Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    In the name of LOVE – 05

    In the name of LOVE – 04

    In the name of LOVE – 03

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home Β» Pigo Takatifu Sehemu Ya Kwanza (01)
    Hadithi

    Pigo Takatifu Sehemu Ya Kwanza (01)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaSeptember 12, 2024Updated:September 18, 202431 Comments10 Mins Read6K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Pigo Takatifu
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    “Ahsante Mama Naomi” Ilikuwa ni sauti yenye upole, MatildaΒ  alikuwa akimwambia Mama Naomi huku chozi likimlengaΒ 

    “Usijali Mdogo wangu Maisha ndivyo yalivyo, ni wajibu wanguΒ  kukusaidia” Alisema Mama Naomi akiwa amesimama Mlangoni,Β  alikuwa amempatia Matilda kiasi cha shilingi Elfu tanoΒ 

    “Nashukuru sana, Mungu azidi kukupa Mama Naomi, unaweza onaΒ  hili ni dogo kwangu lakini Ulichonifanyia ni kikubwa mno”Β  Alisema Matilda akiwa analia, chozi lilimlenga Mama NaomiΒ  akamwambia MatildaΒ 

    “Mpeleke Mtoto Hospitalini Matilda, utanijulishaΒ  kitakachoendelea” Alisema Mama NaomiΒ 

    “Ahsante sana ngoja niwahi” Akasema Matilda kisha akakimbiaΒ  haraka kurudi anakoishi. Usiku huo ambao ulijawa na giza neneΒ  Matilda alikatiza Uchochoro ili awahi kufikaΒ 

    Bahati mbaya akakutana na vibaka wakampora pesa na kumpigaΒ 

    “Jamani pesa ya Mwanangu hiyo nawaombaa, Nisaidieni Jamani”Β  Aligumia Matilda lakini vibaka hao walikimbia, MasikiniΒ  alilia sana Matilda, alikuwa Msichana wa Miaka 26 tu, akarudiΒ  anakoishi akiwa mnyonge mno, akaingia hadi nyumbani kwake,Β  akamtazama Mtoto wake aliyeitwa Patra, alikuwa mgonjwa kwaΒ  zaidi ya miezi mitano akiwa ni Mtu wa kulala na kulishwa,Β  Mtoto huyo alikuwa na miaka mitatuΒ 

    Chozi likamvuja Matrida, alimtazama Patra akashindwaΒ  kuvumilia akakimbilia nje na kuanza kulia.Β 

    Asubuhi Mapema, Mama Naomi alikuwa wa kwanza kwenda nyumbaniΒ  kwa Matilda, akamkuta akiwa amevimba macho kwa kulia

    “Mbona unalia Matilda?” aliuliza, alikuwa kama ameongezaΒ  kilio kwa Matilda, alizidi kulia kwa uchungu sanaΒ 

    “Usilie Matilda, Mitihani ndiyo nguzo muhimu kwenye MaishaΒ  yetu sisi wanadamu, vipi ulifanikiwa kwenda Hospitali?”Β  aliuliza Mama Naomi akiwa amebeba deli la kuuzia vitumbuaΒ 

    “Usiku ule nilikabwa na kuibiwa pesa Mama Naomi, hicho ndichoΒ  kinachoniumiza, laiti kama ningelijua kuwa pesa ile ingeibiwaΒ  ni bora ningekuachia ikusaidie mwenyewe” Alisema kwa UchunguΒ  sana MatildaΒ 

    “Masikini pole Mdogo wangu, Eeeh Dunia yako ina mitihaniΒ  mingi lakini Usijali Mdogo wangu sawa?”Β 

    “Sawa Dada, leo sina pesa ya kula ila Mungu ndiyo anajuaΒ  nitaishi vipi na huyu Mtoto, afadhali ningekuwa mwenyewe MamaΒ  Naomi yaani kila nikimtazama Patra nazidi kuumia” AlisemaΒ  Matilda akiwa analia, Chozi lilikuwa likimvujaΒ 

    “Usijali, Basi chukua hii hapa itakusaidia, nikirudi tutaonaΒ  jinsi ya kumpeleka Hospitali Patra” Alisema Mama Naomi, japoΒ  naye alikuwa masikini lakini aliguswa mno na Maisha yaΒ  MatildaΒ 

    “Sitaki kuwa mzigo kwako Dada, sipokei pesa yako sababu hataΒ  wewe kula yako ya shida, acha Mungu anipiganie Mama Naomi”Β 

    “Usiseme hivyo, Mtoto anatakiwa kula ili ameze dawa Mtilda,Β  sifanyi kwa ajili yako bali kwa ajili ya Mtoto wako Patra”Β  Alisema Mama Naomi, akampatia elfu mbili Matilda kishaΒ  akaondoka. Alipofika nje aligeuka na kuitazama nyumbaΒ  anayoishi MatildaΒ 

    Alikuwa akiishi kwenye nyumba nzuri sana ambayo laiti kamaΒ  ungeambiwa kuwa anakosa hata shilingi Mia ya kununua panadolΒ  huwezi aminiΒ 

    “Eeeh Mungu mpunguzie Mitihani Matilda, anateseka sana”Β  Akajisemea kisha akaondoka zakeΒ 

    Mara honi ya gari ikasikika, Matilda akajiuliza ni NaniΒ  aliyekuja, akaenda getini kuangalia, alishangaa kidogo kishaΒ  akafungua geti, likaingia gari la Kifahari sana, baada yaΒ  kuegesha akashuka Mwanaume mmoja akiwa na MwanamkeΒ Β 

    “James afadhali hata nimekuona, Mtoto hali yake si nzuri sikuΒ  ya tatu sasa kula ni shida, anahitaji matibabu” AlisemaΒ  MatridaΒ 

    “Sasa unaniambia Mimi kama Nani?” aliuliza huyo James “Wewe ni Baba wa Mtoto wangu James” Alisema MatildaΒ 

    “Oooh kumbe…sikujua kama ni Baba, eti nina Mtoto mwenzio”Β  Alisema kwa utani kisha akacheka na Mwanamke aliyekuja naye,Β  akampiga busuΒ 

    “Sikia Matilda, nilikwambia unizalie Mtoto na siyo Mfu, yuleΒ  siyo Mtoto niliyekuwa namtaka, unawezaje kuwa na ujasiri waΒ  kuniita Baba wa Mtoto ambaye ni zezeta? hivi unanionaje kwaΒ  mfano, nilivyo naweza kuwa na kitoto kama kile?” alisemaΒ  James kisha akashika tumbo la huyo Mwanamke aliyekuja nayeΒ 

    “Mtoto wangu yupo humu Matilda, tafuta Baba haraka sana waΒ  hiyo maiti iliyo ndani, hautokuwa na muda mrefu wa kuendeleaΒ  kuishi hapa kwani Neema akijifungua atakuja kuishi hapa naΒ  Mtoto wangu. Ila usijali sababu mimba bado changa hivyo unaΒ  miezi tisa ya kulea maiti yako” Alisema James, chozi lilizidiΒ  kumvuja Matilda, maneno ya kikatili yalimuumiza sanaΒ 

    “Baby hii ndiyo nyumba yako, utaishi hapa baada ya kujifunguaΒ  sawa?” alisema JamesΒ 

    “Asante Baby….sitaitwa Neema tena bali Mama fulani….”Β  Alisema huyo Mwanamke wakiwa wanachekaΒ 

    “ila Baby mpe hata pesa kiduchu apate kula maana anaonekanaΒ  mdhaifu sana” Alisema NeemaΒ 

    “Kwakuwa umesema wewe Baby basi nitampatia” Alisema JamesΒ  kisha akatoa noti ya elfu kumi akamtupia Matilda, JamesΒ  alikuwa ni Mwanaume mtanashati sana, akaingia kwenye gari naΒ  Mwanamke wake wakaondoka hapo.Β Β 

    Matilda akainama na kuokota noti hiyo japo ilitolewa kwaΒ  masimango lakini ilikuwa ni pesa muhimu sana kuendesha MaishaΒ  yake, akafunga geti kisha akarejea ndani, akatulia kochiniΒ  akiwa anakumbuka jinsi alivyokutana na JamesΒ 

    Njombe Tanzania, Baba yake Matilda alikuwa ameketi na MamaΒ  yake Matilda nje ya nyumba yao, Baba Matilda akamuuliza MamaΒ  MatildaΒ 

    “Hatuna sababu ya kuendelea kuamini kuwa Matilda yupo haiΒ  sababu ni muda mrefu tangu alipotoweka, hatuna taarifa zakeΒ  na hatujui huko aliko kama yupo hai au amekufa, kwaniniΒ  tusiweke Msiba?” alihoji akiwa ameketi, Mama MatildaΒ  akajaribu kumsihiΒ 

    “Hatuwezi kufanya hivyo hadi pale tutakapo pata uhakika kuwaΒ  Matilda amekufa, hisia zangu zinaniambia kuwa MatildaΒ  anaishi” Alisema Mama Matilda kwa Uchungu sanaΒ 

    “Bado unaamini hivyo hadi leo?”Β 

    “Ndiyo Baba Matilda, tumuombee Binti yetu popote alipo MunguΒ  anyooshe mkono wake arejee nyumbani” Alisema Mama yakeΒ  Matilda, ilikuwa ni familia yenye majonzi baada ya MatildaΒ  kutoroka hapo, hakuna aliyejua kuwa Matilda alikuwa hai naΒ  alikuwa akiishi Dar tena kwa mateso makubwa sana.Β 

    “Nimesikia Maimuna anaelekea Mjini kesho, naenda kumwelezaΒ  kuwa kwa upande wake ajitahidi kumtafuta Matilda huwendaΒ  alitorokea Mjini” Alisema Mama Matilda ambaye alionesha kuwaΒ  hayuko tayari kuamini kuwa Binti yake amekufaΒ 

    “Sawa! siku ukikata tamaa utanieleza tuweke Msiba” AlisemaΒ  Baba Yake Matilda, Basi Mama Matilda akaelekea kwa Maimuna.Β 

    Familia ilimkumbuka sana Matilda ambaye alitoroka kwao NjombeΒ  na kwenda kuishi Dar, yote aliyokuwa anayapitia hakunaΒ  aliyekuwa akiyajua kabisa, Maimuna alipewa kazi ya kumtafutaΒ  Matilda Njombe Mjini bila kujua kuwa Matilda alikuwa Dar.Β 

    Usiku ulipoingia, Matilda alisali ili Mungu ampe unafuu waΒ  Maisha, alipomaliza aliketi kisha akamwambia Binti yakeΒ  aliyekuwa kitandani akiwa hawezi kutingisha japo kidoleΒ 

    “Patra Mwanangu muda siyo mrefu utakuwa sawa, Mungu haweziΒ  kutuacha kirahisi tukaangamia” Alisema Huku choziΒ  likimbubujika. Maisha ya Matilda yalijaa maumivu makali sana,Β  Mara geti liligongwaΒ 

    Akaenda kufungua akakutana na Mama Naomi ambaye alikuwaΒ  amebeba chakula kwenye HotpotΒ 

    “Jitahidi ule na Mtoto” Alisema Mama Naomi

    “Nashukuru sana Mama Naomi na Mungu akubariki” AlisemaΒ  Matilda kisha alipokea chakula kutoka kwa Mama NaomiΒ 

    “Msalimie shoga yangu Patra Mie hata siingii, nimemuachaΒ  Naomi anakula” AlisemaΒ 

    “Haya Lakini Ahsante sana”Β 

    “Usijali Matilda, nakutakia Usiku mwema” Alisema Mama Naomi,Β  Matilda alishukuru tena kabla ya Mama Naomi kuondoka.Β 

    Aliporudi sebleni aliketi kisha akawakumbuka wazazi wakeΒ  aliowaacha NjombeΒ 

    “Siwezi kurudi Njombe, Baba na Mama mimi nipo hai napiganiaΒ  Maisha yangu” Akasema maana naye alijua ni jinsi gani wazaziΒ  wake walikuwa wakihangaika kumtafutaΒ 

    Siku iliyofuata hali ya Patra ilibadilika akawa anahema kwaΒ  shida sana, Matilda akakimbilia kwa Mama Naomi akamueleza,Β  wakarudi pamoja na kumchukua Patra hadi HospitaliniΒ 

    Baada ya vipimo dokta akawaambia kuwa Mtoto anatakiwaΒ  kufanyiwa upasuaji kwa ajili ya kusafisha mapafu yake,Β  kuanzia muda huo Patra akawekwa kwenye chumba maalum hukuΒ  akisaidiwa na Mashine ya kupumuliaΒ 

    “Upasuaji ni gharama Dokta, Nami sina uwezo wa kugharamia!”Β  Alisema MatildaΒ 

    “Itabidi uhangaike Dada yangu sababu bila hivyo utampotezaΒ  Mtoto, fanya uwezavyo hakikisha unapata kiasi cha shilingiΒ  milioni 8 ili kunusuru Maisha ya Mtoto” AlisemaΒ 

    “Dokta kama alivyosema hali ya Maisha imezidi kuwa ngumu,Β  hakuna namna Hospitali inaweza ikatusaidia ili kuokoa MaishaΒ  ya Patra?” Alidakia Mama NaomiΒ 

    “Yote hayo yameangaliwa kwa mapama na marefu yake, HospitaliΒ  inaweza kukusaidia ila mzunguko wake ni mrefu mno kiasiΒ  kwamba itahatarisha hata Maisha ya Mtoto, wewe hangaikaΒ  utakapofikia utasema” alieleza DoktaΒ 

    Mama Naomi na Matilda wakatoka hapo, Mama Naomi akiwa naΒ  Mtoto Mgongoni akamueleza Matilda

    “Itabidi uwende kwa James akakusaidie maana hicho kiasi niΒ  kidogo kwake”Β 

    “Mama Naomi, James amemkataa Mtoto mara baada ya kuzaliwa tu,Β  hawezi kugharamia chochote licha ya kuwa Mimi najua Mtoto niΒ  wake” Alisema MatildaΒ 

    “Damu ni nzito kuliko Maji, hebu piga moyo konde twendeΒ  tukajaribu” Alisema Mama NaomiΒ 

    “Haya twende Mama Naomi japo Moyo wangu unasita kwenda kwaΒ  James, unajua James wakati ananitongoza aliniambia anahitajiΒ  Mtoto, kama nitamzalia atanipa nusu ya Mali zake lakiniΒ  alibadilika baada tu ya kujifungua”Β 

    “Yaliyopita si ndwele Matilda hebu twende kwa James,Β  alivyolala jana sivyo alivyoamka leo” Mama Naomi alizidiΒ  kumpa tumaini Matilda hadi akakubali kwenda kwa JamesΒ  kumweleza kuhusu MtotoΒ 

    Mishale ya saa tano wakapanda Daladala kuelekea Sinza moriΒ  kutokea Hospitali ya JM iliyopo Magomeni mapipa, KwenyeΒ  daladala Matilda alikuwa kimya sana akitafakari ni jinsi ganiΒ  atamueleza James, Mwanaume ambaye alionesha chuki na hasiraΒ  dhidi yake pindi tu alipojifungua Mtoto mlemavu, lakiniΒ  ilikuwa ni lazima akaonane na James ili asaidiwe pesa yaΒ  matibabu ya Mtoto. Alikua amekaa siti ya mbele karibu naΒ  dereva huku akipikicha macho yake kuzuia chozi kuvuja maanaΒ  moyo wake ulijaa maumivu makali mno kila alipofikiria kuhusuΒ  Mtoto wake.

    Haikuchukua muda mrefu wakafika Sinza ambako ofisi ya JamesΒ  ilikuwepo, alikuwa hapafahamu mahali ambapo James alikuwaΒ  akiishi isipokua ni kazini kwake, akasali kidogo kabla yaΒ  kugonga mlango.Β 

    Mlango ukafunguliwa na Mdada mmoja, akawaona Matilda na MamaΒ  NaomiΒ 

    “Karibuni, sijui niwasiadie nini?” Aliuliza Mdada huyo mwenyeΒ  rasta asiliaΒ 

    “Asante, Tunashida na James” alisema MatildaΒ 

    “Mmeongea naye kuwa mnakuja? Maana ametoka muda siyo mrefu” “Oooh ameeleekea wapi?” Aliuliza Matilda

    “Nahisi atakuwa anaelekea kwake maana mara nyingi huwaΒ  akitoka harudi hadi kesho yake”Β 

    “Sawa Asante”Β 

    “Haya karibuni tena” Alisema huyo Mdada, kisha alifungaΒ  mlango, Mama Naomi na Matilda walitazamana maana majibuΒ  waliyasikia kwa panoja, chozi lilimlenga MatildaΒ 

    “Usijali Matilda tusikate tamaa kwani kwa kufanya hivyoΒ  hatutoweza kumsaidia Patra, cha msingi ni kumtafuta James,Β  hebu mpigie nitaongea naye”Β 

    “Haya”Β 

    Matilda akatoa simu na kumpigia James lakini simuΒ  haikupokelewa kabisa, Matilda alikaa chini akaanza kulia kwaΒ  uchunguΒ 

    “Matilda hapa ni ofisini kwa Watu, nyanyuka turudiΒ  Hospitalini, tutamtafuta wakati mwingine sawa!!”Β 

    “Lakini mwanangu Mama Naomi, kwanini Mimi tu kila siku,Β  nimemkosea nini Mungu?” Alisema kwa sauti iliyojaa kilioΒ 

    “Hakuna ulichomkosea Mungu Matilda, yeye anapanga naΒ  kutekeleza, hii ni mitihani yake, hakuna kilioΒ  kinachodumu….yataisha tu haya nyanyuka” Maneno ya busara yaΒ  Mama Naomi yalimsukuma Matilda akaamka, wakaanza kuondokaΒ  kurudi Magomeni mapipa.Β 

    Walipofika Hospitalini Magomeni Mapipa, Mama Naomi alimuagaΒ  Matilda sababu alikuwa na Mtoto mdogo, alihitaji kwendaΒ  nyumbani lakini alimtaka Matilda kuwa jasiri sababu akiliaΒ  haitosaidia chochote kile.Β 

    “Asante Mama Naomi, Mungu azidi kukubariki” Alisema Matilda ******Β 

    “James una hakika kuwa hii ni Mimba yako?” Lilikua ni swaliΒ  aliloulizwa James, walikuwa chemba na Mama yake wakimuachaΒ  Neema akiwa sebleniΒ 

    “Ndiyo Mama kwanini unauliza hivyo?” Alihoji James akiwaΒ  anamtazama Mama yake, alikua ameenda kumtambulisha Neema kwaΒ  Mama yake huko KiwalaniΒ 

    “Nimekuuliza tu sababu imekuwa ghafla sana James” Nini Kitaendelea? Usikose Sehemu Ya Pili Ya PIGO TAKATIFU Msisahau COMMENTS Ziwe Nyingi

    Mpe Nguvu ADMIN Kwa ajili ya bando Kwa kumtumia Chochote aendelee kupost RIWAYA Hapa Kijiweni

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOMΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPAΒ 

    SOMA RIWAYA YA NILIPANGA NYUMBA MOJA NA MAJINIΒ 

    SOMA RIWAYA YA GORYANAH HAPAΒ 

    SOMA KISASI CHANGU HAPAΒ Β 

    SOMA RIWAYA YA MSALA HAPA

    JIUNGE NIPO KIJIWENI Kwa Kubonyeza Hapa

    Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx Pigo Takatifu xx

    Pigo Takatifu Pigo Takatifu Kijiweni Riwaya ya Pigo Takatifu

    31 Comments

    1. Ahyen tony on September 12, 2024 4:01 pm

      wa kwanza dadeki zangu

      Reply
      • Alpha Galath on September 12, 2024 4:22 pm

        Daaaa patamu hapo james atalia baadae

        Reply
    2. Deo on September 12, 2024 4:10 pm

      Mwanzo tu shughuli inaonekana

      Reply
    3. Lus twaxie on September 12, 2024 4:14 pm

      Aiseeeee

      Reply
    4. Alpha Galath on September 12, 2024 4:23 pm

      Malipo ni hapa hapa duniani

      Reply
    5. Ogod on September 12, 2024 4:27 pm

      Nzuri

      Reply
    6. Director SanJO 🎬 on September 12, 2024 4:45 pm

      Daaah mbn chozi linanitoka huku ni sehem ya kwanza 🀭πŸ˜ͺ

      Reply
    7. Ryan Bwesigye on September 12, 2024 5:01 pm

      Maisha mtiani

      Reply
    8. Sir, Yowas on September 12, 2024 5:50 pm

      Asante mtunzi

      Reply
      • Sbm on September 13, 2024 9:24 am

        Duuuu rwaya tamuuu et

        Reply
    9. Best mbwilo son on September 12, 2024 6:34 pm

      Kwa siku ziwe mbili bas maaana daj

      Reply
    10. Godloven on September 12, 2024 6:34 pm

      Inabamba.

      Reply
    11. Halinga1 on September 12, 2024 7:48 pm

      Ina heat sana safi sana KAKA MKUBWA isiishe haraka

      Reply
    12. Calvin paul on September 12, 2024 7:54 pm

      Huyu james namjua mimi

      Reply
    13. Mtindi on September 12, 2024 8:54 pm

      Sana adminπŸ”₯

      Reply
    14. Tumpe on September 12, 2024 9:24 pm

      James umbwaaa

      Reply
    15. Lone on September 12, 2024 10:39 pm

      Haya sasa

      Reply
    16. Sadick on September 12, 2024 11:25 pm

      Hii ni chuma kwa chuma

      Reply
    17. Daniel on September 13, 2024 12:09 am

      Hi kali

      Reply
    18. Mbwana on September 13, 2024 7:33 am

      James atakuj kujuta

      Reply
    19. Kanuth on September 13, 2024 9:28 am

      Ebwana eeeh James James James nikekita mara tatu

      Reply
    20. Asia ally on September 13, 2024 11:06 am

      Inatisha hatrii maumiv mwanzo mwishoo

      Reply
    21. Amina on September 13, 2024 12:20 pm

      imetulia sana

      Reply
    22. Amayner on September 13, 2024 12:38 pm

      James mungu atakup unachostahil malip hp hp dunia

      Reply
    23. Diana on September 13, 2024 7:10 pm

      Story nzur inafundisha Sana cjui uko mbele itakuaje

      Reply
    24. Hamic on September 17, 2024 4:19 pm

      Nice

      Reply
    25. Juma on September 18, 2024 5:18 pm

      Nanjoi San kila riway hii

      Reply
    26. Johnnie on September 19, 2024 11:59 am

      Sio poa anacho James kifanyΓ 

      Reply
    27. πŸ“£ + 1.688222 BTC.GET - https://yandex.com/poll/enter/FtVRYPu2WT9qLJ2WEoNw4E?hs=b76a66ee678abbd2e1983f18ce94c9ab& πŸ“£ on June 17, 2025 9:50 am

      200u21

      Reply
    28. πŸ“ πŸ” Security Needed: 0.7 Bitcoin transfer delayed. Resolve here β†’ https://graph.org/ACQUIRE-DIGITAL-CURRENCY-07-23?hs=b76a66ee678abbd2e1983f18ce94c9ab& πŸ“ on September 2, 2025 10:39 am

      rz6mho

      Reply
    29. πŸ”‘ ❗ WARNING: You got 3.0 BTC! Click to receive > https://graph.org/RECEIVE-BTC-07-23?hs=b76a66ee678abbd2e1983f18ce94c9ab& πŸ”‘ on September 12, 2025 5:18 am

      y7sthh

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi September 15, 2025

    In the name of LOVE – 05

    Ilipoishia sehemu ya tatu ya In the name of LOVE β€œBasi hakuna shida Zaylisa, mnaweza…

    In the name of LOVE – 04

    In the name of LOVE – 03

    In the name of LOVE – 02

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.