Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 05

    In the name of LOVE – 04

    In the name of LOVE – 03

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home ยป Pigo Takatifu Sehemu Ya Tatu (03)
    Hadithi

    Pigo Takatifu Sehemu Ya Tatu (03)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaSeptember 14, 2024Updated:September 18, 202410 Comments11 Mins Read4K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Pigo Takatifu
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “James!! tumepima DNA na majibu unayajua kua Patra ni Mtotoย  wako, kwanini damu yako unaiacha iteseke kisa ulemavu?”ย  alisema Matilda, alipigwa kofi hadi waliokua karibuย  walishtukaย 

    “Wewe Mshenzi sitaki urudie hiyo kauli, nakwambia nitakufanyaย  kitu kibaya endapo utaendelea kusema kua yule kiwete ni Mtotoย  wangu, Mtoto halali kwangu atazaliwa kwa Neema na siyoย  vinginevyo, kwanini unapenda kuniharibia siku Mjinga wewe?”ย  alifoka James, japo alikua kijana mtanashati lakini alikua naย  hasira sana.ย 

    Matilda alikasirika, sababu alipigwa mbele za Watu, Mamaย  Naomi alikua akiona pia japo alikua kwa mbali kidogo lakiniย  ilikua ni aibu kubwa, alikimbilia Hospitalini. James nayeย  aliondoka huku akiacha minong’ono kwa kilichotokea hapo,ย  aliondoa gari haraka sana.ย  Endeleaย 

    SEHEMU YA TATU

    Mama Naomi akamkimbilia Matilda kujua kwanini James alifikiaย  uamuzi wa kumpiga, hakuna alichokizungumza Matilda sababuย  bado alikua akilia kutokana na kilichotokea, Mwanaumeย  aliyesababisha akatoroka kwao, akawapa Mawazo wazazi wakeย  aliishia kumpiga na siyo kujali hali ya Mtoto kisa tu ulemavuย 

    “Matilda usilie hebu nieleze kimetokea nini hadi akakupiga?”ย  aliuliza Mama Naomiย 

    “Niache Mama Naomi, ilipofikia nimechoka na mateso ya hiiย  Dunia ni bora hata nife tu” Alisema kwa hasira Sana Matildaย  huku akilia kwa uchungu sana.

    “Huo ni uamuzi wa kijinga sana Matilda, ukifa Patra atazidiย  kuteseka, angalia jinsi anavyoteseka sasa hivi je ukifaย  itakuwaje?”ย 

    “Sasa nitakaa nikimwangalia Binti yangu akifa mbele ya machoย  yangu alafu Baba yake akiwa na uwezo wa kumsaidia lakiniย  hafanyi hivyo, ni bora kufa kuliko kumwangalia Patra akifa”ย  Alisema Matilda.ย 

    “Nakuomba Matilda kwasasa turudi nyumbani tutafakari jinsi yaย  kuipata pesa ya Matibabu, hebu nyanyuka” Mama Naomiย  alimnyanyua Matilda kisha aliondoka naye.ย 

    ********ย 

    “Mimi nina wao wazo Matilda, kwanini usiende kanisani kwenuย  ukaomba Msaada kwa waumini wakakusaidia?” alisema Mama Naomi,ย  yalipita Masaa matatu baada ya kurejea nyumbaniย 

    “Wataweza nisaidia kweli?”ย 

    “Ndiyo nina imani kubwa watakusaidia sababu wewe ni Muuminiย  mwenzao”ย 

    Ushauri wa Mama Naomi aliufanyia kazi, jioni ilipoingiaย  alienda kanisani, wengi walimshangaa maana baada yaย  kujifungua hakuonekana tena kanisani, aliofahamiana naoย  walikua wakimuuliza jinsia ya Mtoto, Maswali ya kuhusu Mtotoย  yalizidi kumfanya Matilda ajisikie vibaya sana.ย 

    “Mbona unalia?” aliuliza Mchungaji mara baada ya Matildaย  kufika ofisini kwa mchungaji wa kanisaย 

    “Mchungaji Mtoto wangu” Alisema Matilda, Mchungaji alishtukaย  akamuulizaย 

    “Mtoto wako amefanyaje?”ย 

    “Mchungaji Mtoto wangu Mimi” Sauti ya kilio ya Matildaย  ilisikikika na kumfanya Mchungaji aingiwe na maswali mengiย  kichwaniย 

    “Matilda Mtoto wako amefanya nini, hebu punguza kuliaย  uniambie” Alisema Mchungaji kwa sauti iliyojaa upole wa Haliย  ya juu sana, kwikwi ilimshika sana Matilda kila alipotakaย  kusema alijikuta akishindwa, kilio kilimuandama katika kilaย  neno alilohitaji kuzungumza, Mtandio wake aliutumia kufutaย  chozi lililomiminika kwa wingi, moyo wake ulijawa na simanziย  ya hali ya juu sana.ย 

    “Matilda tambua unanichanganya sana Mimi, sielewi hata niniย  unataka kuzungumza. Nakuomba acha kulia sababu ukilia Mimiย  siwezi kujua kilichokusibu” Alisema tena Mchungaji wakati huoย  Matilda akiwa ameegemea Meza akiwa analia, hata Mchungajiย  alilengwa na Mchozi kwa jinsi ambavyo Matilda alikua akiliaย  kwa uchungu, dakika tano zilikatika Matilda akishindwa kusemaย  chochoteย 

    “Unasikia Matilda, kua na imani hakuna kinachomshinda Munguย  aliye hai, nijuze Mimi ili tujue tunakusaidiaย ย 

    vipi….Unasikia….” Mchungaji alirudia kumbembelezaย  Matilda, angalau kilio kilianza kupunguaย 

    “Na hapo shavuni umekumbwa na nini?” Aliuliza Mchungaji,ย  shavuni Matilda alikua na alama ya kofi alilopigwa na Jamesย  kule Hospitalini.ย 

    “Mchungaji napitia wakati Mgumu sana katika Maisha yangu,ย  Mtoto wangu yupo Hospitalini..” Matilda alijikaza akazungumzaย 

    “Ulipotea kanisani kila Mtu akawa anajiuliza upo wapiย  Matilda, kumbe ulijifungua….Enhee nini kinamsumbua Mtotoย  wako?” Aliuliza Mchungaji ambaye alionekana kua na umriย  mkubwa, ngozi nyeusi na mvi iliyokolea vizuri kichwani, akiwaย  amevalia mavazi ya kanisa na msalaba mkononi.ย 

    “Mtoto wangu ni Mlemavu, anasumbuliwa na Mapafu, anahitajikaย  kufanyiwa upasuaji na kibaya zaidi Baba yake Amemkana”ย  Alisema Matilda, kilio kilianza upya baada ya kumalizaย  kumuelewesha Mchungaji ambaye alishikwa na butwaa, Matildaย  alikua Muumini wa kabisa hilo sababu hata kwao alikotokaย  alikua Binti wa kanisa hivyo alivyofika Dar alijiunga naย  kanisa pia.ย 

    “Yesu kristo! pole Binti yangu Matilda, hakuna linalomshindaย  Mungu wetu aliye hai, yeye halali kwa ajili yetu, Mtoto yupoย  Hospitali gani?”ย 

    “JM Hospital, inahitajika Milioni nane aweze kufanyiwaย  upasuaji, hapa nilipo sina hata senti tano na kadiri sikuย  zinavyozidi kwenda tumaini la Binti yangu kua hai linazidiย  kupotea” Alisema Matilda akizidi kulia kaa uchungu sana.ย 

    “Twende kwanza Hospitali kwa ajili ya maombi, baada ya hapoย  kanisa litaangalia utaratibu wa kukusaidia” Alisema Mchungajiย  akiwa ameshasimama,

    “Asante Mchungaji George” Alisema Matilda, waliondoka hapoย  kanisani kuelekea Magomeni Mapipa ilipo Hospitali ya JM,ย  waliondoka kwa gari maalum ya kanisa, Wakiwa barabaraniย  Mchungaji alimwambia Matildaย 

    “Hili jambo litaisha kwa namna nzuri Matilda, kua na imaniย  thabiti usitetereke. Kupitia Mtihani huu shetani anawezaย  akajipenyeza na kukuingiza kubaya zaidi endapoย  hautojiimarisha kiimani” Matilda aliitikia kwa kichwa kishaย  alijishika tama.ย 

    ********ย 

    “Una uhakika?” lilikua ni swali aliloulizwa Neema, alikuaย  kituo cha polisi.ย 

    “Ndiyo sababu yeye ndiye anayeishi pale” alisema Neema kwaย  kujiamini kisha akatoa kitita kidogo cha pesa kwa siri sana,ย  Polisi akatabasamu sababu ilikua ni ishara kua alichokuaย  akikizungumza Neema kilihitaji kutengenezwa zaidi ili kiweย  kikubwa.ย 

    “Jina lako?” Aliuliza Polisi akiwa anaandika jalada la kesi “Neema Ngushi, Miaka 32”ย 

    “Mshtakiwa?”ย 

    “Matilda John, Miaka 28” Alisema Neemaย 

    “Vitu vilivyopotea vina thamani gani?”ย 

    “Milioni 16” Alisema tena Neemaย 

    Baada ya kumaliza kuandika maelezo marefu aliyoyatoa, alipewaย  RB ya kumkamata Matilda, alichofanya Neema ni kwendaย  kumfungulia kesi ya upotevu wa vitu kwenye nyumba anayoishiย  Matilda, hakutaka kuendelea kumwona Matilda katika Maishaย  yake, pembeni alikua amesimama Mwanaume mmoja ambaye kaziย  yake ilikua ni kutingisha kichwa tu.ย 

    Alipohakikisha amemfungulia kesi, walitoka na Mwanaume huyoย  wakaingia kwenye gari, wakaondoka kituo cha polisi.ย 

    “Unajua huyu Mwanamke anaweza kua kikwazo kikubwa sababuย  James alikiri kua Mtoto ni wake lakini anaona aibu kuleaย  Mtoto ambaye ni kiwete, sasa hofu yangu ni kwamba akili yaย  Matilda ikifunguka alalfu akaenda kudai haki, huwenda Jamesย  akajirudi kwake sababu atatakiwa kumtunza Mtoto kwa lazima naย  pengine akachukuliwa hatua za kisheria alafu Mimiย  nikahangaika” Alisema Neema akiwa anaendesha gariย 

    “Hapo usiwe na huruma hakikisha unamsotesha hadi akili imkaeย  sawa, James akijua itakuaje?”ย 

    “Hata akijua hawezi kufanya chochote sababu nimeshamwambiaย  kua nataka nitengeneze mchezo ili Matilda akubali kurudi kwaoย  Njombe” Alisema Neemaย 

    “Bingoo!!! Sasa tunaenda wapi?”ย 

    “Naenda kukuacha kwako Sadam alafu Mimi nirudi nyumbani,ย  kesho tunamkamata Matilda, naamini kitisho hiki kitamfanyaย  akubali kurudi kwao”ย 

    “Umetisha sana hakika wewe ni jembe la kujivunia Neema”ย  Alisema Mwanaume huyo kisha akaweka Mkono wake kwenye paja laย  Neema ambaye alikua na Ujauzito wa Miezi mitatu tu.ย 

    *****ย 

    Saa 12 Jioni, Gari ya kanisa ilikua ikiingia kwenye geti laย  Hospitali ya JM Magomeni Mapipa, Matilda alikua amelia sanaย  hadi macho yalimvimba, wakashuka na kuelekea Nje ya chumbaย  ambacho Patra alikua amelazwa, Macho ya Mchungaji na Macho yaย  Matilda yaligongana na macho ya Daktari ambaye alikua akitokaย  ndani ya Chumba hicho.ย 

    “Dokta samahani hali ya Mwanangu inaendeleaje?” aliulizaย  Matilda kwa presha.ย 

    “Matilda Mtoto anaendelea vizuri kwasasa, aliamka kishaย  akalala hadi sasa hivi”ย 

    “Tunaweza kumwona?”ย 

    “Ndiyo lakini hampaswi kumsumbua” Alisema Dokta akiwaย  anaondokaย 

    “Asante Dokta, Mchungaji twende” Alisema Matilda kishaย  alifungua mlango wa chumba hichoย 

    “Mwanangu!!” Alisema Matilda baada ya kumwona Binti yakeย  akiwa anapumulia Mashine, Roho ilimuuma sana.

    “Oooh Jesus” Alisema Mchungaji, Chozi likaanza kumbubujikaย  tena Matilda, alikua Mtu wa kulia kila dakika kwa namnaย  ambavyo hali ya Binti yake ilikua, Mchungaji akamwambiaย  Matildaย 

    “Kulia hakusaidii chochote, ngoja tufanye kwanza Maombi iliย  tumkabidhi Mtoto huyu na hali yake mbele za Mungu” Alisemaย  Mchungaji Georgeย 

    Alianza kufanya Maombezi kwa Mtoto Patra, aliomba kwa imaniย  kubwa sana, Matilda naye alizama kwenye Maombi akisaidiana naย  Mchungaji huyo, maombi yalifanyika kwa sauti ya chini sanaย  ili wasimsumbue Mtoto kama ambavyo Daktari alikua amewaambia.ย  Zilitumika dakika arobaini na tano hadi kumaliza kumwombeaย  Patra, Jasho lilikua likimvuja Mchungaji huyo ambaye kilaย  alivyomwangalia Patra alijiskia vibaya sana kwa jinsi hli yaย  Mtoto huyo ilivyokua.ย 

    “Mungu amepokea Maombi Matilda, anaenda kutenda kwa ajiliย  yako na Mtoto, atafungua minyororo ya mateso kwa Mtoto huyu,ย  amini kua amekwisha kombolewa” Ilikua ni kauli ya kutia moyoย  ya Mchungaji huyo ambaye alikua amemshika bega Matilda, maraย  aliingia Daktari akawaambia Muda umeisha.ย 

    “Baby leo nimefanya kitu ambacho kitakuondolea hasira sana”ย  Alisema Neema akiwa anakula embe bichi, alikua akimwambiaย  James wakiwa chumbani Usiku.ย 

    “Jambo gani hilo?”ย 

    “Ni kuhusu Matilda”ย 

    “Sitaki hata kumsikia huyo Mwanamke Neema, katika Maishaย  yangu sijawahi pata ona Mwanamke King’ang’anizi kama Matilda”ย  Alisema kwa hasira James, alionesha wazi hataki kusikiaย  kuhusu Matilda ambaye alitoka kumpiga Kule Hospitalini.ย 

    “Usikasirike sababu hili jambo litaenda kumfanya aondoke hapaย  Dar bila kupenda Bby”ย 

    “Nakusikiliza”ย 

    “Hii hapa ni RB ya kumkamata kwa kosa la wizi wa vitu kwenyeย  ile nyumba, naamini akilala polisi siku moja akili itamkaaย  sawa” Alisema Neema kisha alimpatia Karatasi kutoka polisi,ย  James akaisoma kwanza kabla ya kusema Chochote, kishaย  akamtazama Neema

    “Umemfungulia kesi?”ย 

    “Ndiyo!! lengo langu apate kitisho kitakachomfanya aiyone Darย  chungu, nimefanya hivyo sababu sitaki kumwona Baba Mtotoย  wangu mtarajiwa anakosa raha” Alisema Neema, Jamesย  alitabasamu sababu aliitwa Baba Mtoto, alihitaji sana Mtotoย 

    “Mbinu yako ni bora sana Neema, naamini kwenye hiliย  hachomoki, ataondoka hapa Dar atake asitake, tena kwa kuondoaย  kero nitampatia na pesa ya kuanzia Maisha huko aendapo”ย  Alisema James kwa furahaย 

    “Umeona jinsi gani nakupenda, nakuhitaji na pia nakuthamini,ย  furaha yako ndiyo furaha yangu Mpenzi” Alisema Neemaย  akiendelea kula embe kwa chumvi.ย 

    Neema alishajua udhaifu wa James, wala hakutumia nguvu nyingiย  kumfanya James afurahi, ni kumweleza tu kuhusu ujauzito,ย  alichotaka alipewa bila hata kulazimisha.ย 

    Siku iliyofuata, Neema alienda kituo cha polisi akaonana naย  yule polisi ambaye aliandika jarada la kesi ya Matilda,ย  akaomba askari kwa ajili ya kwenda kumkamata Matilda, akapewaย  askari polisi wawili akaenda nao moja kwa moja JM Hospital.ย 

    Muda huo Matilda alikua kanisani, zoezi la kukusanya pesa kwaย  ajili ya kuratibu matibabu ya Patra lilikua likiendeleaย  kanisani hapo chini ya uangalizi wa karibu wa Mchungajiย  George ambayo alimwambia Matilda kua atasimama naye bega kwaย  bega hadi Patra apone, Mama Naomi alikua miongoni mwa Watuย  waliofika kanisani hapo baada ya kupewa taarifa na Matildaย  kua litaendeshwa zoezi la Uchangiaji wa matibabu ya Patra.ย 

    Chozi halikuacha kutoka kwenye macho ya Matilda baada yaย  kuona uchangwaji wa pesa hiyo, muitikio ulikua mkubwa sanaย  kiasi cha kumtia moyo hata Mchungaji wa kanisa hilo ambaye niย  Mchungaji George. Nyimbo za kusifu zilikua zikiimbwa, kilaย  mwenye kua nacho alitoa kidogo alicho nacho kwa moyo woteย  bila kujaliย 

    Waumini waliungana kwa pamoja ili kurejesha furaha ya Matildaย  ambaye alikua haamini macho yake jinsi kapu lilivyokuaย  linajaa noti. Mikono ya Matilda ilikua kwenye mdomo wake hukuย  chozi likiendelea kuvuja, tabasamu pana lilionekana kwenyeย  sura ya Mama Naomi ambaye alitoa wazo la Matilda kurejeaย  kanisani. Mchungaji George alimtia moyo sana Matilda katikaย  kila hatua ambayo walikuwepo, baadaye Mchungaji alikabidhiwaย  kapu lenye fedha hizo.

    Watu maalum wa kuzihesabu walianza kazi hiyo huku Mchungajiย  George akitoa neno kanisani hapoย 

    “Hakika leo Bwana ameinuliwa, kwa moyo huu uliooneshwa hakikaย  roho mtakatifu yupo ndani yetu, kusimama na Mwenye matatizoย  kunaongeza Baraka, hamjui ni kiasi gani Mungu anaendaย  kuongeza kilichopungua kwenu. Mungu awabariki sana kwa jinaย  la yesu” Alisema Mchungaji huku kanisa likiitika haswa kwaย  kusemaย 

    “Aaameen” Matilda alizidi kulia kwa uchungu sana,ย  kilichomliza siyo tu kuumwa kwa Binti yake bali ni maishaย  anayopitia baada ya kuitwa Mama, jinsi watu bakiย  wanavyosimama na yeye wakati Mwanaume aliyemfanya akatorokaย  kwao hajigusi kwa lolote lile, alipiga magoti na kusemaย 

    “Asante Yesu” Mikono yake ikiwa juu, Mchungaji akaja naย  kumwinuaย 

    “Matilda, kanisa linakuhitaji useme neno” Mchungaji Georgeย  alimsogeza Matilda hadi Madhabauni, akampa kipaza sauti.ย  Aseme nini? ndicho ambacho Matilda alikua akiwaza, umatiย  ulikua mwingi hapo kanisani, macho yote yakawa kwa Matildaย  Msichana wa miaka 28ย 

    Alikua akitetemeka kwa kila alichofikiria kukisema, alikuaย  kama amepigwa shoti vile, alimtazama Mama Naomi ambaye alimpaย  ishara ya kumtia moyo kua aseme chochote hapo kanisaniย 

    Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya NNE Ya PIGO TAKATIFU Msisahau COMMENTS Ziwe Nyingi

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMย ย 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAย 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIย 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAย 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAย ย 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

    Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx

    Pigo Takatifu Pigo Takatifu Kijiweni Riwaya ya Pigo Takatifu

    10 Comments

    1. Nelca on September 14, 2024 8:06 pm

      Daaaah jmn
      Kama naangalia tamthia vileee๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ

      Reply
    2. Halinga1 on September 14, 2024 8:06 pm

      Wakati wa Mungu ukifika Kila lililoshindikana litafanyika kwani hakuna jambo gumu kwake

      Reply
    3. Asia ally on September 14, 2024 9:43 pm

      Mungu hakosei kwakweli

      Reply
    4. Farnoush on September 14, 2024 10:27 pm

      Mambo Yazidi kuwa motooo

      Reply
      • Ryan Bwesigye on September 15, 2024 3:47 pm

        God’s ears are not deaf that he cannot hear your ๐Ÿ˜ญ cry ..

        Reply
    5. G shirima on September 15, 2024 8:25 pm

      Kuna funzo apa

      Reply
    6. Amayner on September 15, 2024 8:45 pm

      Mamb ni moto

      Reply
    7. B on September 17, 2024 1:50 pm

      Am I crying too ๐Ÿ˜ญ

      Reply
    8. Abraham on September 18, 2024 10:23 am

      Daah pole san kam wap

      Reply
    9. ๐Ÿ“Ÿ Email; Operation 1,423307 bitcoin. Withdraw >>> https://yandex.com/poll/T1TnDbUc4R9aLX7Nzhj1Cy?hs=a73c2adc95104ac3006196a7934c8646& ๐Ÿ“Ÿ on May 25, 2025 6:20 am

      ge6l84

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi September 15, 2025

    In the name of LOVE – 05

    Ilipoishia sehemu ya tatu ya In the name of LOVE โ€œBasi hakuna shida Zaylisa, mnaweza…

    In the name of LOVE – 04

    In the name of LOVE – 03

    In the name of LOVE – 02

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.