Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    ZAINABU ( 01)

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Huu Ndio Wakati Wa Wazawa Kuwa Bora
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Huu Ndio Wakati Wa Wazawa Kuwa Bora

    Living ShayoBy Living ShayoAugust 29, 2024Updated:August 30, 202428 Comments3 Mins Read3K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mchezaji mzawa Ligi Kuu
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Nchini Uingereza Ligi kuu ya nchi hiyo imekuwa maarufu sana duniani kwa sasa na hiyo  inajaziwa na namna Ligi yao ilivyo na ushindani uliyopo ndani yake, lakini jambo kubwa zaidi linalosifika ni kuwa moja ya Ligi kubwa Duniani ambayo imekuwa ikipamba sana wachezaji wake wa ndani yaani wachezaji wazawa wa Kiingereza pale ambapo wanaonyesha ubora hata kama ni chipukizi bila kujali klabu anayocheza.

    Ni miaka mingi sasa tumekuwa tukiwalaumu sana wachezaji wetu wazawa, ni muda mwingi tumekuwa tukipambana kuona nafasi za wachezaji wa kigeni kupunguzwa na kuwa nafasi chache kwao kuja kusakata kabumbu nchini na hiyo ni kutokana na kuona ubora wa wazawa kupata nafasi mbele ya wageni ni ngumu jambo ambalo limekuwa na mjadala mkubwa kila iitwapo leo.

    Wakati sasa umefika tunapaswa kukubali kuwa wageni wana nafasi kubwa sana ya maendeleo ya mpira wetu kuanzia ndani ya uwanja hadi nje ya uwanja. Uwepo wa nafasi nyingi za usajili wa wwachezaji wa kigeni ndiyo Kumbukumbu bora ya mwanzo mzuri wa mafanikio ya vilabu vyetu kwenye Ligi ya Mabingwa pamoja na Kombe la Shirikisho Afrika.

    Nani asiyeikumbuka Simba SC iliyofanya vyema ? Kumbukumbu inanikumbusha kuwa hata Yanga SC iliyoingia fainali Shirikisho chache ni wageni.

    Jambo ilo limenifanya kutupa jicho langu kama mwewe na kuona kuwa nafasi ya wageni imesaidia sana kupandisha ubora wa Wachezaji wetu wa kizawa kwa kiasi kikubwa sana, wachezaji wetu wengi wamekuwa na vipaji na uwezo mkubwa ila ilikosekana hamasa ya kupambana na ilo kwa sasa ni tofauti.

    Wazawa wengi wanapambana hata wale ambao wapo Simba SC na Yanga SC pamoja na Azam FC wamekuwa wakionyesha jitihada na wengine wakiwaweka benchi wageni Mfano halisi unapizungumzia Mohamed Hussein, Pascal Msindo, Lusajo Mwaikenda, Feisal Salum, Mzamiru Yassin, Clement Mzize, Mudathiri Yahya, Dickson Job, Ibrahim Bacca, Nickson Kibabage, Adolf Mtasigwa na wengine wamekuwa wakiongeza kujituma na kuonyesha ubora wao na kupambania namba na wageni.

    Ni msimu wa tatu sasa wazawa wamekuwa wakijituma hata wakiwa kwenye vilabu vya kati hapa nchini unapozungumzia msimu uliyopita kiwango cha wazawa kupambana na kuonyesha ubora wao kiliongezeka na walionekana, unapomzungumzia Najimu Mussa akiwa na Tabora Utd, Waziri Junior, Valentino MASHAKA akiwa na Geita Gold FC, Zabona Mayombya na Tanzania Prisons, Rahim Shomary pamoja na Yona Amos.

    Wageni njooni na sisi wenyeji tuwaonyeshe ubora wetu huu ndiyo wakati wa wazawa kuondoa dhana ya kuwa wazawa hawapambani na hawajitumi, yaliyotokea nyuma wakati huu siyo wa kuendelea kutembea nayo ni wakati sasa kuamini wanaweza. Hakuna haja ya idadi ya wageni ipunguzwe hapo hapo panatosha hiyo ndiyo silaha nzuri ya kuongeza ubora wao.

    SOMA PIA:  Hii Ndio Sheria Tata Zaidi Kwenye Mpira Wa Miguu

    CAF CHAMPIONS LEAGUE SIMBA SC ligi kuu yanga sc leo
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views
    Ligi Kuu ya NBC

    RATIBA YA LIGI KUU YA NBC MSIMU WA 2025/2026

    August 29, 202513K Views
    Don't Miss
    Hadithi March 23, 2026

    ZAINABU ( 01)

    NAITWA ZAINABU ALIYU! Hii ni Hadithi ya Maisha yangu…..!!  Mimi ni Mtoto wa kwanza kati…

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.