Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    ZAINABU ( 01)

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    Baraka JohanessBy Baraka JohanessJune 27, 2024Updated:July 22, 202435 Comments3 Mins Read14K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Baadhi ya tetesi zinadai kuwa huenda kiungo wa Zambia na mchezaji wa Simba Clatous Chota Chama anaweza kujiunga na klabu ya Yanga akitokea Simba. Klabu ya Simba haijafanya juhudi zozote za kumuongezea mkataba mchezaji huyo na tetesi nyingi zikidai tayari klabu ya Yanga imeshaweka donge nono mezani kwajili ya usajili wa kiungo huyo

    Kama Chama atajiunga na miamba hiyo yaani mabigwa wa kombe la NBC Premier League (Yanga) ataongeza upana wa kikosi na kufanya kikosi hicho kinachonolewa na kocha Miguel Gamondi kuwa na wachezaji watatu wa kariba moja na wenye uwezo wa kucheza namba 10 uwanjani kwa ufasaha.

    Swali ni je kama Yanga watamnasa Chama ipi ni hatima ya Aziz ki na Pacome kama watalazimika kubaki muundo wa uchezaji wa Yanga utakuwaje nani atapata nafasi ya kucheza nafasi ya namba 10 yani kiungo mshambuliaji nyuma ya striker namba 9 namba ambayo wachezaji wote watatu wanakuwa huru sana wakiicheza.

    Kwanza pichani hapo juu ni muonekano wa eneo la kati hadi mbele litakavokuwa kama chama atafanikiwa kujiunga na yanga sasa tudadavue msitari wa Chama, Aziz Ki na Pacome utachezaje

    Kwanza nikuhakikishie kuwa wachezaji wote hao watatu wanaweza kucheza katika nafasi ya namba 10 ndani ya mechi moja kwa lugha ya kisoka inaitwa (Triple ten) au (3 10’s) tujue ili kucheza namba kumi watatu unahitaji nini.

    Kitu cha muhimu ni kuwa unahitaji namba kumi wawili wenye uwezo wa kucheza maeneo ya pembeni na kufanya mikimbio kwenye eneo la kati kwajili ya kutengeneza idadi ya namba kumi 3 nikukumbushe Chama na Saido walicheza kama namba 10 wawili Simba msimu jana Saido akisimama kama namba kumi asilia na Chama akitokea eneo la namba 7 na mikimbio kuelekea namba 10

    Pia nikukumbushe Pacome na Aziz Ki wamewahi kucheza kama namba kumi wawili Pacome akitokea eneo la namba saba au kumi na moja hivyo wachezaji wote hao watatu wanauwezo wa kufanya ivoo kucheza pembeni kisha wakakimbilia kati kutengeneza namba 10 3 tazama

    Hivi ndivyo Yanga watacheza kama wakiamua kutumia namba kumi watatu (Lomalisa na Yaoyao watatumika kama mawinga muda wa kushambulia muda ambao Pacome na Max wataingia katikati ) Swali kwa kocha Je kikosi kitakuwa na uwiano mzuri muda wa kushambuliwa yaani wakiwa hawana mpira hii nitaelezea kwenye andiko lijalo itakuwa mada pana ya Yanga akiwa na mpira na bila ya mpira muundo wao wa kiuchezaji

    Swali ni Je Nani anafaa kuanza nafasi ya namba kumi kwa maoni yako Chama, Pacome au Aziz Ki?  

    SOMA ZAIDI:  Je Simba Wana Mradi Mpya Au Wanataka Kurudisha Wa Zamani?

    chama na pacome usajili wa chama yanga
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views
    Ligi Kuu ya NBC

    RATIBA YA LIGI KUU YA NBC MSIMU WA 2025/2026

    August 29, 202513K Views
    Don't Miss
    Hadithi March 23, 2026

    ZAINABU ( 01)

    NAITWA ZAINABU ALIYU! Hii ni Hadithi ya Maisha yangu…..!!  Mimi ni Mtoto wa kwanza kati…

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.