Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Heritier Makambo Kitabu Cha Simulizi Walichokataa Wazawa
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Heritier Makambo Kitabu Cha Simulizi Walichokataa Wazawa

    Cosmasy ChogaBy Cosmasy ChogaAugust 13, 2024Updated:August 13, 20247 Comments3 Mins Read906 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Makambo
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kifo kipo katika miguu tunatembea nacho,Siyo kwamba tunatembea nacho tu katika miguu tu pengine tunasafiri nacho katika vyombo vya majini,angani na barabarani.

    Hadithi inapokuwa tamu kwenye gazeti , kitabu au runinga hukatizwa na chini yake utakutana na maneno “Itaendelea toleo lijalo”.Lazima utakuwa na hamu ya kuendelea kutaka kuisoma ama kuitazama.

    Mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Young Africans (Yanga Sc) kutoka nchini Congo,Heritier Makambo aliikacha klabu hiyo na kusaini mkataba wa miaka mitatu wa kuitumikia klabu ya Horoya ya nchini Guinea misimu kadhaa iliyopita.

    Kitendawili kilichozungumzwa na baadhi ya wadau wa soka pamoja na mashabiki ilikua ni je Makambo ameuzwa au kaondoka bure?. Maswali hayo yalikuja baada ya mwenyekiti wa Yanga  kusema watafanya mazungumzo angali tayari alikua amesaini,wasiwasi huo ikawa ni siri iliyowekwa hasa katika wakati huu wa utandawazi wa habari.

    Lakini lengo langu haswa sio kutazama aliondokaje Yanga Sc na kujiunga Horoya Fc. Makambo alikuja Yanga Sc kwa bei rahisi sana huku wengine wakitupia dongo usajili wake lakini alifanikiwa kujibu kwa vitendo.

    Katika takwimu Makambo alicheza mechi 40 na kufanikiwa kufumania nyavu takribani mara 21 ni wastani mzuri kwa mshambuliaji hasa katika msimu wa kwanza tu kwenye klabu tena klabu yenye iliyokua na ukata na uhaba wa wachezaji wenye ubora wakati ule.

    Katika muda mfupi ambao alikuwa na Yanga Sc miguu yake  na kichwa chake alivitumia kuwaachia simulizi tamu  Wanayanga ikichagizwa na aina yake ya ushangiliaji. Akili na kalamu za wachambuzi vilikuwa vinaandaa maneno mapya kila siku.

    Makambo hakuwa na kashifa ya Donald Ngoma au Obrey Chirwa kusikia amegomea mazoezi au kukuta anatajwa kwa lolote baya juu ya klabu yake jambo ambalo hata wazawa kama Kelvin Yondani au Ajibu liliwashinda,jambo ambalo Haruna Niyozima licha ya ufundi wake lilimshinda, ni jambo dogo tu “Nidhamu”.

    Achana na simulizi tamu ya Makambo, kama kuna jambo linaumiza kichwa changu ukiacha changamoto za maisha binafsi basi ni kuona hawa vijana wetu wanashindwa kuwa na viwango endelevu,ukitazama wachezaji wengi wazawa wanapotea muda mfupi tu baada ya kuibuka kwenye soka wachezaji kama Habib Kiyombo,Jofrey Mwashiuya mchezaji aliyenifanya niandike Choga 19 katika jezi yangu kuna wengine kama Abrahaman Musa Salim Aiyee, Crispin Ngushi na wengine wengi wamepotea haraka.

    Unakaa unajiuliza inakuwaje Makambo wa msimu mmoja aliwaacha hapa hapa Tanzania?,Ni maswali magumu yenye matundu madogo ya kupitisha maji.

    Vijana wetu wanatakiwa kujitambua kuwa na nidhamu ya kutosha naposema nidhamu sio kuwaheshimu wanajamii inaokuzunguka tu hata kuheshimu vipaji vyao ni nidhamu ya hali ya juu sana.

    Makambo alikuwa anajielewa pengine hata mwalimu wake Zahera Mwinyi alimwambia hapa Yanga Sc fanya njia ya kupita tu,Fanya kama barabara ya vumbi huku ukiitafuta lami kwa haraka zaidi,amefanikiwa.

    Makambo aliacha simulizi tamu inayoendelea hadi sasa lakini Aiyee,Mwashiuya,Ajibu,Paul Godfrey,Rashidi Juma,Said Ndemla na wengine wengi simulizi zao zimeishia nyumbani kwao.

    Watanzania ni watu wa matukio hasa kwa waliofanya vizuri na huwa na heshima sana  pitia kurasa mbalimbali utakutana na maneno haya “TBT” wakiwa na maana ya kumbukumbu, wanajali sana.

    Wachezaji wetu wanatakiwa kujitambua wao ni akina nani katika soka la Tanzania, wajue wanataka nini kwenye ramani ya soka letu.

    Amkeni vijana chipukizi Mbwana Samata hakufika Ulaya kwa bahati mbaya bali ni kujitambua yeye ni nani.

    SOMA PIA: Mashabiki Na Wachezaji Wana Nguvu Kubwa Ya Uchumi

     

    Makambo Makambo Simba Makambo Yanga Sc

    7 Comments

    1. Imma MK on August 13, 2024 12:09 pm

      Kwani Mim sijaelewa Makambo kafanya nini sasa

      Reply
      • TP on August 13, 2024 5:51 pm

        Alfu kweli
        Niljua kafa, lakn cjaona wap kasema.
        Cjui kafanya nn?

        Reply
    2. Stanley on August 13, 2024 3:25 pm

      Babu kubwa

      Reply
    3. Gachy Mr money on August 13, 2024 7:30 pm

      Ama kweli kipaji ni Kam mshumaa kaka ukiweka katikati ya upépó basi hàkuna mda mrefu wa kuwaka🥺🥺🥺

      Reply
    4. Hammy Chlumba on August 15, 2024 3:33 pm

      Kuna jambo gan lnaendelea juu ya H.Makambo?

      Reply
    5. Pingback: Ni Wakati Wa Vilabu Kula Matunda Ya Timu Za Vijana

    6. Pingback: MVP Wa Ligi Mbalimbali Kuja Kucheza NBCPL Ina Maana Gani?

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.