Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Pigo Takatifu Sehemu Ya Nane (08)
    Hadithi

    Pigo Takatifu Sehemu Ya Nane (08)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaSeptember 19, 2024Updated:September 20, 202412 Comments11 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Pigo Takatifu
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Muda huo Magari mawili yalikua yakiingia Hospitalini hapo kwaΒ  kupishana dakika tano, aliyekua wa kwanza kuingia alikua niΒ  James, alipotoka tu kwa Chilo aliona ni bora alekee HospitaliΒ  kumwona Patra sababu nafsi ilikua ikimsuta sana. AkaketiΒ kwenye gari iliyo Paking kwa dakika kadhaa akitafakari namnaΒ  mambo yalivyokua yakiendelea, Gari ya pili ilikua ni gari yaΒ  Neema, kila mmoja aliegesha gari kwa upande wake lakini JamesΒ  alikua na nafasi ya kumwona Neena sababu alikua amepakiΒ  sehemu yenye magari mengi, akaliona gari la Neema likiingiaΒ  akajiuliza Neema amefuata nini pale Hospitalini. EndeleaΒ Β 

    SEHEMU YA NANE

    Hofu ikatanda kwenye moyo wake sababu Neema alishasema kuaΒ  atamuuwa Patra, katika hali isiyo ya kawaida James akajikutaΒ  akiumia ndani ya moyo wake, akatamani kushuka ili amfwatilieΒ  lakini moyo wake ukawa unamsuta mara kadhaa huku akimshuhudiaΒ  Neema akishuka na kuanza kutembea kwa Mguu kuelekea ndaniΒ  zaidi. Akawa kwenye vita kubwa sana ndani yake hadiΒ  aliposhinda na kuamua kushuka kisha akaanza kumfwatiliaΒ  Neema, kumbuka Neema alikua amepewa ile dawa na Babu yakeΒ  akaiweke katikati ya Hospitali ya Muhimbili ili Mtoto PatraΒ  aonekane kusudi auaweΒ 

    “Huyu amefwata nini hapa Hospitalini?” akajiuliza James akiwaΒ  anaendelea kumfwatilia, James alifahamu mahali alipolazwaΒ  Patra, Neema akawa anaelekea huko pasipo kujua kua ndikoΒ  aliko Patra, lakini baadaye akabadilisha uelekeo kitu ambachoΒ  kilimfanya James ashushe presha yake. Neema alikua makiniΒ  sana tena akionekana ni mwenye kujiamini kabisa, JamesΒ  hakutaka kukubali kushindwa akataka kujua ni jambo ganiΒ  limempeleka Neema Hapo Hospitalini.Β 

    Matilda akiwa katika chumba chenye giza, hakujua mahali hapoΒ  ni wapi isipokua alijua kua alikua amehamishwa kutoka paleΒ  alipokua zamani, alimfikiria sana Binti yake, akawa anasikiaΒ  walinzi wakizungumza, tena wakibishana masuala ya Mpira,Β  Chumba alichopo hakikumpa ruksa ya kuona kilichokuaΒ  kikiendelea nje isipokua aliisikia kelele za hao walinziΒ  pekee, alijua yupo mafichoni, akaanza kupiganisha akili iliΒ  ajue anaweza vipi kutoroka hapo.Β 

    Basi, James akaendelea kumfwatilia Neema taratibu tena kwaΒ  umakini huku akiwa na maswali mengi sana kichwani. Neema nayeΒ  akazidi kuongeza mwendo huku lengo likiwa kufanya kamaΒ  ambavyo Babu yake alimwambia, alipofika katikati yaΒ  Hospitali, akageuka huku na kule huku James akijibanza mahaliΒ  ili aone Neema anaelekea wapi.Β 

    Akazuga kidogo kabla ya kuingiza mkono kwenye Mkoba kishaΒ  akatoa hicho alichopewa na Babu yake alafu akakitupa naΒ kukificha kwa Majani kwa kutumia Mguu wake, James alikuaΒ  akiona kila kitu, baada ya kumaliza akaangaza tena huku naΒ  kule kisha haraka akageuka na kurudi alipotoka, akampitaΒ  James bila kumwona kisha akaelekea Kwenye maegesho lakiniΒ  wakati anatoka hapo akaliona gari la James ndipo akapataΒ  uhakika zaidi kua Patra yupo hapo Hospitalini, akatabasamuΒ  kisha akampigia simu Babu yake na kumwambia kua ameshamaliza,Β  kweli Babu yake alipoangalia tena alimwona Patra kishaΒ  akacheka na kutengeneza bomu kwa ajili ya kummaliza PatraΒ 

    James akafikiria sana ni kitu gani ambacho Neema alikiwekaΒ  pale, hakutaka kukipa uzito sana badala yake akarudi nyumaΒ  kisha akaelekea ilipo wodi ambayo Patra amelazwa, kumbukaΒ  ndani ya wodi hiyo alikuwepo Mama yake MzaziΒ 

    Basi James akasogea hadi mlangoni, Patra alilazwa katika wodiΒ  ambayo ilikua ya hadhi kubwa sana, kitendo cha kufika tuΒ  mlangoni alifanikiwa kumwona Mama yake Mzazi akiwaΒ  anazungumza na Mchungaji, alimwona kupitia kioo cha hapoΒ  Mlangoni, akashtuka sana, Mara akashikwa begaΒ 

    Akageuka na kukutana na Daktari ambaye alikua amezungumzaΒ  naye na kumwambia kua kwa lolote litakalo hitajika basiΒ  amweleze, na ndiye aliyekua akimweleza kuhusu hali ya MtotoΒ 

    “Oooh Mr. James….Karibu sana” Alisema Daktari kisha akampaΒ  mkono James ambaye alikua katika butwaa zito sanaΒ 

    “Ndiyo unakuja au unaondoka?” akauliza Daktari huyo, BadoΒ  James alikua kwenye Butwaa maana hakutegemea kumwona MamaΒ  yake pale Wodini.Β 

    “Nili….kua…Naondoka” Akasema James kwa kujiuma umaΒ 

    “Basi sawa, namshukuru Sana Mungu hali ndiyo kamaΒ  ulivyoiyona, Mtoto anaendelea vizuri kwasasa” Akasema DakatriΒ  kisha akafungua mlango na kuingia wodini, Haraka JamesΒ  akaondokaΒ 

    “Mmemwona Mfadhili?” akauliza Daktari, wote wakashangaa “Mfadhili?” akauliza Mama yake JamesΒ 

    “Ndiyo…..si alikua hapa kumwona Mtoto, ametoka sasa hiviΒ  nimepishana naye hapa Mlangoni”Β 

    “Hapana Dokta, Hakuna Mtu aliyefika hapa wodini tokeaΒ  ulipotuacha” Akasema Mama yake James, ikampa Mshangao Dokta,Β  akaelekea mlangoni kumwangalia James lakini hakufanikiwaΒ  kumwona tena

    “Mbona nimekutana naye mlangoni akanambia kua ametoka hapaΒ  wodini, yeye amekua akichangia pesa za matibabu ya Mtoto”Β  Alisema, kisha akatoa Kadi ya Biashara ambayo alipewa naΒ  James, akamwonesha Mama James, ndipo Mama James nayeΒ  alipogundua kua James alikuja Hospitalini na bila shakaΒ  alimwona Mama yake, lakini kilichomshtua Mama James niΒ  kusikia kua James anachangia matibabu ya Mtoto.Β 

    Muda huo tayari James alishaondoka Hospitalini, alikuaΒ  Barabarani akiendesha gari yake kwa sapidi sana kuelekea njeΒ  ya Jiji ambako alimwacha Matilda, hakujua kua MatildaΒ  alishaondolewa. Alitumia masaa zaidi ya mawili hadi kufika,Β  alipoingia ndani ya jumba hilo lililo msituni hakumwonaΒ  Matilda pia hakukuta Mtu yeyote yule kitu ambacho kilianzaΒ  kumchanganya. Akaingia tena kwenye gari na kurudi MjiniΒ 

    Wakati huo Matilda akiwa bado anapiganisha akili anawezajeΒ  akatoroka hapo ili kunusuru Maisha yake, Walinzi walikuaΒ  wakikagua chumba chake mara kwa mara kuhakikisha haondokiΒ  hapo kama ambavyo Neema alikua ameagiza, ilimpa wakati mgumuΒ  sana MatildaΒ 

    Mama yake James aliporudi nyumbani kwake alihisi mwiliΒ  ukipata moto, kwanza kujua tu kua James amshamwona paleΒ  Hospitalini kulimpa mashaka makubwa sana sababu hakutakaΒ  ajuwe chochote lakini kingine kilichomuwazisha zaidi ni paleΒ  aliposikia kua James alikua akitoa pesa za matibabu ya Mtoto,Β  maana yake ni kwamba James alikua na mapenzi na Patra.Β 

    Siku iliyofuata mapema sana, taarifa mbaya ilianza kueneaΒ  kwenye simu, ilikua ni kuhusu hali ya Patra ambayoΒ  ilibadilika ghafla sana, tena ikidaiwa kua mapigo yake yaΒ  moyo yalikua yakishuka kwa kasi kitu ambacho kilikuaΒ  kinaashiria kifo kwa Mtoto huyo, miongoni mwa waliotumiwaΒ  ujunbe huo alikua ni James, Mama yake James, Mama Naomi, JackΒ  na Mchungaji GeorgeΒ 

    Haraka wote wakafika Hospitalini isipokua James ambaye alikuaΒ  akifikiria ni namna gani ataingia hapo kwa ajili ya kumwonaΒ  Patra, ilionekana wazi kua Patra anaweza kutangazwa kuaΒ  amefariki muda wowote, Mchungaji alijitahidi sana kufanyaΒ  maombi lakini Mishale ya saa nne Asubuhi Patra alifarikiΒ  Dunia, Daktari akathibitisha hilo

    “Poleni sana, tumejitahidi kuokoa uhai wake lakini juhudiΒ  zetu zimegonga mwamba” Akasema Daktari huku akishuhudia mvuaΒ  ya vilio, Mchungaji George akashindwa kuvumilia akakimbiliaΒ  kulia nje kama Mwanaume, ilikua ni huzuni kwa kilaΒ  aliyesikia. Mama James hakuona kama kulikua na sababu yaΒ  kuendelea kulificha hilo sababu alihitaji msiba ukafanyikeΒ  nyumbani kwake, akampigia simu James na kumwambia kuaΒ  anahitaji kuonana nayeΒ 

    Haraka James akaenda nyumbani kwa Mama yake, akamkuta MamaΒ  yake akiwa mwingi wa huzuni, akaketi kando ya Mama yake kablaΒ  ya kumuuliza kiunyonge kilichopelekea huzuni hiyoΒ 

    “Amekufa” Alisema Mama yake James huku chozi likizidiΒ  kumvuja, James akashtuka sana, moja kwa moja akajua ni PatraΒ  lakini akajikaza huku akizidi kumuuliza Mama yakeΒ 

    “Nani huyo Mama”Β 

    “Mtoto wako, Kwanini ulifanya siri James, Mtoto ameteseka MnoΒ  hadi amefariki” Akasema Mama yake James huku akiangushaΒ  kilio, chozi likambubujika James, hakua na la kufanya,Β  hakuweza kubeba ukatili wa kukana mbele ya Mama yakeΒ 

    “Kisa ulemavu James umegeuka kua Mnyama, Mama wa Mtoto hadiΒ  sasa hajulikani yupo wapi….James, hapana shaka upo nyuma yaΒ  hili jambo, nakuhakikishia kua Patra hatozikwa kama Mama yakeΒ  Patra hatopatikana” Alisema Mama yake James, kila jamboΒ  lilikua tayari limefunguka, hapakua na siri tena. JamesΒ  akainamia chiniΒ 

    “Kama kuna siku nimeumia katika Maisha yangu James basi niΒ  leo, James wewe ni katili sana Mwanangu, hustahili kuitwaΒ  Binadamu, Nenda kamlete Mama yake Patra hapa” Akasema kwaΒ  hasira Mama yake James, Basi James akawa kama Budi akasimamaΒ  asijuwe aingilie wapi kumtafuta Matilda, akatoka huku choziΒ  likiendelea kumbubujika, alipofika getini alipishana na gariΒ  iliyowabeba Mchungaji, Mama Naomi na JackΒ 

    Alipotoka hapo James akaelekea Baa, akaagiza pombe kali naΒ  kuinywa kama anakunywa maji, alihisi kufanya hivyo kungeondoaΒ  Mawazo yote, licha ya kua na pesa nyingi ambazo wengi huaminiΒ  kua na pesa kunamaliza matatizo lakini upande wa James ilikuaΒ  tofauti, pesa ndiyo iliyoleta matatizo kwake.Β 

    Giza liliingia huku James akiendelea kuagiza moja baridi,Β  moja moto hadi akalewa kabisa na kushindwa kujitambua,Β  akasaidiwa na baadhi ya waliomjua sababu alikua maarufu,Β  akarudishwa nyumbani kwake.

    Usiku huo tafrani ikawa nzito nyumbani kwa Mama James,Β  Mchungaji aliomba Patra azikwe lakini Mama James aligomeaΒ  kabisa akihitaji kwanza Matilda afike ili amshuhudie BintiΒ  yake, wakambembeleza sana lakini akagoma huku akiwaambiaΒ  James atamleta Matilda sababu anajua ni wapi alipo na kamaΒ  hatomleta basi Patra hatozikwa. Mama Naomi na MchungajiΒ  wakatoka kwa ajili ya kuzungumzaΒ 

    “Huyu Mama anamaumivu makali sana, amemjua Mjukuu wake tu naΒ  Mjukuu amefariki, hali aliyonayo ni ngumu sana kuelewaΒ  chochote kile, cha Msingi kukipambazuka tumtafute JamesΒ  pengine anajua ni wapi alipo Matilda” Akasema Mchungaji,Β  Asbuhi mapema sana wakampigia simu James, wakapanga waonaneΒ  ili kuweka mambo sawa, James hakua na ujanja akawaelekezaΒ  mahali anapoishi, walipofika walikuta mazingira ya hovyo sanaΒ  sbaabu wafanyakazi wote waliondolewa na Neema, aliyebakiaΒ  alikua ni mlinzi tu ambaye alikua hafanyi usafiΒ 

    “Kilichotuleta hapa ni kuhusu Matilda, Mama yako amekataaΒ  kumzika Mjukuu hadi pale Mama yake Patra atakapofika, JamesΒ  kama unapajua alipo Matilda tafadhali tuambie ili tumsitiliΒ  yule Mtoto” Alsema Mchungaji, Mama Naomi akawa anafuta choziΒ  lakeΒ 

    “Mchungaji kiukweli sijui mahali alipo Matilda,, NimehangaikaΒ  sana kumtafuta bila mafanikio yoyote yale, ilipofikiaΒ  nimekata tamaa” Akasema James, hakutaka kabisa kusema kuaΒ  Neema ndiye anayejua mahali alipo Matilda, sababu alihofiaΒ  usalama wa Neema kwakua alikua MjamzitoΒ 

    “Mbona Macho yako yanasema ukweli lakini mdomo wako unaongopaΒ  James, wewe ndiye ulimshtaki Matilda, akaenda polisi lakiniΒ  akatoweka katika Mazingira tata, unajua alipo..” akadakiaΒ  Mama yake Naomi kwa hasira sanaΒ 

    “Jamani ningekua najua alipo ningemleta lakini sijui alipo,Β  nawaahidi nitaendelea kumtafuta” Akasema James huku akikunaΒ  nywele zakeΒ 

    Mchungaji akasimama na kusemaΒ 

    “Kumbuka kua Mtoto hatozikwa kama Matilda hatopatikana”Β  Alisema kisha akaongoza nje, Mama Naomi akamwambia JamesΒ 

    “Hadi kifo kinamchukua Mtoto ukiwa unaendelea kumkana, hakikaΒ  wewe ni miongoni mwa matajiri wajinga sana Duniani” AlisemaΒ  kisha naye akaondoka hapo, James hakua na jeuri tena sababuΒ  alikua katika nyakati ngumu sana

    Walipoondoka Mchungaji na Mama Naomi, James akaingia kwenyeΒ  gari yake, akampigia Jack kua asimamie majukumu ofisini kishaΒ  akawasha injini ya gari na kutimka hapo, kichwa chake kilijaaΒ  mkanganyiko, zilipita siku mbili bila kuzungumza na Neema,Β  akili yake ikawa inawaza atafanya nini ikiwa Neema ndiyeΒ  anayemshikilia Matilda.Β 

    Injini ya gari ikazima katika geti la Nyumba ya Neema, MlinziΒ  akatoka na kumwambia James kua hapaswi kuingia ndaniΒ 

    “Hivi unajua unamzuia Nani, Mimi ndiye niliyeinunua hiiΒ  nyumba, hebu pisha” Akasema James kwa hasira, alihitajiΒ  kuzungumza na NeemaΒ 

    “Hii siyo amri yangu, nimeambiwa nikuzuie James” AkasemaΒ  MlinziΒ 

    “Bali ni amri ya Nani?” akahoji James, Mlinzi akachunguliaΒ  ndani kisha akamwambiaΒ 

    “Neema”Β 

    “Neema? hebu nipishe..” Akasema James huku akijikutaΒ  akisukumana na Mlinzi pale getini mara gari ya Neema ikafika,Β  Neema alikua ndani ya gari hiyo, hakutaka kushuka, JamesΒ  akasogea kisha akamwambia NeenaΒ 

    “Shuka nahitaji kuzungumza nawe” Licha ya James kusema kwaΒ  jazba lakini Neema hakutaka kutii amri hiyo, alishajua niniΒ  kimemleta James nyumbani kwake, James akafungua mlango naΒ  kumchomoa NeemaΒ 

    “Wewe vipi kwani kuna ulazima wa kuzungumza na Mimi?” akahojiΒ  kwa dharau Neema, James akampiga kibao Neema, ilikua ndiyoΒ  mara ya kwanza James anampiga Neema, wakati huo Mama yakeΒ  Neema alikua ameshatoka ndani, akamsukuma JamesΒ 

    “Wewe una Kichaa? unampiga ulimzaa wewe huyu?” akauliza MamaΒ  yake Neema huku akimtaka James ajibuΒ 

    “Mama, Neema ananiletea dharau wakati nataka kuzungumza naye”Β 

    “Kwahiyo ukidharauliwa ndiyo umpige Mtu, adabu ya wapi hiyoΒ  wewe Kijana, hujui kama upo nyumbani kwa Neema, tena siyo tuΒ  kwa Neema bali Mimi nikiwepo alafu unampiga?” Neema akawaΒ  anajilizaΒ 

    “Mama nataka kujua Matilda yupo wapi” Akauliza James

    “Matilda, ndiyo Nani…si nakuuliza wewe huyo Matilda niΒ  Nani?” akahoji Mama NeemaΒ 

    “Ni Mwanamke niliyezaa naye, Neema anajua yupo wapi!”Β 

    “Hivi wewe una utimamu wa akili, yaani Mwanamke uzae nayeΒ  wewe alafu uje umtafute kwa Neema, Dunia itakushangaa kwaΒ  uzuzu wako, kama Matajiri wote Duniani wana akili kama yakoΒ  basi kua na pesa siyo kua na heshima, alafu si ulisema hunaΒ  Mtoto, leo unakubali kua una Mtoto tena umekuja kwa NeemaΒ  kumtafuta Uliyezaa naye” Akasema Mama yake Neema, James akawaΒ  mpole na mwenye kunywea, Mama Neema akamshika mkono NeemaΒ  kisha akaingia naye ndaniΒ 

    “Simtaki huyo Mtu, tafadhali muondoe” Mama Neema akatoaΒ  maagizo kwa Mlinzi. James akaingia kwenye gari kishaΒ  akaondoka, Baada ya kusikia kua James ameondoka…NeemaΒ  akamwambia Mama yake kama si yeye aliyekua akijilizaΒ 

    “Mama umemyoosha sana”Β 

    “Ndiyo dawa yake, mwache tu. Hawezi kufanya chochote kileΒ  sababu anajua una ujauzito wake, atakapo kuja kufungukaΒ  kiakili utakua umemaliza kila kitu, cha Msingi huyo MsichanaΒ  Mshikilie hadi mwisho.”Β 

    “Asante Mama kwa ushauri wako unanisaidia mno”Β 

    “Nisipokusaidia wewe nimsaidie Nani tena”Β 

    “Nahitaji kujisaidia” Matilda alipaza sauti yake, mara kiatuΒ  kikasikika kikija chumba alichokua amefungiwa, kikafunguliwa,Β  akaingia Mwanaume mmoja..

    Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya TISA Ya PIGO TAKATIFU Msisahau COMMENTS Ziwe Nyingi

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAΒ 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

    Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx

    Β 

    Pigo Takatifu Pigo Takatifu Kijiweni Riwaya ya Pigo Takatifu

    12 Comments

    1. Sir yowas on September 19, 2024 5:52 pm

      Jamani, mbona inahuzunisha

      Reply
    2. Hamic on September 19, 2024 6:49 pm

      Ni hataree

      Reply
      • Ibraah on September 19, 2024 11:27 pm

        β„³umetisha xaba

        Reply
    3. Xavi on September 19, 2024 6:53 pm

      Mtunzi upo vzr unajua kugusa hisia za watu

      Reply
    4. Temba on September 19, 2024 7:18 pm

      AloooohπŸ™ŒπŸ™Œ

      Reply
      • G shirima on September 19, 2024 10:32 pm

        Tamu ial fupi sana jamani

        Reply
    5. Exploration on September 19, 2024 7:50 pm

      😨😨😨😨

      Reply
    6. Revina on September 19, 2024 8:15 pm

      Upo vzur san

      Reply
    7. Daud on September 19, 2024 9:01 pm

      Daaah maskini akipata matako hulia mbwata mbwata mbwata πŸ˜—

      Reply
    8. Farnoush on September 19, 2024 11:31 pm

      Patra kufa cjapendaπŸ˜ͺ

      Reply
    9. Noel on September 20, 2024 10:27 pm

      Nimeipendq coz
      inatufundisha sanaaa

      Reply
    10. πŸ” πŸ”” Important: 0.6 BTC sent to your address. Receive funds >> https://graph.org/SECURE-YOUR-BITCOIN-07-23?hs=e6a96f34cbc3822ac6a80d04469eae5e& πŸ” on July 26, 2025 7:03 am

      q989sy

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi July 23, 2025

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-09

    Ilipoishia Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa) sehemu ya nane β€œNakufahamu Zahoro, wewe ndiye jibu la Laana hii.…

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-08

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-07

    Nzena (Kijiji Kilicholaaniwa)-06

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.