Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » KOTI JEUSI (Sehemu Ya Sita) KOTI JEUSI – 06
    Hadithi

    KOTI JEUSI (Sehemu Ya Sita) KOTI JEUSI – 06

    Kaka MkubwaBy Kaka MkubwaMay 4, 2024Updated:May 5, 202418 Comments10 Mins Read5K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Riwaya Ya Koti Jeusi
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilipoishia “Jambo hilo lilimwacha Sofia akiwa mwenye tabasamu sana, kwa namna alivyokua na chuki za wazi kwa Salma asingeliweza kukubali Mali hizo zisimamiwe na Salma ambaye ndiye Mama yao Mdogo, kifo cha Salma kilijaza Tabasamu kwa Sofia, tabasamu lililoonekana waziwazi kabisa.  “

    Tuendelee
    SEHEMU YA 06 

     

    ( Miaka kadhaa iliyopita) 

    Sauti ya Mtoto Mchanga ilisikika kutoka katika kitanda alicholala Mama mmoja aliyechoka, alikua akitabasamu huku akikitazama Kichanga kilichozaliwa masaa kadhaa yaliyopita kwenye maegesho ya magari ya hospitali hiyo, palikua na gari moja aina ya Benz iliyokua imeegeshwa, mara moja Injini yake ilizimwa.

    Alishuka Bwana Mmoja tajiri sana, alikua na haraka ya kuelekea wodini kumwona Mtoto aliyezaliwa, Bwana huyu ndiye ambaye Sasa kifo chake kinawasumbua Wapelelezi. Anaitwa Yusuf Balun

    Alifika wodini na kumwona Mtoto aliyezaliwa, tabasamu lilikua juu alipogundua kua Mtoto huyo 

    alikua wa kike, pale pale akampa jina la Sofia, jina ambalo alilichukua kutoka kwa marehemu Mama yake.

    “Kila mara nimwonapo nitakua namkumbuka Mama yangu” alisema Mzee Yusuf akiwa amembeba Mtoto Sofia aliyezaliwa masaa kadhaa yaliyopita. Kando yao alikuwepo Mtoto mwingine, huyu alikua ni Hamza.

    Mtoto wa kwanza wa Bilionea Yusuf, Mapenzi ambayo aliyaona kwa mara ya kwanza kutoka kwa Baba yake kwenda kwa Mdogo wake yalimfanya akasirike na kuondoka kabisa pale wodini. Kadili alivyozidi kukua ndivyo alivyozidi kua na chuki na Mdogo wake Sofia, alionesha chuki za Wazi wazi hadi ikawa shida kwa Mzee Yusuf.

    Siku moja alimchukua Hamza na kumpeleka kwa daktari wa Saikolojia, kwani mwanzo waliamini huwenda ni wivu wa kawaida ambao Mtoto wa kwanza hua nao pale anapozaliwa Mtoto mwingine, lakini Dokta huyo alipomwona tu Hamza aligundua ana tatizo kubwa zaidi ya wivu hivyo akamshauri 

    Mzee Yusuf amtenganishe Hamza na Sofia kwa muda mrefu, pia aongeze mapenzi kwa Hamza

    Baada ya kumaliza walitoka kwa Daktari, nje walikutana na Mtoto mmoja mdogo mwenye makamo ya chini zaidi ya Hamza na Sofia, Binti huyu ndiye sasa anajulikana kama Martha, Hamza alitokea kumpenda Mtoto huyo akamwambia Baba yake wamchukue

    Mzee Yusuf alicheka kidogo akamwambia Hamza

    “Huyu ni Mtoto wa watu, hatuwezi kumchukua kama Bidhaa mwanangu” alisema, mara muda huo huo alifika Baba yake Martha, alipomwona Mzee Yusuf alimtambua kwani ni mfanyabiashra Mkubwa sana Tanzania.

    Kuanzia hapo Mzee Yusuf na Baba yake Martha walianza kufahamiana, wakawa marafiki wazuri 

    sababu Hamza alimpenda sana Martha hata ule wivu kwa mdogo wake uliondoka wenyewe. 

    Miaka mitatu ya kufahamiana walitengeneza undugu, baadaye Baba yake Martha alikufa kwa ajali ya gari akiwa anatoka kazini kwa Mzee Yusuf, kuanzia siku hiyo Martha alilelewa na MzeeYusufu hadi alipokua na Umri mkubwa.

    ( Turudi Maisha ya sasa )

    Hamza alitambulishwa kwenye kampuni kama Mkurugenzi mpya baada ya kifo cha Mzee Yusuf, 

    alimtoa Dada yake kwenye kitengo cha kusimamia wafanyakazi wote wa Kampuni, nafasi ya Salma ikajazwa na Sofia. Maisha mapya ndani ya kampuni yalianza ili kukuza kampuni iliyoachwa na Baba yao, sehemu ndogo ya Mali walipewa ndugu wa Salma kama mirathi.

    Siku moja Sofia na Hamza waliomba kuonana na Mpelelezi Daudi, ilikua ni miezi mitatu baada ya 

    wapelelezi kushindwa kumpata Muuwaji, wakakutana Johari Rotana. Katika mazungumzo yao, Sofia na Hamza walimuomba Mpelelezi Daudi aifunge kesi ya kifo cha Baba yao kwani waliamini wapo salama na pasingetokea Mauwaji mengine.

    Uamuzi huo ulikuja baada ya mashauriano kati ya Mtu na Dada yake na wakakubaliana kuifunga kesi hiyo iliyoonekana kukosa Mashiko kwani kwa zaidi ya miezi mitatu hapakua na dalili yoyote ya kumjua Muuwaji, licha ya uamuzi huo kutoka kwa ndugu hao hata Mpelelezi Daudi na jopo lake waliona kesi hiyo inawaelemea kwa namna ilivyokua inaenda.

    Kesi iliondoa ufanisi wa Daudi kama mpelelezi, muda ulienda bila kupatikana kwa Muuwaji 

    kuliashiria kuwa wapelelezi wameshindwa kumnasa Muuwaji, kila taarifa iliwachanganya na 

    kuwapoteza kabisa. Moyoni Daudi hakuacha kuhisi kuwa Muuwaji anatoka kwenye familia ya Mzee Yusuf, yaani hapa alihisi atakua mmoja kati ya Martha na Sofia lakini kadili alivyowachunguza hapakua na dalili yoyote kua Sofia au Martha wana viashiria vya Uharifu kwani hata simu zao walikua wakizungumza mambo ya kawaida tu.

    Japo alikubali kuifunga kesi lakini moyoni alijua ipo siku kesi hiyo itapata tena uhai na itarudi kwa kasi. 

    “Nawatakia Maisha ya Amani, utulivu. Kwa chochote kitakachojili nitawajuza na nyie pia msisite kunieleza, hisia zangu bado zinaniambia kua Muuwaji atarudi tena” alisema Mpelelezi Daudi kisha akapiga unywaji

    “Tutaonesha ushirikiano kwa lolote tutakujuza, kama ulivyosema kufunga kesi haina maana tutaacha kuwasiliana” alisema Hamza, nyuso za ndugu hawa wawili zilionekana kua na nuru kubwa sana ya furaha, nuru iliyoonesha kuanza Maisha mapya na kukubali uhalisia kua Mzee Yusuf amefariki, japo Muuwaji hakupatikana lakini walitabasamu.

    Saa sita Usiku, fax moja iliingia kwenye jumba la Mpelelezi Daudi. Fax hiyo ilitoka Makao makuu ya polisi, alipoifungua aliona palikua na uhamisho wake kutoka Dar-es-salaam kuelekea Uvinza Kigoma. 

    Alijulishwa kua huko ataenda kupeleleza kuhusu Uingiaji na utokaji wa Watu katika Mji huo kuelekea nje ya Nchi bila kufuata utaratibu.

    Kazi ya upolisi ni kazi ambayo imejikita zaidi katika amri, Daudi alikubali kuhama Dar huku moyoni akiwa na maumivu makali ya kushindwa kesi ya kumnasa Muuwaji wa Mzee Yusuf, aliamini uhamisho huo umekuja baada ya kushindwa kwake kwa kesi, alijawa na hasira sana akachukua Pombe kali na kuigida.

    Asubuhi, aliwahi makao makuu, alipewa kila kitu kuhusu kazi mpya ya Mkoani Kigoma katika Mji wa 

    Uvinza. Aliondoka ofisini kwa Mkuu wake akiwa anajisonya na kujitukana, taarifa ya kuhama kwake ilitangazwa na vyombo vya habari ambavyo vingi vilihoji kuhusu kesi ya Mzee Yusuf na Marehemu Salma.

    Jeshi la polisi likaingia kwenye dosari ya kushindwa kwa kesi hiyo, Mkuu aliyemhamisha Mpelelezi Daudi ambaye ni IGP Saimoni Kuga aliamua kuihamisha kesi hiyo kutoka kwa Polisi wapelelezi hadi ofisi ya Majasusi wabobevu. Alifanya hivyo ili kukwepa aibu ya kushindwa kwa kesi ya Mauwaji ya Mzee Yusuf na Mke wake Salma, vifo vilivyoitingisha Tanzania lakini viliishia kuchunguzwa na kutolewa ufafanuzi wa kawaida tu.

    Sasa Jalada la kesi limefika mikononi mwa Malcom maarufu kama Agent X ambaye ametoka 

    mafunzoni Nchini Misri chini ya kitengo kidogo cha Majasusi kutoka Katika kitengo cha Kijasusi cha Nchini Israel kinachoitwa Mossad. Alipelekwa masomoni baada ya kuingizwa kwemye mfumo wa Majasusi ikiwa ni mwezi mmoja baada ya kuisaidia Tanzania kupambana na Rais na Deusi ambao walidhamiria kuisambaratisha kariakoo kwa Bomu

    xxx

    Kurudi kwa Muuwaji 

    Alfajiri moja iliyojaa Baridi kali sana, haikua kawaida Jiji la Dar-es-salaam kukabiliwa na hali hii tena katikati ya Mwaka. Japo palikua na Baridi lakini ilionekana kua hali nzuri kwao, wapo waliovalia makoti kuelekea kwenye mihangaiko yao. Uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere ulikua ukipokea ugeni

    Ndege Mpya aina ya Boeng ilikua ikishusha abiria wachache waliofanya safari kutoka Misri, miongoni mwao alikua ni Jasusi Malcom. Kutokana na kazi nzito aliyoifanya, Serikali ya Tanzania chini ya Rais Mpya David Chota ilifanya maamuzi ya kuibadilisha sura ya Malcom ambaye alikua maarufu sana baada ya ule Mkasa mzito wa kuikomboa Tanzania juu ya Shambulio la Bomu na Ugaidi uliotaka kufanywa na Watu kutoka Urusi wakiongozwa na Deusi na Rais wa Tanzania kwa wakati huo.

    Malcom alishuka akiwa na mwonekano mwingine kabisa, hata jina lake lilibadilishwa akawa anaitwa Agent Marcus. Serikali ilifanya hivi ili kumlinda na Maadui ambao waliamini wangerejea tena Tanzania baada ya jaribio la kwanza kufeli.

    Malcom ambaye sasa tunamtaja kama Agent Marcus alipanda Tax kama abiria wa kawaida huku 

    akiliangalia eneo ambalo ndege ilidondoka Usiku ule wa kutisha

    Alifika makao makuu ya idara ya Ujasusi Tanzania, akampatia pesa yule dereva wa Tax 

    “Asante, karibu Tanzania” alisema yule dereva akiamini Marcus si Raia wa Tanzania hasa 

    alijitambulisha kua ni Raia wa Kenya, Marcus alirejea akiwa mwenye ujuzi wa kufanya upelelezi wa kesi kuliko kawaida.

    Alioneshwa Ofisi yake. Lakini kabla hajaondoka hapo aliambiwa kuna Ujumbe kutoka kwa IGP 

    Saimon Kuga, faili la kesi ya Bilionea Mzee Yusuf ikawekwa mbele ya Macho ya Jasusi huyu 

    aliyebadilisha sura na utambulisho wa jina.

    “Kazi yako hii kutoka kwa IGP Saimon Kuga. Nakutakia Mafanikio Agent Marcus” alisema Askari wa kitengo aliyekua akimwonesha Marcus ofisi alimpatia funguo ya gari na nyumba

    “Ramani ya unapoishi imeshatumwa kwenye simu yako” alisema Askari huyo, akapiga saluti kisha akaondoka. Marcus akalitia faili hilo kwenye begi lake dogo kisha alielekea maegesho ya magari, akakutana na Kulger nyeusi, akatabasamu kwa maana anazijua gari hizo namna zilivyo nyepesi

    Alipotekenya mara moja alianza safari ya kuifuata ramani ili afike anapotakiwa kuishi, Mfumo wa Majasusi ulibadilishwa sana baada ya usaliti uliofanywa na Majasusi ambao waliungana na Rais kufanya Ugaidi, sasa palikua na siri nzito sana na ilikua ngumu kuwajua Majasusi.

    Marcus alifika mbele ya nyumba moja iliyopo Tabata Kinyerezi, alifurahishwa na namna nyumba hiyo ilivyoandaliwa, chumba chake cha kazi kilikua kimeshaandaliwa vyema, vifaa vyote vilikua humo, aliketi kwenye kiti akijizungusha.

    ***

    Chuo kikuu cha Dar-es-salaam maarufu kama UDSM ilikutwa mchoro mmoja uliowaacha wengi 

    kwenye Mataa, Mchoro ulikutwa kwenye meza moja wakati Wanachuo wapya wakiwa wanafanya Usafi humo. Aliyeuona mchoro huo alikua na Msichana mmoja, aliwaita baadhi ya wanachuo wapya watatu ambao alikua nao karibu. 

    Wote walipoutazama mchoro huo waliogopa sana, wakamshauri Msichana huyo anayeitwa Riyama aupeleke Mchoro ofisini kwa Mkuu wa chuo. Naye alifanya hivyo, Mkuu wa Chuo aliukagua mchoro huo ambao naye ulimuogopesha sana. Haraka Mkuu huyo alipiga simu polisi, mara moja Polisi walifika hapo ili kuuangalia Mchoro huo uliowatisha Wanachuo hata Mkuu wa chuo.

    Polisi nao walistaajabu sana kuhusu mchoro huo ulioelezea Mauwaji, Polisi wakauliza mchoro huo umekutwa wapi, Riyama akawaambia.

    Polisi mara moja wakaelekea darasani, wakaliona eneo hilo ambalo alikua akikaa Mwanachuo 

    mmoja wa kiume anayeitwa Michael Jomo, mara moja waliomba taarifa za Kijana huyo aliyekua 

    akisomea masuala ya Sanaa katika Chuo hicho, Mkuu wa chuo akawapa na kuwathibitishia kua 

    Michael alikua mchoraji mzuri sana ambaye Chuo hicho kilikua kilimtegemea kwenye Uchoraji, 

    aliweza kumchora Mtu na kumtoa kama alivyo kama vile alikua amepigwa picha.

    Picha hiyo ikafikishwa polisi, ikasambazwa kwa Polisi walio Dar-es-salaam, cha ajabu picha hiyo ilifanana vile vile na kifo cha Mzee Yusuf, namna alivyokua amekufa akiwa amelalia meza, kisu mgongoni na vyote vilivyomo eneo la tukio. Picha hiyo ikazua mjadala mkubwa, mara moja 

    Mwanachuo Michael akaanza kusakwa na Mamlaka huku akihusishwa sasa moja kwa moja na kifo cha Mzee yusuf, kesi ya upelelezi ikaibuka upya.

    Picha hiyo ikamfikia Mpelelezi Marcus, jasusi ambaye ndiye amekabidhiwa kesi hiyo. Hapo sasa 

    akalivalia njuga jambo hilo, kwanza akataka kuisoma ripoti iliyoachwa na Mpelelezi Daudi Mbaga aliyehamishiwa Uvinza Kigoma.

    Akaisoma kwa makini sana pia akazitazama picha za eneo la tukio, hata yeye akasadiki hivyo kua Mchoraji alilichora eneo la tukio, lakini swali la Msingi kumjia alijiuliza Kijana huyo alikua Nani hasa hadi akafika eneo la tukio na kuchora picha ya Mauwaji.

    Polisi walifanikiwa kufika nyumbani kwao Kijana Michael Jomo, alikua akiishi Ukonga Banana, alikua akiishi na Mama yake Mzee na paka wao ambaye baada ya mahojiano mafupi na Mama yake Michael aliwaambia jina la Paka huyo kua anaitwa Michael Junior, jambo hilo liliwafanya polisi waone kua Kijana hakua wa kawaida.

    Kwa maelezo ya Mama yake Michael aliwaambia Polisi kua Kijana wake alikua akiishi kwa hofu sana kwa zaidi ya Miezi miwili, siku moja aliwahi kumwambia Mama yake kua kuna ndoto anaiota anaogopa sana, Michael alimweleza Mama yake kua anamwota Mwanamke Mmoja akifanya Mauwaji ya Kutisha.

    Akili za Polisi zilisisimka baada ya kusikia hivyo

    “Yuko wapi Michael?” Mama yake Michael alinywea baada ya kuulizwa swali hilo, alikaa kimya kwa sekunde kadhaa kisha akawaonesha mlango wa chumba kimoja chenye herufi kubwa Mlango iliyoandikwa ‘J’ ikiwa ni kifupi cha jina JOMO

    Polisi wakaenda hadi mlangoni na kugonga, walijibiwa na Ukimya. Wakajaribu kufungua lakini 

    waligundua mlango ulifungwa kwa ndani, Polisi wakafikia makubaliano ya kuuvunja Mlango ili wampate Michael, wakati huo Jasusi Malcom ambaye anatambulika kama Marcus alikua kwenye gari akienda hapo nyumbani kwa Michael.

    Walipouvunja mlango walistaajabu sana, macho yaliwatoka kwa Mshangao. Japo walikua Maaskari polisi lakini washika vichwa vyao na wengine walishika viuno vyao, waliona jambo la ajabu lenye kutisha na kusisimua sana.

    Ni Jambo Gani? Usikose Sehemu Ya 07

    Jiunge WhatsApp Channel Ya KIJIWENI Ili Kuwa Wa Kwanza Kupata Updates Za RIWAYA Hii Kwa Kubonyeza Hapa 

    SOMA Uchambuzi Na Makala Mbalimbali Kwa Kubonyeza Hapa

     

     

     

     

    KOTI JEUSI Koti Jeusi Kijiweni riwaya ya koti jeusi

    18 Comments

    1. Mikidadi Sibati on May 4, 2024 11:02 am

      Jambo gani Hilo jmn utamu juu ya utamu

      Reply
      • Phoady on May 4, 2024 12:49 pm

        Loh! Story tamu lakin inaweka suspendion mapema

        Reply
      • Moderich on May 4, 2024 10:23 pm

        Doooh mambo ni moto

        Reply
    2. Lus twaxie on May 4, 2024 11:21 am

      Jamaaanii mbn inaishia patamuu

      Reply
    3. Rumbyambya Jr on May 4, 2024 11:22 am

      Sasa hyo sehemu ya 7 iwe leo Jioni Admin

      Reply
    4. Seif on May 4, 2024 11:28 am

      Jamb gan mbona kunoga mpka usogoni

      Reply
    5. Veronica kitundu on May 4, 2024 11:34 am

      Jmn mpaka lini tena kesho au leo jion

      Reply
      • Esther Emmanuel on May 4, 2024 7:23 pm

        Ni nzuri sana jaman pongezi zimfikie mwandishi wetu

        Reply
    6. Djkelly255.. on May 4, 2024 11:42 am

      Hii riwaya ingempata director mzuri apa bongo lingetoka bonge la movie viwango vy Netflix

      Reply
    7. Gabriel Marwa on May 4, 2024 11:57 am

      oyaaa hiii ya Leo kali sana🙌🙌

      Reply
    8. Mon_dee_beat on May 4, 2024 12:11 pm

      Sehemu ya 7 tunaomba iwe leo jion

      Reply
    9. Valence on May 4, 2024 12:14 pm

      Aisee nimeshtuka Kariakoo ilitaka kulipuliwa kwa bomu! Ha ha ja anyways natania,,,,, kazi ni nzuri

      Reply
      • Ms chunnie on May 4, 2024 12:36 pm

        😂😂😂me nkaanza kuwaza wameripua kariakoo nmepotezana na mtu angu🤧🥱 ikapita miaka kadhaa nkaja onana nae anyway namii nkaanza kujitungia stor apo😂😂💔

        Reply
    10. Jenipha on May 4, 2024 2:18 pm

      😄🤔🤔🤔mambo yanazidi kuwa🔥🔥🔥🔥

      Reply
    11. Consolatha issaya Edward on May 4, 2024 5:52 pm

      Daaaah! Sema mwandishi unajua mpk unajua tena, 🙏🙏🫂

      Reply
    12. Esther Emmanuel on May 4, 2024 7:21 pm

      Ni nzuri sana jaman pongezi zimfikie mwandishi wetu

      Reply
    13. Alhajmwema on May 4, 2024 11:17 pm

      🤝🏿

      Reply
    14. Omary on May 5, 2024 10:43 pm

      Noma yani

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.