Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » KOTI JEUSI (Sehemu Ya Kumi Na Nne) KOTI JEUSI – 14
    Hadithi

    KOTI JEUSI (Sehemu Ya Kumi Na Nne) KOTI JEUSI – 14

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaMay 9, 2024Updated:May 23, 202427 Comments7 Mins Read4K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Riwaya Ya Koti Jeusi
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia ” “Muda siyo mrefu nitamnasa Muuwaji, mtakua huru lakini msirudie kuficha mambo mazito kama haya” akawapa tumaini na kuwaacha hapo Mahabusu wakiwa wanafuraha wakijua muda siyo mrefu watarudi Uraiani. Nini kitaendelea? Miss Laya ndio muuaji mkuu?  

    Tuendelee 

    SEHEMU YA 14 

    Giza nene likiwa limeifunga anga ya Jiji la Dar-es-salaam, Mtu mmoja alikua akishuka kwenye gari moja nyeusi aina ya Toyota Crown, Mtu huyo alikua ni Miss Laya. Mbele yake palikua na jengo la Hospitali ambapo Adela alikua akipatiwa matibabu baada ya kukutwa Mochwari kwenye jokofu la kuhifadhia Maiti.

    Kwa ajili ya Usalama wa Adela, Marcus aliagiza ulinzi wa Polisi kuzunguka wodi hiyo ili atakapokaa sawa aeleze alichokiona Usiku ule, kukawa na hisia kua huwenda aliwaona wauwaji wote, lakini walichohitaji zaidi wapelelezi ni kujua Mtu wa kwanza kuingia kwenye kile chumba cha Bilionea Yusuf ni Nani.

    Miss Laya alishuka kisha akaishika korido akiwa na taarifa ya wapi anaelekea, alielekea moja kwa moja kwenye chumba alicholazwa Adela, namna alivyovaa alionekana kuwa ni Daktari wa Hospitali hiyo, wale polisi wakamruhusu kuzama ndani.

    Humo alimkuta Hamza akiwa amejiegesha kwenye sofa, Adela akiwa anasaidiwa kupumua na 

    Mashine, hakuna aliyekua na fahamu hapo ndani, Hamza alikua Usingizini , Adela alikua hajitambui. Kitu cha kwanza kufanya Miss Laya ni kutazama Mashine inayomsadia kupumua, haikujulikana ana lengo lipi hapo huku tayari akiwa anafahamika kua ni Jasusi wa siri wa Serikali.

    Mashine ilionesha kiwango cha Oksijeni ambacho Adela alikua akikipata, akamsogelea kisha 

    akamwambia

    “Mungu alikulinda sana Adela, imefika wakati ambao ameshindwa kufanya hivyo” akachomoa ile mashine, Adela akaanza kuhema kwa shida kisha haraka Miss Laya akachomoka ndani ya wodi hiyo bila wale Polisi kushtuka kuwa Mtu huyo hakua Daktari na alikuja hapo kwa lengo baya dhidi ya Adela.

    Adela akawa anahema kwa shida huku akiwa ametoa macho, akawa anajaribu kutaka kupiga kelele kuomba msaada lakini alikua anashindwa, akawa anapoteza nguvu huku chozi likimbubujika akimtazama Hamza akiwa amejilaza. Adela akawa anajaribu kutaka kusukuma enga iliyotumika kuwekea dripu, akawa anajaribu kujisukuma lakini anashindwa. 

    Hali yake ikawa mbaya zaidi, akakosa hewa huku akiitumia kidogo aliyonayo kuvuta nguvu kisha akaisukuma enga ikamwangukia Hamza ambaye alishtuka na kumwona Adela akipupa pale kitandani, haraka akairudisha ile Mashine ya kupumulia, akaita Madaktari mara moja

    Polisi ndiyo wakafahamu kuwa aliyeingia pale hakua Daktari bali ni Mtu mbaya, wakazunguka kumsaka Hospitali nzima lakini hawakumwona, tayari Miss Laya akawa ametoka nje ya Hospitali, akiwa kwenye gari akapiga simu mahali

    “Tayari, hakikisha unaihama hii Nchi haraka sana. Majasusi wamenifikia hiyo ni ishara kua kuna 

    taarifa zako zinazoweza kuvuja” alisema Miss Laya, ikasikika sauti ya kike kwenye simu ikisema

    “Sitoondoka hadi Nimuuwe Mama yangu, yeye ni Mtu wa mwisho. Endelea kunificha” Miss Laya akaikata simu kwa hasira huku akigonga Usukani. Akakanyaga mafuta akiamini ameshamuuwa Mtoto Adela, Usiku ule Madaktari wakamwamisha Adela na kumpeleka wodi nyingine kuhofia Muuwaji angeliweza kurudi tena kumdhuru.

    Saa 6:10 Usiku, mpango wa Marcus ulikua ni kurudi kwenye ile nyumba ya Miss Laya. Alipofika hapo Usiku huo aliona gari moja aina ya Range Rover nyeusi ikitoka hapo, akajificha kwenye maua yaliyo nje ya Nyumba hiyo, kisha Akamwona Miss Laya akilifunga geti hilo.

    “Nani anatoka hapa?” alijiuliza Marcus akiwa amebana vizuri mahala hapo, Miss Laya wakati 

    analifunga akahisi jambo, akatoka nje na kuangaza huku na kule kuona kama kuna Mtu amekuja 

    hapo. Hisia zake zikamwelekeza kwenye Maua, mahala hapo ndipo alipojificha Marcus, kwa namna yoyote kama atafika hapo basi atamwona Marcus na kugundua kuwa anapelelezwa kwa siri.

    Akasogea taratibu akiwa amevalia pensi nyeusi na tisheti jeupe, akaziweka vizuri rasta zake, mara simu yake ilianza kuita, ikamtoa kwenye njia kabisa, akaipokea na kusahau alichopaswa kukifanya kisha akafunga geti na kurudi ndani.

    Marcus akapumua kwa pumzi kuu ya kushusha, akaelekea kuchungulia kwenye geti akamwona Miss Laya akiufunga mlango wa kuingilia ndani ya jumba hilo, kuna kitu kimoja tu kilichomleta Marcus, alihitaji kupeleleza uwepo wa eneo la nyuma ya nyumba hiyo mahali ambapo Denis alisema aliiyona Maiti

    Aliamini hapo angepata shahidi fulani za kimazingira kuelekea Ushindi wa kesi ya kumsaka Muuwaji

    Miss Laya alifunga Milango yote huku akizungumza na Mtu kwa njia ya simu lakini hisia zake 

    zilimwambia kitu japo alionekana kuongea na simu ila hisia zote alizielekeza nje ya Jumba lake la Kifahari. Marcus akautumia ukuta uliozungushiwa vyuma vidogo vinavyokata, alishajiandaa kwa hilo mikononi alivalia Glavu ngumu zenye kumkinga. Kisha akatua ndani ya jumba hilo, akatulizana kwa makini kwa zaidi ya dakika moja kuona kama Miss Laya ameshtuka.

    Alipoona hali ni shwari akanyata taratibu hadi nyuma ya jumba hilo, akamulika tochi. Ni kweli palikua na dalili zote kua ni eneo la kutesea Watu, palikua na vifusi vidogo vya udongo vilivyofanana na Makaburi hivi, Marcus akajua sasa kua Muuwaji ni huyo Miss Laya. 

    Hakutaka kupoteza Muda akapanga kumvamia ili amnase Usiku huo, kwanza akatuma Meseji kwa Polisi anayemwanini sana akamtaka aende hapo nyumbani kwa Miss Laya.

    Hata Marcus alijua kuwa si rahisi kumnasa Mwanamke huyo sababu ni Jasusi wa kuaminika hivyo ni lazima atakua na ujuzi mkubwa sana wa mapigano ya aina yote. 

    Marcus akasogea hadi kwenye mlango wa kioo ambao hutumika kuingia ndani ya Mjengo huo wa kifahari, alipofika alishangaa kuukuta uko wazi hivyo akajua sasa hata Miss Laya yupo mawindoni akimwinda Mtu aliyeingia ndani ya nyumba yake.

    Kabla hajapiga hatua yoyote aliwekewa Bastola kichwani, nyuma yake alisimama Miss Laya, akamwita Marcus kwa jina lake halisia, hapo Marcus akajua kua Miss Laya aliamua kujidhihirisha kua yeye ndiye Muuwaji, akakumbuka kuwa hata Sakina aliye magereza alimwita kwa jina lake halisi hivyo huwenda Miss Laya ndiye aliyempandikiza Sakina na kujifanya ndiye Muuwaji. Maswali mengi yalizunguka kichwa cha Jasusi Marcus

    “Dondosha Bastola yako” alisema Miss Laya kwa sauti ya kukaza isiyo na Mchezo, Marcus akaweka Bastola bila kufanya mchezo wowote ule kisha akaambiwa ageuke

    “Isukume kwangu hiyo Bastola” akasema tena Miss Laya, Marcus akaisukuma Bastola kwa Jasusi huyo, kisha Miss Laya akainyanyua na kuisweka kiunoni

    “Unataka nini Marcus?” akauliza Miss Laya kwa sauti ile ile yenye mkazo sana

    “Nataka kumjua Muuwaji anayeisumbua idara ya Upelelezi” alijibu Marcus mikono yake ikiwa juu kama alivyoambiwa na Miss Laya

    “Unafikiria baada ya kumjua Muuwaji itakuaje, utaendelea kuishi?” alihoji Miss Laya

    “Kitu muhimu kwangu ni Kumjua Muuwaji, nitaendelea kuishi au nitakufa hilo sitojali lakini nataka kujua Muuwaji ni Nani?” alisema Marcus kwa Kujiamini sana akiamini pia kua Polisi anayemtumaini atafika hapo na kumsaidia endapo itatokea akahitaji kumwua.

    Miss Laya akashusha Bastola yake kisha akamwambia Marcus

    “Kama leo itakua ndiyo siku yako ya mwisho kuishi basi yote uliyoifanyia Serikali yatazikwa pamoja na jina lako, pengine hata wasijue uko wapi, vipi kama nitakuzika hapa kwangu Marcus?” maelezo haya yakampa taswira Marcus kua Miss Laya ndiye Muuwaji. 

    “Ina maana wewe ndiye Muuwaji unayewatesa Watu?” 

    Miss Laya akacheka kidogo kisha ukaonekana Mwanga wa taa ya gari getini, akili ya Marcus ikamwambia kuwa Polisi wake amefika lakini kicheko cha Miss Laya kilimpa hofu ikabidi atulie kwanza huku akipiga mahesabu baada ya Miss Laya kuonesha Dalili zote kuwa ndiye Muuwaji.

    Miss Laya alionekana kujiamini, akairejesha Bastola nyingine kiunoni kisha akasogea getini akimwacha Marcus akiwa huru kitu ambacho hata Marcus alikishangaa, ikabidi asubirie kuona ni Nani amefika hapo. Range moja ya kitajiri sana iliingia hapo, Marcus akajua huyo si Polisi wake kwani asingeliweza kuja na gari ya kitajiri namna ile.

    Akashuka Msichana mmoja ambaye sura yake Marcus alishawahi kuiyona zaidi ya mara moja, akapiganisha kumbukumbu zake alimwona wapi, akakumbuka kua alimwona kwenye nyumba ya Mzee Yusuf, alimwona mara kadhaa akiwa na Sofia.  Msichana huyo ni nani? Na kwanini anamtumia Miss Laya?  Usikose Sehemu Ya 15  Zikifika Comments 200 Naiachia Asubuhi Mapema Tu

     

    Wewe Ni Mwandishi? Unapenda kuendeleza Taaluma yako ya uchambuzi kwenye masuala ya michezo? Mtandao wa uchambuzi wa michezo kijiweni.co.tz unakupa uwanja wa kuendeleza kipaji chako na kufikia maelfu ya wapenzi wa michezo Tanzania na nje ya Tanzania.

    Tutumie makala au uchambuzi wa michezo katika barua pepe hii [email protected] 

    KOTI JEUSI (Sehemu Ya Kwanza) KOTI JEUSI – 01

    KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Pili) KOTI JEUSI – 02

    KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Tatu) KOTI JEUSI – 03 

    KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Nne) KOTI JEUSI – 04 

    KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Tano) KOTI JEUSI -05

    KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Sita) KOTI JEUSI -06 

    KOTI JEUSI (Sehemu Ya Saba) KOTI JEUSI – 07

    KOTI JEUSI (Sehemu Ya Nane) KOTI JEUSI -08 

    KOTI JEUSI (Sehemu Ya Tisa) KOTI JEUSI -09 

    KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Kumi) KOTI JEUSI -10 

    KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Kumi Na Moja) KOTI JEUSI -11

    KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Kumi Na Mbili) KOTI JEUSI -12

    KOTI JEUSI ( Sehemu Ya Kumi Na Tatu) KOTI JEUSI -13

    KOTI JEUSI Koti Jeusi Kijiweni riwaya ya koti jeusi

    27 Comments

    1. Patrick on May 9, 2024 10:14 pm

      Mbona kama imekua fupi!!🤔🤔

      Reply
    2. Ms chunnie on May 9, 2024 10:17 pm

      Martha anataka kumuua mamaake????🥺🥺🥺🤒.. anhaaa kisa alimuua babaakee bhn na Mr george😅😅🥲… yaaniii watafarikiiiii hiii ni kila paradox cjui double killer mulemule

      Reply
      • Zacharia john on May 10, 2024 10:03 am

        Mdada mwenyewe ni martha

        Reply
    3. Zeyy Tabasamu✨🥰 on May 9, 2024 10:20 pm

      Bila shaka ni Martha🙌😂

      Reply
    4. Enock S on May 9, 2024 10:24 pm

      💯

      Reply
    5. Henderson Didas on May 9, 2024 10:29 pm

      I cant wait to see Martha 🤩…the last killer💯

      Reply
      • Ediger on May 10, 2024 7:38 am

        Dah!!! Hii ni Atari sana wazee

        Reply
        • Bintii kimmy on May 10, 2024 12:09 pm

          🔥🔥🔥

          Reply
    6. Esther Emmanuel on May 9, 2024 10:29 pm

      Leo umetupiga imekuwa fupi

      Reply
    7. Tobias Mzopola on May 9, 2024 10:35 pm

      Hatimaye Muuaji sugu ni Martha….

      Reply
    8. Frank on May 9, 2024 10:44 pm

      Ya moto

      Reply
    9. Kasomelo sadick on May 9, 2024 10:44 pm

      Stor tamuuu sana

      Reply
    10. Kasomelo sadick on May 9, 2024 10:46 pm

      Endelea kutushushia vitu admin

      Reply
    11. Veronica kitundu on May 9, 2024 11:01 pm

      💯

      Reply
    12. Godwin Clemence on May 9, 2024 11:05 pm

      Nilikuwa nishaanza kuumwa kichwa kama Adela angefariki,

      Reply
    13. Mifupa 206 on May 9, 2024 11:46 pm

      Hii ndio raha ya riwaya,huenda muuaji asiwe martha😁

      Reply
      • Stuart on May 10, 2024 12:27 am

        Good story but very short

        Reply
    14. Becka on May 10, 2024 7:38 am

      Piga spana mzee

      Reply
    15. walter Massawe on May 10, 2024 8:17 am

      🔥🔥

      Reply
    16. Lizzy on May 10, 2024 8:33 am

      Huyo ni Martha 100% 😂🙌

      Reply
    17. Ammar Hassanain on May 10, 2024 8:41 am

      Nilikuwa najiuliza Martha anarudi vp mchezoni? Huyo ss ameingia

      Reply
    18. Scalion mgisha on May 10, 2024 9:55 am

      Daahhh inazidi kunoga asee huyo ni Martha na si mwingine

      Reply
    19. The chiza on May 10, 2024 1:27 pm

      Leo wanapost saa ngap ep15?

      Reply
    20. Czer on May 10, 2024 2:13 pm

      Admin umetish🙌🏿🙌🏿

      Reply
    21. Martin on May 10, 2024 3:30 pm

      Kali

      Reply
    22. Godlove4 on May 10, 2024 4:25 pm

      Imekuwa fupi sana

      Reply
    23. Pingback: KOTI JEUSI (Sehemu Ya Kumi Na Tano) KOTI JEUSI – 15 - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.