Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    ZAINABU ( 01)

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Yanga Dhidi Ya Simba Tutegemee Mchezo Wa Aina Gani?
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Yanga Dhidi Ya Simba Tutegemee Mchezo Wa Aina Gani?

    Living ShayoBy Living ShayoApril 20, 2024Updated:April 20, 20249 Comments3 Mins Read819 Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    yanga vs simba
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Moja ya mchezo mkubwa sana nchini mchezo ambao umekuwa ukiteka hisia kali za watu wengi huku ukiwa unafatiliwa ndani na nje ya nchi ya Tanzania, Mchezo huu maarufu nchini kama “Derby ya Kariakoo” ambao daima umekuwa ukiwakutanisha Simba SC pamoja na Yanga SC kwa nyakati tofauti.

    Siku zote Yanga SC na Simba SC wakicheza umekuwa mchezo mzuri sana na vita zao mara nyingi ufanyika ndani na nje ya uwanja, ukizungumzia nje ya uwanja ni mbwembwe pamoja na hisia na tambo za mashabiki mbalimbali wa soka, na unapozungumzia ndani ya uwanja ni wachezaji wa timu zote kucheza kiwanjani na kushuhudia vita ya mbinu, mifumo na ufundi wa Wachezaji na makocha kwa pande zote mbili.

    Takwimu na Kumbukumbu za timu hizi kwenye michezo yote misimu yao 7 ya mwisho kwenye Ligi kuu ya Tanzania kurudi nyuma kuanzia msimu huu imekuwa migumu sana kwa timu zote mbili ambapo ushindi kwa timu zote mbili haupishani sana kwani Yanga SC amefanikiwa kushinda jumla ya michezo hiyo ameshinda 2 huku akiwa na Sare 4, ambapo kinyume chake ni kuwa Simba SC amefanikiwa kushinda mchezo mmoja (1) na kutoka sare 4 ikiwa ni utofauti wa ushindi kwa mchezo mmoja pekee.

    Hata hivyo mpaka sasa mchezaji anayeongoza kufunga magoli kwenye michezo hiyo 7 ya mwisho ya “Derby” walipokutana ni Stephane Aziz Ki wa Yanga SC pamoja na Kibu Denis wa Simba SC ambao wote wana magoli mawili na uzuri ni kuwa wana uwezo wa kuongeza magoli hayo kwani bado ni sehemu ya vikosi vya timu zote mbili.

    Hata hivyo nje ya takwimu na kumbukumbu hizo kwa ujumla ndani ya michezo 7, kwenye upande wa michezo mitano ya mwisho ya Ligi kuu ya NBC na michuano mingine ni kuwa Simba SC wamepoteza michezo miwili, wakitoa sare moja pamoja na kushinda michezo miwili na kwa uoande wa Yanga SC amepoteza mchezo mmoja na kutoa sare 2 na kushinda michezo 2, kwenye kufunga magoli Yanga SC amefunga magoli 5 akiruhusu 1 na uoande wa Simba SC amefunga magoli 6 huku akiruhusu magoli 5 tofauti ya goli moja la kufunga na kufungwa.

    Ukija kwenye upande wa uchezaji kiwanjani Yanga SC amekuwa bora zaidi kuliko Simba SC msimu huu, kwanini ? Timu yao imekuwa na muunganiko mzuri kuanzia nyuma mpaka eneo la mwisho la ushambuliaji wakiwa na uwiano mzuri wa kukaba na kushambulia pia, ila kwa upande wa Simba SC wamekuwa vizuri kutoka nyuma kwenda mbele changamoto kubwa ni eneo lao la kati kwenye kukaba wamekuwa wakiruhusu nafasi kwa mpinzani kuwashambulia kwa kukosa muunganiko mzuri wa kukaba hususa eneo la kati.

    Timu zote zimekuwa zimekuwa zikitumia zaidi eneo lao la kati ambapo ndiyo imekuwa eneo lao mama zaidi kuanzia kukaba na kushambulia. Tofauti yao hiko wapi ? Moja ni eneo la kiungo, upande wa Simba SC wamekuwa wazuri eneo la ushambuliaji ila changamoto ipo kwenye kiungo ukabaji wameshindwa kuwa na kiungo mkabaji ambaye atailinda vizuri eneo lao la beki jambo ambalo linafanya wanapitika kirahisi tofauti na Yanga SC ambao wanakiungo cha ukabaji kizuri kuliko Simba SC.

    Eneo hatari zaidi kwenye mchezo wa leo ni kiungo hususa kiungo cha ushambuliaji kwa pande zote mbili wamekuwa vizuri kwenye kutengeneza nafasi za ufungaji nyingi zaidi.

    Changamoto kubwa liko kwenye eneo lao la ushambuliaji wachezaji wa timu zote mbili wanaocheza eneo la ushambuliaji wamekuwa na chanagamoto ya kutumia nafasi, tofauti ni kuwa Yanga SC wamekuwa na wachezaji wengine nje ya washambuliaji ambao wamekuwa wakitumia vizuri nafasi wanazotengeneza jambo ambalo ni tofauti kwa upande wa Simba SC ambao wanatengeneza nafasi ila bado hazitumiki.

    SOMA ZAIDI: Tabiri Sasa Matokeo Ya Dabi Ya Kariakoo Hapa Kijiweni

    simba sc yanga sc leo yanga vs simba sc
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views
    Ligi Kuu ya NBC

    RATIBA YA LIGI KUU YA NBC MSIMU WA 2025/2026

    August 29, 202513K Views
    Don't Miss
    Hadithi March 23, 2026

    ZAINABU ( 01)

    NAITWA ZAINABU ALIYU! Hii ni Hadithi ya Maisha yangu…..!!  Mimi ni Mtoto wa kwanza kati…

    Mkeka Wa Leo Jumatatu 16/03/2026 Wa Magoli OVER 1.5

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (09)

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua

    Niliolewa Na Mtu Nisiyemjua SEASON 2 (08)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2026 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.