaย 

    “Mnitoe humu nitakufa, kwanini mnakuwa wakatili kiasi hicho,ย  mnanitendea hivi kama nimeuwa?” Nilisema kwa sauti ya juu,ย  sauti ya Mtu kutembea ilikoma kisha ukimya ulisikika,ย  niligeuza macho yangu kwenye ile bakuliย 

    Nilisogea kuangalia kulikuwa kuna nini, niliifungua kishaย  niliona Mchuzi mwepesi sana na kipande kidogo cha Muhogoย  kilicho pikwa. Nililishika lile bakuri huku moyo ukiniumaย  sana, yaani kukaa siku mbili bila kula alafu niletewe mchuziย  na kipande kidogo cha muhogo? Nilitamani nimwage tu maanaย  sikuona kama nilistahili, ila nilipokumbuka kuwa nipo Jelaย  nilifakamia mchuzi huo kisha nilikula muhogo.ย 

    Angalau kidogo nilikuwa nimekata kiu lakini njaa ilibakiaย  pale pale. Sekunde chache nilikuwa nimemaliza kula kishaย  nilikaa chini, Muda ulizidi kwenda, siku zilienda nikiwaย  ndani ya chumba hicho cha Mateso.ย 

    Macho yangu yakazoea giza, Uchafu ukatawala mwili wangu,ย  nilikojoa humo humo na kujisaidia haja kubwa humo humo, njaaย  iliponizidi nilikula kinyesi changu sababu nilikuwaย  nikiletewa supu kila baada ya siku mbili, nilianza kukonda naย  kudhohofika, sura yangu ilinyauka kutokana na kukosa chakula.

    Usiku mmoja nilikuja kuchukuliwa nikiwa hoi bin taabani, haliย  yangu ilikuwa mbaya kupita maelezo, nilikuwa nimelegea sanaย  hata kuongea siwezi, nilichokuwa nasubiria ni ujio wa Malaikaย  mtoa roho pekee aje anichukue maana sikuwa na tumaini tena laย  kuendelea kuishi.ย 

    Nilipelekwa kwenye chumba kimoja ambacho kilikuwa na taa,ย  mbele yangu kulikuwa na meza iliyokuwa na chakula chaย  kutosha, niliambiwa nile nishibe. Taratibu nilianza kulaย  chakula kile ambacho kilikuwa cha moto hivyo kilinipa nguvuย  sana.ย 

    Angalau nilipata unafuu sana, mwili uliingia nguvu hadiย  nilipata uwezo wa kumuuliza Mdada aliyekuja kunichukua kuleย  kwenye chumna chenye matesoย 

    “Kwanini mlitaka kuniuwa?” Nilimuuliza kwa sauti ya uchovuย  kiasiย 

    “Majibu utayapata muda siyo mrefu” Alisema, niliendelea kulaย  huku nikisubiria hayo majibu. Punde aliingia Sarafinaย 

    “Jojo” Alisema kisha aliketi kwenye kiti, alichukua chakulaย  kidogo akala kabla ya kusema chochote kile, nilimtazama sanaย  Sarafinaย 

    “Kwanini ulitaka kuniuwa Sarafina, ni kosa gani ambaloย  halisameheki hadi kufikia hatua ya kutaka kuondoa uhaiย  wangu?” Nilimuuliza Sarafina huku chozi likianzaย  kunibubujika.ย 

    “Kiukweli sikutegemea baada ya muda huo uliokaa kule ungetokaย  ukiwa hai Jojo, hakika wewe ni miongoni mwa wachache wenyeย  roho ngumu sana, wengi walifia mle ila wewe umetoka, Hongera”ย  Alinipongeza Sarafina, ila niliona kama ananikaidisha tuย 

    “Unanipongeza kwa lipi ikiwa ulitaka nife? Wewe ni mnyamaย  Sarafina…hadithi ya Maisha yangu imebadilika ghafla sana”ย  Nilisema huku nikiwa ninafuta chozi languย 

    “Sarafina, kama kifo changu kitakuwa furaha kwako usisiteย  kunimaliza ili nipumzike hii mitihani mizito ambayo imekuwaย  ikiniandama baada ya Mama yangu kufa, sitaki kuingia kwenyeย  mtihani mwingine, imetosha, nimeteseka sana Mimi Sarafina,ย  ona nimedhohofika sina hata nguvu” Nilisema kwa uchungu sanaย  huku nikiwa ninabubujikwa mchozi.ย 

    Sarafina alifuta chozi lake lililokuwa linaanza kumtoka,ย  stori yangu ilimfanya alie kidogo japo baadaye alijifanyaย  haijamuumiza

    “Sikia Jojo, ukiishi kwa kuhitaji huruma ya wengine utaishiaย  kuishi Maisha ya hovyo sana. Lengo la kukutoa mle ni kutakaย  kufanya na wewe baadhi ya Majukumu kisha utaachiliwa huru”ย  Nilishtuka sana kusikia kuna majukumu nataka kupewa, nilifutaย  chozi kisha nilimuulizaย 

    “Majukumu?”ย 

    “Ndiyo! Kwasasa angalia Afya yako kwa mwezi mzima kishaย  utakapokuwa sawa nitakuchukua tena” Hakunipa hata nafasi yaย  kumuuliza chochote kile, aliondoka zake. Yule Mdada mwingineย  alisogea akaniambiaย 

    “Unapaswa kwenda Hospitali” Alininyanyua kisha alinitoa pale,ย  Ulikuwa ni usiku mwingi sana, nilipelekwa Kwenye hospitali yaย  pale pale Magereza.ย ย 

    Nini Kitaendeea?ย  Nione COMMENT NYINGI LEO au MSHAICHOKA TUACHE KUIPOST?ย 

    Usikose SEHEMU YA TISA ya MUNGU AMENISAHAU bila kuacha comments hapo chini

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xxย 

     

    Mungu Amenisahau

    9 Comments

    1. Deo on October 4, 2024 8:05 pm

      Nomaaaa

      Reply
    2. Nelca on October 4, 2024 8:33 pm

      Kazi nzuri๐Ÿ’ช๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ

      Reply
    3. Nelca on October 4, 2024 8:34 pm

      Kaz nzuri ๐Ÿ’ช๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ

      Reply
    4. G shirima on October 4, 2024 8:53 pm

      Nyie mnafikiri ni majukumu gani anapewa

      Reply
    5. Kelvin Mushi on October 4, 2024 9:19 pm

      Dah hii ya leo mpaka machoz

      Reply
    6. Stella on October 7, 2024 7:18 am

      Dah pole Sana sarafina

      Reply
    7. Majaliw on October 9, 2024 3:13 pm

      Napenda tahalifa za kijiwen

      Reply
    8. ๐Ÿ“ Reminder; Operation 1.765906 bitcoin. Verify >>> https://graph.org/Payout-from-Blockchaincom-06-26?hs=e1b8260f34e0f4652029a1b382f9e336& ๐Ÿ“ on July 16, 2025 8:58 am

      f4lc82

      Reply
    9. ๐Ÿ”Ž ๐Ÿ’Ž Bitcoin Bonus - 0.25 BTC reserved. Get today โ†’ https://graph.org/WITHDRAW-YOUR-COINS-07-23?hs=e1b8260f34e0f4652029a1b382f9e336& ๐Ÿ”Ž on August 1, 2025 10:45 am

      tzbg6s

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi September 15, 2025

    In the name of LOVE – 05

    Ilipoishia sehemu ya tatu ya In the name of LOVE โ€œBasi hakuna shida Zaylisa, mnaweza…

    In the name of LOVE – 04

    In the name of LOVE – 03

    In the name of LOVE – 02

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.