Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Nilitegemea Haya AFCON Hatua Ya Makundi
    Africa | CAF

    Nilitegemea Haya AFCON Hatua Ya Makundi

    Living ShayoBy Living ShayoJanuary 26, 20241 Comment2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Baada ya hatua ya makundi ya Michuano ya Mataifa barani Afrika AFCON kutamatika na kujua timu 16 ambazo zimefanikiwa kufuzu hatua ya 16 bora na kujua ratiba kamili ya hatua hii kabla ya kwenda robo fainali kujulikana. Karibu sana tutazame tuzo za hatua ya makundi zimeenda kwa nani na nani?

    1.MCHEZAJI BORA KIJANA HATUA YA MAKUNDI

    Mchezaji bora kijana hatua ya makundi Lamine Camara

    Mpaka hatua ya makundi inatamatika tumeshuhudia vijana wengi wakifanya vizuri ila kijana mdogo kutokea kikosi cha Senegal Lamine Camara ameibuka kuwa Mchezaji bora wa hatua ya makundi.Camara ambaye ana miaka 20 tu akiichezea klabu ya Metz huku akitumia zaidi mguu wa kulia, amevaa jezi namba 18 kwenye AFCON hii na amecheza Dakika 179 sawa na mchezo mmoja na mchezo mwingine akitolewa dakika ya 89.

    Hata hivyo amefanikiwa kufunga jumla ya goli 2 tu na yote dhidi ya Gambia na akipata kadi moja ya njano.Ikumbukwe kuwa Lamine Camara ndiyo Mchezaji bora wa AFCON U-20 iliyofanyika Misri. 

    2.KIPA BORA HATUA YA MAKUNDI

    Golikipa bora wa hatua ya makundi Jesus Owono

    Kipa wa timu ya taifa ya Equatorial Guinea Jesús Owono ndiyo amekuwa kipa bora wa michezo yote ya Hatua ya makundi. Jesus Owono amefanikiwa kufanya jumla ya save 25 za Hatari katika michezo yote mitatu kwa ujumla, huku akiwa na pasi moja ya goli dhidi ya Guinea Bissau akimpa Josete Miranda akifunga goli la pili la mchezo huo. 

    Ikumbukwe kuwa Jesus Owono anavaa jezi namba 31 kwenye kikosi chake cha Equatorial Guinea akiwa na umri wa miaka 22 tu akihudumu ndani ya Kikosi cha Deportivo Alaves ya Hispania na anatumia zaidi mguu wa kulia. 

    3.KOCHA BORA

    Kocha bora wa hatua ya makundi katika AFCON ALIOU CISSE

    Kocha mkuu wa kikosi cha timu ya taifa ya Senegal Aliou Cisse ameibuka kuwa Kocha bora wa michezo yote ya makundi ya AFCON, huyu ndiye kiongozi wa benchi nzima la Ufundi la Senegal.Cisse ameongoza jumla ya michezo mitatu ya Makundi akifanikiwa kushinda michezo yote mitatu, wakifunga jumla ya magoli 8 na wakiruhusu nyavu zao kutikiswa mara moja tu, huku likiwa taifa pekee lililofungwa goli moja tu katika hatua ya makundi.

    Kikosi cha Senegal ndiyo taifa pekee lililofanikiwa kushinda michezo yake yote ya hatua ya makundi na kukusanya jumla ya alama 9.Ikumbukwe kuwa Aliou Cisse ana umri wa miaka 47 na ni Nahodha wa zamani wa taifa hilo, na aliaanza kama Kocha msaidizi wa Senegal kwa miezi 10 na Marchi 2015 akateuliwa kuwa Kocha mkuu wa Senegal. 

    SOMA ZAIDI: Mchezaji Huyu Yanga Kutinga Robo Fainali AFCON

    AFCON 2023 wachezaji afcon

    1 Comment

    1. Pingback: AFCON Imepita Na Vichwa Vya Makocha Hawa - Kijiweni

    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.