Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Dondoo Na Takwimu Zote Simba Dhidi Ya Tanzania Prisons
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Dondoo Na Takwimu Zote Simba Dhidi Ya Tanzania Prisons

    Living ShayoBy Living ShayoMarch 6, 20241 Comment3 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    simba na Tanzania Prisons
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Ni zaidi ya misimu kumi sasa vilabu hivi vinashiriki Ligi kuu ya Tanzania kwa nyakati tofauti tofauti huku ikiitwa majina ya wadhamini mbalimbali, vilabu hivyo vimekutana mfululizo kila msimu kwa zaidi ya muongo mmoja sasa tokea ikiitwa Vodacom Premier League maarufu kama VPL, ikaaitwa tena Tanzania Premier League (TPL) na sasa inaitwa NBC Premier League bado wanaendelea kukutana.

    Wanaozungumziwa hapo ni vilabu viwili ambavyo vinakutana kwenye mchezo wa pili wa raundi ya pili, mchezo wa Ligi kuu ya NBC 2023/2024 ambavyo ni Simba SC na Tanzania Prisons huku mchezo wa kwanza msimu huu walipokutana Simba SC alishinda 3-1 kwa magoli ya Clatous Chama, John Bocco na Saidi Ntibazonkiza kwa upande wa Simba SC huku Edwin Balua akiwafungia Tanzania Prisons.

    Kitakwimu mpaka sasa vilabu hivi vimekutana mara Saba kuanzia msimu wa 2020/2021 hadi msimu huu, ambapo Simba SC amekuwa akimuonea Tanzania Prisons kwa kushinda michezo minne (5) kati ya saba huku Tanzania Prisons akiibuka na ushindi kwenye mitanange miwili tu tena kwa ushindi unaofanana wa goli moja kila mchezo waliopata ushindi pamoja na kushuhudia sare kwenye mchezo mmoja baina yao.

    Uzuri ni kuwa michezo yote waliyokutana tokea 2020 imezaa magoli huku jumla ya magoli 18 yakifungwa na timu zote hata hivyo Simba SC wamefanikiwa kufunga jumla ya magoli 13 kati ya hayo na Tanzania Prisons akifunga magoli 5 tu na kati ya hayo magoli mawili yalifanikiwa kuwapa alama 6, ambapo 2020/2021 waliibuka na ushindi wa 1-0 wakiwa nyumbani pamoja na msimu wa 2021/2022 wa kuibuka tena na ushindi wa 1-0 nyumbani huku wakifunga goli moja kwenye sare ya 1-1 msimu wa 2020/2021 ugenini na magoli mawili waliyofunga wakifunga walipopoteza 7-1 ugenini nakwenye msimu wa 2022/2023  3-1 nyumbani kwenye mchezo wa kwanza msimu huu.

    Ndani ya michezo mitatu ya mwisho takwimu zinampa nafasi kubwa Simba SC kuibuka na ushindi kwenye mchezo wao wa leo ambapo ndani ya michezo hiyo ameibuka na ushindi mfululizo huku akifunga magoli 11 na akiruhusu magoli mawili.

    Tanzania Prisons wamebadilika sana kiucheza kwenye msimu huu wamekuwa wakicheza mpira wa kuvutia sana tokea kikosi hicho kuwa chini ya Kocha Ahmad Ally, wamekuwa wakitumia zaidi mfumo wa 4-4-2 ambapo muda mwingi mashambulizi yao yake kuwa yakianzia nyuma kwa walinzi kwenda mbele muda mwingi wa mchezo wamekuwa wakiweka mpira chini na kutengeneza nafasi kupitia winga na wakati mwingine kupitia katikati huku silaha yao kubwa ikiwa ni eneo Lao la kiungo na kwenye kutengenza magoli wakimtumia zaidi Zabona Hamis Mayombya, Kibaya ni kuwa namna ya uchezaji wao wakikutana na timu yenye kasi pembeni na viungo wanaopiga mipira ya pembeni wanapata shida.

    Upande wa Simba SC wamekuwa hawana kiwango cha muendelezo kwa msimu huu licha ya kupata ushindi kwenye michezo yao, silaha yao kubwa kwa sasa ni kiungo wao Saidi Ntibazonkiza kutengeneza magoli na kusaidia kukaba kuanzia juu jambo ambalo limemfanya kuwa kati ya wachezaji wa kumchunga unapokutana na Simba SC. Mfumo wa 4-2-3-1 umekuwa moja ya mifumo wanaoutumia zaidi huku wakibadilika Mara kadhaa hadi kwenye 4-3-3 kwa kutumia zaidi eneo la pembeni kuingia kati. Tokea mzunguko wa pili umeanza imekuwa ngumu kwao kudondosha alama na wachezaji wao wengi wamekuwa na kiwango bora sana na kitu ambacho kimewafanya kuruhusu magoli machache.

    Kitakwimu za wao kwa wao nafasi kubwa anapewa Simba SC kuibuka na ushindi na hiyo ni kutokana na kuwa na matokeo mazuri kwenye michezo yao ya mwisho kwa kushinda yote na kufunga magoli 11, hata hivyo ubora na namba Ya uchezaji wa sasa wa Tanzania Prisons unafanya kuweka matarajio ya kushuhudia mchezo mzuri wenye mbinu na Ufundi kutoka kwa wachezaji wa timu zote mbili.

    SOMA ZAIDI: Barua Kwako Mwanamfalme Prince Dube

    kikosi cha simba leo simba vs tanzania prisons wachezaji simba

    1 Comment

    1. Pingback: Simba Waliichukulia Poa Prisons Wameadabishwa - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.