Close Menu
Kijiweni

    Subscribe to Updates

    Get the latest updates from Kijiweni.

    Za moto

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Facebook X (Twitter) Instagram
    • Wasiliana Nasi
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest Vimeo
    Kijiweni
    • Home
    • CAF
    • Soka la Bongo
    • Ulaya
    • Chuo Cha Kubeti
    • Hadithi za Kijiweni
    • Forum
    Kijiweni
    You are at:Home » Kocha Mgunda Kutemwa Simba? Mwenyewe afunguka
    Ligi Kuu | Soka la Bongo

    Kocha Mgunda Kutemwa Simba? Mwenyewe afunguka

    David MohamedBy David MohamedJune 16, 2023No Comments2 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram LinkedIn Tumblr Email Reddit
    Share
    Facebook Twitter LinkedIn Pinterest WhatsApp Email

    Kocha wa Simba, Juma Mgunda amefafanua maneno yanayotembea mitandaoni kwamba si sehemu ya kikosi kipya cha Mnyama.

    Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya kujiridhisha kwamba Kocha Robertinho, amewaambia Simba wampe mkataba Mnyarwanda, Hategekimana Corneille wa Rayon kama Kocha wa viungo lakini awali akiwa nae Rwanda alikuwa akimtumia kama mshauri wake.

    Kocha Mgunda ambaye ni mzoefu na miongoni mwa wazawa wasomi akiwa na leseni A ya CAF, ameeleza kuwa bado yupo sana Simba, akizikana tetesi za kutaka kurejea kwenye timu yake ya zamani Coastal Union ya Tanga.

    Amefafanua kwamba kwanza Coastal licha ya kuwa washikaji zake lakini ana matatizo nayo binafsi ambayo hakutaka kuyaweka wazi.

    Mgunda ambaye kwa sasa yupo mapumzikoni Tanga baada ya kumalizika msimu wa Ligi Kuu Bara amesema bado ataendelea kuwatumikia wana Msimbazi hadi mkataba wake utakapomalizika ndipo atakapojua kinachofuata na bosi wake, Robertinho hajamwambia kama kuna mabadiliko yoyote kwenye kibarua chake.

    “Mmefanya vizuri kuniuliza, kwani majibu yangu yatawapa kujua bado ni mfanyakazi wa Simba. Kuhusu Coastal siwezi kukataa kwamba ni timu yangu ambayo nimetoka nayo mbali, tukirekebisha matatizo yetu tutaendelea salama,” alisema kocha huyo ambaye amejiwekea rekodi nzuri Simba.

    “Nipo Tanga kwa mapumziko utakapofika muda wa kurejea kwenye majukumu Simba mashabiki wangu wataniona,”alisema na kuongeza kuwa msimu uliomalizika aliuona ushindani mkubwa ambao unawapa picha ya kufanya maandalizi makubwa zaidi kwa ajili ya ujao.

    “Ligi ina ushindani mkali na soka linakuwa, hivyo kila timu itakuwa inajipanga kulingana na mahitaji yake ya msimu mwingine,”alisema.

    Kocha Mgunda ana mchango mkubwa Simba, aliivusha kipindi anakaimu ukocha mkuu baada ya kuondoka Zoran Maki, aliitengeza timu licha ya kushinda mechi nyingi za Ligi Kuu pia alifanya vizuri kimataifa.

    Kwa taarifa zaidi za michezo ulimwenguni tufuatilie hapa.

    caf coastal union habari za simba habari za usajili juma mgunda msimbazi simba. simba sc tetesi za usajili usajili
    Leave A Reply Cancel Reply

    Social Media Image
    Top Posts
    UEFA EURO 2024 Trophy

    Yote Unayopaswa Kufahamu Kuhusu UEFA EURO 2024 German

    May 30, 202425K Views
    Ligi Kuu

    Hii Vita Ya GAMONDI Na FADLU Inaichangamsha Vipi Ligi Kuu?

    October 3, 202417K Views

    Chama, Aziz Ki Na Pacome Watachezaje Yanga?

    June 27, 202414K Views

    Ratiba Ya Ligi Kuu Tanzania Bara (NBCPL) 2024/2025

    August 9, 202413K Views
    Don't Miss
    Hadithi June 9, 2025

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Tisa-09)

    Ilipoishia Return of Faudhia sehemu ya nane  “Safi” sauti ya pili nayo ilisema kutokea chumba…

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Nane-08)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Saba-07)

    Return Of Faudhia ( Sehemu Ya Sita-06)

    Stay In Touch
    • Facebook
    • X
    • Pinterest
    • Instagram
    • YouTube
    • Vimeo

    Subscribe to Updates

    Get the latest creative news from Kijiweni.

    © 2025 Kijiweni. A Product of Jamii Media.
    • Home
    • Wasiliana Nasi

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.