Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    ZAINABU ( 01)

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Ligi Kuu Inakaribia Hivi Ndivyo Wazawa Wanatakiwa Kufanya
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Ligi Kuu Inakaribia Hivi Ndivyo Wazawa Wanatakiwa Kufanya

    Living ShayoBy Living ShayoJuly 26, 2024Updated:July 26, 20244 Comments3 Mins Read2K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mchezaji wa Ligi Kuu Feisal Salum
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ni mashariki mwa Afrika sehemu ambayo Bahari ya Hindi imepita, nchi ambayo imefunikwa na maeneo makubwa yenye mito na maziwa, ardhi yenye udongo wenye rutuba na vivutio mbalimbali vya utalii pamoja na safu za milima na mabonde.

    Tanzania nchi yangu, hii ndiyo fahari yetu sote, tunajivunia nawe kwenye pande zote za duniani, na ndiyo maana halisi ya Soka la nyumbani limenoga, tumeungana watu wa rika tofauti kuitazama burudani hii ya Kabumbu popote pale nchini, wazawa na wageni kwenye Ligi yetu wanatupa Ladha ya Ligi kuu pamoja na Championship.
    Wacha leo niwaambie nikiwa kwenye ardhi ya Chief Mkwavinyika Mwinyigumba, naamini hata watoto na wajukuu wa Kinjekitile Bokero Ngwale wataisikia, msimu ujao unatarajiwa kuwa mgumu sana kila timu inahitaji kufanya vizuri usajili umefanyika na timu zote kambini maandalizi ya msimu mpya.

    Zaidi ya miaka minne sasa wageni wamekuwa Lulu nchini, sifa mbwembwe wamekuwa wakipewa wao, ni wakati sasa na sisi wazawa kuonyesha ubora wetu, uwezo Ufundi na vipaji tunavyo vya kutosha, kwa sasa hatuhutaji kupendelewa Bali wazawa wanahitajika kupambana zama zinakwenda sana muda unasonga mbele, uwekezaji umeongezeka watu wanaweka hela.

    Vituo mbalimbali vinafunguliwa vijana wanafundishwa na vipaji mitaani vinaonekana, hakuna haja ya kupunguza idadi ya wageni 12 wanatosha sana na Wala siyo wengi, kilichobora ni kupambana na kujituma ukionyesha uwezo jitihada hakuna Kocha atakunyima nafasi kosa kuna wageni.

    Mara ngapi tumeshuhudia wageni wakiwekwa benchi na wazawa, mara ngapi vijana wamepambana mbele ya wageni na wakatoboa na kuwa na nafasi ya uhakika ya kucheza mbele ya wageni? Vijana wangapi wamekwenda kucheza Soka la kulipwa kupitia Ligi ya nyumbani. Ni wakati sasa wa kuendelea kupambana Feisal Salum, Mohamed Hussein, Ibrahim Bacca, Dickson Job, Mudathiri Yahya Pascal Msindo ni baadhi ya wazawa wanaopata nafasi kwa kuwaweka wageni kwenye mbao ndefu.

    Nikukumbushe kuwa Saimon Msuva, Himid Mao walipata nafasi ya kucheza nje ya nchi kupitia Ligi ya nyumbani, hakuhitaji kutafutiwa nafasi ya lazima ili wazawa wacheze. Mnaocheza Ligi kuu sasa Academy ni nyingi sana nchini vijana wanawaangalia nyie kama kioo chao, wanawatazama kama watu wenye ushawishi mkubwa sana kwao na kuwafanya kuwa na matamanio makubwa kupitia nyie.

    Ni wakati sasa kuwaonyesha kuwa wazawa wanaweza hakuna haja ya kuonekana wanatafutiwa nafasi maana wana ubora wa kushindana na wageni.

    Wageni wamefanya Ligi yetu kama daraja kwao kufika mbali Kimataifa tena kwenda kwenye vilabu vikubwa barani Afrika na Mfano halisi Upo Kipre Junior, Luis Miquisone, Fiston Mayele wamekwenda vilabu hivyo baada ya kuonyesha uwezo wakiwa nchini sasa kwanini isiwezekane kwetu?
    Mimi sina mengi sana Wacha niwaache na hayo machache tu ila Imani yangu ni kuwa wazawa wana uwezo tu mkubwa na ilo kadri miaka inakwenda taratibu wanadhihirisha ilo.

    SOMA ZAIDI: Baada Ya Usajili Tuitegemee Yanga Ya Namna Gani Msimu Huu?

    ligi kuu NBC Premier League ngao ya jamii 2024/2025 simba vs yanga
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views
    Ligi Kuu ya NBC

    RATIBA YA LIGI KUU YA NBC MSIMU WA 2025/2026

    August 29, 202513K Views
    Don't Miss
    Hadithi March 23, 2026

    ZAINABU ( 01)

    NAITWA ZAINABU ALIYU! Hii ni Hadithi ya Maisha yangu…..!!  Mimi ni Mtoto wa kwanza kati…

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.