Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Nilipanga Nyumba Moja Na Majini (03)
    Hadithi

    Nilipanga Nyumba Moja Na Majini (03)

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaMay 27, 2024Updated:May 27, 202432 Comments5 Mins Read727 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Nyumba Moja Na Majini
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Kazini siku hiyo nilishinda sina amani, sina raha, mwili ulikuwa kama umetoka kufanya kazi nzito ambayo sijawahi kuifanya kwa siku nyingi, wenyeji wa Pwani wanaita mavune.

    Kwa upande mwingine nilitamani sana jioni ifike ili nikaone siku hiyo kitatokea kitu gani kipya kwenye nyumba ile. Jioni ilifika, nikaondoka kazini, sikutaka kupitia popote, dukuduku langu lilikuwa kwenda nyumbani tu.”

    ENDELEA: SEHEMU YA TATU-03

    Nilichukua kama saa moja kutoka kazini hadi kufika nyumbani. Nje nilikuta mfuko wa rambo  mweusi, ndani yake ulionekana kuwa na kitu kwani ulikuwa umetuna sana. Niliinama kuipekenyua ili nijue ndani kulikuwa na nini, nilishangaa kuona ni vipande vya nyama za kuchoma tena vilikuwa vya moto.

    “Kha! Atakuwa nani ameweka?” nilijiuliza mwenyewe, nikauacha palepale, mimi nikapanda ngazi za kuingia ndani. Mlango ulikuwa wazi hali iliyoashiria kwamba, wenzangu walisharudi. Nilisukuma mlango, nikaingia. Nilikutana na harufu ya pafyumu, nikahisi walikuwa wakijiandaa kutoka.

    “Jamani za leo?” nilisalimia kwa sauti ya juu licha ya kwamba, mlango wao ulikuwa umefungwa, hakuna aliyeniitikia, hilo sikulijali sana kwani niliamini kwa kuwa walikuwa ndani, isingekuwa rahisi wasikie salamu yangu.

    Niliingia sebuleni kwangu, kisha nikaenda chumbani, kuna kitu kilinishangaza, nikasimama kwa mshtuko. Nilikuta sehemu nilipoweka kiberiti asubuhi siyo, nilikiacha juu ya meza, nikakikuta juu ya kitanda. Niliacha kioo na kitana juu ya kitanda, lakini nikavikuta kwenye stuli, niliguna!

    Nilikishika kioo na kukiangalia kwa umakini kama kina mabadiliko yoyote, lakini sikuona, nikashika kitana. Nilipokigaua sana pia sikuona kitu cha tofauti, nikaamua kuchania, nikahisi kuguswa na kitu kama nywele ndefu kama za mtu aliyefuga. Nilikiweka kitana juu usawa wa dirishani, nikaona nywelenywele nene, nyeusi, mwili wote ukasisimka.

    Ninavyojua mimi, mwanamke mwenye nywele nyingi akichania kitana, ndiyo huacha nywele, sasa mimi nilikuwa na nywele fupi sana zisingeweza kuacha nywele ndefu kwenye kitana.

    “Mh! Hapa kuna kinachoendelea,” nilisema moyoni huku nikikaa. Nilishtuka zaidi kuona soksi zikiwa kwenye msumari nyuma ya mlango wakati niliacha chini.

    “Huyu ni nani?” niliuliza kwa sauti ya ukali.

    Ghafla nikasikia kicheko kutoka chumbani kwa wale wenzangu.

    Nilikaa kwenye kochi, nikaanza kuangalia sehemu mbalimbali za mle ndani ambazo niliamini naweza kuona mabadiliko mengine mbali na yale ambayo nilishayaona, lakini sikubahatika.

    Nilitoka, nikaenda sebuleni ambako nako nilianza kuangalia kila kona ya sebule. Nilishangaa kuona glasi ya maji ya kunywa ambayo niliitumia asubuhi kisha nikaacha maji yamejaa, ikiwa haina hata tone la maji mbaya zaidi, iliwekwa juu ya kabati ambapo mimi niliiweka kwenye meza ya katikati ya sebule.

    “Mh! Hii kali sasa,” nilijikuta nikisema kwa sauti, mara nikasikia kicheko tena kutokea upande wa pili kule kwa wenzangu. Sasa nikaanza kama kuhisi kitu kuhusu watu hao. Ni kwa nini kila nilipoongea kwa sauti ndipo na wao waliangua kicheko?

    Niliamua kujaribu tena, nikasema kwa sauti:

    “Nitakuja kuua mtu, kweli tena.” Nikasikia kicheko tena, safari hii kilidumu kwa muda.

    Moyoni nikasema naanza kufanyia kazi uhusiano wa maneno yangu na vicheko vya wale majirani. Nilitoka kurudi chumbani, wakati napita kwenye korido, nilisimama jirani na mlango wao. Walikuwa wakiongea, lakini niliposimama mimi, kukawa kimya ghafla kama hakuna watu.

    Nilipozama chumbani, nyuma wakaanza kuongea tena. Sikufunga mlango ili niweze kusikia wanachokiongea, lakini jamani kwa kusema ule ukweli wa Mungu, sikujua walikuwa wakitumia lugha gani katika kuwasiliana hata pale nilipojitahidi kutega masikio kwa umakini wa hali ya juu sana.

    Kuna wakati utadhani wanatumia sana neno dotikom, lakini ukisema usikilize zaidi unasikia wakisema sana kotoko au kiburate, wakati mwingine sauti ya kike ilisema kaunto, ya kiume ikarudia hivyohivyo, kaunto.

    Nia yangu kubwa ilikuwa kuwaona kwa sura na kufahamu kama ni ngozi nyeusi au nyeupe. Hilo peke yake lingenipa mwanga ni watu wa aina gani naishi nao pale ndani ya nyumba.

    Nilisikia mlango wa chumbani kwao ukifunguliwa na mimi nikatoka haraka sana, cha ajabu sikuona mtu akitoka lakini mlangoni kulikuwa na kandambili pea moja tu wakati zilikuwa pea mbili.

    Hilo lilimaanisha kwamba, mmoja wao alitoka kwenda chooni, nilichofanya ni kuamua kusimama katikati ya mlango wangu ili huyo aliyekwenda chooni akirudi nimuone. Ni kweli mmoja wao alikwenda chooni kwani nilisikia mlio wa maji.!!

    Nilijitahidi kusimama mlangoni kwangu kumsubiria. Kwa ramani ya nyumba ile ilivyo, asingeweza kutoka chooni bila mimi kumwona hata kama angekuwa anataka kutoka kwenda nje au uani.

    Mlio wa maji ulikosa kusikika, nikawa natumbulia macho kule huku moyoni nikisema:

    “Leo ndiyo leo, asemaye kesho mwongo, hata afanyaje, hawezi kunichenga hapa hata kidogo kwenye hii nyumba,” nilisema moyoni, ingawa wakati huo mapigo ya moyo yalikuwa yakinienda kwa kasi.

    Nilipoanza kuhisi muda unakwenda na hakuna mtu aliyetoka, nikampa dakika tatu kwamba lazima atakuwa anavaa ndiyo maana anachelewa:

    “Labda alikuwa anajisaidia haja kubwa, maana wengine huwa wanavua nguo zote, lakini mimi nipo, siendi kokote,” nilisema moyoni nikiwa bado nimesimama mlangoni kwangu.

    Baada ya muda, nikasikia watu wakiongea chumbani kwao, nikashtuka, nilijikuta nikisema:

    “Haa!”

    Haraka sana nilitupa macho mlangoni kuangalia kandambili, nikazikuta pea mbili, nikashangaa:

    Nini Kiliendelea? Usikose sehemu ya nne

    SOMA RIWAYA YA KOTI JEUSI KWA KUBONYEZA HAPA 

    SOMA RIWAYA YA FUNGATE KWA KUBONYEZA HAPA 

    Una Enjoy Nyumba Ya Majini? Mtumie ADMIN Ahsante

    Lipa Namba: 57900454
    Jina: LIPA KIJIWENI TIPS
    Mtandao: VODACOM 

    Wewe Ni Mwandishi? Unapenda kuendeleza Taaluma yako ya uchambuzi kwenye masuala ya michezo? Mtandao wa uchambuzi wa michezo kijiweni.co.tz unakupa uwanja wa kuendeleza kipaji chako na kufikia maelfu ya wapenzi wa michezo Tanzania na nje ya Tanzania.

    Tutumie makala au uchambuzi wa michezo katika barua pepe hii [email protected]  

    Nyumba Ya Majini Riwaya Nyumba Ya Majini Kijiweni

    32 Comments

    1. Jimmy elias mkanila on May 27, 2024 6:24 pm

      Nime cheka kweli . Eti nitakuja kumuua mtu

      Reply
      • Anthony jaden on May 27, 2024 7:44 pm

        Alaaaah

        Reply
      • Joel Twalipo on September 23, 2024 10:51 am

        Daaaa ii atar kwel

        Reply
    2. Stranger Guy on May 27, 2024 6:31 pm

      Daaaah!! Nzuri Sana hiiii meioenda ila mjitahd kutoa vingi

      Reply
    3. Lus twaxie on May 27, 2024 6:37 pm

      Daaaaaah naogopa jmn hzi nyumba za kupanga ……. Admin tuma ndefu kdg

      Reply
    4. Valence on May 27, 2024 6:42 pm

      Nyieeee he he he he he hatari sanaaa

      Reply
    5. [email protected] on May 27, 2024 6:48 pm

      Acha ujinga admin UmEdisconecti 😂😂😂😂😂

      Reply
    6. Ammar Hassanain on May 27, 2024 6:54 pm

      Haiyaa

      Reply
    7. Sebeku on May 27, 2024 7:00 pm

      Admin unatukata stim unatuma fupi sana ila hongera hii ya safari imefunika zote congratulations 👏👏👏👍👍👍

      Reply
      • Anthony jaden on May 27, 2024 7:45 pm

        Kipande kingine plz,nalipia 10k

        Reply
    8. EDSON MOLLEL on May 27, 2024 7:02 pm

      Duuuu hii ni Kali sana Mkuu

      Reply
    9. Shabani Jumbe on May 27, 2024 7:13 pm

      Tunaolala peke etu tunafurahi 😂😂😂

      Reply
      • Madam p on May 27, 2024 11:37 pm

        Mmmmh tenah umeme umekata 👀

        Reply
    10. Yusuf on May 27, 2024 7:34 pm

      Sehem ya pili sijaiona

      Reply
    11. Bryson on May 27, 2024 7:58 pm

      Nzuriiii

      Reply
    12. Nuru on May 27, 2024 7:58 pm

      Uhondo mtupu

      Reply
    13. Hussein Lucas on May 27, 2024 8:26 pm

      Is so nice big up

      Reply
    14. Mninawi on May 27, 2024 8:42 pm

      Mmmmh kama inatisha Sana Hahaha wale wa nyumba za kupanga kula chuma hiko

      Reply
    15. Jumaa vesso on May 27, 2024 8:53 pm

      admn bhaan ety kandamblii alaf pea n mbili

      Reply
    16. Elia on May 27, 2024 11:18 pm

      Hahahaa nimecheka lugha zaa awa jamaa mbona kama wasukuma. kotoko kibulate kaunto

      Reply
    17. Madam p on May 27, 2024 11:35 pm

      Hahahhahah ntaua mtu humu ndani 😁😁😁😁 ten minutes later 🤣🤣🤣🤣

      Reply
    18. Given Gihsy on May 28, 2024 3:24 am

      Mim admn nmeamua hii stry niisome mida ya saa nane plus ucku ili nipate muhaho naashum ndo mim , haujui😎

      Reply
    19. Kidunda on May 28, 2024 7:35 am

      Mwamba anataka ajichabganye 😂😂😂 naqubal adimin

      Reply
    20. Cesilia Nkunga on May 28, 2024 9:49 am

      Hatarii 🤣🤣

      Reply
    21. Zeyy Tabasamu✨🥰 on May 28, 2024 10:07 am

      😂😂😂Aaah Mhandishi una sifa sanaaa imagen mtu unaogopa kwa kitu cha kusoma Yan Unavuta picha🤣😂🤣Big up kwakooo

      Reply
    22. Chrispin on May 28, 2024 10:37 am

      Nilala nyuma. Moja na majin time

      Reply
    23. Chrispin on May 28, 2024 10:38 am

      Nilala nyumba. Moja na majin time

      Reply
    24. Muuh on May 28, 2024 1:09 pm

      Mbona fupi jomony🥺🥺

      Reply
    25. Tyseem on May 28, 2024 2:25 pm

      Hich kipand nmesom nkiw hospital yan mpak watu wananikodolea macho kw kicheko.kongore mtungaj

      Reply
    26. Baybezuuh on May 28, 2024 2:38 pm

      Balaa

      Reply
    27. isco on May 28, 2024 7:02 pm

      leo ndio leo asemaye kesho muongo 🤣🤣🤣

      Reply
    28. Kobossa on May 28, 2024 10:32 pm

      Duh…mambo ya mlabani

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.