Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    ZAINABU ( 01)

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Hatukatai Umefanya Vingi Ila Hili Ni Deni Kubwa Sana Kwako
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Hatukatai Umefanya Vingi Ila Hili Ni Deni Kubwa Sana Kwako

    Cosmasy ChogaBy Cosmasy ChogaJuly 26, 2024Updated:July 26, 20247 Comments4 Mins Read3K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Rais wa Yanga
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Yeyote aliyekujua ukiwa mtoto mdogo hatakuheshimu ukiwa mkubwa.Ni methali ya kiarabu,Kwa ufupi mazoea huleta dharau,mazoea huzaa hata wivu.

    Wagiriki wa zamani walizungumzia mtu mwenye shamba la ngano lenye ukamilifu.Watu walilistaajabia shamba lake.Mabua yote yalikuwa na urefu sawa.Walipomuuliza ni namna gani mabua yote ya ngano yalikuwa na urefu sawa alijibu.”Rahisi.Kila mbegu inayotokeza kichwa chake kuzidi nyingine nakata kichwa”.

    Hapo awali kulikuwa kuna historia moja tu kubwa katika klabu ya Young Africans sports club nayo ni kuanzishwa kwa klabu hiyo mwaka 1935 nyingine zote ambazo zilifata zilikuwa ni ndogo ambazo pia zinatajwa kuwa historia.

    July 9,2022 wanachama wa Young Africans Sports club waliongeza historia nyingine kwa kupata uongozi mpya uongozi ambao uliingia kwa kishindo cha kura zote ama kwa lugha nyepesi bila kupingwa hii ni baada ya mgombea Hersi Said kuwa peke yake kwenye kiti cha urais wa klabu.

    Aliingia Young Africans kukiwa tayari kuna mataji mengi sana ya ligi kuu kuliko timu nyingine yoyote Tanzania.

    Tangu kuingia kwa Eng. Hersi Said klabu hiyo imepata mafanikio makubwa zaidi mojawapo ikiwa ni kufika fainali ya kombe la shirikisho, kuingia makundi ya klabu bingwa na hatimae kufika robo kitu ambacho hakikufanyika kwa miaka mingi sana.

    Mafanikio hayo hayajatokea kwa bahati mbaya bali ni amani na utawala bora ndani ya klabu hiyo.

    Kalamu yangu leo ngoja ikupitishe katika maeneo machache ambayo ndio imekua chachu kubwa ya mafanikio ya uongozi wa Hersi Said.

    Kama kuna kitu kiliweza  kuathiri akili za Wanayanga ni jina la tajiri Yusuf Manji kwa muda mrefu, licha ya uwepo wa kiongozi  Dr Mshindo Musola bado kulikuwa na makundi mawili wanaoamini Yanga Sc bila Manji haitasimama na wanaoamini inawezekana.

    Katika uongozi wake Eng Hersi Said amehakikisha makundi haya mawili yanaamini kitu kimoja tu nacho ni Young Africans sports club.

    Kama mkulima wa ngano alivyoweza kukata vichwa vya mbegu zilizotaka kuwa juu ya nyingine ndicho amekwenda kufanya Hersi Said.

    Nyakati zimeenda sana na mambo pamoja na mitazamo ya kuifanya klabu itulie Kwa kuwa na watu makini.

    Timu ya Digital waliporecruit na kuibuka na Priva ilikuwa ni Moja kati ushindi mkubwa katika kujenga Yanga katika ushindani huko mitandaoni.

    Idara hii imewatumia sana Alwatan Abdulaziz vizuri. Kila mwanayanga hupata taarifa zake kupenda kufuatilia Yanga Tv.

    Idara ya digital imefanya nchi isimame imara katika kuitangaza Yanga.

    Kama kuna jambo ambalo kilikua kilio kikubwa sana kwa baadhi ya mashabiki basi ni klabu kutokuwa na mpangilio wa mauzo ya jezi za timu. Ilikuwa ni aibu kubwa kwa klabu kongwe kukosa mpangilio mzuri wa kuona ni jinsi gani inanufaika na mauzo hayo.

    Kuna Wanayanga walishajiapia hawatanunua jezi za timu yao kwa sababu kama klabu haipati chochote zaidi ya kunufaisha watu wa mipango yao.Katika hili amekwenda kujenga mfumo bora ikiwemo kuingia ubia na makampuni ya kutengeneza vifaa vya michezo pamoja na kuwa na duka lao  pale makao makuu ili kuweza kuambulia chochote.

    Natambua ugumu ambao ulikuwepo lakini chini ya uongozi wake hili wameamua kwa pamoja na imewezekana.

    Katika uongozi wake ambao unakwenda kutimia miaka miwili sasa amehakikisha klabu inakuwa na wanachama wapya ambao ni hai sio bora wanakadi, klabu imeanza kuwa na takwimu sahihi za idadi ya wanachama wake tofauti na awali ambapo walikuwa wakitajwa kwa kujumlisha mashabiki ambao hawana kadi.

    Chini ya uongozi wake Eng Hersi Said amekaribisha makampuni mengi kuingia kuidhamini klabu hii kongwe nchini katika maeneo tofauti tofauti miongoni ni wale ambao waliingia kwaajili ya ukarabati wa jengo lao pale Jangwani, uwepo wa makampuni mengi kumefanya klabu hiyo kukusanya pesa nyingi za kuweza kuendesha timu kiujumla.

    Haya ambayo tunayaona kwa sasa hayaji bahati mbaya bali ni utawala bora ambao ni lazima tuupongeze kabla ya mengine kutokea(Hatuombei iwe hivyo), hatuwezi kupindisha mafanikio ya watu kwa kumpa mtu kwenye dhana ya matani.

    Lakini nitakuwa mchoyo ikiwa sitaweza kuendelea kuukumbusha uongozi huu juu ya jambo hili muhimu, historia zote zipo lakini Wanayanga na wadau wa soka wanasubiri historia moja kubwa sana nayo ni klabu kumiliki uwanja wake.

    Hayo ni machache ambayo nimewaza kama mdau wa michezo kwa leo kazi ni kwenu kuyachambua na kufanyia kazi.

    SOMA ZAIDI: Ligi Kuu Inakaribia Hivi Ndivyo Wazawa Wanatakiwa Kufanya

    kikosi chayanga leo yanga sc
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views
    Ligi Kuu ya NBC

    RATIBA YA LIGI KUU YA NBC MSIMU WA 2025/2026

    August 29, 202513K Views
    Don't Miss
    Hadithi March 23, 2026

    ZAINABU ( 01)

    NAITWA ZAINABU ALIYU! Hii ni Hadithi ya Maisha yangu…..!!  Mimi ni Mtoto wa kwanza kati…

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.