Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Ningeshangaa Sana Kama Simba Wasingeshinda
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Ningeshangaa Sana Kama Simba Wasingeshinda

    Living ShayoBy Living ShayoFebruary 12, 2024No Comments3 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Mchezaji wa simba
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Timu zote mbili kwa nyakati tofauti walionekana kuwa watulivu sana hususa ni kikosi cha Simba SC licha ya kuwa nyuma kwa goli 0-0 ila walikuwa watulivu sana kwa dakika 90 za mchezo huo. Utulivu huo uliifanya Simba SC kuendelea kucheza kwenye mbinu yake na hata goli walilopata lilichangiwa na utulivu wao kuanzia nyuma kwenda mbele kufanya shambulizi.

    Licha ya kujaribu mara kadhaa wa kadhaa kucheza mipira ya juu ila Geita walionekana kuimudu vizuri mipira na muda mwingi wa mchezo walikuwa wakiiondoa kwenye eneo lao. Kuingia kwa Nassoro Saadun kwa upande wa Geita Gold FC kuliipa balance upande wa kulia wa Geita Gold na kulimnyima Mohamed Hussein “Zimbwe” kupanda mara kwa mara kama alivyokuwa anafanya kipindi cha kwanza, hii ndiyo Sub iliyoleta tofauti zaidi kwa timu zote mbili.

    Luis Miquisone pamoja na Saido Ntibazonkinza iliongeza kasi ya mashambulizi kwa upande wa Simba SCna sababishi wa goli la Simba SC.

    Mchezo ulichezwa zaidi na upande wa Simba SC utulivu wa Beki Che Malone Fondoh pamoja na kiungo Fabrice Ngoma uliendelea kuifanya Timu ya Simba SC kutulia mipira mingi iliyokuwa ikitua eneo lao walitulia na kuipeleka eneo sahihi.

    Mbinu kubwa ya Geita Gold FC waliyoitumia ni kujilinda zaidi kipindi cha kwanza waliingia na 4-4-2 mbele akibaki Ramadhani Kapera pamoja na Edmund John huku wachezaji wengi wa Geita wakiwa eneo lao na kuziba mianya mingi ya mpira kupita.

    Kipindi cha pili walibaki kwenye mbio yao ile ile ila Saadun alibaki kama mchezaji anayepanda na kushuka pamoja na Eric Mwijage wakisaidia mashambulizi pamoja na mshambuliaji Tariq Seif aliyechukua nafasi ya Ramadhani Kapera, hivyo iliongeza kasi kidogo ya kishambulia hususa mipira ikitokea pembeni kwa Mwijage pamoja na Saadun.

    Upande wa Simba SC waliingia na 4-3-3 ambapo Clatous Chama, Kibu Denis pamoja na Pa Omar Jobe wakitumika kwenye eneo la ushambuliaji, mabadiliko ya kimfumo yalikuwa yakitokea kuna wakati Simba SC waliamia kwenye mfumo wa 4-2-3-1 na Jobe alibaki kwenye eneo la mwisho Chama pamoja na Kibu Denis wakiungana na Sadio Kanoute kwenye kiungo zaidi kwenye kuipandisha timu huku Mzamiru Yassin na Fabrice Ngoma wakibaki zaidi eneo la ukabaji.

    Kipindi cha pili kwa Simba SC kilibadilika na walitumia zaidi maeneo yao ya Pembeni na hiyo ilifanya kumuingiza Luis Miquissone na Saidi Ntibazonkiza wakiwa wanatokea pembeni muda mwingi wa Mchezo na hata goli pekee la mchezo huo lilitokea upande wa pembeni.

    Kongole kwa waamuzi wa mchezo wa leo walijitahidi na mchezo ulikuwa na maamuzi sahihi kwa muda mwingi wa mchezo huo.

     

    SOMA ZAIDI: Mayele Ana Laana Ya Ligi Kuu?

    ligi kuu bara simba sc
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.