Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Barua Kwenu Washambuliaji Kuelekea Msimu Wa 2024/2025
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Barua Kwenu Washambuliaji Kuelekea Msimu Wa 2024/2025

    Living ShayoBy Living ShayoJuly 30, 2024Updated:July 30, 20245 Comments3 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mshambuliaji wa Klabu ya Simba Mukwala
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Hongereni kwa washambuliaji wote kwenye Ligi kuu ya NBC kwa msimu uliopita 2023/2024 moja kati ya msimu ambao ulikuwa mgumu sana kwenu, msimu uliyodhihirisha kuwa msimu mbaya sana kwenu washambuliaji wote na hilo halikwepeki kuwa ndani ya wafungaji bora 10 wa msimu ni washambuliaji wawili tu ambao ni Wazir Junior pamoja na Samson Mbangula walioingia.

    Imetuchukua zaidi ya misimu 10 mfululizo bila kushuhudia jambo kama hilo kutokea, nikurejeshe nyuma kidogo hadi mwaka 2014 mpaka 2023 wafungaji bora walikuwa ni, 2014/2015 & 2015/2016 Amisi Tambwe (19) na (21), 2016/2017 Simon Msuva na Abraham Mussa (14), 2017/2018 Emmanuel Okwi (20), 2018/2019 Medie Kagere (23), 2019/2020 Medie Kagere (21), 2020/2021 John Bocco (16), 2021/2022 George Mpole (17), 2022/2023 Fiston Mayele na Saido Ntibazonkiza (17) pamoja na 2023/2024 ambapo mfungaji bora alikuwa Stephane Aziz Ki.

    Takwimu zinaonyesha ndiyo msimu ambao ulikuwa mgumu na mbovu ambao ulikosa washambuliaji hatari zaidi kuliko misimu kumi nyuma ambayo mwisho wa Ligi Mfungaji bora alikuwa mshambuliaji.

    Jambo ilo limenifanya niandike barua hii kwa washambuliaji wote kwa msimu ujao kuanzia Yanga SC iliyo na Prince Dube, Simba SC yenye Valentino Mashaka, Steven Mukwala na Fredy Michael, Azam FC yenye Jlacor Blanco, Singida Blacks Stars yenye Elvis Rupia, Joseph Guede na Habibu Kiyombo, Dodoma Jiji yenye Reliant Lusajo na Wazir Junior, Tanzania Prisons ambayo ina Samson Mbangula, JKT Tanzania ya John Bocco na Edward Songo, KMC FC yenye Ali Shabani pamoja na vilabu vingine vyote.

    Kichwa cha habari hapo juu kinajieleza, rejeeni tena misimu ya nyuma mjione namna ambavyo washambuliaji walidhihirisha ushiriki na uwepo wao kwenye Ligi kuu ya Tanzania kwa nyakati tofauti tokea ikiitwa Vodacom Premier League, Tanzania Premier League na sasa NBC Premier League.

    Tarehe ya Kumbukumbu namba 2014/2015 hadi 2022/2023 inaelezea kuwa hakuna msimu ambao mfungaji bora wa msimu alikuwa ni kiungo na hata kwenye 5 hadi 10 bora basi orodha ilikuwa ikijaa majina ya washambuliaji wengi kuliko wachezaji wa nafasi nyingine, ni dhahiri kuwa kulikuwa na washambuliaji hatari ambao hawakuhitaji nafasi nyingi sana kufunga magoli bali wao walihitaji nafasi ya kucheza kupachika magoli ya aina tofauti tofauti.

    Rejea msimu ambao ulikuwa na Obrey Chirwa, Medie Kagere, John Bocco, Chris Mugalu, Prince Dube na wengine, magoli yao yalionyesha uchu wa kufunga na matumizi sahihi ya nafasi chache walizokuwa wakipata. Hakuna namna kwa msimu ujao kuhitaji washambuliaji bora wa kufumani nyavu kila mara na siyo wakaaji benchi.

    Natumaini barua hii mmeisoma na kuipitia, ila naomba kuwajuza kuwa mpira umebadilika kiuchezaji ila siyo silaha ya kukosa washambuliaji wenye magoli mengi, uwanja wa mazoezi ndiyo sehemu ya kuonyesha uwezo wenu ila kwenye mechi ni mahala pa kuonyesha namna kazi yako unavyoifanya kiusahihi, nitarejea tena mwakani kukumbushia barua yangu ya 2024.

    SOMA ZAIDI: Sio Vibaya Kuwaiga Simba Kwa Jambo Hili Ambalo Walilianzisha

    habari za yanga mshambuliaji wa simba simba sc tanzania

    5 Comments

    1. Bplm1664 on July 30, 2024 10:31 am

      N kweli kabisa yaani hii ni fact muhimu kwa washambuliaji wetu

      Reply
    2. Antony on July 30, 2024 10:44 am

      YAH, MAOMBI GA KUFUNGA MAGOLI YA KIKATIRII
      Ndg washambuliaji kwaheshima na tadhima SS mashabiki wa simba SC tunaomba mtulize akili zenu mjue tunawategemea sna na tumewapa Imani yetuu ko tunaomba mtulize MAGOLI ya viwango tukianza na utopolo tah 8

      Reply
    3. Bamdogo on July 30, 2024 10:45 am

      Wasijivunje watumikie nafasi zao

      Reply
    4. Pingback: Udhaifu Na Ubora Wa Yanga Kwenye Mifumo Hii Kiwanjani

    5. Kevoo on July 30, 2024 1:07 pm

      Yeah ni vizur san

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.