Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Jonas Mkude Kutua rasmi Yanga SC… Mwenyewe afunguka
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Jonas Mkude Kutua rasmi Yanga SC… Mwenyewe afunguka

    David MohamedBy David MohamedJune 28, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Muda wowote kuanzia sasa zinaweza kusikia habari za kushtua. Jonas Mkude yuko kwenye mazungumzo na Yanga na atasaini mkataba wa kazi.

    Mkude ambaye aliichezea Simba kwa miaka 13 mfululizo alikula ‘Thank You’ wiki iliyopita, sababu kubwa ikielezwa kwamba ni kiwango kushuka.

    Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya Yanga  kimeeleza kuwa staa huyo aliyekulia Simba, Yanga watampa mkataba wa mwaka mmoja wenye masharti ya kuongeza kama kiwango kitamridhisha Kocha Miguel Gamondi.

    Chanzo hicho kilisema mkataba wa kiungo huyo umeambatana na makubaliano ya staa huyo kuahidi kuwa mtiifu na kufanya kilichompeleka ndani ya timu hiyo na kutumika kwa asilimia zote na sio vingine.

    Mwanaspoti lilimtafuta Mkude mwenyewe ambaye alisisitiza kuwa yeye ni mchezaji huru kwa sasa baada ya kumalizana na waajiri wake wa zamani Simba.

    “Mimi ni mchezaji na sasa nipo huru sina timu ninayoitumikia lolote linaweza kutokea kuhusu Yanga hii taarifa ndio kwanza naisikia kutoka kwako siwezi kuizungumzia sana muda utaongea;

    “Hiki ni kipindi cha usajili mengi yanazungumzwa lakini ukweli wa mimi kucheza wapi utajulikana muda sio mrefu kwasasa mimi nipo naendelea na mambo yangu mengine lakini msimu ujao nitacheza, kuhusu timu mtajua tu kwani mpira ni mchezo wa wazi.” alisema Mkude.

    Jonas Mkude

     

    Swali kubwa kwa mashabiki baada ya kusikia tetesi za Mkude kusaini Yanga, ni nini kitatokea kikosini haswa kwenye eneo la kati anapokwenda kucheza.

    Je, yule namba 6 ndiyo huyo? Je, kati ya Khalid Aucho na Yanick Bangala nani atakwenda benchi? Ni suala la muda, lakini habari za ndani zinasema kwamba Yanga huenda wakapumua kama Mkude ataweza kuwa kwenye ubora wake kwani Bangala tayari walishaanza kumtafutia mbadala kutokana na kiwango chake pamoja na mengine ya nje ya uwanja.

    Kocha Gamondi, anaweza kuanza na Mkude na Aucho katikati mbele wakasimama Makabi Lilepo(Al Hilal) na Fiston Mayele.

    Tutaendelea kukujuliza undani wa taarifa hii kadri itakavyotufikia kupitia ukurasa wetu huu. Ungana Nasi.

    jona mkude yanga jonas mkude ligi kuu bara mkude kwenda yanga simb sc tetesi za usajili usajili wa mkude yanga sc
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.