Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Ukiizungumzia Nusu Fainali AFCON Huwezi Yaacha Majina Haya
    Africa | CAF

    Ukiizungumzia Nusu Fainali AFCON Huwezi Yaacha Majina Haya

    Living ShayoBy Living ShayoFebruary 9, 20241 Comment3 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Moja kati ya mechi ambayo bila shaka watu wengi kwa maoni yao walitamani iwe ndio fainali yenyewe ni mchezo wa AFCON  uliowakutanisha Nigeria dhidi ya Afrika Kusini moja kati ya mechi bora sana iliyochezwa ya nusu fainali kutokana na matukio ambayo yalijitokeza katika mchezo huo.

    Ukiizungumzia nusu fainali hii basi kuna majina ambayo huwezi kuyaacha kuyataja ambayo katika nusu fainali hii walikua na balaa kubwa sana na hapa tumekuandalia majina haya matatu ambayo yalionesha mambo ya kushtukiza sana.

    Stanley Nwabali:

    Huyu unaweza kusema katika hatua ya nusu fainali ndio shujaa wa Nigeria kwenye toleo la 34 la AFCON aliyezaliwa kwenye kijiji cha River’s state kwenye jamii ya Okwuzi miaka 27 iliyopita akiwa na urefu wa futi 6.

    Nwabali anaitumikia klabu ya Chippa United ya Afrika Kusini na kwenye hatua ya nusu fainali alikuwa na kiwango bora sana dhidi ya Afrika Kusini nchi ambayo sehemu kubwa ya kusakata kwake kabumbu anafanyia kazi huko.

    Kwenye mchezo huo alicheza Dakika 120 akiwa ndiyo Mchezaji bora wa mechi kwani alifanya save 7 za hatari huku akipiga pasi 24 na 12 kati ya hizo zikifika kwa usahihi, pia alipiga pasi 17 ndefu na 5 zikifika kwa wahusika, akiokoa mipira ya juu (Punches) mara 3, akifanya recover mara 13.

    Mchezo huo ulikwenda hadi kwenye hatua ya mikwaju ya penalti na kipa huyu alifanikiwa kuokoa mikwaju miwili ya penalti, mkwaju wa kwanza kwa upande wa Afrika Kusini uliyopigwa na Teboho Mokoena aliokoa pamoja na penalti ya mshambuliaji Evidence Makgopa.

    Nwabali amefanikiwa kucheza michezo yote ya AFCON kwa upande wa Nigeria kuanzia hatua ya Makundi na kabla ya mchezo wa nusu fainali alicheza mechi 6 bila kuruhusu goli lolote lile.

    Golikipa wa timu ya taifa ya Nigeria Stanley Nwabali

     

    Teboho Mokoena:

    Kiungo wa Bafana Bafana mzaliwa wa eneo la Bethlehem ya Afrika Kusini akiwa na Futi 5 na umri wa miaka 27 akiwatumikia miamba ya African Football League, Mamelod Sundowns ya nyumbani kwao Afrika Kusini.

    Teboho Mokoena alikuwa na kiwango bora sana kwenye mchezo wa hatua ya Nusu Fainali dhidi ya Nigeria na alikuwa mchezaji wa pili kwa kuwa na nyota 8.1 nyuma ya kipa Stanley Nwabali ambaye alikuwa na 8.3.

    Alicheza dakika 120 akifanikiwa kufunga goli moja kwa mkwaju wa penalti, alipiga pasi 84 na pasi 70 zilifika kwa usahihi, akitengeneza nafasi moja na akipiga mashuti mawili “On target” akiwa kwenye eneo la kushambulia aligusa mipira mara 99 na alipiga pasi 15 kwenye eneo la mwisho la mpinzani “Final third” huku akifanikiwa kupiga kupiga krosi 3 na moja tu ndiyo ilifanikiwa kufika huku akipiga pasi ndefu 9 na 5 zikafika pamoja na kona moja.

    Nje ya kusaidia mashambulizi Teboho Mokoena alifanikiwa kusaidia ulinzi kwa kufanya clearance moja na “Recover” mara 7.

    Kiungo wa timu ya taifa ya Afrika Kusini Teboho Mokoena

    Ronwen Williams

    Ukiizungumzia timu ya taifa ya Afrika Kusini kwenye michuano ya mataifa barani Afrika haswa hatua ya Robo Fainali huwezi kuacha kumtaja kapteni wa timu hiyo ambaye ni golikipa Ronwen Williams mzaliwa wa Port Elizabeth kwenye jamii ya Gelvandale eneo la Gqeberha mwenye umri wa miaka 32 ambaye pia ni kipa wa klabu ya Mamelod Sundowns.

    Alikuwa mchezaji wa tatu aliyekuwa na kiwango bora na nyota 8.0 nyuma ya Stanley Nwabali na Teboho Mokoena kwenye mchezo wa nusu fainali.

    Amekuwa sehemu muhimu ya kikosi cha Afrika Kusini na nusu fainali alicheza dakika 120 akifanikiwa kufanya save 9, akirusha mipira 5, pia alipiga mipira 12 mirefu na kati ya hiyo mipira 5 tu ilifika kwa wahusika na kufanya “Recover” mara 10.

    Golikipa wa timu ya taifa ya Afrika Kusini Ronwen Williams

    SOMA ZAIDI: Safari Ya Afcon Na Heshima Kubwa Kwa Ligi Za Afrika

    afcon AFCON 2023 afcon leo Afcon today

    1 Comment

    1. Pingback: Afrika Kusini vs DR Congo Wachezaji Hawa Ni Balaa - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.