Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Njia Ipi Bora Kwa Mzize? Aende AZAM au Abakie Yanga Au Ulaya?
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Njia Ipi Bora Kwa Mzize? Aende AZAM au Abakie Yanga Au Ulaya?

    Living ShayoBy Living ShayoApril 18, 2024Updated:April 18, 202411 Comments3 Mins Read4K Views
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Clement Mzize
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ilimchukua msimu mmoja na nusu kuhudumu kwenye kikosi cha vijana cha timu hiyo na baada ya hapo nyota yake ilianza kung’ara akianzia kwenye kikosi cha timu ya vijana na kuibuka mfungaji bora wa michuano hiyo, ni kama ilionekana anaweza na ana kitu licha ya kuwa bado alikuwa akicheza kwenye kikosi cha vijana ila nyota nzuri iling’ara kwake.

    Kocha mkuu wa kikosi hicho alimuona na kuamua kumoa nafasi ya kufanya mazoezi na kikosi cha timu ya wakubwa na alipoingia kwenye mfumo basi Kocha mkuu wa kikosi hicho kwa wakati huo aliamua kumpa nafasi ya kuwa sehemu ya mchezo mmoja wa Ligi kuu akitazama akiwa kwenye benchi jambo ambalo kadri muda ulivyokuwa unaenda kijana huyo akapata nafasi ya kuingia kwenye moja ya mchezo wa timu hiyo na kilichobaki ilikuwa ni historia tu kwake na jamii yote.

    Kwa sasa kijana huyo amekuwa mchezaji muhimu ndani ya kikosi cha Yanga SC na siyo kwa bahati mbaya bali kwa kile anachoonyesha akiwa na kikoai chake cha Yanga SC kwa misimu miwili sasa na kupelekea kuwaweka benchi wachezaji wa kigeni anaocheza nao nafasi hiyo.

    Huyu siyo mwingine ni Clement Mzize kijana ambaye maisha yake ya mpira muda mwingi yalikuwa mkoani Iringa eneo la Semtema, miguu yake ikicheza sana kwenye uwanja wa Kihesa, Kigonzile na Samora pia. Ila kwa sasa kijana huyo miguu yake imekuwa ikicheza viwanja vikibwa ndani ya nje ya Tanzania

    Clement Mzize ni kijana ambaye ameonyesha ubora wake kwa muda mfupi licha ya kutopita kwenye misingi bora ya mpira wa miguu ukilinganisha na vijana wengine kama Dickson Job, Israel Mwenda, Kibwana Shomari. Licha ya yote hayo bado ameonyesha ubora jambo ambalo linapelekea kuibua tetesi mbalimbali kuhitajika na baadhi ya vilabu vikubwa ndani ya nje.

    Kitendo cha Azam FC kuhitaji huduma ya kijana huyo tena kwa kuweka kiasi kikubwa sana cha pesa mezani ili kupata saini yake ni dhahiri kuwa kwa sasa thamani yake ipo juu na ni wakati wake sasa. Licha ya yote hayo ila kijana huyu amekuwa bora sana akiingia kwenye mifumo mbalimbali ya makocha, kivipi ?.

    Wakati wa kocha Nasredine Nabi, alikuwa akitumika zaidi akitokea katikati zaidi na alikuwa akionyesha ubora wa hali ya juu akiungana (aki link) vizuri na viungo wa ushambuliaji kwa kutengeneza magoli na kufunga pia. Ila kwa sasa chini ya Miguel Gamondi amekuwa akitokea katikati ila mara nyingi amekuwa akitumika zaidi kama mshambuliaji ila akitokea pembeni zaidi akitengeneza nafasi na ndiyo sababu ya kuwa mshambuliaji pekee kwenye Ligi aliyetengeneza (Assist) magoli mengi akiwa nazo 5 mbili nyuma ya kinara wa (Assist) Ligi kuu.

    Anaweza kuingia kwenye mfumo wa Azam FC? Jibu ni ndiyo kwani namna wanavyocheza Azam FC wamekuwa wakitumia mawinga zaidi na kwa nmana anavyocheza Clement Mzize ni dhahiri ataingia kirahisi sana na hiyo inabebwa na uwezo wake wa kutokea pembeni na katikati pia.

    Ni ipi njia bora kwake kubaki Yanga SC au kwenda Azam?. Kwa mujibu wangu sioni shida kwa yeye kwenda Azam FC au kuamua kubaki Yanga SC na sababu ni kuwa vyote ni vilabu vikubwa. Ila kwenye upande mwingine ni angalie upande ambao utampa zaidi mafanikio kwenye uoande wa maokoto nikimaanisha malipo kuanzia usajili hadi mshahara wake kwani maisha ya wacheza mpira ni mafupi mno hivyo ni vyema akaanza kutengeneza njia nzuri sasa.

    Kiasi walichoweka Azam FC ni kikubwa sana na kimeonyesha kumpa thamani mchezaji huyo na hiyo ni faraja sana kuona mzawa anapewa thamani kubwa hivyo, ila yote ya yote Azam FC kuna nafasi kubwa kwake yeye kucheza zaidi tena kwenye kikosi kinachoanza.

    SOMA ZAIDI: Barua Nzito Ya Shabiki Kwa Viongozi Wa Simba Kuhusu Inonga 

    mzize kwend ulaya mzize kwenda azam fc yanga kumuuza Clement Mzize

    11 Comments

    1. Timoth komba on April 18, 2024 10:57 am

      Asikurupuke afanye maamuzi sahh ambayo kamwe hatojutia sababu umri wake unaruhusu kufanya makubwa zaid

      Reply
    2. Tobias Mzopola on April 18, 2024 11:40 am

      Azam fc ndiyo chaguo lake Kwa sasa. Hauhitaji kufikiria mara mbili kufanya maamuzi hayo hata kama wewe ndo ungekuwa mzize.

      Reply
    3. Imaninho30 on April 18, 2024 12:11 pm

      Age bado hipo msingi aende ulaya tu maana huko kuna kitu atajenga mguu wa kutoka mtume kauombea

      Reply
      • Mashaka Lugoma on April 18, 2024 1:23 pm

        Ulaya hapawezi kuwa sawa na Chamazi wala Kariakoo bila kufikiria ni namna gan ataweza kufanikiwa au kutofanikiwa ila Watford ni miongoni mwa timu kubwa kwa level ya wachezaji kutoka kwenye taifa kama letu (Tanzania)

        So kama Watford wapo serious kwel basi Mzize na watu wanaomsimamia hawatakiwi kupepesa macho kwenye deal hilo kwani kucheza championship ya England ni tayar profile ya mchezaji inaanza kukua na kuanzisha safari nyingine ya soka kwa mchezaji yeye binafsi na Taifa letu

        Reply
    4. Agripina mwang'onda on April 18, 2024 12:16 pm

      Me nadhani Clement mzize ni wakati wake wa kuchagua Azam au Abaki yanga Ila wanayanga bado tunamhitaji Sana na kwakuwa Ana uwezo mkubwa ni bora tumpeleke Ulaya kipaji kikukue zaid

      Reply
    5. Collins collinho on April 18, 2024 12:34 pm

      Kupata offer ya kwenda ulaya then ukatae uende azam itakua ujinga yatakua kama ya ibrahim ajibu kapata offer kwenda tp mazembe akagoma et anaipenda simba nini kilimkuta sasa yupo costal union mzize anatakiwa kukaa na kufikilia kwa makini sana

      Reply
    6. Baxeo Africa on April 18, 2024 1:05 pm

      Mm Kama mhanga wa maendeleo ningependa kumshauri kijana huyu chipukizi alinganishe uwiano wa mambo mawili kabla ya kufanya maamuzi ambayo ni;
      1.upande wa maokoto kwa manufaa yake binafsi
      2.ni uwezekano wake kucheza katika kikosi Cha kwanza kwa AJILI ya kipaji chake

      Reply
    7. Rumbyambya Jr on April 18, 2024 1:19 pm

      Wenyewe wanamuita waridi Mzinze. Ipo hivi Clement yampasa atumie busara kubwa sana kufanya maamuzi ambayo yatamletea manufaa yafuatayo;
      1.kutokupotea katika rada za Soka
      2.Kujitengenezea nafasi za kuwa bora zaidi ili kwenda Katika soko la Football
      Kwa upande wangu ni bado mapema saana kwa mzinze kwenda Ulaya .
      Bora zaidi akienda kwa Wana lamba lamba mwisho wa Msimu kwa sababu Yanga watasajili na hope atakuja mtu atakempa Mzinze wakati mgumu sana kuwika mitaa ya Jangwani

      Reply
    8. Big sam on April 18, 2024 1:23 pm

      Uamuzi niyeye mwenyewe atachagua mbivu nambichi

      Reply
      • Joseph kusekwa on April 18, 2024 2:16 pm

        Ni Yeye tu achague kipi Bora ila kwangu Mimi Abakie jangwani kwanza najua jina litazidi kujua mno na kuimbwa na Kila mtu
        Na kwa badae naiona kabisa safar ya ulaya😂

        Reply
    9. Official DG on April 18, 2024 5:17 pm

      Abaki Yanga kwa kua bado chipkiz akienda huko mambele ataishia kupigwa sub na ku under performe ni bora achezee yanga kwa msimu mwingine aivee vizuri kisha ndo atembee mamble ila sio Azam . maana atakua anajishusha kutoka juu kwenda chini

      Reply
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.