Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Kwa Maboresho Haya Wadhamini Wa Ligi Kuu Mmetisha
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Kwa Maboresho Haya Wadhamini Wa Ligi Kuu Mmetisha

    Living ShayoBy Living ShayoAugust 22, 2024Updated:August 22, 20244 Comments3 Mins Read766 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Wachezaji wa Ligi Kuu
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Moja ya njia bora ya kutaka mafanikio ni kukubali kukuwa, kukubali kubadilika na kuongeza juhudi na wakati mwingine kukubali kuiga mazuri yaliyofanywa na wengine waliyojuu yako kimafanikio na maendeleo pia.

    Aliwahi kusema Raisi wa zamani wa Marekani John Kennedy kuwa “Things do not happen, things are made to happen” alimaanisha kuwa “Vitu havitokei, vitu vinafanywa vitokee.”

    Hapo sasa ndipo mahali ambapo tupo kwa sasa, vitu ambavyo vilikuwa havifanyiki au hatufanyi kwa sasa vinafanyika, na moja ya sifa ya kutaka kufanya kitu ni kuanza kukifanya kitakupa nafasi ya kujua ni wapi bora nipaendeleze na wapi hapajakaa sawa ni pa boreshe zaidi.

    Imetuchukua miaka mingi sana na zaidi ni tokea pale ambapo soka lilianza kubadilika na kuwa inatoa nafasi na pongezi kwa waliyofanya vizuri ndani ya uwanja na nje ya uwanja pia, tumeona viongozi kadhaa wakitunukiwa Tuzo kutokana na uongozi wake alikadhalika tunaona kila kukicha wachezaji nao wakitunukiwa tuzo.

    Hapa nyumbani Tanzania soka imekuwa mchezo pendwa sana na kiasi kikubwa ni kutokana na mapenzi makubwa ya mashabiki wengi kwa vilabu viwili vikubwa nchini Simba SC na Yanga SC, kuna nyakati Simba SC walikuwa na Tuzo zao za msimu wanazitoa kwa wachezaji wao waliyofanya vizuri kwa msimu husika kwenye kila nafasi kiwanjani jamboa ambalo kwa kiasi kikubwa iliongeza hamasa, upendo na kujituma kwa wachezaji.

    Ni takribani misimu mitano sasa Ligi yetu imepiga hatua kubwa sana hamasa viwanjani imeongezeka, ubora wa wachezaji wazuri na wenye uwezo unaongezeka kila kukicha, udhamini kwa vilabu na matatizo mbalimbali yaliyokuwa yanavikumba vilabu yamepungua kama siyo kuisha kabisa.

    Jambo kubwa na la pongezi kwa msimu huu mpya wa 2024/2025 ni maboresho ya haraka au ongezeko la haraka lililotokea kwenye michezo kadhaa ya Ligi iliyochezwa mpaka sasa na jambo ilo siyo lingine bali ni uwepo wa Tuzo ya Mchezaji bora wa mchezo au mechi ya Ligi kuu, kitu ambacho tulikuwa tunakiona tu kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi Zanzibar kwa hapa nyumbani na nje ya mipaka ni kwenye Ligi kuu ya nchini Misri na ligi nyingine kubwa duniani.

    Pongezi kubwa sana kwenye eneo ilo iwafikie Bodi ya Ligi kuu Tanzania pamoja na mdhamini mkuu wa tuzo hiyo Benki ya NBC, ni jambo kubwa sana kama taifa kwani siyo jambo dogo ukilitazama kwa ukubwa wake kwani itaongeza ushindani kiwanjani.

    Lakini jambo kubwa la kuomba ni muendelezo wa jambo ilo liwe endelevu na la daima kwenye Ligi msimu huu na kuendelea, na hapo ndipo ninapokumbuka msemo wa aliyekuwa raisi wa Afrika Kusini Hayati Nelson Mandela alipowahi kusema kuwa “It’s always seems impossible, until it’s done.”

    SOMA PIA:  MVP Wa Ligi Mbalimbali Kuja Kucheza NBCPL Ina Maana Gani?

     

    4 Comments

    1. Makshilina Juma on August 22, 2024 11:04 am

      Hii IMEENDA

      Reply
    2. Calvin~360 on August 22, 2024 12:03 pm

      ubaya ubwela 👍

      Reply
    3. Thabit on August 22, 2024 12:28 pm

      Ligi yetu imekua nakutambulika kwa kasi Africa yote na dunian kwa sasa na ninafikili kadli ya siku zinavyo enda itakua bora zaid ya hapa..

      Reply
    4. Pingback: Yanga Wana Matatizo, Hawajitambui. Je Ni Lini Watajielewa?

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.