Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 12

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Mungu Amenisahau Sehemu Ya Sita (06)
    Hadithi

    Mungu Amenisahau Sehemu Ya Sita (06)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaOctober 1, 2024Updated:October 2, 202411 Comments10 Mins Read1K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mungu Amenisahau
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Haraka nikiwa nimevalia pensi na tisheti nilielekea huko,ย  kweli niliona Kijiwe cha Watu watatu hivi ambao baada yaย  kuniona Mimi walikaa tayari, nilitoa ishara ya vidole ambayoย  Juma Baro aliniambia, ilikuwa ni ishara ya kuwaambia kuwaย  kuna amani, ishara hiyo ilikuwa ikitumiwa na Wauza ungaย  pekee, walipoona Ishara hiyo walikaa kisha nilisogea hadiย  hapo, nilinunua kete mbili za madawa kwa shilingi elfu 20ย  kisha nilirudi kwa Mama Nesha nikiwa na shahuku ya kutulizaย  kiu yangu.ย 

    “Jojo?” Alisema Mama Nesha baada ya kusikia mlangoย  ukifunguliwaย 

    “‘Ni Mimi Mama, nimerudi” Nilisema mkononi nikiwa na Juisiย  ili kusiwe na maswali. Endeleaย 

    SEHEMU YA SITA

    “Haya namalizia kupika kikiwa tayari nitakuja kukuita”ย  alisema Mama Nesha kwa sauti ya mbali akiwa Jikoni namiย  nilimjibuย 

    “Sawa Mama” Basi nilipitiliza hadi Chumbani kwangu huku ileย  kiu ikizidi kuongezeka hadi nilisahau kufunga mlango, nguvuย  zilianza kuniisha nikawa nafungua kete huku nikiwaย  natetemeka, nilikuwa nimekaa chini, nilifanikiwa kufunguaย  kisha nilianza kuvuta madawa kwa pupa sana, kwakuwa nilikuwaย  nimeshazoea wala hayakunipa shida sana.ย 

    Nilivuta kwa nusu saa hadi niliona akili ikisizi kama vileย  nilikuwa nataka kuingia usingizini, kumbe Mama Nesha alikujaย  Chumbani kuniambia kuwa chakula kipo tayari, aliniona nikiwaย  ninavuta madawa sababu mlango ulikuwa waziย 

    “Jojo” alisema Mama Nesha kwa mshituko Mkubwaย 

    “Unatumia madawa ya kulevya Jojo?” Aliuliza kwa mshitukoย  akiwa amenisogelea, alinikata hamu zote nikamtazama kamaย  mwizi aliyefumwa akiiba, sikutaka Mtu yeyote ajuwe kuwaย  nilikuwa natumia madawa ya kulevyaย 

    “Kumbe ndiyo maana ulipoteza fahamu kwa siku mbili ni sababuย  unatumia madawa ya kulevya, hii taarifa nampa Baba Neshaย  kisha naenda polisi sitaki uje utuletee matatizo” Alisemaย  Kisha alianza kuondoka kwa haraka pale chumbani, kiukweliย  madawa yaliniondoa utu wangu kabisa, nilibadilika kutokana naย  Maisha niliyoishi mwote nilimopita, nilifikiria kumuuwa Mamaย  Nesha

    Haraka nilimkimbilia Mama Nesha hata kabla hajafika chumbaniย  kwake, nilimkaba shingo yake kwa nguvu sana sababu madawaย  yalikuwa yakinipa nguvu, nilihakikisha namuuwa Mama Neshaย  bila huruma huku madawa yakishinikiza kufanya hivyo.ย 

    “Jooo Joo, unanii…uwaa” Alisema Mama Nesha lakini sikujaliย  hata mateso aliyokuwa akiyapata, sikutaka kuingia matatizoniย  kabisa. Niliendelea kukaba shingo yake hadi hatua ya mwishoย  ambapo alilegea kabisa na kufariki. Nilipomuuwa Mama Neshaย  ndipo akili yangu ya kawaida iliporejea, niliwaza kukimbiaย  msala huo.ย 

    Haraka nilirudi chumbani kwangu, nilichukua begi na vituย  vyangu vyote kisha niliondoka, nilikimbilia stendi nilipandaย  gari ya kurudi Dar. Nilikuwa nimechanganikiwa kabisa, uzuriย  ni kuwa Baba Nesha alikuwa amesafiriย 

    “Dada futa pua yako kuna uchafu” Alisema Mkaka aliyekaa sitiย  moja na Mimi, aliuwona ule unga eneo la pua yangu ilaย  hakujuwa kama ulikuwa ni Unga wa madawa ya Kulevyaย 

    “Asante sana” Nilijibu kisha nilijifuta haraka sana, ilikuwaย  ni mishale ya saa 9 Mchana, nilifika Dar saa 1 Usiku.ย  Sikujuwa niingilie wapi usiku ule, pesa iliyobakia ilikuwaย  chache sana. Usiku ule niliona ni bora nitafute Gesti nilaleย 

    Nilipata gesti maeneo ya Temeke Mwisho kule kwa nyuma,ย  nililala hapo Usiku huo hata sikukumbuka kula. Asubuhiย  niliona taarifa ya habari ikielezea juu ya Mauwajiย  niliyoyafanya ila uzuri ni kuwa hakuna aliyekuwa na pichaย  yangu ila tu jina la Jojo ndilo lililo tajwa, nilimuona piaย  Baba Nesha akisema kwa uchungu na maumivu makali sana,ย  alielezea jinsi alivyoniokota Shambani kwake na kunifanyiaย  wema, yalikutwa madawa ya kulevya kwenye kile chumba ambachoย  nilikuwa nikiishi. Roho iliniuma sana ila sikuwa na jinsiย  sababu tayari nilishaamuwa kukimbiza Maisha yangu vinginevyoย  ningekamatwa na polisi.ย 

    “Nimekuwaje Mimi Jojo?” Nilisema kwa maumivu makali sanaย  ndani ya moyo wangu, sikutegemea kabisa kama ningefikia hatuaย  ya kuwa Muuwaji. Nilifikiria sana niliona ni bora nitafuteย  pesa nirudi nyumbani kwetu ila sikuwa na kazi. Nilibakiwa naย  shilingi Elfu 10 tu ambayo ilikuwa ndiyo pesa pekeeย  niliyonayo, niliiangalia huku nikitafakariย 

    Ghafla mlango uligongwa, nilishtuka sana, nilihisi ni polisiย  maana kesi ya kuuwa ni kubwa mno, niliulizaย 

    “Nani?”

    “Nahitaji kufanya Usafi” nilisikia sauti, nilijuwa tu atakuwaย  ni Mtu wa Usafi wa ile Gest, niliangalia saa ya ukutaniย  niliona ni saa 3 asubuhi, muda wa Mimi kuondoka pale Gestย  uliwadia, nilienda kumfungulia kisha aliniulizaย 

    “Unalipia tena au unaondoka?”ย 

    “Naondoka, ila nitarudi, naomba nikuachie Begi languย  tafadhali”ย 

    “Mh! Labda ukamuombe yule Mkaka wa mapokezi maana mimiย  sihusiki kabisa na hayo, muombe atakukubalia tu ilimradi kuweย  na usalama”ย 

    “Usalama upo Dada yangu” Basi, kwakuwa nilikuwaย  nimeshajiandaa, nilikuwa nimevalia suruali nyeusi na rabaย  nyeusi, juu shati jeupe nilielekea Mapokezi kumuomba Mkaka waย  Mapokezi anihifadhie begi languย 

    “Habari Kaka yangu”ย 

    “Salama” alinijibu akionesha sio Mtu wa Stori nyingiย 

    “Samahani Kaka yangu naomba unihifadhie Begi langu kunaย  mihangaiko nikaifanye nikirudi nitalichukua” Nilisema kwaย  kujiamini kama vile mfanyabiashara aliyetokea mkoani kuja Darย  kununua bidhaa, yule Mkaka kwa umakini sana kisha aliniulizaย 

    “Kuna usalama?” Nilijichekesha kidogo kisha nilimjibu “Ndiyo Kaka yangu”ย 

    “Fungua tuone kuna nini!” Alisema akiwa ananikodolea machoย  kama Askari wa Barabaraniย 

    Nilijiamini sababu sikuwa na chochote cha kushangaza,ย  nilifungua begi nikatoa nguo zoteย 

    “Ni nguo zangu tu Kaka yangu”ย 

    “Sawa liache ila hakikisha unalirejea leo leo” Alinisistizaย  kwa ishara ya Kidole, nilimuaminisha kuwa nitalifuata japoย  sikuwa na uhakika maana hata sehemu ya kwenda kuliweka lileย  begi sikuwa nayo, nilirejesha nguo kwenye begi haraka sanaย  kisha nilimpatia lile begiย 

    “Asante Kaka yangu jioni nitarudi Baada ya Mizunguko”

    Basi niliondoka pale, hadi kituo cha magari ya kuelekeaย  Mjini. Niliona Magari ya Kariakoo, Tabata, Ubungo, niliona niย  bora nielekee Ubungo maana jina hilo halikuwa ngeni kwanguย  kuliko Kariakoo na Tabata.ย 

    Nilikuwa mwingi wa kuwaza, nilitoa ile Elfu 10 kisha kondaktaย  aliniambia hana Chenji atanipatia mbele, basi nikatuliaย  zangu. Nakumbuka ndani ya gari waliweka redio ya Cloudsย  kipindi cha Leo tena ikawa inasikika ile habari ya Mimiย  kumuuwa Mama Nesha.ย 

    Nilishtuka sana nikahisi kama nimegundulika kuwa ndiyeย  niliyeuwa maana niliona kama watu wananiangalia kumbe hataย  haikuwa hivyo bali ni wenge langu tuย 

    “Konda nashuka” Nilisema huku nikiwa kwenye hekaheka zaย  kupishana na watu kwa nguvu ili nishukeย 

    “We Dada si ushuke taratibu” Alisema Mdada mmoja, walaย  sikujali nilisukuma Watu hadi nilipofika mlangoni, hataย  sikukumbuka chenji yangu nilishuka kisha niliingia mtaani,ย  niliona kabisa nilikuwa nimechanganikiwa kabisa. Kilaย  niliyekutana naye niliona ni Polisi na anakuja kunikamata,ย  nikawa kama Chizi jumlisha na madawa ya kulevya amabyoย  nilikuwa nikiyatumia. Ilikuwa ni maeneo ya Buguruni Sheli,ย  niliongoza njia ya kuelekea Vingunguti kupitia kwa Mnyamani.ย 

    Nilitembea kwa umbali mrefu sana bila hata kuhisi kuchokaย  hadi nilipofika Machinjio ya Vingunguti, nilishuka na ileย  barabara ya kuelekea Barakuda, nilipofika Kwenye Darajaย  nilituliza wenge langu. Nilikuwa wa hovyo sana kuliko hataย  ninavyoweza kuelezea hapaย 

    Nilitembea taratibu, njaa ilianza kunichapa huku ile hamu yaย  kuhitaji madawa ya kulevya ikizidi kuniingia. Kilaย  aliyenitazama aligundua haraka kuwa nilipoteza uwezo waย  kujiamini, rangi na asili yangu ya uarabu ilifunikwa naย  mawazo nikawa kama Muarabu aliyefirisika. Ilifika mahali hataย  viatu niliviona vizito, nilivivua na kuvishika mkononi,ย  nilitafuta sehemu nikakaaย 

    Mwili ulijaa arosto ya Madawa ya kulevya mno, nilijilazaย  chini ya Mti nikiwa nimejikunyata. Niliwaza nikutane naย  Shonaa anisaidie lakini sikujuwa alikuwa akiishi wapi, sikuwaย  na simu wala nilikuwa simfahamu Mtu yeyote ndani ya Jiji laย  Dar-es-salaam.ย 

    Nilikuja kushtuka giza lilikuwa limeingia, mwili ulikuwaย  hauna nguvu kabisa. Kumbe pale nilipokuwa nimelala palikuwaย ni maskani ya wavuta bangi, moshi wa Bangi ulipopita kwenyeย  pua zangu nilijikuta nikisisimka sana, nilimuomba jamaaย  aliyekuwa anavuta akanipaย 

    Niliivuta haraka haraka kama vile Mtu mwenye njaa kaliย  anapopata chakula katika mazingira asiyoyategemea.ย 

    Wahuni wote walinishangaa sana kisha ukimya ukawa umetawala,ย  hata sikuchukua dakika moja nilikuwa nimeumaliza ule msokoto,ย  basi liliibuka shangwe kutoka kwao wakinisifu kuwa Mimi niย  jembe. Nilicheka pia maana nguvu ilikuwa imeshaniingiaย  mwilini, wahuni walikuwa ndiyo wanangu.ย 

    Basi tulikaa pale wakiwa wanapiga stori zao, kulikuwa naย  ubaridi fulani hivi ambao kila nilipovuta Bangi nilihisi jotoย  la kutisha lenye raha ndani yake. Kadhaa waliondoka akabakiaย  Jamaa mmoja tu ambaye alianza kuniuliza maswali ya hapa naย  paleย 

    “Unaitwa Nani mrembo?” Aliuliza akiwa anacheka cheka, alikuwaย  tejaย 

    “Jojo”ย 

    “Oh Jojo jijooo…Hahaha! Naitwa Domingo, mimi ndiyeย  niliyepiga kampeni zote za CCM mwaka 1890 Nchini Japani”ย  Alisema, zilikuwa ni stori za kuchekesha sana ambazo kwa mudaย  huo niliona zilikuwa kweli kwasababu nilikuwa muathirika waย  madawa hivyo akili yangu ilijaa uteja mnoย 

    “Ha!ha!ha! Wewe ni noma” nilisema nikiwa ninafurahiย 

    “Sema nini Jojoo…twenzetu mageto tukale raha au unasemaje?”ย  Aliuliza Domingoย 

    “Poaa” Nilijibu hata sikufikiria Chochote, Tuliondoka tukiwaย  tunapiga Stori za ajabu ajabu zilizotokana na bangiย 

    Gheto lenyewe lilikuwa ni kiota kilichojengwa kwa mifukoย  kando ya Mto msimbazi.ย 

    “Hili ndiyo ghorofa langu Jojo, nimekuelewa sana ujuwe”ย  Alisema Domingo, Bangi zilinifanya nione ni kweli ghorofa,ย  basi tulilala na kufanya mapenzi hapo bila hata kujuwa afyaย  ya Domingo, Maisha yangu Mimi Jojo yalizidi kuharibikaย 

    Asubuhi, Bangi ilikuwa imeondoka. Nilijishangaa mahaliย  nilipokuwa nimelala, huyo Domingo nilimtazama mara mbili,ย  alikuwa amejawa na chawa kwenye mwili wake, alikuwa naย ukurutu wa kutosha alafu nywele zake zilibadili rangi na kuwaย  za dhahabu kutokana na uchafuย 

    “Nini hiki Jojo?” Nilijiuliza, nilitema Mate, japo nilikuwaย  teja lakini sikufikia hatua ya kuwa Mchafu. Haraka nilitafutaย  viatu nikaondoka zangu pale nikamuacha Domingo akiwa amelala.ย  Watu walioniona nikiwa ninatoka Pale walinishangaa kutokanaย  na uzuri nilionaoย 

    Basi nilirudi kule Buguruni kwa kufuata ile barabaraย  niliyokuja nayo Barakuda. Nilipoteza muelekeo wa Maishaย  kabisa, Jojo hali yangu ilikuwa mbaya sikula Tokea nilipokulaย  kule Rufiji, niliona Vijana waliokuwa wakiomba omba kwenyeย  magari yaliyo kwenye foleni, nilijiangalia nikaona ni boraย  nami nikaombe msaada mana kuna Wakati nilikuwa najitambuaย  kabisa na kujuwa kuwa sipaswi kuyaishi maisha ya Utejaย 

    Niliomba kwenye gari moja badala ya Jingine, wengineย  walinikebehi, wengine hawakutaka kunisikiliza kabisa, gari yaย  mwisho nilimkuta Msanii mkubwa sana wa kike hapa Tanzaniaย  ambaye siwezi kumtaja jina lake, alikuwa ndani ya gari nzuriย  sana akiwa naye anasubiria gari zianze kuondoka, niligongaย  kioo chake, alipofungua ndipo nilipomuona kwa uzuri,ย  alinifanya nitabasamu sababu sikuwahi kumuona ana kwa anaย 

    “Nikusaidie nini?” Aliuliza huyo Msanii maana nilikuwaย  namkodolea macho tu hata kusema nilikuwa siweziย 

    “Naomba msaada Dada yangu sina pa kuishi, sina kazi, nahitajiย  kurudi kwetu Tabora” Nilisema, aliniangalia kwa muda mrefuย  bila kusema chochote kisha alimgeukia Mwanaume aliyekuwa nayeย  kwenye gari nahisi alimuuliza kwa ishara kama anisaidie auย  aniache, yule Mwanaume alinitazama juu chini kisha akamwambiaย 

    “Mchukue”ย 

    “Ingia kwenye gari” ilikuwa kama ndoto vile, nilifunguaย  mlango wa gari ili niingie kwenye gari. Kabla hata sijaingiaย  nilihisi uzito kwenye mgongo wangu alafu nilipata nguvu yaย  kuulizaย 

    “Nani wewe!” Niliuliza kwa sauti ya juu mno kisha nilionaย  kama vile Dunia ilikuwa imesimama, ghafla nilisikia sauti yaย  kugongwa kwa mlango. Mara nilijikuta nikirushwa pembeni,ย  nilitumia nguvu ya mwisho kuangalia niliona pikipikiย  ikianguka kando yangu ndipo nilipogundua kuwa nilikuwaย  nimepata ajali ya Pikipiki. Sikuelewa kilichoendelea, mzimuย  wa laana na matatizo uliendelea kuniandana. Nini Kitaendeea?ย  Nione COMMENT NYINGI LEO au MSHAICHOKA TUACHE KUIPOST?ย 

    Usikose SEHEMU YA SABA ya MUNGU AMENISAHAU bila kuacha comments hapo chini

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Mpya Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

     

    ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xx ย Mungu Amenisahau xxย 

     

    ย ย 

    Mungu Amenisahau

    11 Comments

    1. Stella on October 1, 2024 2:16 pm

      Awesome thanks
      ๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜

      Reply
      • Daniel on October 1, 2024 4:28 pm

        Daah imenoga atar kiongoz

        Reply
    2. Ibrahimu on October 1, 2024 4:20 pm

      Daaaah

      Reply
      • Lucas George on October 1, 2024 5:24 pm

        Unge onganisha ya saba tu maana umetuacha na alosto

        Reply
      • Fatma on October 2, 2024 2:39 pm

        Lahaulaa

        Reply
    3. Daniel on October 1, 2024 4:28 pm

      Daah imenoga atar kiongoz

      Reply
    4. Ignasi on October 1, 2024 5:01 pm

      Nimeipenda pia nimefunzwa kitu

      Reply
    5. Farnoush on October 1, 2024 7:06 pm

      Jojo jijooo๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚ ila mateja bana

      Reply
    6. G shirima on October 1, 2024 8:10 pm

      Sijui kwanini nakua n arosto ya hii kama Jojo na dawa zake

      Reply
    7. yuzzo sailor official on October 2, 2024 3:13 pm

      sehemu ya saba please

      Reply
    8. Patrick paul on October 3, 2024 1:16 am

      Mzigo hatari unazidi kuelekea pazuri keep it up…..

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi October 1, 2025

    In the name of LOVE – 12

    Ilipoishia sehemu ya Kumi na moja ya In the name of LOVE Moyo Wangu na…

    In the name of LOVE – 11

    In the name of LOVE – 10

    In the name of LOVE – 09

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.